1 Wafalme 7 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 7:1-51

Solomoni Ajenga Jumba Lake La Kifalme

17:1 Ezr 4:7; Neh 2:1; 1Nya 6:14Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme. 27:2 1Fal 2:35; Neh 11:11Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100,7:2 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini,7:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi zilizorembwa. 3Ilipauliwa kwa mierezi juu ya boriti zile zilizolala juu ya nguzo arobaini na tano, kumi na tano kwa kila safu. 4Madirisha yake yaliwekwa juu kwa safu tatu, yakielekeana. 5Milango yote ilikuwa na miimo ya mstatili, ilikuwa upande wa mbele katika safu tatu, ikielekeana.

67:6 Neh 12:36; Ezr 5:5; Isa 41:20; Mwa 32:28; Neh 1:10-11Akajenga ukumbi wa nguzo, ambao urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini7:6 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na upana wake dhiraa thelathini. Mbele ya jengo hilo kulikuwepo baraza. Mbele ya baraza kulikuwepo na nguzo na paa lililoningʼinia.

77:7 Ezr 8:1; 2:43Akajenga ukumbi wa kiti cha enzi, Ukumbi wa Hukumu, mahali ambapo angelitolea hukumu, akaufunika kwa mierezi kutoka sakafuni hadi darini. 8Kwenye jumba la kifalme ambamo angeliishi, aliiweka nyuma zaidi, ikiwa na mjengo wa aina moja na hiyo nyingine. Pia Solomoni akajenga jumba la kifalme linalofanana na huo ukumbi mkubwa kwa ajili ya binti Farao, aliyekuwa amemwoa.

97:9 Neh 2:8Ujenzi huu wote, kuanzia nje mpaka kwenye ua mkuu na kuanzia kwenye msingi hadi upenuni, ulifanywa kwa mawe ya ubora wa hali ya juu yaliyokuwa yamechongwa kwa vipimo na kusawazishwa kwa msumeno nyuso zake za ndani na za nje. 107:10 Kum 33:10; Neh 8:1-8; 2Tim 4:2; 1Sam 7:3; 2Nya 12:14; Za 10:18; 119:45; Mal 2:7Misingi iliwekwa kwa mawe makubwa yaliyo bora, yenye urefu wa dhiraa kumi7:10 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na mengine yenye urefu wa dhiraa nane7:10 Dhiraa nane ni sawa na mita 3.6. 11Sehemu za juu kulikuwepo na mawe yenye ubora wa hali ya juu, yaliyokatwa kwa vipimo na boriti za mierezi. 127:12 Dan 2:37; Ezr 4:10Ule ua mkuu ulizungukwa na ukuta wa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa, kama ulivyokuwa ua wa ndani wa Hekalu la Bwana na baraza yake.

Samani Za Hekalu

(2 Nyakati 4)

13Mfalme Solomoni akatuma watu Tiro kumleta Hiramu, 147:14 Es 1:14ambaye mama yake alikuwa mjane kutoka kabila la Naftali na baba yake alikuwa mtu wa Tiro tena fundi wa shaba. Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu na mzoefu katika aina zote za kazi ya shaba. Alikuja kwa Mfalme Solomoni na kufanya kazi zake zote alizopangiwa.

157:15 Kum 12:5; 1Nya 29:6; 2Nya 6:2; Za 135:21Hiramu akasubu nguzo mbili za shaba, kila moja ikiwa na urefu wa dhiraa kumi na nane,7:15 Dhiraa 18 ni sawa na mita 8.1. kila nguzo ikiwa na mzingo wa dhiraa kumi na mbili7:15 Dhiraa 12 ni sawa na mita 5.4. kwa mstari. 167:16 Kut 3:22; Ezr 8:25; Zek 6:10; 1Nya 29:6Pia alitengeneza mataji mawili ya shaba ya kusubu ili kuyaweka juu ya hizo nguzo; kila taji lilikuwa na kimo cha dhiraa tano7:16 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. kwenda juu. 177:17 2Fal 3:5; Hes 15:5-12Wavu wa mikufu iliyosokotewa kwenye zile taji juu ya zile nguzo, saba kwa kila taji. 18Akatengeneza makomamanga katika safu mbili kuzunguka kila wavu kuremba mataji yaliyo juu ya nguzo. Alifanya hivyo kwa kila nguzo. 197:19 Ezr 5:14; Yer 27:22Mataji yaliyokuwa juu ya nguzo kwenye baraza, yalikuwa katika umbo la yungiyungi, kimo chake ni dhiraa nne7:19 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 207:20 Ezr 6:4; 1Kor 4:1-2Juu ya mataji ya zile nguzo mbili, juu ya ile sehemu yenye umbo kama bakuli, karibu na ule wavu, kulikuwa na yale makomamanga 200 katika safu kuzunguka pande zote. 217:21 Ezr 4:16-20; 5:3-6Hiramu akasimamisha nguzo kwenye baraza ya Hekalu. Nguzo ya upande wa kusini akaiita Yakini,7:21 Yakini maana yake Mungu atafanya imara. na ile ya upande wa kaskazini Boazi.7:21 Boazi maana yake Ndani ya Mungu kuna nguvu. 22Mataji yaliyokuwa juu yalikuwa na umbo la yungiyungi. Hivyo kazi ya nguzo ikakamilika.

237:23 Ezr 6:10; Isa 60:12; Yer 12:14; Za 68:29; 1Tim 2:1-2Hiramu akasubu Bahari ya chuma, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Mzunguko wake ulikuwa dhiraa thelathini. 247:24 Ezr 4:13; 8:36Chini ya ukingo, ilizungukwa na maboga, kumi kwenye kila dhiraa moja. Maboga yalikuwa yamesubiwa katika safu mbili ili kuwa kitu kimoja na hiyo bahari.

257:25 Kut 18:21-26; 16:18; Za 19:7; Kol 1:28; Kum 16:18; 2Nya 17:7; Mal 2:7; Mt 13:52Bahari iliwekwa juu ya mafahali kumi na wawili, watatu wakielekea kaskazini, watatu wakielekea magharibi, watatu wakielekea kusini na watatu wakielekea mashariki. Bahari iliwekwa juu yao na sehemu zao za nyuma zilielekeana. 267:26 Eze 6:11Ilikuwa na unene wa nyanda nne7:26 Nyanda nne ni sawa na sentimita 32. Nyanda moja ni sawa na upana wa kiganja kimoja, ambacho ni sawasawa na sentimita 8. na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 2,000.7:26 Bathi 2,000 ni sawa na lita 40,000.

277:27 Ezr 6:22; 1Nya 29:12; Neh 2:12; 2Kor 8:16; Flp 4:10; Mit 16:7Pia akatengeneza vitako kumi vya shaba vinavyoweza kuhamishika, kila kimoja kilikuwa na urefu wa dhiraa nne, upana dhiraa nne na kimo chake dhiraa tatu7:27 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. 287:28 2Fal 25:28; Ezr 5:5; 9:9; Neh 1:11Hivi ndivyo vile vitako vilivyotengenezwa: Vilikuwa na mbao za pembeni zilizoshikamanishwa na mihimili. 29Juu ya mbao kati ya hiyo mihimili kulikuwa na simba, mafahali na makerubi, pia kwenye mihimili yake. Juu na chini ya simba na mafahali kulikuwa kumesokotewa taji za kufuliwa. 30Kila kitako kilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na vyuma vya katikati vya kuyazungusha hayo magurudumu na kila kimoja kilikuwa na sinia kwenye vishikizo vinne vya taji iliyosubiwa kila upande. 31Ndani ya kitako kulikuwa na nafasi ya wazi iliyokuwa na umbile la mviringo lenye kina cha dhiraa moja.7:31 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. Nafasi hii ya wazi ilikuwa ya mviringo, pamoja na kitako chake ilikuwa dhiraa moja na nusu.7:31 Dhiraa moja na nusu ni sawa na sentimita 67.5. Kuzunguka huo mdomo wake kulitiwa nakshi. Papi za vitako zilikuwa mraba na si za mviringo. 32Magurudumu manne yalikuwa chini ya papi, na vyuma vya katikati vya kuzungushia magurudumu hayo vilikuwa vimeunganishwa kwenye kitako. Kipenyo cha kila gurudumu kilikuwa dhiraa moja na nusu. 33Magurudumu yalitengenezwa kama ya magari ya vita ya kukokotwa, vyuma vya katikati vya magurudumu, duara zake, matindi yake na vikombe vyake vyote vilikuwa vya kusubu.

34Kila kitako kilikuwa na mikono minne, moja kwenye kila pembe, ukitokeza kutoka kwenye kitako. 35Juu ya kitako kulikuwepo na utepe wa mviringo wenye kina cha nusu dhiraa. Vishikio na papi vilishikamana upande wa juu wa kitako. 36Alitia nakshi za makerubi, simba na miti ya mitende juu ya uso wa vishikio na juu ya papi, katika kila nafasi iliyopatikana, pamoja na mataji yaliyosokotwa kuzunguka pande zote. 37Hivi ndivyo Hiramu alivyotengeneza vile vitako kumi. Vyote vilikuwa vya kusubu kwenye kalibu za kufanana kwa vipimo na kwa umbo.

38Kisha akatengeneza masinia kumi ya shaba, kila moja likiwa na ujazo wa bathi arobaini,7:38 Bathi 40 ni sawa na lita 800. yakiwa na kipenyo cha dhiraa nne7:38 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. kila sinia moja kwa kila kimoja ya vile vitako kumi. 39Aliweka vitako vitano upande wa kusini wa Hekalu na vingine vitano upande wa kaskazini. Akaweka ile bahari upande wa kusini, katika pembe ya kusini ya Hekalu. 40Pia akatengeneza masinia, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi zote katika Hekalu la Bwana kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:

41nguzo mbili;

mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;

nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;

42makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);

43vitako kumi pamoja na masinia yake kumi;

44ile Bahari ya chuma na yale mafahali kumi na wawili chini yake;

45masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Vyombo hivi vyote ambavyo Huramu alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyongʼarishwa. 46Mfalme akaamuru wavisubu katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani ulio kati ya Sukothi na Sarethani. 47Solomoni akaviacha vitu hivi vyote bila kupima uzani wake, kwa sababu vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.

48Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana:

madhabahu ya dhahabu;

meza ya dhahabu za kuweka mikate ya Wonyesho;

49vinara vya taa vya dhahabu safi (vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto, mbele ya Patakatifu pa Patakatifu);

kazi ya maua ya dhahabu na taa na makoleo;

50masinia ya dhahabu safi, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, vyano na vyetezo;

na bawaba za dhahabu kwa ajili ya milango ya chumba cha ndani sana, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na pia kwa ajili ya milango ya ukumbi mkuu wa Hekalu.

51Hivyo Mfalme Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Bwana.

Thai New Contemporary Bible

1พงศ์กษัตริย์ 7:1-51

โซโลมอนทรงสร้างพระราชวัง

1แต่กษัตริย์โซโลมอนทรงใช้เวลาก่อสร้างพระราชวังของพระองค์ทั้งสิ้นสิบสามปี 2พระองค์ทรงสร้างพระตำหนักพนาเลบานอนยาว 100 ศอก7:2 คือ ประมาณ 46 เมตร กว้าง 50 ศอก7:2 คือ ประมาณ 23 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 6 สูง 30 ศอก7:2 คือ ประมาณ 13.5 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 6 และ 23 ใช้เสาไม้สนซีดาร์สี่แถวรองรับคานไม้สนซีดาร์ไว้ 3ทำหลังคาด้วยคานไม้สนซีดาร์ 45 อัน ซึ่งวางอยู่บนเสา โดยแบ่งวางเป็นแถว แถวละ 15 อัน 4มีหน้าต่างอยู่ด้านบนเรียงเป็นชุด ชุดละสามช่อง แต่ละชุดหันหน้าเข้าหากัน 5ประตูทุกบานเป็นกรอบทรงสี่เหลี่ยมผืนผ้า อยู่ด้านหน้าห้องโถงมีสามชุด ชุดละสามบานหันหน้าเข้าหากัน

6พระองค์ทรงสร้างระเบียงเสาหานยาว 50 ศอกและกว้าง 30 ศอก มีมุขด้านหน้าซึ่งมีเสาหานและหลังคาด้วย

7ทรงสร้างห้องบัลลังก์หรือท้องพระโรงวินิจฉัยเป็นที่ประทับตัดสินความ กรุด้วยไม้สนซีดาร์ตั้งแต่พื้นจนถึงเพดาน 8ถัดจากท้องพระโรงวินิจฉัยไปด้านหลัง พระองค์ทรงสร้างวังที่ประทับส่วนพระองค์และวังของมเหสีซึ่งเป็นธิดาของฟาโรห์ตามแบบท้องพระโรงวินิจฉัย

9ตัวอาคารเหล่านี้ทั้งหมดจากด้านนอกถึงลานใหญ่ และจากฐานรากถึงชายคาสร้างด้วยหินอย่างดี ซึ่งวัดให้ได้ขนาดก่อนที่จะสกัด และใช้เลื่อยแต่งทั้งด้านในและด้านนอก 10ฐานรากเป็นหินก้อนใหญ่คุณภาพดี มีขนาดหน้าตัด 8 ศอก7:10 คือ ประมาณ 3.6 เมตรบ้าง และ 10 ศอก7:10 คือ ประมาณ 4.5 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 23บ้าง 11บนชั้นฐานรากวางด้วยหินอย่างดี ตัดให้ได้ขนาด และสลับด้วยคานไม้สนซีดาร์ 12ทรงสร้างผนังล้อมรอบลานใหญ่จากหินที่ตัดแต่งไว้แล้วสามชั้น สลับด้วยชั้นคานไม้สนซีดาร์ ตามแบบลานชั้นในและมุขหน้าของพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า

การตกแต่งพระวิหาร

(2พศด.4:2-6,10—5:1)

13กษัตริย์โซโลมอนทรงให้นำชายคนหนึ่งชื่อหุราม7:13 หรือฮีรามมาจากเมืองไทระ 14มารดาของเขาเป็นหญิงม่ายจากเผ่านัฟทาลี ส่วนบิดาเป็นชาวเมืองไทระและเป็นช่างทองสัมฤทธิ์ หุรามเชี่ยวชาญและมีฝีมือในงานทองสัมฤทธิ์ทุกชนิด เขามาเข้าเฝ้าโซโลมอนและทำงานทุกอย่างที่ได้รับมอบหมาย

15หุรามหล่อเสาหานทองสัมฤทธิ์สองต้น แต่ละต้นสูง 18 ศอก7:15 คือ ประมาณ 8.1 เมตร เส้นรอบวง 12 ศอก7:15 คือ ประมาณ 5.4 เมตร 16เขาหล่อหัวเสาทองสัมฤทธิ์สูง 5 ศอก7:16 คือ ประมาณ 2.3 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 23 เพื่อติดบนยอดเสาหาน 17มีตาข่ายโซ่ระย้าประดับหัวเสา เสาละเจ็ดสาย 18เขาทำผลทับทิมสองแถว ติดรอบโซ่ระย้าประดับหัวเสาทั้งสองต้น 19ส่วนหัวเสาหานที่มุขหน้าตกแต่งเป็นรูปดอกลิลลี่สูง 4 ศอก7:19 คือ ประมาณ 1.8 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 27 และ 38 20บนหัวเสาทั้งสองต้น เหนือบัวคว่ำ ถัดจากสร้อยระย้าขึ้นไปเป็นแถวผลทับทิมสองร้อยผลโดยรอบ 21เขาตั้งเสาหานทั้งสองไว้ที่มุขหน้าของพระวิหาร เสาทางใต้ตั้งชื่อว่ายาคีน7:21 คงจะมีความหมายว่าพระองค์ทรงสถาปนาไว้ เสาทางเหนือตั้งชื่อว่าโบอาส7:21 คงจะมีความหมายว่าในพระองค์คือกำลัง 22หัวเสามีรูปทรงเป็นดอกลิลลี่ เป็นอันว่างานเสาหานก็เสร็จเรียบร้อย

23หุรามหล่อขันสาครทรงกลมด้วยโลหะสูง 5 ศอก เส้นผ่าศูนย์กลาง 10 ศอกและเส้นรอบวง 30 ศอก 24ใต้ขอบขันด้านนอกตกแต่งเป็นลายเครือเถาสองแถว ศอกละสิบรูป7:24 คือ สิบรูปทุกๆ 45 เซนติเมตร หล่อเป็นเนื้อเดียวกันกับขันสาคร

25ขันสาครนี้ตั้งอยู่บนวัวทองสัมฤทธิ์สิบสองตัว หันหลังเข้าหากันตรงกลาง หันหน้าไปทางทิศเหนือ ใต้ ตะวันออก และตะวันตก ทิศละสามตัว 26ขันสาครหนาหนึ่งฝ่ามือ7:26 คือ ประมาณ 8 เซนติเมตร ปากขันเหมือนขอบถ้วยซึ่งเหมือนกับดอกลิลลี่บาน จุน้ำได้ประมาณ 44 กิโลลิตร7:26 ภาษาฮีบรูว่า2,000 บัท

27หุรามยังทำแท่นเคลื่อนที่ด้วยทองสัมฤทธิ์สิบแท่น แต่ละแท่นกว้างยาว 4 ศอก สูง 3 ศอก7:27 คือ ประมาณ 1.3 เมตร 28แท่นเหล่านี้สร้างขึ้นในลักษณะนี้คือ มีผนังที่ยึดติดอยู่กับกรอบในแนวตั้ง 29เขาสลักรูปสิงโต วัว และเครูบไว้บนกรอบและบนผนังนั้น ด้านบนและล่างของสิงโตและวัวเป็นลวดลายพวงมาลาที่สลักลายด้วยค้อน 30แต่ละแท่นมีล้อทองสัมฤทธิ์สี่ล้อและเพลาทองสัมฤทธิ์ แต่ละแท่นรองรับอ่างซึ่งตั้งอยู่บนที่หนุนทั้งสี่ ซึ่งหล่อขึ้นโดยมีพวงมาลาประดับแต่ละด้าน 31ภายในแท่นนี้มีช่องเปิดเป็นรูปทรงกลมลึก 1 ศอก7:31 คือ ประมาณ 0.5 เมตร วัดรอบช่องเปิดทรงกลมรวมฐานได้ 1 ศอกครึ่ง7:31 คือ ประมาณ 0.7 เมตร เช่นเดียวกับข้อ 32 มีลายสลักรอบช่องเปิด ผนังของแท่นตั้งเป็นทรงสี่เหลี่ยมจัตุรัส ไม่ใช่วงกลม 32ล้อทั้งสี่อยู่ใต้ผนัง และเพลาล้อติดเข้ากับตัวแท่น เส้นผ่าศูนย์กลางของล้อ 1 ศอกครึ่ง 33ล้อทำขึ้นคล้ายกับล้อรถรบ ทั้งเพลา ซี่ล้อ ขอบและดุมล้อล้วนหล่อขึ้นจากโลหะ

34แต่ละแท่นมีที่จับที่มุมทั้งสี่ มุมละอัน ยื่นออกมาจากแท่น 35ที่ด้านบนของแท่นมีปลอกทรงกลมลึกครึ่งศอก7:35 คือ ประมาณ 0.2 เมตร ทั้งที่หนุนกับผนังยึดติดเข้ากับด้านบนของแท่น 36เขาสลักรูปเครูบ สิงโต ต้นอินทผลัม บนพื้นผิวของที่หนุนและบนผนังตลอดจนที่ว่างทุกแห่ง และมีพวงมาลาอยู่โดยรอบ 37แท่นทั้งสิบสร้างขึ้นตามนี้ โดยมีขนาดและรูปทรงเดียวกัน หล่อจากพิมพ์เดียวกัน

38จากนั้นเขาทำอ่างทองสัมฤทธิ์สิบใบ เส้นผ่าศูนย์กลาง 4 ศอก ตั้งไว้บนแท่น แท่นละใบ แต่ละใบจุน้ำได้ประมาณ 880 ลิตร7:38 ภาษาฮีบรูว่า40 บัท 39เขาตั้งแท่นเหล่านี้ไว้ที่ด้านใต้ของพระวิหารห้าแท่นและด้านเหนือห้าแท่น ส่วนขันสาครนั้นอยู่ทางด้านใต้ที่มุมด้านตะวันออกเฉียงใต้ของพระวิหาร 40เขายังได้ทำชาม อ่าง ทัพพี และชามประพรมด้วย

ในที่สุดหุรามจึงทำงานทั้งหมดที่กษัตริย์โซโลมอนทรงมอบหมายในพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้าสำเร็จครบถ้วน ได้แก่

41เสาหานสองต้น

หัวเสารูปบัวคว่ำสองหัว

ตาข่ายประดับหัวเสาสองชุด

42ทับทิมสี่ร้อยผล สำหรับตาข่ายสองชุด (ตาข่ายแต่ละชุดมีทับทิมสองแถว ประดับอยู่บนหัวเสารูปบัวคว่ำ)

43แท่นทองสัมฤทธิ์สิบแท่นพร้อมอ่าง

44ขันสาคร และวัวสิบสองตัวซึ่งรองรับขัน

45หม้อ ทัพพี และชามประพรม

หุรามได้ทำสิ่งเหล่านี้ถวายกษัตริย์โซโลมอนสำหรับพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า โดยใช้ทองสัมฤทธิ์ขัดเงา 46กษัตริย์ทรงให้หล่อสิ่งเหล่านี้ขึ้นด้วยเบ้าดินเหนียวในที่ราบแห่งแม่น้ำจอร์แดน ระหว่างเมืองสุคคทและเมืองศาเรธาน 47กษัตริย์โซโลมอนไม่ได้ให้ชั่งน้ำหนักสิ่งเหล่านี้เพราะว่ามีจำนวนมากมาย จึงไม่ทราบน้ำหนักที่แน่นอนของทองสัมฤทธิ์

48โซโลมอนยังได้ทรงทำเครื่องใช้ทั้งปวงที่อยู่ในพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า ได้แก่

แท่นบูชาทองคำ

โต๊ะทองคำสำหรับวางขนมปังเบื้องพระพักตร์

49คันประทีปทองคำบริสุทธิ์ (วางไว้ด้านหน้าอภิสุทธิสถาน ทั้งด้านซ้ายและขวา ด้านละห้าคัน) ลวดลายดอกไม้

ตะเกียงและคีมทำด้วยทองคำ

50ขันทองคำบริสุทธิ์ กรรไกรตัดไส้ตะเกียง อ่างประพรม จานชาม และกระถางไฟ

เบ้าทองคำของประตูห้องชั้นในสุดคือประตูอภิสุทธิสถาน และของประตูห้องโถงกลางของพระวิหาร

51เมื่องานทั้งปวงสำหรับพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้าเสร็จเรียบร้อยแล้ว โซโลมอนทรงนำเงิน ทอง และเครื่องใช้ไม้สอยต่างๆ ซึ่งดาวิดราชบิดา ถวายไว้เพื่อการนี้มาเก็บไว้ในคลังพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า