1 Wafalme 10 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 10:1-29

Malkia Wa Sheba Amtembelea Solomoni

(2 Nyakati 9:1-12)

110:1 2Nya 20:9; Dan 9:20Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu. 210:2 Ezr 9:2; Kut 34:13; Neh 13:27; Kum 30:8-10Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. 310:3 2Fal 11:17; 2Nya 34:31; Kut 34:16; Kum 7:2-3; Ezr 9:4; Za 119:53, 120; Isa 66:2Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea. 410:4 1Nya 28:10; Isa 35:3-4Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga, 510:5 Neh 5:12; 13:25chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.

610:6 Kum 9:18; Yn 3:7; Za 102:4Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli. 7Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia. 810:8 Law 27:28; Yos 6:19Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako! 910:9 1Sam 12:18; Ezr 1:5Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”

10Naye akampa mfalme talanta 12010:10 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 4.5. za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.

1110:11 Kum 24:1; Mit 28:13; Mal 2:10-16; Yer 3:13; Isa 1:16-17; Rum 12:2(Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani. 1210:12 Yos 6:5Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)

13Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.

Fahari Ya Solomoni

(2 Nyakati 9:13-28)

1410:14 Kum 16:18; Hes 25:4; 2Nya 30:8; 2Fal 23:26; 2Nya 28:11-13; 29:10; 30:8; Za 78:38; Isa 12:1Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,10:14 Talanta 666 za dhahabu ni sawa na tani 25. 1510:15 Neh 11:16mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.

16Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 60010:16 Shekeli 600 za dhahabu ni sawa na kilo 3.5. 17Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu10:17 Mane tatu za dhahabu ni sawa na kilo 1.7. za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.

1810:18 Ezr 5:2; 2:2; Amu 3:6; Zek 6:1Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi. 1910:19 2Fal 10:15; Law 5:15; 6:4-6; 1Nya 29:24; 2Nya 30:8; Gal 2:9; Mit 22:26Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono. 2010:20 1Nya 24:14Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote. 2110:21 1Nya 24:8Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni. 2210:22 1Nya 9:12Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara10:22 Au: za Tarshishi (ona pia 1Fal 22:48; 2Nya 9:21; 20:36; Isa 2:16; 60:9). baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.

2310:23 Neh 8:7; 9:4Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia. 2410:24 Neh 3:1; 12:10Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake. 2510:25 Ezr 3:2; 8:3; Neh 7:13Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.

2610:26 Kum 17:16Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu. 2710:27 Ay 27:16; 1Nya 27:28Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 28Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue.10:28 Yaani Kilikia ilioko Syria. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue. 2910:29 Hes 13:29Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha10:29 Shekeli 600 za fedha ni sawa na kilo 7. na farasi kwa shekeli 150.10:29 Shekeli 150 za fedha ni sawa na kilo 1.7. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.10:29 Waaramu hapa ina maana ya Washamu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

列王紀上 10:1-29

示巴女王拜訪所羅門

1示巴女王聽說所羅門因耶和華而名聲大震,便來用難題考問他。 2她率領許多隨從,用駱駝馱著香料、寶石和大量黃金到耶路撒冷晉見所羅門王,與所羅門談論她心中的疑問。 3所羅門王解答了她所有的問題,沒有一樣難得住他。 4示巴女王見所羅門智慧非凡,又看見他建的宮殿、 5席上的美味、入座的群臣、侍立一旁的僕人及其服裝、酒政以及他在耶和華殿裡獻的燔祭,感到萬分驚奇。

6她對所羅門說:「我在本國聽到的有關你的功業和智慧原來都是真的。 7若不是親眼目睹,我不會相信。事實上,我聽到的還不到一半!你的智慧和財富遠超過我聽到的傳聞。 8你的臣僕能經常侍立在你面前聆聽智慧之言,真有福氣! 9你的上帝耶和華當受稱頌!祂喜愛你,立你為以色列的王。因為祂永遠愛以色列,所以立你為王,使你秉公行義。」

10示巴女王將四噸黃金、大量香料和寶石獻給所羅門王。此後,再無人像示巴女王那樣獻給所羅門王那麼多香料。

11希蘭王的船隻從俄斐運來黃金、大量的檀香木和寶石。 12所羅門王用這些檀香木為耶和華的殿和王宮造欄杆,又為歌樂手製作琴瑟。此後,再沒有人運來或見過這樣的檀香木。

13所羅門王除了厚贈示巴女王禮物以外,還滿足了她的一切要求。之後,女王和隨從就回示巴去了。

所羅門的財富

14所羅門每年收到的黃金約二十三噸。 15此外,還有商人、阿拉伯諸王和國中各總督送來的貢稅。 16所羅門用錘好的金子打造了二百面大盾牌,每面用七公斤金子; 17又用錘好的金子打造了三百面小盾牌,每面用三點五公斤金子,全部存放在黎巴嫩林宮。

18王又造了一個象牙寶座,外面用純金包裹。 19這寶座有六級臺階,靠背是圓形的,兩旁有扶手,扶手兩邊各站著一頭獅子。 20六級臺階上共站著十二頭獅子,每級臺階兩端各站一頭。這寶座舉世無雙。 21所羅門王所有的杯子都是金的,黎巴嫩林宮裡的所有器皿都是純金的,沒有一件是用銀子造的,因為所羅門年間銀子不算什麼。 22王有他施船隊和希蘭的船隊一起出海,每三年就運回金銀、象牙、猿猴和孔雀。

23所羅門王的財富和智慧超過天下諸王。 24天下的人都紛紛來朝見他,聆聽上帝賜給他的智言慧語。 25他們年年都帶來禮物,有金銀器皿、衣服、兵器、香料和騾馬。

26所羅門組建了戰車和騎兵,有一千四百輛戰車、一萬二千名騎兵,駐紮在屯車城和他所在的耶路撒冷27王使耶路撒冷的金銀多如石頭,使香柏木多如丘陵的無花果樹。 28所羅門的馬匹都是由王室商隊從埃及古厄按定價買來的。 29他們從埃及買來車馬,每輛車六百塊銀子,每匹馬一百五十塊銀子,他們也把車馬賣給人諸王和亞蘭諸王。