1 Samweli 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 1:1-28

Kuzaliwa Kwa Samweli

11:1 Mwa 18:25; 1Sam 9:5; Yos 17:17-18; 21:20-22; 1Nya 6:27-34; Rut 1:2Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu. 21:2 Mwa 4:19; Kum 21:15-17Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.

31:3 Kut 23:14; 1Sam 2:19; 20:6; Lk 2:41; Kum 12:5-7; 1Sam 2:31; 14:3; Yos 18:1; Amu 18:31; Za 78:60; Yer 7:12-14Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana. 41:4 Law 7:15-18; Kum 12:17-18; Mwa 29:34Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake. 51:5 Mwa 37:3; 11:30; 29:31Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo. 61:6 Mwa 16:4-5Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi. 71:7 2Sam 12:17; Za 102:4; Kut 23:14; Kum 16:16; Kut 23:14Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula. 81:8 Rut 4:15Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”

91:9 1Sam 3:3Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana. 101:10 Ay 3:20; 7:11; 10:1; 21:25; 23:2; 27:2; Isa 38:15; Yer 20:18Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana. 111:11 Amu 11:30; 13:7; 13:5; Lk 1:15; Mwa 17:1; 8:1; Za 24:10; 46:7; Isa 1:9; Hes 6:1-21; 21:2; 30:3-8; Mhu 5:4; Mwa 29:32; Kut 4:31Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”

12Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake. 13Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa 14naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”

151:15 2Fal 4:27; Za 42:4; 62:8; Mao 2:19Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana. 161:16 Za 55:2; 2Kor 6:15Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”

171:17 Hes 6:26; 1Sam 20:42; 2Fal 5:19; Mdo 15:33; Mwa 25:21; Za 20:3-5; Mwa 33:15; Yn 16:24Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”

181:18 Mwa 18:3; Rut 2:13; Rum 15:13; Ufu 2:13; Mhu 9:7Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.

191:19 Yos 18:25; Mwa 8; 1; 29:31Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka. 201:20 Mwa 17:19; 29:32; 30:6; Kut 2:10; Mt 1:21; 1Sam 7:5; 12:23; 1Nya 6:27; Yer 15:1; Ebr 11:32Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”

Hana Anamweka Samweli Wakfu

211:21 Mwa 28:20; Hes 30:2; Kum 12:11Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake, 221:22 Lk 2:22; Kut 13:2; 1Sam 2:11; 3:1Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”

231:23 Mwa 25:21; 21:8; Hes 30:7; 2Sam 7:25Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.

241:24 Hes 15:8-10Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga1:24 Efa moja ya unga ni sawa na kilo 22. na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo. 25Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli, 26naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana. 271:27 1Sam 2:20; Za 66:19-20; Mit 7:7Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba. 281:28 Amu 13:7; Mwa 24:26, 52Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.

King James Version

1 Samuel 1:1-28

1Now there was a certain man of Ramathaim-zophim, of mount Ephraim, and his name was Elkanah, the son of Jeroham, the son of Elihu, the son of Tohu, the son of Zuph, an Ephrathite: 2And he had two wives; the name of the one was Hannah, and the name of the other Peninnah: and Peninnah had children, but Hannah had no children. 3And this man went up out of his city yearly to worship and to sacrifice unto the LORD of hosts in Shiloh. And the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, the priests of the LORD, were there.1.3 yearly: Heb. from year to year

4¶ And when the time was that Elkanah offered, he gave to Peninnah his wife, and to all her sons and her daughters, portions: 5But unto Hannah he gave a worthy portion; for he loved Hannah: but the LORD had shut up her womb.1.5 worthy: or, double 6And her adversary also provoked her sore, for to make her fret, because the LORD had shut up her womb.1.6 provoked: Heb. angered 7And as he did so year by year, when she went up to the house of the LORD, so she provoked her; therefore she wept, and did not eat.1.7 when…: or, from the time that she, etc: Heb. from her going up 8Then said Elkanah her husband to her, Hannah, why weepest thou? and why eatest thou not? and why is thy heart grieved? am not I better to thee than ten sons?

9¶ So Hannah rose up after they had eaten in Shiloh, and after they had drunk. Now Eli the priest sat upon a seat by a post of the temple of the LORD. 10And she was in bitterness of soul, and prayed unto the LORD, and wept sore.1.10 in…: Heb. bitter of soul 11And she vowed a vow, and said, O LORD of hosts, if thou wilt indeed look on the affliction of thine handmaid, and remember me, and not forget thine handmaid, but wilt give unto thine handmaid a man child, then I will give him unto the LORD all the days of his life, and there shall no razor come upon his head.1.11 a man…: Heb. seed of men 12And it came to pass, as she continued praying before the LORD, that Eli marked her mouth.1.12 continued…: Heb. multiplied to pray 13Now Hannah, she spake in her heart; only her lips moved, but her voice was not heard: therefore Eli thought she had been drunken. 14And Eli said unto her, How long wilt thou be drunken? put away thy wine from thee. 15And Hannah answered and said, No, my lord, I am a woman of a sorrowful spirit: I have drunk neither wine nor strong drink, but have poured out my soul before the LORD.1.15 of a sorrowful…: Heb. hard of spirit 16Count not thine handmaid for a daughter of Belial: for out of the abundance of my complaint and grief have I spoken hitherto.1.16 complaint: or, meditation 17Then Eli answered and said, Go in peace: and the God of Israel grant thee thy petition that thou hast asked of him. 18And she said, Let thine handmaid find grace in thy sight. So the woman went her way, and did eat, and her countenance was no more sad.

19¶ And they rose up in the morning early, and worshipped before the LORD, and returned, and came to their house to Ramah: and Elkanah knew Hannah his wife; and the LORD remembered her. 20Wherefore it came to pass, when the time was come about after Hannah had conceived, that she bare a son, and called his name Samuel, saying, Because I have asked him of the LORD.1.20 when…: Heb. in revolution of days1.20 Samuel: that is, Asked of God 21And the man Elkanah, and all his house, went up to offer unto the LORD the yearly sacrifice, and his vow. 22But Hannah went not up; for she said unto her husband, I will not go up until the child be weaned, and then I will bring him, that he may appear before the LORD, and there abide for ever. 23And Elkanah her husband said unto her, Do what seemeth thee good; tarry until thou have weaned him; only the LORD establish his word. So the woman abode, and gave her son suck until she weaned him.

24¶ And when she had weaned him, she took him up with her, with three bullocks, and one ephah of flour, and a bottle of wine, and brought him unto the house of the LORD in Shiloh: and the child was young. 25And they slew a bullock, and brought the child to Eli. 26And she said, Oh my lord, as thy soul liveth, my lord, I am the woman that stood by thee here, praying unto the LORD. 27For this child I prayed; and the LORD hath given me my petition which I asked of him: 28Therefore also I have lent him to the LORD; as long as he liveth he shall be lent to the LORD. And he worshipped the LORD there.1.28 lent him: or, returned him, whom I have obtained by petition1.28 he shall…: or, he whom I have obtained by petition shall be returned