1 Samweli 31 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 31:1-13

Sauli Ajiua

(1 Nyakati 10:1-12)

131:1 1Sam 28:4; 1Nya 10:1-12; 1Sam 29:1; 1Nya 8:33Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa. 231:2 1Sam 28:19; 18:1; 14:49; 1Nya 8:33Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua. 331:3 1Sam 28:4; 2Sam 1:6Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.

431:4 Amu 9:54; Mwa 34:14; 1Sam 14:6; 2Sam 1:6, 10Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.”

Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia. 5Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye. 631:6 1Sam 26:10; 12:25; 1Nya 10:6; Rum 6:23Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.

7Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.

831:8 2Sam 1:20Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa. 931:9 1Sam 1:20; 4:4; Amu 16:24Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao. 1031:10 Amu 2:12-13; 1Sam 7:3; Yos 17:11; 2Sam 21:12; 1Sam 21:9; Amu 1:27Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.

1131:11 Amu 21:8; 1Sam 11:1Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli, 1231:12 Za 76:5; Mwa 38:24; Amo 6:10; 2Nya 16:14; 1Sam 11:1-11; 2Sam 2:4-7; Yer 34:5; Amo 6:10mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto. 1331:13 2Sam 21:12-14; Mwa 21:33; 2Sam 3:35; 12:19-23; 1:12; Mwa 50:10; 1Sam 22:6; Mwa 50:10; Ay 2:13Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

撒母耳记上 31:1-13

扫罗之死

1非利士人与以色列人交战,以色列人败逃,许多人在基利波山被杀。 2非利士人穷追扫罗及其众子,杀了扫罗的儿子约拿单亚比拿达麦基舒亚3扫罗周围战事激烈,他被弓箭手发现、射成重伤, 4就对为他拿兵器的人说:“拔出你的刀来刺死我吧,免得那些未受割礼的人来刺杀和凌辱我。”但拿兵器的人非常害怕,不敢动手,扫罗就自己伏刀自尽了。 5侍从看见扫罗已死,也伏刀自尽了。 6这样,扫罗和他三个儿子,以及为他拿兵器的人和他的军队都死了。 7平原一带和约旦河对面的以色列人见以色列军败逃、扫罗及其众子已死,都弃城而逃。于是,非利士人占据了那些城邑。

8次日,非利士人来剥阵亡者的衣物,发现扫罗和他的三个儿子横尸基利波山, 9就割下了扫罗的头颅,剥下他的盔甲,并派人走遍非利士全境,在他们偶像的庙里及民众中通告消息。 10非利士人把扫罗的盔甲放在亚斯她录神庙里,把他的尸体钉在伯·珊城墙上。 11基列·雅比人听说非利士人对扫罗的所作所为, 12他们所有的勇士就连夜赶到伯·珊,从墙上取下扫罗和他儿子们的尸体,带到雅比火化, 13把骨灰葬在雅比的垂丝柳树下,又为他们禁食了七天。