1 Wafalme 7 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 7:1-51

Solomoni Ajenga Jumba Lake La Kifalme

17:1 Ezr 4:7; Neh 2:1; 1Nya 6:14Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme. 27:2 1Fal 2:35; Neh 11:11Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100,7:2 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini,7:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi zilizorembwa. 3Ilipauliwa kwa mierezi juu ya boriti zile zilizolala juu ya nguzo arobaini na tano, kumi na tano kwa kila safu. 4Madirisha yake yaliwekwa juu kwa safu tatu, yakielekeana. 5Milango yote ilikuwa na miimo ya mstatili, ilikuwa upande wa mbele katika safu tatu, ikielekeana.

67:6 Neh 12:36; Ezr 5:5; Isa 41:20; Mwa 32:28; Neh 1:10-11Akajenga ukumbi wa nguzo, ambao urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini7:6 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na upana wake dhiraa thelathini. Mbele ya jengo hilo kulikuwepo baraza. Mbele ya baraza kulikuwepo na nguzo na paa lililoningʼinia.

77:7 Ezr 8:1; 2:43Akajenga ukumbi wa kiti cha enzi, Ukumbi wa Hukumu, mahali ambapo angelitolea hukumu, akaufunika kwa mierezi kutoka sakafuni hadi darini. 8Kwenye jumba la kifalme ambamo angeliishi, aliiweka nyuma zaidi, ikiwa na mjengo wa aina moja na hiyo nyingine. Pia Solomoni akajenga jumba la kifalme linalofanana na huo ukumbi mkubwa kwa ajili ya binti Farao, aliyekuwa amemwoa.

97:9 Neh 2:8Ujenzi huu wote, kuanzia nje mpaka kwenye ua mkuu na kuanzia kwenye msingi hadi upenuni, ulifanywa kwa mawe ya ubora wa hali ya juu yaliyokuwa yamechongwa kwa vipimo na kusawazishwa kwa msumeno nyuso zake za ndani na za nje. 107:10 Kum 33:10; Neh 8:1-8; 2Tim 4:2; 1Sam 7:3; 2Nya 12:14; Za 10:18; 119:45; Mal 2:7Misingi iliwekwa kwa mawe makubwa yaliyo bora, yenye urefu wa dhiraa kumi7:10 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na mengine yenye urefu wa dhiraa nane7:10 Dhiraa nane ni sawa na mita 3.6. 11Sehemu za juu kulikuwepo na mawe yenye ubora wa hali ya juu, yaliyokatwa kwa vipimo na boriti za mierezi. 127:12 Dan 2:37; Ezr 4:10Ule ua mkuu ulizungukwa na ukuta wa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa, kama ulivyokuwa ua wa ndani wa Hekalu la Bwana na baraza yake.

Samani Za Hekalu

(2 Nyakati 4)

13Mfalme Solomoni akatuma watu Tiro kumleta Hiramu, 147:14 Es 1:14ambaye mama yake alikuwa mjane kutoka kabila la Naftali na baba yake alikuwa mtu wa Tiro tena fundi wa shaba. Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu na mzoefu katika aina zote za kazi ya shaba. Alikuja kwa Mfalme Solomoni na kufanya kazi zake zote alizopangiwa.

157:15 Kum 12:5; 1Nya 29:6; 2Nya 6:2; Za 135:21Hiramu akasubu nguzo mbili za shaba, kila moja ikiwa na urefu wa dhiraa kumi na nane,7:15 Dhiraa 18 ni sawa na mita 8.1. kila nguzo ikiwa na mzingo wa dhiraa kumi na mbili7:15 Dhiraa 12 ni sawa na mita 5.4. kwa mstari. 167:16 Kut 3:22; Ezr 8:25; Zek 6:10; 1Nya 29:6Pia alitengeneza mataji mawili ya shaba ya kusubu ili kuyaweka juu ya hizo nguzo; kila taji lilikuwa na kimo cha dhiraa tano7:16 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. kwenda juu. 177:17 2Fal 3:5; Hes 15:5-12Wavu wa mikufu iliyosokotewa kwenye zile taji juu ya zile nguzo, saba kwa kila taji. 18Akatengeneza makomamanga katika safu mbili kuzunguka kila wavu kuremba mataji yaliyo juu ya nguzo. Alifanya hivyo kwa kila nguzo. 197:19 Ezr 5:14; Yer 27:22Mataji yaliyokuwa juu ya nguzo kwenye baraza, yalikuwa katika umbo la yungiyungi, kimo chake ni dhiraa nne7:19 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 207:20 Ezr 6:4; 1Kor 4:1-2Juu ya mataji ya zile nguzo mbili, juu ya ile sehemu yenye umbo kama bakuli, karibu na ule wavu, kulikuwa na yale makomamanga 200 katika safu kuzunguka pande zote. 217:21 Ezr 4:16-20; 5:3-6Hiramu akasimamisha nguzo kwenye baraza ya Hekalu. Nguzo ya upande wa kusini akaiita Yakini,7:21 Yakini maana yake Mungu atafanya imara. na ile ya upande wa kaskazini Boazi.7:21 Boazi maana yake Ndani ya Mungu kuna nguvu. 22Mataji yaliyokuwa juu yalikuwa na umbo la yungiyungi. Hivyo kazi ya nguzo ikakamilika.

237:23 Ezr 6:10; Isa 60:12; Yer 12:14; Za 68:29; 1Tim 2:1-2Hiramu akasubu Bahari ya chuma, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Mzunguko wake ulikuwa dhiraa thelathini. 247:24 Ezr 4:13; 8:36Chini ya ukingo, ilizungukwa na maboga, kumi kwenye kila dhiraa moja. Maboga yalikuwa yamesubiwa katika safu mbili ili kuwa kitu kimoja na hiyo bahari.

257:25 Kut 18:21-26; 16:18; Za 19:7; Kol 1:28; Kum 16:18; 2Nya 17:7; Mal 2:7; Mt 13:52Bahari iliwekwa juu ya mafahali kumi na wawili, watatu wakielekea kaskazini, watatu wakielekea magharibi, watatu wakielekea kusini na watatu wakielekea mashariki. Bahari iliwekwa juu yao na sehemu zao za nyuma zilielekeana. 267:26 Eze 6:11Ilikuwa na unene wa nyanda nne7:26 Nyanda nne ni sawa na sentimita 32. Nyanda moja ni sawa na upana wa kiganja kimoja, ambacho ni sawasawa na sentimita 8. na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 2,000.7:26 Bathi 2,000 ni sawa na lita 40,000.

277:27 Ezr 6:22; 1Nya 29:12; Neh 2:12; 2Kor 8:16; Flp 4:10; Mit 16:7Pia akatengeneza vitako kumi vya shaba vinavyoweza kuhamishika, kila kimoja kilikuwa na urefu wa dhiraa nne, upana dhiraa nne na kimo chake dhiraa tatu7:27 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. 287:28 2Fal 25:28; Ezr 5:5; 9:9; Neh 1:11Hivi ndivyo vile vitako vilivyotengenezwa: Vilikuwa na mbao za pembeni zilizoshikamanishwa na mihimili. 29Juu ya mbao kati ya hiyo mihimili kulikuwa na simba, mafahali na makerubi, pia kwenye mihimili yake. Juu na chini ya simba na mafahali kulikuwa kumesokotewa taji za kufuliwa. 30Kila kitako kilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na vyuma vya katikati vya kuyazungusha hayo magurudumu na kila kimoja kilikuwa na sinia kwenye vishikizo vinne vya taji iliyosubiwa kila upande. 31Ndani ya kitako kulikuwa na nafasi ya wazi iliyokuwa na umbile la mviringo lenye kina cha dhiraa moja.7:31 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. Nafasi hii ya wazi ilikuwa ya mviringo, pamoja na kitako chake ilikuwa dhiraa moja na nusu.7:31 Dhiraa moja na nusu ni sawa na sentimita 67.5. Kuzunguka huo mdomo wake kulitiwa nakshi. Papi za vitako zilikuwa mraba na si za mviringo. 32Magurudumu manne yalikuwa chini ya papi, na vyuma vya katikati vya kuzungushia magurudumu hayo vilikuwa vimeunganishwa kwenye kitako. Kipenyo cha kila gurudumu kilikuwa dhiraa moja na nusu. 33Magurudumu yalitengenezwa kama ya magari ya vita ya kukokotwa, vyuma vya katikati vya magurudumu, duara zake, matindi yake na vikombe vyake vyote vilikuwa vya kusubu.

34Kila kitako kilikuwa na mikono minne, moja kwenye kila pembe, ukitokeza kutoka kwenye kitako. 35Juu ya kitako kulikuwepo na utepe wa mviringo wenye kina cha nusu dhiraa. Vishikio na papi vilishikamana upande wa juu wa kitako. 36Alitia nakshi za makerubi, simba na miti ya mitende juu ya uso wa vishikio na juu ya papi, katika kila nafasi iliyopatikana, pamoja na mataji yaliyosokotwa kuzunguka pande zote. 37Hivi ndivyo Hiramu alivyotengeneza vile vitako kumi. Vyote vilikuwa vya kusubu kwenye kalibu za kufanana kwa vipimo na kwa umbo.

38Kisha akatengeneza masinia kumi ya shaba, kila moja likiwa na ujazo wa bathi arobaini,7:38 Bathi 40 ni sawa na lita 800. yakiwa na kipenyo cha dhiraa nne7:38 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. kila sinia moja kwa kila kimoja ya vile vitako kumi. 39Aliweka vitako vitano upande wa kusini wa Hekalu na vingine vitano upande wa kaskazini. Akaweka ile bahari upande wa kusini, katika pembe ya kusini ya Hekalu. 40Pia akatengeneza masinia, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi zote katika Hekalu la Bwana kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:

41nguzo mbili;

mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;

nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;

42makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);

43vitako kumi pamoja na masinia yake kumi;

44ile Bahari ya chuma na yale mafahali kumi na wawili chini yake;

45masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Vyombo hivi vyote ambavyo Huramu alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyongʼarishwa. 46Mfalme akaamuru wavisubu katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani ulio kati ya Sukothi na Sarethani. 47Solomoni akaviacha vitu hivi vyote bila kupima uzani wake, kwa sababu vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.

48Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana:

madhabahu ya dhahabu;

meza ya dhahabu za kuweka mikate ya Wonyesho;

49vinara vya taa vya dhahabu safi (vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto, mbele ya Patakatifu pa Patakatifu);

kazi ya maua ya dhahabu na taa na makoleo;

50masinia ya dhahabu safi, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, vyano na vyetezo;

na bawaba za dhahabu kwa ajili ya milango ya chumba cha ndani sana, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na pia kwa ajili ya milango ya ukumbi mkuu wa Hekalu.

51Hivyo Mfalme Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Bwana.

Swedish Contemporary Bible

1 Kungaboken 7:1-51

Salomo bygger sitt palats

1Sedan byggde Salomo sitt eget hus som det däremot tog tretton år att få färdigt.

2Han byggde Libanonskogshuset som var 50 meter långt, 25 meter brett och 15 meter högt, med fyra rader av cederpelare och med huggna cederbjälkar på pelarna. 3Taket var av cederträ över bjälkarna som låg på pelarna, 45 bjälkar, 15 i varje rad. 4Fönstren var placerade mitt emot varandra i rader om tre. 5Alla dörröppningar var fyrkantiga och i den främre delen fanns tre dörrar i varje grupp mitt emot varandra.7:5 Grundtextens innebörd i denna vers är osäker.

6Han gjorde också en pelarhall. Den var 25 meter lång och 15 meter bred och hade ett förrum med en baldakin som hölls upp av pelare.

7Han byggde också tronrummet eller domsalen där Salomo satt när han dömde folket. Det hade panel av cederträ från golv till tak.

8Rummen som han själv skulle bo i längre in i byggnaden var av liknande utseende. Han byggde också ett hus i samma stil åt faraos dotter som var en av hans hustrur. 9Alla dessa byggnader, från grunden till utsidan av den stora förgården, uppfördes av stora stenblock av dyrbar sten som huggits ut efter mått både på insidan och utsidan. 10Grundstenarna var utvalda stora stenar 4 till 5 meter långa. 11Ovanpå dem låg också utvalda stenar uthuggna efter mått och cederträ. 12Den stora förgårdsmuren var gjord av tre varv uthuggna stenar och ett varv cederbjälkar på samma sätt som vid den inre förgården till Herrens hus.

Templets utrustning

13Salomo lät sända bud efter Hiram från Tyros, 14son till en änka av Naftalis stam och hans far var en kopparsmed från Tyros. Hiram var en skicklig och begåvad konstnär och kunde göra alla slags koppararbeten. Han kom nu för att utföra alla kung Salomos arbeten.

15Hiram tillverkade två pelare av koppar, var och en 9 meter hög och med en omkrets av 6 meter. 16På toppen av varje pelare gjorde han ett kapitäl av gjuten koppar, 2,5 meter högt. 17Varje kapitäl var dekorerat med flätverk med sju kedjor i form av hängprydnader 18och han gjorde granatäpplen i två rader runt varje flätverk, likadant på båda kapitälen. 19Kapitälen på pelartopparna vid förhuset var liljeformade och 2 meter höga.7:19 Den senare delen av versen är mycket svårförståelig och översättningen därför osäker. 20På båda pelarhuvudena ovanför den skålformade delen nära flätverket var 200 granatäpplen i rader som omgav vart och ett av dem.7:20 Innebörden i versens första del är högst osäker och därmed också översättningen av versen i sin helhet. 21Hiram placerade dessa pelare vid templets ingång. Den till höger kallades Jakin7:21 Betyder troligen: han befäster och den till vänster Boas7:21 Betyder troligen: i honom finns styrka.. 22Pelarhuvudena var liljeformade. Så blev arbetet med pelarna fullbordat.

23Han gjorde Havet av gjutgods, runt, 5 meter i diameter och hälften så högt, med en omkrets på 15 meter. 24Runt dess kant fanns två rader av kurbitsdekorationer, tio stycken per varje halvmeter, gjutna i samma stycke som själva Havet. 25Havet stod på tolv oxar. Tre av dem var vända mot norr, tre mot väster, tre mot söder och tre mot öster. Havet vilade på dem, och deras bakdelar var vända inåt. 26Havet var en handsbredd tjockt och kanten var formad som i en skål, så att den liknade en utslagen lilja. Det rymde 60 000 liter7:26 På hebreiska 2 000 bat. 1 bat var lika med 1 efa, mellan 20 och 40 liter. Här är beräkningen gjord utifrån 30 liter..

27Därefter gjorde han tio flyttbara ställ. De var 2 meter långa, 2 meter breda och 1,5 meter höga. 28De var tillverkade på följande sätt: De hade sidoplåtar som var fästa mellan hörnlisterna. 29Sidoplåtarna var dekorerade med lejon, oxar och keruber, liksom hörnlisterna. Under och över lejonen och oxarna fanns hamrade blomsterkransar. 30Vart och ett av dessa ställ hade fyra hjul av koppar med axlar av koppar. Vart och ett av dem vilade på fyra gjutna stöd under fatet med blomsterkransar på varje sida. 31På insidan av stället fanns en öppning, en halv meter hög. Dess mitt var rund, 75 centimeter djup, och runt öppningen var utsirade blomsterkransar. Listerna var fyrkantiga, inte runda. 32Ställen hade fyra hjul som satt under sidoplåtarna på hjulaxlar fästade i ställets hörn. Hjulen var 75 centimeter höga 33och gjorda som vagnshjul, i alla delar gjutna i brons, axlar, ekrar, hjulringar och hjulnav. 34I vart och ett av de fyra hörnen fanns ett handtag, gjort i ett stycke med stället i övrigt. 35Överst på varje ställ fanns en rund kant, 25 centimeter hög och hållare med sina lister. 36Keruber, lejon och palmer omgivna av blomsterkransar var ingraverade på hållarnas ytor där det fanns utrymme. 37Alla tio ställen var gjutna exakt lika i samma storlek och form.

38Till detta gjorde han tio fat av koppar. Varje fat var 2 meter i diameter och rymde 1 200 liter7:38 På hebreiska 40 bat. Se not till 7:26. vatten. Han satte ett fat på vart och ett av de tio ställen. 39Fem av ställen placerade han i rummets södra del och fem i den norra. Havet ställde han i det hörn av templet som låg mot sydost. 40Hiram gjorde också grytorna, skovlarna och offerskålarna. Han fullbordade allt det arbete som han fått i uppdrag att göra åt kung Salomo i Herrens hus:

41De två pelarna,

de skålliknande pelarhuvudena,

de två flätverken som dekorationer på pelarhuvudena,

42400 granatäpplen till de båda flätverken, två rader granatäpplen för varje flätverk, som dekorerade de skålformade pelarhuvudena,

43de tio ställen med tio fat,

44Havet och de tolv oxarna under det,

45grytorna, skovlarna och skålarna med alla tillhörande föremål.

Mäster Hiram tillverkade alla föremålen åt kung Salomo till Herrens hus i polerad koppar. 46Kungen lät gjuta dem i lerformar på Jordanslätten mellan Suckot och Saretan. 47Salomo gjorde så mycket av alla dessa ting att vikten av koppar inte kunde fastställas.

48Salomo gjorde alla föremålen i Herrens hus:

det gyllene altaret,

det gyllene bordet för skådebröden,

49lampställen av rent guld, fem på högra sidan och fem på vänstra framför det inre rummet, blomsterdekorationerna, lamporna och tängerna, allt av guld,

50faten, knivarna, skålarna, pannorna och fyrfaten av rent guld,

gångjärnen till dörrarna in till det allra heligaste och till templets huvudingång. Allt detta gjordes alltså av guld.

51När allt arbete Salomo gjorde för Herrens hus var klart, förde han in det som blivit helgat åt Herren av hans far David: silvret och guldet och alla kärlen och lade dem i skattkammaren i Herrens hus.