1 Samweli 21 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 21:1-15

Daudi Huko Nobu

121:1 1Sam 22:9; Neh 11:32; Isa 10:32; 1Sam 16:1Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”

221:2 Mwa 27:20-24; 1Sam 19:11; 22:22; 1Fal 13:18; Za 119:29; 141:3; Mit 29:25; Gal 2:12, 13; Kol 3:9Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani. 3Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”

421:4 Law 24:8-9; Mt 12:4; Kut 19:15; Law 15:18; 24:5; Zek 7:3Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”

521:5 Kum 23:9-11; Yos 3:5; 2Sam 11:11; 1Tim 4:4; 1The 4:4; Law 8:26Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?” 621:6 Kut 25:30; 1Sam 22:10; Mt 12:3-4; Mk 2:25-28; Lk 6:1-5; Law 24:8Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.

721:7 1Sam 22:9; 14:47; Za 52Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.

8Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”

921:9 1Sam 17:51; 17:2, 4Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.”

Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”

Daudi Huko Gathi

1021:10 1Sam 25:13; 27:2-3; 18:7Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi. 1121:11 1Sam 18:7; 29:5; Za 50Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema:

“ ‘Sauli amewaua elfu zake,

naye Daudi makumi elfu yake’?”

12Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi. 1321:13 Za 34Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.

14Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu? 15Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”

New International Version – UK

1 Samuel 21:1-15

David at Nob

In Hebrew texts 21:1-15 is numbered 21:2-16. 1David went to Nob, to Ahimelek the priest. Ahimelek trembled when he met him, and asked, ‘Why are you alone? Why is no-one with you?’

2David answered Ahimelek the priest, ‘The king sent me on a mission and said to me, “No-one is to know anything about the mission I am sending you on.” As for my men, I have told them to meet me at a certain place. 3Now then, what have you to hand? Give me five loaves of bread, or whatever you can find.’

4But the priest answered David, ‘I don’t have any ordinary bread to hand; however, there is some consecrated bread here – provided the men have kept themselves from women.’

5David replied, ‘Indeed women have been kept from us, as usual whenever21:5 Or from us in the past few days since I set out. The men’s bodies are holy even on missions that are not holy. How much more so today!’ 6So the priest gave him the consecrated bread, since there was no bread there except the bread of the Presence that had been removed from before the Lord and replaced by hot bread on the day it was taken away.

7Now one of Saul’s servants was there that day, detained before the Lord; he was Doeg the Edomite, Saul’s chief shepherd.

8David asked Ahimelek, ‘Don’t you have a spear or sword here? I haven’t brought my sword or any other weapon, because the king’s mission was urgent.’

9The priest replied, ‘The sword of Goliath the Philistine, whom you killed in the Valley of Elah, is here; it is wrapped in a cloth behind the ephod. If you want it, take it; there is no sword here but that one.’

David said, ‘There is none like it; give it to me.’

David at Gath

10That day David fled from Saul and went to Achish king of Gath. 11But the servants of Achish said to him, ‘Isn’t this David, the king of the land? Isn’t he the one they sing about in their dances:

‘ “Saul has slain his thousands,

and David his tens of thousands”?’

12David took these words to heart and was very much afraid of Achish king of Gath. 13So he feigned insanity in their presence; and while he was in their hands he acted like a madman, making marks on the doors of the gate and letting saliva run down his beard.

14Achish said to his servants, ‘Look at the man! He is insane! Why bring him to me? 15Am I so short of madmen that you have to bring this fellow here to carry on like this in front of me? Must this man come into my house?’