1 Samweli 23 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 23:1-29

Daudi Aokoa Keila

123:1 Yos 15:44; Hes 18:27; Amu 6:11Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,” 223:2 1Sam 22; 10; 30:8; 2:1; 2Sam 5:19; Za 50:19; Hes 27:21; Amu 1:1; 1Sam 28:6; 30:8; 1Nya 10:14; 14:10; Za 32:8; 37:5; Mit 3:5, 6; Yer 10:23; Yak 1:5akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?”

Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”

3Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”

423:4 1Sam 9:16; Yos 8:7; Amu 7:7Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.” 5Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila. 623:6 1Sam 22:20; 2:28; Ay 1:15-19(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)

Sauli Anamfuata Daudi

723:7 Kum 32:30; Za 31:21; Kut 15:9; 1Sam 24:4-6; 26:8, 9; Za 79:11Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.” 8Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.

923:9 1Sam 22:20; 2:28; 30:7Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.” 1023:10 1Sam 22:19; 2Sam 20:20; Es 3:6; Za 44:22Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu. 11Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.”

Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”

12Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?”

Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”

1323:13 1Sam 22:2; 25:13Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.

1423:14 Za 55:7; Yos 15:24; Za 54:3-4; 32:7; 11:1; Yos 15:55; 1Sam 27:1; Mit 1:16; 4:16; Kum 33:3; 1Sam 2:9; Za 32:7; 33:18; Mit 2:8; Rum 8:31; 2Tim 3:11; 4:17, 18Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.

1523:15 1Sam 20:1Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue. 1623:16 1Sam 30:6; Za 18:2; 27:14Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu. 1723:17 1Sam 20:31; 24:20Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.” 1823:18 1Sam 18:3; 2Sam 9:1; 21:7Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.

1923:19 1Sam 26:1; Za 54; 1Sam 26:3Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni? 20Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”

2123:21 Rut 2:20; 2Sam 2:5; 1Sam 22:8Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria. 22Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana. 2323:23 Mwa 31:36Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”

2423:24 Yos 15:55; 1Sam 26:1; 25:2Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni. 25Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.

2623:26 Za 17:6; 1Sam 19:12; 20:38; 2Sam 15:14; Za 31:22; 2Nya 20:12; 2Kor 1:8Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake, 2723:27 Kum 32:36; 1Sam 14:6; 2Sam 22:1-51; 2Fal 19:9; Za 18:1-50; Isa 37:6-9; 59:1; Yer 15:20, 21mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.” 28Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.23:28 Sela-Hamalekothi maana yake Mwamba wa Kutengana. 2923:29 1Sam 24:22; Yos 15:62; 2Nya 20:2; Wim 1:14Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.

La Bible du Semeur

1 Samuel 23:1-28

David délivre la ville de Qeïla

1On vint prévenir David que les Philistins avaient attaqué la ville de Qeïla23.1 Ville de Juda, à 4 ou 5 kilomètres de la grotte d’Adoullam (22.1), proche de la frontière de la Philistie. et qu’ils pillaient les céréales sur les aires. 2David consulta l’Eternel pour savoir s’il devait aller attaquer les Philistins et s’il les vaincrait. L’Eternel23.2 Par Abiatar (v. 6) et par l’ourim et le toummim. lui répondit : Va, tu battras les Philistins et tu délivreras Qeïla.

3Mais les hommes de David répondirent : Déjà ici, dans le territoire de Juda, nous vivons constamment dans la crainte, qu’est-ce que ce sera si nous allons à Qeïla nous battre contre les bataillons des Philistins ?

4David consulta une nouvelle fois l’Eternel qui lui répondit : Mets-toi en route, va à Qeïla, car je te donne la victoire sur les Philistins.

5David marcha donc avec ses hommes sur Qeïla et ils attaquèrent les Philistins. Ils s’emparèrent de leurs troupeaux et leur infligèrent une lourde défaite. Ainsi David délivra les habitants de Qeïla. 6Il faut dire que quand Abiatar, fils d’Ahimélek, s’était enfui auprès de David à Qeïla, il avait emporté avec lui l’éphod servant à consulter l’Eternel.

7On fit savoir à Saül que David était allé à Qeïla ; alors il s’écria : Dieu l’a livré en mon pouvoir, car il s’est lui-même enfermé dans un piège en entrant dans une ville qui a des portes et des verrous.

8Il mobilisa tous ses hommes pour marcher sur Qeïla et assiéger David et sa troupe. 9David apprit quel mauvais dessein Saül méditait contre lui. Aussi demanda-t-il au prêtre Abiatar d’apporter l’éphod. 10Il pria : Eternel, Dieu d’Israël, ton serviteur a appris que Saül s’apprête à marcher sur Qeïla pour détruire la ville à cause de moi. 11Les autorités de Qeïla me livreront-elles à lui ? Saül viendra-t-il vraiment comme ton serviteur l’a entendu dire ? Eternel, Dieu d’Israël, je t’en prie, informe ton serviteur.

L’Eternel répondit : Il viendra.

12David ajouta : Les autorités de Qeïla me livreront-elles à Saül, moi et mes hommes ?

L’Eternel répondit : Oui, elles vous livreront.

13Alors David se mit en route avec sa troupe d’environ six cents hommes et ils quittèrent Qeïla, marchant à l’aventure. On informa Saül que David avait quitté Qeïla et il renonça à son expédition.

La visite de Jonathan

14David gagna la région désertique de Ziph23.14 Au centre du désert de Judée, au sud-est d’Hébron (Jos 15.55). et s’installa dans des refuges escarpés de la montagne. Saül le cherchait jour après jour ; mais Dieu ne le fit pas tomber entre ses mains.

15David s’aperçut que Saül s’était mis en campagne pour lui ôter la vie, et il resta dans le désert de Ziph du côté de Horsha. 16Jonathan, le fils de Saül, se mit en route et se rendit auprès de David à Horsha pour l’encourager en affermissant sa confiance en Dieu. 17Il lui dit : Sois sans crainte ! Mon père ne réussira pas à mettre la main sur toi ; tu régneras sur Israël, et moi je serai au second rang près de toi ; mon père lui-même sait bien qu’il en sera ainsi.

18Tous deux renouvelèrent leur pacte d’amitié devant l’Eternel. David resta à Horsha et Jonathan rentra chez lui.

David échappe de peu à Saül

19Quelques hommes de Ziph allèrent trouver Saül à Guibéa pour lui dire23.19 Voir Ps 54.2. : Sais-tu que David se tient caché dans notre région dans des refuges escarpés à Horsha, dans les collines de Hakila au sud des steppes23.19 Ou : du Yéshimôn, nom désignant une steppe inculte. Il pourrait avoir valeur de nom propre ici (voir v. 24 ; 26.1, 3). ? 20Maintenant, ô roi, quand tu le désireras, viens, et nous nous chargerons de te le livrer.

21Saül répondit : Vous êtes bénis par l’Eternel, vous qui avez eu pitié de moi ! 22Allez donc, confirmez vos renseignements, observez et tenez-vous au courant de ses déplacements, sachez qui l’a vu dans ces endroits-là, car on m’a dit qu’il est très rusé. 23Repérez toutes ses cachettes, et revenez me voir avec des informations sûres ; alors j’irai avec vous, et s’il est dans le pays, je fouillerai au besoin chaque recoin du territoire de Juda pour le chercher.

24Les gens de Ziph quittèrent Saül et repartirent chez eux, précédant le roi. David et ses hommes se trouvaient au désert de Maôn23.24 Au sud du désert de Ziph, près de la localité de Karmel (15.12)., dans la plaine qui se trouve au sud des steppes.

25Saül partit à sa recherche avec ses hommes. On en informa David, et il descendit dans un endroit rocheux du désert de Maôn où il s’installa. Saül l’apprit et se mit à le poursuivre dans cette région. 26Saül marchait sur l’un des flancs de la montagne, tandis que David et ses hommes s’enfuyaient sur le flanc opposé. David précipitait sa marche pour échapper à Saül. Mais déjà le roi et ses hommes les cernaient et allaient les capturer. 27Alors un messager vint dire à Saül : Reviens tout de suite, car les Philistins ont fait une incursion dans le pays.

28Aussitôt Saül cessa de poursuivre David pour aller affronter les Philistins. C’est pourquoi on a appelé cet endroit le Rocher des Séparations.