1 Samweli 17 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 17:1-58

Daudi Na Goliathi

117:1 1Sam 13:5; Yos 15:35; 2Nya 28:18; Yos 10:10, 11Wakati huu Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka. 217:2 1Sam 21:9Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti. 3Wafilisti wakawa katika kilima kimoja na Waisraeli katika kilima kingine, hilo bonde likiwa kati yao.

417:4 1Sam 21:9; Yos 11:21-22; 2Sam 21:19; 1Nya 20:5; 8:13; 18:1; 2Nya 26:6; Amo 6:2Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.17:4 Dhiraa sita na shibiri moja ni sawa na mita 3, au futi 9 na inchi 8. 5Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.17:5 Shekeli 15,000 ni sawa na kilo 50. 617:6 1Sam 18:10Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake. 717:7 2Sam 21:19; 1Nya 11:23; 20:5Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita.17:7 Shekeli 600 ni sawa na kilo 7. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.

817:8 2Sam 2:12-17; 1Sam 8:17; 1Nya 21:3Goliathi alisimama na kuwapigia kelele majeshi ya Israeli, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi. 917:9 1Sam 11:1Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini kama nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu na mtatutumikia.” 1017:10 2Sam 21:21; Hes 23:7-8; Neh 2:19Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.” 11Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.

1217:12 Mwa 35:16; 48:7; Za 132:6; Rut 4:17, 22; 1Sam 16; 11; Mwa 35:19; 1Sam 16:10, 11; 1Nya 2:13Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee tena wa umri mkubwa. 1317:13 1Sam 16:6-9; 1Nya 2:13Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama. 14Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli, 1517:15 1Sam 16:19; Mwa 37:2lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.

16Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionyesha.

1717:17 Mwa 37:14Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa17:17 Efa moja ni sawa na kilo 22. ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao. 1817:18 Law 19:36; 23:14; 1Sam 25:18Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao. 19Wao wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”

20Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga kelele za vita. 21Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana. 2217:22 Mwa 37:14Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake. 2317:23 Mwa 43:27; Amu 18:15Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia. 24Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.

2517:25 Yos 1:11; 15:16Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”

2617:26 1Sam 18:17; 8:15; Yos 15:16; Kum 5:26; Yer 10:10Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atafanyiwa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”

27Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”

2817:28 Mwa 27:41; Mit 18:19; Mwa 37:8, 11; Mt 10:38; Mwa 37:4; Mhu 4:4; Mk 3:21Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”

2917:29 Mit 15:1Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.” 30Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo. 31Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.

3217:32 Kum 20:3; Za 18:45; Isa 7:4; Yer 4:9; 38:4; Dan 11:30; Hes 13:30; 14:9; Ebr 12:12; Isa 30:3Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako atakwenda kupigana naye.”

3317:33 Hes 13:31; Kum 9:2Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”

3417:34 Ay 10:16; Isa 31:4; Yer 49:19; Hos 13:8; Amo 3:12Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Wakati simba au dubu alikuja na kuchukua kondoo kutoka kundi, 3517:35 Amu 14:6nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua. 3617:36 1Nya 11:22Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai. 3717:37 2Kor 1:10; 2Tim 4:17; 1Sam 16:18; 18:12; 1Nya 22:11, 16; 1Sam 7:12; Za 18:16, 17Bwana ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.”

Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Bwana na awe pamoja nawe.”

3817:38 Mwa 41:42Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake. 39Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo.

Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua. 40Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.

41Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi. 4217:42 1Sam 16:12; Za 123:3-4; Mit 16:18; 1Kor 1:27, 28Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau. 4317:43 1Sam 24:14; 2Sam 3:8; 9:8; 2Fal 8:13Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake. 4417:44 Mwa 40:19; Ufu 19:7; 2Sam 21:10; Yer 34:20; 1Fal 20:10-11Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”

4517:45 Kum 20:1; 2Nya 13:12; 14:11; 32:8; Za 20:7-8; 124:8; Ebr 11:32-34; 2Sam 22:33, 35; 2Nya 32:8; Za 124:8; 125:1; Mit 18:10; Flp 4:13Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana. 4617:46 1Sam 14:12; Kum 28:26; Yos 4; 24; Isa 11:9; 1Fal 18:36; 2Fal 5:8; 19:19; Isa 37:20; Za 44:6-7; Zek 4:6Siku hii leo Bwana atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli. 4717:47 1Sam 25:29; 2Sam 23:21; Za 44:6, 7; Hos 1:7; Zek 4:6; 2Nya 20:15Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Bwana, naye atawatia wote mikononi mwetu.”

48Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye. 49Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka chini kifudifudi.

5017:50 Ebr 11:34; 1Sam 21:9; 22:10; Amu 3:31; 15:15; 2Sam 23:21Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mikononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.

5117:51 Ebr 11:34Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga.

Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia. 5217:52 Yos 15:11; 15:36Ndipo watu wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti mpaka kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni. 53Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao. 54Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.

5517:55 1Sam 16:21; 26:5Sauli alipomwona Daudi anakwenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?”

Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”

56Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”

57Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.

5817:58 Rut 4:17Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?”

Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記上 17:1-58

大衛迎戰歌利亞

1非利士人在猶大梭哥招聚軍隊,準備作戰。他們在梭哥亞西加之間的以弗·大憫紮營。 2掃羅以色列人也聚集起來在以拉谷安營,擺好陣勢準備迎戰。 3雙方的軍隊在兩邊的山上對峙,中間隔著山谷。 4非利士營中有個名叫歌利亞的巨人出來討戰。他來自迦特,身高三米, 5頭戴銅盔,身穿重達五十七公斤的鎧甲, 6腿上有銅護膝,肩背銅戟。 7戟柄粗如織布機的軸,鐵戟頭重七公斤。有衛士拿著他的盾牌走在前面。 8他挑戰以色列人,說:「你們為什麼列陣打仗呢?我是非利士人,你們是掃羅的僕人,你們選一個人下來跟我一比高下。 9如果他打得過我,將我殺了,我們就做你們的奴隸。但如果我戰勝他,把他殺了,你們就要做我們的奴隸,服侍我們。 10我今天向以色列軍隊罵陣,你們找一個人出來跟我比個高下吧!」 11掃羅和所有以色列人聽了非利士人的這些話,都嚇得驚恐不已。

12大衛以法他耶西的兒子。掃羅執政期間,耶西已經年紀老邁,住在猶大伯利恆,有八個兒子。 13他的三個兒子已經跟隨掃羅去打仗了,他們是長子以利押、次子亞比拿達和三子沙瑪14大衛年紀最小,他的三個哥哥跟隨掃羅期間, 15他有時去掃羅的軍營,有時回伯利恆為他父親放羊。 16非利士人早晚都出來罵陣,長達四十天。

17一天,耶西大衛說:「你帶上十公斤烤麥和十個餅,趕快到軍營中送給你的哥哥們。 18再帶十塊奶餅送給他們的千夫長,看望一下他們,帶個信兒回來。 19他們跟隨掃羅率領的以色列軍在以拉谷跟非利士人打仗。」

20大衛清早起來把羊交給一個牧人看顧,然後照父親的吩咐帶著食物出發了。他來到軍營的時候,大軍正吶喊著出戰。 21以色列人與非利士人擺好陣勢,兩軍對壘。 22大衛把帶來的東西交給負責看守的人保管,自己跑到陣中去問候哥哥們。 23他們正在交談的時候,非利士軍中的迦特歌利亞出來像往常一樣向以色列軍罵陣,大衛都聽見了。 24以色列人一看見歌利亞都競相奔逃,極其害怕。 25以色列人彼此議論說:「看那個人!他是來向以色列軍罵陣的。誰要能殺死他,王必有重賞,還會把女兒嫁給他為妻,並免去他父親家在以色列應繳的賦稅。」 26大衛問站在旁邊的人:「如果有人殺了這非利士人,洗掉以色列人的羞辱,他會得到什麼呢?這個未受割禮的非利士人是誰?竟敢向永活上帝的軍隊罵陣!」 27他們就把剛才的話一一告訴大衛

28大衛的長兄以利押聽見他跟人說話,就憤怒地對他說:「你來這裡做什麽?你把曠野的那幾隻羊交給誰了?我知道你驕傲自大,心懷惡意,你來只是想看打仗。」 29大衛說:「我做錯了什麼?我問一下都不行嗎?」 30他又去問其他人同樣的問題,得到了同樣的答覆。 31有人聽見了大衛的話,就去告訴掃羅掃羅便派人來召大衛32大衛掃羅說:「大家不要因這個非利士人而喪膽,讓僕人去戰他。」 33掃羅說:「你不能去,你年紀還小,他卻是一個久經沙場的戰士。」 34大衛說:「我一直替父親放羊,有時候獅子或熊會從羊群中叼走羊, 35我會去追打牠,把羊從牠口中救出來。如果牠起來攻擊我,我就揪著牠的鬍子把牠打死。 36我曾打死過獅子和熊。這未受割禮的非利士人竟敢向永活上帝的軍隊罵陣,他的下場也必像獅子和熊一樣。 37耶和華曾經從獅子和熊的利爪下拯救我,祂也必從非利士人手中拯救我。」掃羅大衛說:「去吧,願耶和華與你同在。」 38掃羅把自己的戰袍給大衛穿上,又給他戴上自己的頭盔,穿上自己的鎧甲。 39大衛把刀挎在戰袍上,試著走了幾步,卻不習慣這種裝束,就對掃羅說:「我穿著這些無法作戰,因為我不習慣。」他便摘下頭盔,卸下鎧甲, 40然後拿著杖,在溪裡撿了五塊光滑的石頭放進牧人用的袋子,拿著投石器向歌利亞走去。

41歌利亞也迎著大衛走來,衛士拿著他的盾牌走在前面。 42歌利亞大衛是個面色紅潤、相貌英俊的少年,就藐視他。 43他對大衛說:「你拿著棍子來戰我,難道我是一條狗嗎?」他就憑自己的神明咒詛大衛44又說:「你過來,我要把你的肉丟給天上的飛禽和地上的走獸。」 45大衛答道:「你是靠刀槍劍戟來攻擊我,我是靠萬軍之耶和華的名,就是你所蔑視的以色列軍隊的上帝來迎戰你。 46今天,耶和華必把你交在我手中,我必殺死你,砍掉你的頭,用非利士軍兵的屍體餵天上的飛禽和地上的走獸,使普天下都知道以色列有上帝。 47這裡所有的人都必知道耶和華拯救人不靠刀槍,因為祂掌管戰爭的勝負。祂必把你們交在我們手中。」 48歌利亞迎面走來的時候,大衛就飛快地跑上去應戰, 49他從袋裡拿出一塊石子用投石器猛力拋去,石子擊中歌利亞的額頭,嵌了進去,他迎面栽倒在地。

50大衛就這樣不用刀劍,只用投石器和一塊石子戰勝了那個非利士人,殺死了他。 51大衛跑到那非利士人身邊,從他刀鞘裡拔出刀殺了他,並割下他的頭顱。非利士人看見自己的英雄死了,紛紛逃跑。 52以色列人和猶大人乘勢吶喊,追殺非利士人,直追到迦特以革倫的城門。通往迦特以革倫沙拉音大道上到處是非利士人的屍體。 53以色列軍隊追殺非利士人回來,又擄掠了他們的營地。 54大衛把那非利士人的頭顱帶到耶路撒冷,把那人的兵器存放在自己的帳篷中。

55掃羅看見大衛出去迎戰歌利亞,就問押尼珥元帥:「押尼珥啊,那少年是誰的兒子?」押尼珥答道:「王啊,我向你發誓,我真的不知道。」 56掃羅王說:「你去查查他是誰的兒子。」 57大衛殺了歌利亞回來,押尼珥就把他帶到掃羅那裡,他手上還拿著那非利士人的頭顱。 58掃羅問他:「年輕人,你是誰的兒子?」大衛答道:「我是你僕人伯利恆耶西的兒子。」