1 Wafalme 16 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 16:1-34

116:1 1Fal 16:7; 2Nya 19:2Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema: 216:2 1Fal 14:7-9“Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao. 316:3 1Fal 16:11; 21:22Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati. 416:4 1Fal 14:11Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”

5Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 6Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.

716:7 1Fal 16:11Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.

Ela Mfalme Wa Israeli

8Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.

916:9 1Fal 20:12; Mit 31:4-5Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa. 1016:10 2Fal 9:31Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.

11Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki. 12Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu: 1316:13 Kum 32:21kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.

14Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

Zimri Mfalme Wa Israeli

1516:15 Yos 19:44Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti. 16Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini. 17Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa. 18Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa, 19kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.

20Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

Omri Mfalme Wa Israeli

21Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri. 22Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.

2316:23 Yos 12:24Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa. 2416:24 1Fal 13:32; Mt 10:5Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili16:24 Talanta mbili za fedha ni sawa na kilo 70. za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.

2516:25 Kum 4:25; Mik 6:16Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia. 2616:26 Kum 32:21Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.

27Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 2816:28 1Fal 13:32Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.

Ahabu Afanywa Mfalme Wa Israeli

29Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili. 3016:30 1Fal 14:9Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia. 3116:31 1Fal 11:2; 2Fal 9:34; Amu 3:6Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu. 3216:32 Amu 6:28; Yer 43:12Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria. 3316:33 Amu 3:7; 2Fal 13:6Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.

3416:34 Yos 6:26Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

New International Reader’s Version

1 Kings 16:1-34

1The Lord’s message about Baasha came to Jehu, the son of Hanani. Here is what the Lord said about Baasha. 2“I lifted you up from the dust. I appointed you king over my people Israel. But you lived the way Jeroboam had lived. You also caused my people Israel to sin. And their sins made me very angry. 3So I am about to destroy you, Baasha, and your royal house. I will make your house like the royal house of Jeroboam, the son of Nebat. 4Some of the people who belong to you will die in the city. Dogs will eat them up. Others will die in the country. The birds will eat them.”

5The other events of Baasha’s rule are written down. What he did and what he accomplished are written in the official records of the kings of Israel. 6Baasha joined the members of his family who had already died. He was buried in Tirzah. Baasha’s son Elah became the next king after him.

7The Lord’s message came through the prophet Jehu, the son of Hanani. It was against Baasha and his royal house. Baasha had done all kinds of evil things in the sight of the Lord. Baasha had also destroyed the royal house of Jeroboam. What Baasha did had made the Lord very angry. So Baasha had become as sinful as the royal house of Jeroboam had been.

Elah King of Israel

8Elah became king of Israel. It was in the 26th year that Asa was king of Judah. Elah ruled in Tirzah for two years. He was the son of Baasha.

9Zimri was one of Elah’s officials. He commanded half of Elah’s chariot drivers. He made plans against Elah. Elah was in Tirzah at the time. He was getting drunk in the home of Arza. Arza was in charge of the palace at Tirzah. 10Zimri came in. He struck Elah down and killed him. It was in the 27th year of Asa, the king of Judah. Zimri became the next king after Elah.

11As soon as Zimri was seated on the throne as king, he killed off Baasha’s whole family. He didn’t even spare one male. It didn’t matter whether it was a relative or a friend. 12So Zimri destroyed the whole family of Baasha. That’s what the Lord had said would happen. He had spoken against Baasha through Jehu the prophet. 13Baasha and his son Elah had committed all kinds of sin. They had also caused Israel to commit the same sins. So Israel made the Lord very angry. They did it by worshiping worthless statues of gods. The Lord is the God of Israel.

14The other events of Elah’s rule are written down. Everything he did is written in the official records of the kings of Israel.

Zimri King of Israel

15Zimri ruled in Tirzah for seven days. It was in the 27th year that Asa was king of Judah. The army of Israel had set up camp near Gibbethon. It was a Philistine town. 16The Israelites in the camp heard that Zimri had made plans against King Elah. They also heard that Zimri had murdered him. So they announced that Omri was king over Israel. He was the commander of the army. They made him king that day in the camp. 17Then Omri and all his men pulled back from Gibbethon. They marched to Tirzah and surrounded it. They attacked it and captured it. 18Zimri saw that they had taken over the city. So he went into the safest place in the royal palace. He set the palace on fire all around him. He died there 19because of the sins he had committed. He had done what was evil in the sight of the Lord. He had lived the way Jeroboam had lived. He had committed the same sin Jeroboam had caused Israel to commit.

20The other events of Zimri’s rule are written down. The way he turned against King Elah and killed him is written down. All these things are written in the official records of the kings of Israel.

Omri King of Israel

21The Israelites divided up into two groups. Half of them wanted Tibni to be king. He was the son of Ginath. The other half wanted Omri. 22But Omri’s followers were stronger than those of Tibni, the son of Ginath. So Tibni died. And Omri began to rule.

23Omri became king of Israel. It was in the 31st year that Asa was king of Judah. Omri ruled for 12 years. He ruled in Tirzah for six of those years. 24He bought the hill of Samaria from Shemer. He weighed out 150 pounds of silver for it. Then he built a city on the hill. He called it Samaria. He named it after Shemer. Shemer had owned the hill before him.

25But Omri did what was evil in the sight of the Lord. He sinned more than all the kings who had ruled before him. 26He lived the way Jeroboam, the son of Nebat, had lived. He committed the same sin Jeroboam had caused Israel to commit. Israel made the Lord very angry. They did it by worshiping worthless statues of gods. The Lord is the God of Israel.

27The other events of Omri’s rule are written down. Everything he did and the things he accomplished are written in the official records of the kings of Israel. 28Omri joined the members of his family who had already died. He was buried in Samaria. Omri’s son Ahab became the next king after him.

Ahab King of Israel

29Ahab became king of Israel. It was in the 38th year that Asa was king of Judah. Ahab ruled over Israel in Samaria for 22 years. He was the son of Omri. 30Ahab, the son of Omri, did what was evil in the sight of the Lord. He did more evil things than any of the kings who had ruled before him. 31He thought it was only a small thing to commit the sins Jeroboam, the son of Nebat, had committed. Ahab also married Jezebel. She was Ethbaal’s daughter. Ethbaal was king of the people of Sidon. Ahab began to serve the god named Baal and worship him. 32He set up an altar to honor Baal. He set it up in the temple of Baal that he built in Samaria. 33Ahab also made a pole used to worship the female god named Asherah. He made the Lord very angry. Ahab did more to make him angry than all the kings of Israel had done before him. The Lord is the God of Israel.

34In Ahab’s time, Hiel from Bethel rebuilt Jericho. When he laid its foundations, it cost him the life of his oldest son Abiram. When he set up its gates, it cost him the life of his youngest son Segub. That’s what the Lord had said would happen. He had spoken it through Joshua, the son of Nun.