1 Samweli 9 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 9:1-27

Samweli Anamtia Sauli Mafuta

19:1 Yos 18:11-20; Rut 2:1; 1Sam 14:51; 1Nya 8:33; 9:39; Es 2:5; Mdo 13:21Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini. 29:2 Mwa 39:6; 1Sam 10:23-24Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.

39:3 1Sam 10:14-16Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.” 49:4 Yos 24:33; 2Fal 4:42; 1Sam 10:2Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.

59:5 1Sam 1:1; 10:1Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”

69:6 Kum 33:1; Amu 13:6; 1Sam 3:19; 1Fal 13:1; 2Fal 6:6; 1Tim 6:11; 1Sam 3:19; Isa 44:26; Mt 24:35Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”

79:7 Mwa 32:20; 1Fal 13:7; 14:3; 2Fal 4:42; 5:5, 15; Yer 40:5; Amu 6:18; 13:17Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”

8Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli.9:8 Robo shekeli ni sawa na gramu 3. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.” 99:9 Mwa 25:22; 2Sam 15:27; 24:11; 17:13; 1Nya 9:22; 21:9; 26:28; 29:29; 2Nya 19:2; Isa 29:10; 30:10; Amo 7:12; Kut 28:30; Hes 27:21; Amu 1:1; 20:18-28; 2Sam 24:11; 2Fal 17:13(Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)

10Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.

119:11 Mwa 24:11-13; Kut 2:16Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”

129:12 Hes 28:11-15; 1Sam 7:17; Law 26:30; 1Fal 3:2Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu. 139:13 Mt 14:19; 1Kor 10:16; 1Tim 4:3-5Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”

14Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.

159:15 1Sam 24:11; Za 25:14; Mk 11:2-4; Mdo 13:11Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili: 169:16 Kut 30:25; 1Sam 2:35; 12:3; 15:1; 26:9; 2Fal 11:12; Za 2:2; 2Sam 7:8; 1Fal 8; 16; 1Nya 5:2; Kut 3:8; 1Sam 23:4; 2Sam 3:18; Mwa 16:11; Za 102:1“Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”

179:17 1Sam 16:12; Hos 13:11Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”

18Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”

19Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako. 209:20 1Sam 12:13; Ezr 6:8; Isa 60:4-9; Dan 2:44; Hag 2:7; Mal 3:1Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”

219:21 Za 68:27; Kut 3:11; Mt 2:6; 1Kor 15:9; Amu 6:15; 20:35, 46; 1Sam 18:18; 15:17Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”

22Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini. 23Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”

249:24 Law 7:24; Hes 18:18; Eze 24:4; Mdo 10:9Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’ ” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.

259:25 Kum 22:8; Yos 2:8; Mt 24:17; Lk 5:19; Mdo 10:9Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake. 26Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja. 27Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”

La Bible du Semeur

1 Samuel 9:1-27

Saül rencontre Samuel

1Un homme de la tribu de Benjamin nommé Qish avait pour ancêtres en ligne ascendante : Abiel, Tseror, Bekorath et Aphiah, qui descendaient d’un Benjaminite. Qish était un guerrier valeureux. 2Il avait un fils nommé Saül. C’était un beau jeune homme9.2 Autre traduction : homme d’élite., aucun Israélite n’avait plus belle allure que lui ; il les dépassait tous de la tête.

3Un jour, les ânesses de son père s’égarèrent et Qish lui dit : Mon fils, emmène l’un des serviteurs et pars à la recherche des ânesses !

4Saül parcourut la région montagneuse d’Ephraïm, puis le territoire de Shalisha sans les trouver. Ensuite ils traversèrent la région de Shaalim sans succès, puis le pays de Benjamin, toujours sans trouver les ânesses.

5Arrivés au territoire de Tsouph, Saül dit au serviteur qui l’accompagnait : Viens, nous allons rentrer, sinon mon père va s’inquiéter à notre sujet sans plus penser aux ânesses.

6Le serviteur lui répondit : Attends, il y a justement dans cette ville9.6 Probablement Rama où résidait Samuel (7.17 ; 8.4). un homme de Dieu très considéré ; tout ce qu’il annonce arrive immanquablement. Allons le voir ! Peut-être nous indiquera-t-il par quel chemin continuer notre route.

7– D’accord, allons-y ! dit Saül. Mais qu’est-ce que nous apporterons à cet homme ? Nos provisions sont épuisées et nous n’avons aucun cadeau que nous puissions offrir à l’homme de Dieu. Il ne nous reste plus rien.

8Le serviteur lui répondit : Il se trouve que j’ai encore sur moi une petite pièce d’argent9.8 En hébreu : un quart de sicle, le sicle valant 12 g., je la donnerai à l’homme de Dieu et il nous indiquera le chemin à prendre.

9Autrefois en Israël, quand on allait consulter Dieu, on disait : « Venez, allons chez l’homme qui reçoit des révélations ! » C’était là le nom par lequel on désignait ceux qu’on appelle aujourd’hui des « prophètes ». 10Saül dit à son serviteur : Tu as raison ! Allons-y !

Et ils se dirigèrent vers la ville où habitait l’homme de Dieu.

11Pendant qu’ils gravissaient la montée qui mène vers la ville, ils croisèrent des jeunes filles qui en descendaient pour aller puiser de l’eau. Ils leur demandèrent : L’homme qui reçoit des révélations est-il là ?

12– Oui, lui répondirent-elles, il est là-haut, droit devant vous ! Mais dépêchez-vous, il vient d’arriver en ville car il y a aujourd’hui un sacrifice pour le peuple sur le haut lieu. 13Dès que vous serez entrés dans la ville, vous allez le trouver avant qu’il monte sur le haut lieu pour le repas9.13 Repas qui accompagnait certains sacrifices (1.4 ; 2.13-16 ; Dt 12.6-7). ; car le peuple ne se mettra pas à table avant son arrivée, parce que c’est lui qui doit bénir le sacrifice ; après cela, les invités prendront part au repas. Si vous montez tout de suite, vous le trouverez sûrement.

Dieu amène Saül auprès de Samuel

14Ils montèrent donc à la ville. Au moment où ils y pénétrèrent par la porte, Samuel sortait dans leur direction pour monter au haut lieu. 15Or, la veille, l’Eternel avait fait cette révélation à Samuel : 16« Demain, à cette même heure, lui avait-il dit, je t’enverrai un homme du territoire de Benjamin, tu lui conféreras l’onction pour l’établir chef de mon peuple Israël, et il le délivrera des Philistins, car j’ai vu la misère de mon peuple, et j’ai entendu sa plainte. »

17Dès que Samuel aperçut Saül, l’Eternel l’avertit : Voici l’homme dont je t’ai dit qu’il gouvernerait mon peuple.

18Saül aborda Samuel au milieu de la porte et lui demanda : Peux-tu m’indiquer où est la maison de l’homme qui reçoit des révélations ?

19Samuel lui répondit : C’est moi cet homme qui reçoit des révélations ! Passe devant moi et montons au haut lieu. Ton serviteur et toi, vous mangerez avec moi aujourd’hui ; demain matin, je te laisserai repartir après avoir répondu à toutes les questions qui te préoccupent. 20Quant aux ânesses disparues il y a trois jours, ne t’en inquiète plus ; elles sont retrouvées. D’ailleurs, à qui est réservé tout ce qu’il y a de précieux en Israël ? N’est-ce pas à toi et à toute ta famille ?

21Saül répliqua : Que dis-tu là ? Ne suis-je pas un Benjaminite, de la plus petite des tribus d’Israël, et ma famille n’est-elle pas la moins importante de toutes celles de ma tribu ? Pourquoi parles-tu donc de cette manière ?

22Samuel emmena Saül et son serviteur et les fit entrer dans la salle du festin. Il les installa à la place d’honneur au milieu d’une trentaine d’invités. 23Ensuite, il ordonna au cuisinier : Sors pour lui le morceau de viande que je t’ai remis pour que tu le mettes de côté.

24Le cuisinier apporta le gigot et sa garniture9.24 Traduction incertaine. La version syriaque a : la queue. Cette partie était normalement réservée au prêtre (Ex 29.22, 27 ; Lv 7.32-33, 35 ; Nb 6.20 ; 18.18). et le déposa devant Saül pendant que Samuel lui dit : Voici la part qui t’a été réservée. Sers-toi et mange, car, pour cette occasion, elle a été gardée exprès pour toi, lorsque j’ai invité le peuple.

Ainsi Saül mangea avec Samuel ce jour-là. 25Puis ils redescendirent ensemble du haut lieu à la ville, et Samuel s’entretint avec Saül sur la terrasse de sa maison.

Samuel confère la royauté à Saül et lui donne ses instructions

26Le lendemain, au lever du jour, Samuel appela Saül sur la terrasse : Mets-toi en route, et je prendrai congé de toi.

Saül se leva et se mit en route. Il sortit en compagnie de Samuel. 27Quand ils arrivèrent à la limite de la ville, Samuel dit à Saül : Ordonne à ton serviteur d’aller devant nous.

Le serviteur s’éloigna.

– Maintenant, tiens-toi là et je te ferai savoir ce que Dieu a dit.