1 Timotheo 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Timotheo 1:1-20

11:1 Tit 1:3; Kol 1:27Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.

21:2 Mdo 16:1; 1Kor 4:17; 1The 2:11Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani:

Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

Maonyo Dhidi Ya Walimu Wa Uongo

31:3 Mdo 18:19; Gal 1:6, 7Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo 41:4 1Tim 4:7; 2Tim 4:4; 1Tim 6:4wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani. 51:5 2Tim 2:22; 1:5Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli. 61:6 1Tim 6:4, 20Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa, 71:7 Efe 4:11; Ay 38:2wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.

81:8 Rum 7:12Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa. 91:9 Gal 3:19; 5:23Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji, 101:10 1Tim 6:3; 2Tim 1:13kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli, 111:11 1The 2:4ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.

Neema Ya Mungu Kwa Paulo

121:12 Flp 4:13Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake. 131:13 Mdo 8:3; 26:9Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu. 141:14 Rum 5:20; 2Tim 1:13Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.

151:15 1Tim 4:9; 2Tim 2:11Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote. 161:16 1Tim 1:13; Rum 2:4; Yn 3:15; Mt 25:46Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. 171:17 Ufu 15:3; Kol 1:15; Rum 11:36Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen.

181:18 1Tim 4:14; 2Tim 4:7Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri, 191:19 1Tim 6:21; Mdo 23:1; 1Tim 6:21; 2Tim 2:18ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao. 201:20 2Tim 2:17; 4:14; 1Kor 5:5Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.

New International Reader’s Version

1 Timothy 1:1-20

1I, Paul, am writing this letter. I am an apostle of Christ Jesus, just as God our Savior commanded. Christ Jesus also commanded it. We have put our hope in him.

2Timothy, I am sending you this letter. You are my true son in the faith.

May God the Father and Christ Jesus our Lord give you grace, mercy and peace.

Paul Warns Timothy to Oppose False Teachers

3Timothy, stay there in Ephesus. That is what I told you to do when I went into Macedonia. I want you to command certain people not to teach things that aren’t true. 4And command them not to spend their time on stories that are made up. They must not waste time on family histories that never end. These things only lead to fights about ideas. They don’t help God’s work move forward. His work is done by faith. 5Love is the purpose of my command. Love comes from a pure heart. It comes from a good sense of what is right and wrong. It comes from faith that is honest and true. 6Some have turned from these teachings. They would rather talk about things that have no meaning. 7They want to be teachers of the law. And they are very sure about that law. But they don’t know what they are talking about.

8We know that the law is good if it is used properly. 9We also know that the law isn’t made for godly people. It is made for those who break the law. It is for those who refuse to obey. It is for ungodly and sinful people. It is for those who aren’t holy and who don’t believe. It is for those who kill their fathers or mothers. It is for murderers. 10It is for those who commit sexual sins. It is for those who commit homosexual acts. It is for people who buy and sell slaves. It is for liars. It is for people who tell lies in court. It is for those who are a witness to things that aren’t true. And it is for anything else that is the opposite of true teaching. 11True teaching agrees with the good news about the glory of the blessed God. He trusted me with that good news.

The Lord Pours Out His Grace on Paul

12I am thankful to Christ Jesus our Lord. He has given me strength. I thank him that he considered me faithful. I thank him for appointing me to serve him. 13I used to speak evil things against Jesus. I tried to hurt his followers. I really pushed them around. But God showed me mercy anyway. I did those things without knowing any better. I wasn’t a believer. 14Our Lord poured out more and more of his grace on me. Along with it came faith and love from Christ Jesus.

15Here is a saying that you can trust. It should be accepted completely. Christ Jesus came into the world to save sinners. And I am the worst sinner of all. 16But for that very reason, God showed me mercy. And I am the worst of sinners. He showed me mercy so that Christ Jesus could show that he is very patient. I was an example for those who would come to believe in him. Then they would receive eternal life. 17The eternal King will never die. He can’t be seen. He is the only God. Give him honor and glory for ever and ever. Amen.

Paul Commands Timothy

18My son Timothy, I am giving you this command. It is in keeping with the prophecies once made about you. By remembering them, you can fight the battle well. 19Then you will hold on to faith. You will hold on to a good sense of what is right and wrong. Some have not accepted this knowledge of right and wrong. So they have destroyed their faith. They are like a ship that has sunk. 20Hymenaeus and Alexander are among them. I have handed them over to Satan. That will teach them not to speak evil things against God.