1 Samweli 31 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 31:1-13

Sauli Ajiua

(1 Nyakati 10:1-12)

131:1 1Sam 28:4; 1Nya 10:1-12; 1Sam 29:1; 1Nya 8:33Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa. 231:2 1Sam 28:19; 18:1; 14:49; 1Nya 8:33Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua. 331:3 1Sam 28:4; 2Sam 1:6Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.

431:4 Amu 9:54; Mwa 34:14; 1Sam 14:6; 2Sam 1:6, 10Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.”

Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia. 5Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye. 631:6 1Sam 26:10; 12:25; 1Nya 10:6; Rum 6:23Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.

7Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.

831:8 2Sam 1:20Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa. 931:9 1Sam 1:20; 4:4; Amu 16:24Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao. 1031:10 Amu 2:12-13; 1Sam 7:3; Yos 17:11; 2Sam 21:12; 1Sam 21:9; Amu 1:27Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.

1131:11 Amu 21:8; 1Sam 11:1Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli, 1231:12 Za 76:5; Mwa 38:24; Amo 6:10; 2Nya 16:14; 1Sam 11:1-11; 2Sam 2:4-7; Yer 34:5; Amo 6:10mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto. 1331:13 2Sam 21:12-14; Mwa 21:33; 2Sam 3:35; 12:19-23; 1:12; Mwa 50:10; 1Sam 22:6; Mwa 50:10; Ay 2:13Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.

New International Reader’s Version

1 Samuel 31:1-13

Saul Takes His Own Life

1The Philistines fought against the Israelites. The Israelites ran away from them. But many Israelites were killed on Mount Gilboa. 2The Philistines kept chasing Saul and his sons. They killed his sons Jonathan, Abinadab and Malki-Shua. 3The fighting was heavy around Saul. Men who were armed with bows and arrows caught up with him. They shot their arrows at him and wounded him badly.

4Saul spoke to the man carrying his armor. He said, “Pull out your sword. Stick it through me. If you don’t, these fellows who aren’t circumcised will come. They’ll stick their swords through me and hurt me badly.”

But the man was terrified. He wouldn’t do it. So Saul took his own sword and fell on it. 5The man saw that Saul was dead. So he fell on his own sword and died with him. 6Saul and his three sons died together that same day. The man who carried his armor also died with them that day. So did all of Saul’s men.

7The Israelites who lived along the valley saw that their army had run away. So did those who lived across the Jordan River. They saw that Saul and his sons were dead. So they left their towns and ran away. Then the Philistines came and made their homes in them.

8The day after the Philistines had won the battle, they came to take what they wanted from the dead bodies. They found Saul and his three sons dead on Mount Gilboa. 9So they cut off Saul’s head. They took his armor from his body. Then they sent messengers through the whole land of the Philistines. They announced the news in the temple where they had set up statues of their gods. They also announced it among their people. 10They put Saul’s armor in the temple where they had set up statues of female gods that were named Ashtoreth. They hung his body up on the wall of Beth Shan.

11The people of Jabesh Gilead heard about what the Philistines had done to Saul. 12So all their brave men marched through the night to Beth Shan. They took down the bodies of Saul and his sons from the wall of Beth Shan. They brought them to Jabesh. There they burned them. 13Then they got the bones of Saul and his sons and buried them under a tamarisk tree at Jabesh. They didn’t eat anything for seven days.