1 Samweli 20 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 20:1-42

Daudi Na Yonathani

120:1 1Sam 24:9; 22:23; 23:15; 24:11; 25:29; Za 40:14; 54:3; 63:9; 70:2Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”

220:2 Mwa 44:7; Yos 22:29Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”

320:3 Kum 6:13Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”

4Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”

520:5 Hes 10:10; 25:11; 1Sam 9:12; 2Fal 4:23; 1Nya 23:31; 2Nya 2:4; Ezr 3:5; Neh 10:33; Za 81:3; Isa 1:13; Eze 45:17; 46:6; Za 55:13; Yn 8:59Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa. 620:6 1Sam 17:58; 1:3; 16:4; 9:12Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’ 720:7 1Sam 10:27; 25:17; 18:11; Kum 1:23Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru. 820:8 1Sam 18:3; 23:18; 2Sam 14:32; Yos 2:14; Rut 1:8Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”

9Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”

10Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”

11Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.

1220:12 1Sam 19:3; Yos 22:22Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha? 1320:13 Rut 1:17; 1Sam 16:18; 18:12Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu. 14Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa, 1520:15 1Sam 24:21; 2Sam 9:7; Mwa 21:23wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”

1620:16 1Sam 18:1-3; 25:22-23; Yos 22:23; 2Sam 4:7; 21:8Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.” 1720:17 Yos 9:18; 1Sam 18:3; 2Sam 1:26Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.

18Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu. 1920:19 1Sam 19:2Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli. 2020:20 2Fal 13:15Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha. 2120:21 Kum 6:13; 10:20; Isa 65:16; Yer 4:2Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari. 22Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako. 2320:23 Mwa 31:50Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”

2420:24 Hes 10:10; Mit 27:12Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale. 2520:25 1Sam 14:50Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi. 2620:26 Law 15:5; 1Sam 16:5; Law 6:2; 7:21; Hes 19:16; 1Kor 15:33; 2Kor 6:17; Efe 2:1-3; 5:11Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.” 27Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”

28Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu. 2920:29 Mwa 8:20Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”

30Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa? 3120:31 1Sam 23:17; 24:20Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”

3220:32 1Sam 19:4-5; Mt 23:27; Mwa 31:36; Lk 23:22; Za 25:3; 69:4; Mit 14:25; 24:11; Mt 27:23; Yn 7:31; 15:25Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?” 3320:33 1Sam 18:11, 17Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.

34Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.

35Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo, 36naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake. 37Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?” 38Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake. 39(Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.) 40Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”

4120:41 Mwa 33:3; Rut 2:10; 1Sam 24:8; 25:23; 2Sam 1:2Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.

4220:42 1Sam 1:17; Mdo 15:33; Mwa 40:14; 2Sam 1:26; Mit 18:24; Isa 48:1; Mwa 31:50; 1Sam 18:3; 2Sam 9; 1Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’ ” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.

New International Reader’s Version

1 Samuel 20:1-42

David and Jonathan

1David was in Naioth at Ramah. He ran away from there to where Jonathan was. He asked him, “What have I done? What crime have I committed? I haven’t done anything to harm your father. So why is he trying to kill me?”

2“That will never happen!” Jonathan replied. “You aren’t going to die! My father doesn’t do anything at all without letting me know. So why would he hide this from me? He isn’t going to kill you!”

3But David strongly disagreed. He said, “Your father knows very well that you are pleased with me. He has said to himself, ‘I don’t want Jonathan to know I’m planning to kill David. If he finds out, he’ll be very sad.’ But I’m very close to being killed. And that’s just as sure as the Lord and you are alive.”

4Jonathan said to David, “I’ll do anything you want me to do for you.”

5So David said, “Tomorrow is the time for the New Moon feast. I’m supposed to eat with the king. But let me go and hide in the field. I’ll stay there until the evening of the day after tomorrow. 6Your father might miss me. If he does, then tell him, ‘David begged me to let him hurry home to Bethlehem. A yearly sacrifice is being offered there for his whole family group.’ 7Your father might say, ‘That’s all right.’ If he does, it will mean I’m safe. But he might become very angry. If he does, you can be sure he’s made up his mind to harm me. 8Please be kind to me. You have made a covenant with me in front of the Lord. If I’m guilty, kill me yourself! Don’t hand me over to your father!”

9“I would never do that!” Jonathan said. “Suppose I had even the smallest clue that my father had made up his mind to harm you. Then I would tell you.”

10David asked, “Who will tell me if your father answers you in a mean way?”

11“Come on,” Jonathan said. “Let’s go out to the field.” So they went there together.

12Then Jonathan spoke to David. He said, “I promise you that I’ll find out what my father is planning to do. I’ll find out by this time the day after tomorrow. The Lord, the God of Israel, is my witness. Suppose my father has kind feelings toward you. Then I’ll send you a message and let you know. 13But suppose he wants to harm you. And I don’t let you know about it. Suppose I don’t help you get away in peace. Then may the Lord punish me greatly. May he be with you, just as he has been with my father. 14But always be kind to me, just as the Lord is. Be kind to me as long as I live. Then I won’t be killed. 15And never stop being kind to my family. Don’t stop even when the Lord has cut off every one of your enemies from the face of the earth.”

16So Jonathan made a covenant of friendship with David and his family. He said, “May the Lord hold David’s enemies responsible for what they’ve done.” 17Jonathan had David promise his friendship again because he loved him. In fact, Jonathan loved David just as he loved himself.

18Then Jonathan said to David, “Tomorrow is the time for the New Moon feast. You will be missed, because your seat at the table will be empty. 19Go to the place where you hid when all this trouble began. Go there the day after tomorrow, when evening is approaching. There’s a stone out there called Ezel. 20Wait by it. I’ll shoot three arrows to one side of the stone. I’ll pretend I’m practicing my shooting. 21Then I’ll send a boy out there. I’ll tell him, ‘Go and find the arrows.’ Suppose I say to him, ‘The arrows are on this side of you. Bring them here.’ Then come. That will mean you are safe. You won’t be in any danger. And that’s just as sure as the Lord is alive. 22But suppose I tell the boy, ‘The arrows are far beyond you.’ Then go. That will mean the Lord is sending you away. 23And remember what we talked about. Remember that the Lord is a witness between you and me forever.”

24So David hid in the field. When the time for the New Moon feast came, the king sat down to eat. 25He sat in his usual place by the wall. Jonathan sat across from him. Abner sat next to Saul. But David’s place was empty. 26Saul didn’t say anything that day. He said to himself, “Something must have happened to David to make him ‘unclean.’ That must be why he isn’t here.” 27But the next day, David’s place was empty again. It was the second day of the month. Finally, Saul spoke to his son Jonathan. He said, “Why hasn’t the son of Jesse come to the meal? He hasn’t been here yesterday or today.”

28Jonathan replied, “David begged me to let him go to Bethlehem. 29He said, ‘Let me go. Our family is offering a sacrifice in the town. My brother has ordered me to be there. Are you pleased with me? If you are, let me go and see my brothers.’ That’s why he hasn’t come to eat at your table.”

30Saul became very angry with Jonathan. He said to him, “You are an evil son. You have refused to obey me. I know that you are on the side of Jesse’s son. You should be ashamed of that. And your mother should be ashamed of having a son like you. 31You will never be king as long as Jesse’s son lives on this earth. And you will never have a kingdom either. So send someone to bring the son of Jesse to me. He must die!”

32“Why do you want to put him to death?” Jonathan asked his father. “What has he done?” 33But Saul threw his spear at Jonathan to kill him. Then Jonathan knew that his father wanted to kill David.

34So Jonathan got up from the table. He was very angry. On that second day of the feast, he refused to eat. He was very sad that his father was treating David so badly.

35The next morning Jonathan went out to the field to meet David. He took a young boy with him. 36He said to the boy, “Run and find the arrows I shoot.” As the boy ran, Jonathan shot an arrow far beyond him. 37The boy came to the place where Jonathan’s arrow had fallen. Then Jonathan shouted to him, “The arrow went far beyond you, didn’t it?” 38He continued, “Hurry up! Run fast! Don’t stop!” The boy picked up the arrow and returned to his master. 39The boy didn’t know what was going on. Only Jonathan and David knew. 40Jonathan gave his weapons to the boy. He told him, “Go back to town. Take the weapons with you.”

41After the boy had gone, David got up from the south side of the stone. He bowed down in front of Jonathan with his face to the ground. He did it three times. Then they kissed each other and cried. But David cried more than Jonathan did.

42Jonathan said to David, “Go in peace. In the name of the Lord we’ve promised to be friends. We have said, ‘The Lord is a witness between you and me. He’s a witness between your children and my children forever.’ ” Then David left, and Jonathan went back to the town.