1 Samweli 28 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 28:1-25

Sauli Na Mchawi Wa Endori

128:1 1Sam 29:1-2Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”

228:2 Rum 12:9Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.”

Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”

328:3 1Sam 25:1; 7:17; Kut 22:18; Isa 57:1, 2; Mdo 16:16, 19; Law 19:31; 20:27; Kum 18:10Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.

428:4 Yos 19:18; 1Sam 31:1-3; 2Sam 1:6, 21; 21:12; Law 19:31; Kum 18:10-11; 2Fal 4:8Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa. 528:5 Kut 19:16; Ay 15:21; 18:11; Za 48:5, 6; 73:19; Isa 57:20; Dan 5:6Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu. 628:6 1Sam 8:18; 14:37; Kum 13:3; Kut 28:30; Law 8:8; Eze 20:3; Amo 8:11; Mik 3:7; Hes 12:6; Mit 1:28; 1Nya 10:13-14Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu,28:6 Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha juu cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha. wala kwa njia ya manabii. 728:7 1Nya 10:13; Mdo 16:16; Yos 17:11; Za 83:10Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.”

Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”

828:8 1Fal 22:30; 2Nya 18:29; 35:22; 2Fal 1:3; Isa 8:19; 1Nya 10:13Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”

928:9 Ay 18:10; Za 31:4; 69:22; Isa 8:14Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”

10Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”

11Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?”

Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”

1228:12 Mwa 27:36; 1Fal 14:6; Isa 57:2; Ufu 14:13Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”

1328:13 Law 19:31; 2Nya 33:6Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?”

Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”

1428:14 1Sam 15:27; 24:8; 2The 2:10, 11Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?”

Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.”

Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.

1528:15 Amu 16:20; Kum 13:3; 1Sam 18:12Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?”

Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”

16Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako? 1728:17 1Sam 15:28Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi. 1828:18 1Sam 15:20; Kum 9:8; 1Sam 15:3; Mwa 14:7; 1Sam 14:48Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo. 1928:19 1Sam 31:2; 1Nya 8:33Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”

2028:20 1Sam 25:37; Za 50:21Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.

2128:21 Amu 9:17; 12:3; Ay 13:14; 1Sam 19:5Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye. 22Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”

2328:23 1Fal 21:4; 2Fal 5:13; Mwa 4:6; Mit 25:20, 21Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.”

Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.

2428:24 Mwa 18:7, 8; Lk 15:23-30Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu. 25Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.

New International Reader’s Version

1 Samuel 28:1-25

1While David was living in Ziklag, the Philistines gathered their army together. They planned to fight against Israel. Achish said to David, “Here is what you must understand. You and your men must march out with me and my army.”

2David said, “I understand. You will see for yourself what I can do.”

Achish replied, “All right. I’ll make you my own personal guard for life.”

Saul and the Woman at Endor

3Samuel had died. The whole nation of Israel was filled with sorrow because he was dead. They had buried him in his own town of Ramah. Saul had thrown out of the land people who get messages from those who have died. He had also thrown out people who talk to the spirits of the dead.

4The Philistines gathered together and set up camp at Shunem. At the same time, Saul gathered together all the Israelites. They set up camp at Gilboa. 5When Saul saw the Philistine army, he was afraid. Terror filled his heart. 6He asked the Lord for advice. But the Lord didn’t answer him through dreams or prophets. He didn’t answer him when Saul had the priest cast lots by using the Urim. 7Saul spoke to his attendants. He said, “Find me a woman who gets messages from those who have died. Then I can go and ask her some questions.”

“There’s a woman like that in Endor,” they said.

8Saul put on different clothes so people wouldn’t know who he was. At night he and two of his men went to see the woman. “I want you to talk to a spirit for me,” he said. “Bring up the spirit of the dead person I choose.”

9But the woman said to him, “By now you must know what Saul has done. He has removed everyone who gets messages from those who have died. He has also removed everyone who talks to the spirits of the dead. He has thrown all of them out of the land. Why are you trying to trap me? Why do you want to have me put to death?”

10Saul made a promise in the name of the Lord. He said to the woman, “You can be sure that the Lord lives. And you can be just as sure that you won’t be punished for helping me.”

11Then the woman asked, “Whose spirit should I bring up for you?”

“Bring Samuel up,” he said.

12When the woman saw Samuel, she let out a loud scream. She said to Saul, “Why have you tricked me? You are King Saul!”

13He said to her, “Don’t be afraid. Tell me what you see.”

The woman said, “I see a ghostly figure. He’s coming up out of the earth.”

14“What does he look like?” Saul asked.

“An old man wearing a robe is coming up,” she said.

Then Saul knew it was Samuel. He bowed down. He lay down flat with his face toward the ground.

15Samuel said to Saul, “Why have you troubled me by bringing me up from the dead?”

“I’m having big problems,” Saul said. “The Philistines are fighting against me. God has left me. He doesn’t answer me anymore. He doesn’t speak to me through prophets or dreams. So I’ve called on you to tell me what to do.”

16Samuel said, “The Lord has left you. He has become your enemy. So why are you asking me what you should do? 17The Lord has spoken through me and has done what he said he would do. The Lord has torn the kingdom out of your hands. He has given it to one of your neighbors. He has given it to David. 18You didn’t obey the Lord. You didn’t show his great anger against the Amalekites by destroying them. So he’s punishing you today. 19He will hand both Israel and you over to the Philistines. Tomorrow you and your sons will be down here with me. The Lord will also hand Israel’s army over to the Philistines.”

20Immediately Saul fell flat on the ground. What Samuel had said filled Saul with fear. His strength was gone. He hadn’t eaten anything all that day and all that night.

21The woman went over to Saul because she saw that he was very upset. She said, “Look, I’ve obeyed you. I put my own life in danger by doing what you told me to do. 22So please listen to me. Let me give you some food. Eat it. Then you will have the strength to go on your way.”

23But he refused. He said, “I don’t want anything to eat.”

Then his men joined the woman in begging him to eat. Finally, he paid attention to them. He got up from the ground and sat on a couch.

24The woman had a fat calf at her house. She killed it at once. She got some flour. She mixed it and baked some bread that didn’t have any yeast in it. 25Then she set the food in front of Saul and his men. They ate it. That same night they got up and left.