1 Samweli 2 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 2:1-36

Maombi Ya Hana

12:1 Lk 1:46-55; Za 13:5; 33:21; 18:2; 89:17; 148:4; 6:8; Hes 10:35; Zek 10:7; Flp 4:6Kisha Hana akaomba na kusema:

“Moyo wangu wamshangilia Bwana,

katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu.

Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu,

kwa kuwa naufurahia wokovu wako.

22:2 Kut 15:11; 8:10; 33:22; Law 11:44; Isa 40:25; 46:5; Mwa 49:25; Kum 32:37; 2Sam 22:2-32; 23:2-3; Za 31:3; 71:3“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana,

hakuna mwingine zaidi yako;

hakuna Mwamba kama Mungu wetu.

32:3 Za 17:10; 31:18; 73:8; 75:4; 94:4; Yos 22:22; 1Sam 16:7; 1Fal 8:39; 1Nya 28:9; 2Nya 6:30; Mit 15:11; 24:11-12; Yer 11:20; 17:16“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo

wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi,

kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye,

na kwa yeye matendo hupimwa.

42:4 2Sam 1:27; Za 37:15; 46:9; 76:3; Ay 17:9; Isa 40:31; 41:1; 52:1; 57:10“Pinde za mashujaa zimevunjika,

lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.

52:5 Lk 1:53; Za 113:9; Isa 54:1; Yer 15:9; Gal 4:27Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe

ili kupata chakula,

lakini wale waliokuwa na njaa

hawana njaa tena.

Mwanamke yule aliyekuwa tasa

amezaa watoto saba,

lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi

amedhoofika.

62:6 Kum 32:39; Ay 5:18; Hos 6:1; Yn 5:25-29; 11:25, 26; Ufu 1:18Bwana huua na huleta uhai,

hushusha chini mpaka kaburini2:6 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. na hufufua.

72:7 Kum 8:18; Ay 5:11; 40:12; Za 75:7; Isa 2:12; 13:11; 22:19; Dan 4:37; Za 75:8Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha,

hushusha na hukweza.

82:8 Za 113:7-8; 72:12; 107:41; 145:14; 146:8; 104:5; Mit 8:29; Mt 23:12; 2Sam 7:8; Ay 36:7; 15:7; 38:4; Isa 22:23; 40:12; Yer 10:12; Eze 21:26; Yak 2:5; 1Fal 16:2Humwinua maskini kutoka mavumbini

na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu;

huwaketisha pamoja na wakuu

na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima.

“Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana;

juu yake ameuweka ulimwengu.

92:9 Za 91:12; 121:3; Mit 3:26; 2:8; Ay 10:22; 37:4-5; 38:1; Za 18:13; 29:3; 96:13; 98:9; 18:1; 21:1; 59:16; 89:24; Kum 33:17; Lk 1:69; Isa 66:6; 5:30; 8:22; 59:9; 60:2; Yer 13:16; Amo 5:18-20; Sef 1:14-15; Mt 8:12; 25:31-32; 1Sam 17:47; 2Sam 22:14Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake,

lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza.

“Si kwa nguvu mtu hushinda;

102:10 Za 96:13wale wampingao Bwana

wataharibiwa kabisa.

Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni;

Bwana ataihukumu miisho ya dunia.

“Atampa nguvu mfalme wake,

na kuitukuza pembe

ya mpakwa mafuta wake.”

112:11 Yos 18:25; Hes 16:9; 1Sam 3:1; 2:18Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.

Wana Waovu Wa Eli

122:12 Yer 2:8; 9:6; Kum 13:13; Rum 1:28Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana. 132:13 Kum 18:3; Law 7:29-36; 1Sam 2:12Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake. 142:14 Hes 15:30; Isa 22:14; Yer 7:16; Ebr 10:26-31Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo. 15Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”

162:16 Law 3:3, 14-16; 7:29-34Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”

172:17 Hes 14:11; Yer 7:21; Eze 22:26; Mal 2:7-9; 1Sam 2:22; Rut 1:17; Mt 26:63Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.

182:18 1Sam 22:18; 23:9; 2Sam 6:14; 1Nya 15:27; Mwa 18:25; 1Sam 16:10-12; Ay 1:21; 2:10; Za 39:9Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani. 192:19 1Sam 1:3; Mwa 18:25; 1Sam 18:14; 2Tim 4:22; 1Sam 9:6Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka. 202:20 1Sam 1:27; Lk 2:34; Amu 20:1Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani. 212:21 Mwa 21:1; Amu 13:24; Lk 1:80; 2:40Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.

222:22 Kut 38:8Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania. 23Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu. 24Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana. 252:25 Kut 4:21; 32:10; Yos 11:20; Hes 11:2; 1Sam 3:14; 1Fal 13:6; Ay 9:33; Za 106:30; Isa 1:18; 22:14; Yer 15:1; Ebr 10:26Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.

262:26 Amu 13:24; Lk 2:52; Mit 3:4; Mdo 2:47; Rum 14:18Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.

Unabii Dhidi Ya Nyumba Ya Eli

272:27 Kum 33:1; Amu 13:6; Kut 4:14-16; 1Fal 13:1Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao? 282:28 Kut 28:1; 30:7; 1Sam 22:18; 23:6-9; 30:7; Law 7:35-36; 8:7-8Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli. 292:29 Kum 12:5; Mt 10:37Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’

302:30 Kut 29:19; Za 50:23; 91:15; Mit 8; 17; Isa 53:3; Neh 3:6; Mal 2:9; Yer 18:10; 1Nya 15:2; Za 18:20; 91:14; Yn 5:44; 12:26; 1Pet 1:7; Hes 11:20“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa. 312:31 1Sam 4:11-18; 22:16-20Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee 322:32 1Sam 4:3; 22:17-20; Yer 7:12-14; 1Fal 2:26-27; Zek 8:4nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee. 332:33 Yer 29:32; Mal 2:12Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.

342:34 Kum 13:4; 1Sam 4:11; 1Fal 13:3“ ‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja. 352:35 1Nya 16:39; 29:22; 2Sam 8:17; 20:25; 1Fal 2:35; 4:4; Eze 44:15-16; 1Sam 10:1; 16:13; 2Sam 2:4; 12:7; 23:1; 1Fal 1:34; Za 89:20Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima. 362:36 Eze 44:10-14; 1Sam 3:12; 1Fal 2:27Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.” ’ ”

Japanese Contemporary Bible

サムエル記Ⅰ 2:1-36

2

ハンナの祈り

1ハンナは祈りました。

「ああ、うれしゅうございます、主よ。

こんなにも祝福していただいて。

私は敵にはっきり答えることができます。

主が悩みを取り去ってくださいましたから。

私は喜びでいっぱいです。

2主のように聖なるお方はありません。

あなたのほかに神はないのです。

私たちの神のような大岩はありません。

3思い上がりも、尊大さも許されません。

主は何もかもご存じで、

すべての行為をおさばきになるのです。

4力を誇った者が弱くなり、

弱かった者が今や強くなっています。

5満ち足りていた者が今は飢え、

飢えていた者が満ち足りています。

不妊の女が今は七人の子持ちとなり、

多産の女がもう子を産めません。

6主は殺し、

主はいのちをお与えになります。

7主は、ある人々を貧しくし、

また、ある人々を裕福になさいます。

主はある者を倒し、

また、ある者を立ち上がらせてくださいます。

8主は、貧しい者をちりの中から、灰の山から引き上げ、

高貴な者のように取り扱い、

栄光の座につかせてくださいます。

この世はすべて主のものですから。

主はこの世界をふさわしくされました。

9主は信仰者を守られます。

しかし、悪者は暗闇に葬り去られます。

だれも自力でははい上がれません。

10主は手向かう者を打ちのめし、

天から彼らに雷鳴をとどろかせます。

主は地を隅々までさばき、

ご自分が選んだ王に特別な力を授け、

主に油注がれた者に大きな栄誉をお与えになるのです。」

11そののちエルカナとハンナは、サムエルを残してラマに帰りました。幼いサムエルは、祭司エリのもとで主に仕える者となりました。

エリの息子たち

12ところでエリの息子たちは、主をないがしろにする、不道徳でよこしまな者たちでした。 13-14いけにえをささげている人がいると、しもべを送り、いけにえの動物の肉が煮えている大なべの中に、そのしもべが三つ又の肉刺しを突き刺して、これらはみなエリの息子のものだと宣告しました。彼らは、いけにえをささげて礼拝するためにシロにやって来るすべてのイスラエル人に対して、このように行っていました。 15時には、祭壇で脂肪を焼く儀式が行われないうちから、しもべをやって、生の肉をよこせと言うことさえありました。焼き肉にして食べるためでした。

16いけにえをささげている人が、「いくらでもお取りになってけっこうです。しかし、まず〔律法のとおりに〕脂肪をすっかり焼いてしまわなければなりません」と答えると、使いの者はこう言うのです。「いや、たった今ほしいのだ。つべこべ言うなら、力ずくでももらうぞ。」

17こんなふうに、彼らは主の前に非常に大きな罪を犯しました。主へのささげ物を侮るようなことをしたからです。

18サムエルはまだ子どもでしたが、一人前の祭司のように、小さな亜麻布の儀式服を着て、主に仕えていました。 19毎年、母親が小さな上着をこしらえ、夫とともに、いけにえをささげに来る時に持って来てくれていたのです。 20エルカナとハンナが家路につく前に、エリは二人を祝福し、主にささげた子の代わりに、もっと子どもが授かるよう主に願い求めてくれました。 21それで主はハンナに、三人の息子と二人の娘を授けました。一方、少年サムエルは、主のもとで成長していきました。

22エリはすでに高齢に達していましたが、身辺の出来事についてはよくわきまえていました。例えば、息子たちが幕屋(聖所)の入口で仕えている女たちを誘惑したことも、ちゃんと知っていました。

23-25エリは息子たちを呼びつけて注意しました。「私は民から、おまえたちのおぞましい悪行についてさんざん聞かされた。よくも民を罪に惑わすようなことをしてくれたものだ。少しの罪でもきびしい罰が下るのに、主に対するおまえたちの罪には、どれほど重い罰が下るか知れたものではない。」

しかし、息子たちは耳を貸そうともしませんでした。というのは、主がすでに、この二人のいのちを絶とうとしていたからです。

26一方、少年サムエルはすくすく育ち、人からも神からも愛されました。

エリへの預言

27ある日、一人の預言者が来て、エリに主のことばを伝えました。「イスラエルの民がエジプトで奴隷だった時、わたしははっきり力を示したではないか。 28そして、なみいる同胞の中からあなたの先祖レビを選んで、祭司としたのではなかったか。その務めは、わたしの祭壇でいけにえをささげ、香をたき、祭司の服を着て仕えることだった。わたしは、あなたがた祭司にも、いけにえのささげ物を分け与えたではないか。 29それなのに、どうしてささげ物を一人占めしようとするのか。わたしよりも息子のほうが大事なのか。よくも親子して最上のささげ物によって肥え太ったものだ。

30それゆえ、イスラエルの神であるわたしは、こう宣言する。レビ族の一門であるあなたの家系が常に祭司となると約束したのは確かだが、今や、それがいつまでも続くと考えたら、大きな間違いである。わたしは、わたしを重んじる者を重んじる。わたしを侮る者は、わたしも軽んじる。 31あなたの家系は断絶する。これ以上、祭司を務めるには及ばない。家族全員、長寿を全うせずに死ぬのだ。よわいを重ねる者は一人もいない。 32あなたがたは、わたしが民に与える繁栄をうらやむだろう。あなたの一族は苦難と窮乏に陥る。だれ一人、長生きできない。 33かろうじて生き残った者も、悲嘆にくれて日を過ごす。子どもたちは、剣によって殺される。 34わたしのことばに偽りがないことを見せよう。二人の息子ホフニとピネハスは、同じ日に死ぬことになる。

35代わりに、わたしは一人の忠実な祭司を起こす。彼はわたしに仕え、わたしが告げるとおり正しく行うだろう。その子孫を末代まで祝福し、その一族を王の前に永遠の祭司とする。 36だから、あなたの子孫はみな、彼に頭を下げ、金と食物を乞うようになる。彼らはこう言ってすがるだろう。『どうか、祭司のどんな仕事でもさせてください。何とか食べていきたいのです』と。」