1 Samweli 28 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 28:1-25

Sauli Na Mchawi Wa Endori

128:1 1Sam 29:1-2Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”

228:2 Rum 12:9Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.”

Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”

328:3 1Sam 25:1; 7:17; Kut 22:18; Isa 57:1, 2; Mdo 16:16, 19; Law 19:31; 20:27; Kum 18:10Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.

428:4 Yos 19:18; 1Sam 31:1-3; 2Sam 1:6, 21; 21:12; Law 19:31; Kum 18:10-11; 2Fal 4:8Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa. 528:5 Kut 19:16; Ay 15:21; 18:11; Za 48:5, 6; 73:19; Isa 57:20; Dan 5:6Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu. 628:6 1Sam 8:18; 14:37; Kum 13:3; Kut 28:30; Law 8:8; Eze 20:3; Amo 8:11; Mik 3:7; Hes 12:6; Mit 1:28; 1Nya 10:13-14Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu,28:6 Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha juu cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha. wala kwa njia ya manabii. 728:7 1Nya 10:13; Mdo 16:16; Yos 17:11; Za 83:10Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.”

Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”

828:8 1Fal 22:30; 2Nya 18:29; 35:22; 2Fal 1:3; Isa 8:19; 1Nya 10:13Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”

928:9 Ay 18:10; Za 31:4; 69:22; Isa 8:14Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”

10Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”

11Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?”

Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”

1228:12 Mwa 27:36; 1Fal 14:6; Isa 57:2; Ufu 14:13Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”

1328:13 Law 19:31; 2Nya 33:6Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?”

Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”

1428:14 1Sam 15:27; 24:8; 2The 2:10, 11Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?”

Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.”

Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.

1528:15 Amu 16:20; Kum 13:3; 1Sam 18:12Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?”

Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”

16Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako? 1728:17 1Sam 15:28Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi. 1828:18 1Sam 15:20; Kum 9:8; 1Sam 15:3; Mwa 14:7; 1Sam 14:48Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo. 1928:19 1Sam 31:2; 1Nya 8:33Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”

2028:20 1Sam 25:37; Za 50:21Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.

2128:21 Amu 9:17; 12:3; Ay 13:14; 1Sam 19:5Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye. 22Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”

2328:23 1Fal 21:4; 2Fal 5:13; Mwa 4:6; Mit 25:20, 21Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.”

Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.

2428:24 Mwa 18:7, 8; Lk 15:23-30Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu. 25Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.

Священное Писание

1 Царств 28:1-25

1В те дни филистимляне собрали свои войска, чтобы воевать с Исраилом. Ахиш сказал Давуду:

– Ты со своими людьми должен выступить со мной в войске.

2Давуд сказал Ахишу:

– Хорошо. Ты узнаешь, что может сделать твой раб.

Ахиш ответил:

– Прекрасно! Я на всю жизнь сделаю тебя своим телохранителем.

Шаул у ендорской колдуньи

3Шемуил умер, и все исраильтяне оплакали и похоронили его в Раме, в его родном городе. Шаул изгнал из страны колдунов и вызывателей умерших.

4Филистимляне собрались, пришли и разбили лагерь в городе Шунеме, а Шаул собрал всех исраильтян и разбил лагерь на горной вершине в Гильбоа. 5Увидев филистимское войско, Шаул испугался, его сердце охватил страх. 6Он спрашивал Вечного, но Вечный не отвечал ему ни в снах, ни через священный жребий28:6 Букв.: «урим («свет»)». См. сноску на 2:28., ни через пророков.

7Тогда Шаул сказал своим слугам:

– Найдите мне женщину-колдунью. Я пойду к ней и спрошу её.

– В Ен-Доре есть одна колдунья, – сказали ему слуги.

8Шаул, изменив свою внешность и надев другие одежды, отправился в путь вместе с двумя спутниками и ночью пришёл к той женщине.

– Спроси для меня духа, – сказал он, – и вызови мне того, кого я тебе назову.

9Но женщина сказала ему:

– Ты, конечно, знаешь о том, что сделал Шаул. Он выгнал из страны колдунов и вызывателей умерших28:9 Или: «Он по всей стране предал смерти колдунов и вызывателей умерших».. Зачем же ты расставляешь ловушку мне на погибель?

10Шаул поклялся ей Вечным:

– Верно, как и то, что жив Вечный, – ты не будешь за это наказана.

11Тогда женщина спросила:

– Кого же тебе вызвать?

– Вызови мне Шемуила, – сказал он.

12Когда женщина увидела Шемуила, она громко вскрикнула и сказала Шаулу:

– Почему ты меня обманул? Ты – Шаул!

13Царь сказал ей:

– Не бойся. Что ты видишь?

Женщина сказала:

– Я вижу духа, который поднимается из земли.

14Как он выглядит? – спросил он.

– Поднимается старик, одетый в верхнюю одежду, – сказала она.

Тогда Шаул понял, что это Шемуил, и почтительно поклонился ему лицом до земли.

15Шемуил сказал Шаулу:

– Зачем ты тревожишь меня? Зачем вызываешь?

– Я в большой беде, – сказал Шаул. – Филистимляне воюют со мной, а Всевышний от меня отвернулся. Он больше не отвечает мне ни через пророков, ни в сновидениях. Поэтому-то я и позвал тебя, чтобы ты сказал мне, что делать.

16– Зачем же ты спрашиваешь меня, если Вечный отвернулся от тебя и стал твоим врагом? – ответил Шемуил. – 17Вечный совершил то, о чем Он предсказал через меня. Вечный вырвал царство из твоих рук и отдал его одному из тех, кто рядом с тобой, – Давуду. 18Так как ты не послушался Вечного и не обрушил на амаликитян Его пылающего гнева, Вечный сегодня и сделал с тобой это. 19Вечный отдаст Исраил вместе с тобой филистимлянам, и завтра ты и твои сыновья будете со мной. А ещё Вечный отдаст филистимлянам исраильское войско.

20Шаул, в ужасе от слов Шемуила, тотчас же рухнул всем телом на землю. Силы оставили его, потому что он ничего не ел весь день и всю ночь. 21Подойдя к Шаулу и увидев, как он потрясён, женщина сказала:

– Твоя рабыня послушалась тебя. Рискнув жизнью, я сделала то, что ты мне сказал. 22Пожалуйста, послушайся и ты своей рабыни и позволь мне предложить тебе кусок хлеба, чтобы ты поел и у тебя появились силы, прежде чем ты тронешься в путь.

23Он сказал:

– Я не буду есть.

Но его люди присоединились к уговорам женщины, и он послушался их. Он поднялся с земли и сел на постель. 24У женщины был упитанный телёнок, которого она немедленно заколола. Она взяла муки, замесила её и испекла лепёшки без закваски. 25Затем она поставила их перед Шаулом и его людьми, и они поели. Той же ночью они встали и ушли.