1 Samweli 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 4:1-22

14:1 1Sam 5:1; 7:12; 29:1; Yos 12:18; 1Fal 20:26Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote.

Wafilisti Wateka Sanduku La Mungu

Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki. 2Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita. 34:3 Yos 6:7; 7:7; 18:1; 1Sam 2:32; 2Nya 13:8Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”

44:4 Mwa 3:24; Kut 25:23; 2Sam 6:2; Za 80:1; Hes 7:89Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.

54:5 Yos 6:5-10Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika. 64:6 Mwa 14:13Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?”

Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini, 74:7 Kut 15:14Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo. 84:8 Kut 12:30; 1Sam 5:12; Ufu 11:6Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani. 94:9 Amu 13:1; 1Kor 16:13; 2Sam 10:12; 1Nya 19:13Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”

104:10 2Sam 18:17; 2Fal 14:12; Kum 28:25; Law 26:17Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu. 114:11 Za 78:64; Yer 7:12; 1Sam 2:32Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.

Kifo Cha Eli

124:12 Eze 24:26; 33:21; Yos 7:6; Neh 9:1; 2Sam 1:2; Ay 2:12Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake. 134:13 1Sam 1:9Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.

14Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?”

Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli, 15wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona. 164:16 2Sam 1:4Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.”

Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”

174:17 1Sam 22:18; Za 78:64; 78:61Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”

184:18 Amu 2:16; 16:31; 1Sam 2:31Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.

19Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu. 204:20 Mwa 35:17Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.

214:21 Mwa 35:18; Kut 24:16; Za 106:26; Yer 2:11; Eze 1:28; 9:3; 10:18Alimwita yule mtoto Ikabodi,4:21 Ikabodi maana yake Utukufu wa Bwana umeondoka. akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe. 224:22 Kut 24:16; Za 78:61; Yer 7:12Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記上 4:1-22

約櫃被擄

1那時,以色列人去迎戰非利士人,他們在以便以謝紮營,非利士人在亞弗紮營。 2非利士人列陣與以色列人交戰,大敗以色列人,殺了他們四千人。 3軍隊回營後,以色列的長老說:「為什麼今天耶和華使我們敗在非利士人手下?我們從示羅把耶和華的約櫃抬來吧,讓它4·3 」或作「祂」。與我們同去,好從仇敵手中救我們。」

4於是,他們派人去示羅把那坐在基路伯天使上的萬軍之耶和華的約櫃抬來。以利的兩個兒子何弗尼非尼哈也隨上帝的約櫃同來。 5以色列人看見耶和華的約櫃到了營中,就高聲歡呼,聲音震天動地。 6非利士人聽見了喊聲就說:「希伯來人在營中喊什麼?」後來他們知道是耶和華的約櫃到了營中, 7就害怕起來,說:「有神明到了他們營中,我們大禍臨頭了,我們從來沒有遇過這種事情! 8我們大禍臨頭了!誰能從這些大能的神明手中救我們?在曠野用各種災禍毀滅埃及人的就是這些神明。 9非利士人啊,要剛強,做大丈夫。不然,我們就會成為希伯來人的奴隸,像他們做我們的奴隸一樣。我們要做大丈夫,奮力征戰。」

10非利士人和以色列人交戰,以色列人敗下陣來,紛紛逃回家中。他們傷亡慘重,損失了三萬步兵。 11上帝的約櫃被擄走了,以利的兩個兒子何弗尼非尼哈被殺身亡。

以利之死

12當天有一個便雅憫人逃出了戰場,他撕爛衣服,頭蒙灰塵,來到示羅13以利正坐在路旁的座位上觀望,因為他心裡為上帝的約櫃擔憂。那個從戰場回來的人進城報信後,全城的人都放聲大哭。 14以利聽見哭喊聲,就問:「人們為何喊叫?」那人趕忙告訴他。 15那時,以利已經九十八歲,眼睛因為年老而失明。 16報信的人對以利說:「我今天是從戰場逃回來的。」以利問:「我的孩子,情況怎麼樣?」 17報信的答道:「以色列人被非利士人擊潰,傷亡慘重,你的兩個兒子何弗尼非尼哈都死了,上帝的約櫃也被擄走了。」 18以利年老體胖,聽到約櫃被擄去,就從門邊的座位上向後跌倒,頸斷身亡。他做士師審理以色列人的事務共四十年。

19以利的兒媳婦、非尼哈的妻子當時懷孕在身,接近產期。她聽說上帝的約櫃被擄、公公和丈夫都死了,就突然陣痛,生下了孩子。 20在她彌留之際,身旁的婦人對她說:「不要怕,你生了一個男孩。」但她既不理會,也不回答。 21她給孩子取名叫以迦博,意思是:「榮耀離開以色列了」。這是因為上帝的約櫃被擄走,她的公公和丈夫都死了。 22她說:「榮耀離開了以色列,因為上帝的約櫃已經被擄走了。」