1 Petro 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Petro 5:1-14

Kulichunga Kundi La Mungu

15:1 Mdo 11:30; Lk 24:48; 1Pet 4:13; Ufu 1:9Kwa wazee waliomo miongoni mwenu, nawasihi mimi nikiwa mzee mwenzenu, shahidi wa mateso ya Kristo, na mshiriki katika utukufu utakaofunuliwa: 25:2 Yn 21:6; 1Tim 3:3lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mkitumika kama waangalizi, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, kama Mungu anavyowataka mwe; si kwa tamaa ya fedha, bali mlio na bidii katika kutumika. 35:3 Eze 34:4; Mt 20:25-28; Flp 3:17; 1Tim 4:12Msijifanye mabwana juu ya wale walio chini ya uangalizi wenu, bali kuweni vielelezo kwa hilo kundi. 45:4 1Kor 9:25; Ebr 13:20; 1Kor 9:25; 2Tim 4:8; Yak 1:12; 1Pet 1:4Naye Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtapokea taji ya utukufu isiyoharibika.

55:5 Efe 5:21; Mit 3:34; Yak 4:6Vivyo hivyo, ninyi mlio vijana watiini wazee. Nanyi nyote imewapasa kujivika unyenyekevu kila mtu kwa mwenzake, kwa kuwa,

“Mungu huwapinga wenye kiburi,

lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

65:6 Yak 4:10Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake. 75:7 Mit 27:5; Mt 6:25; Ebr 13:5Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo yenu.

85:8 Ay 1:7; Lk 21:34, 36; 1The 5:6; 1Pet 4:7; Ufu 12:12Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mtu ili apate kummeza. 95:9 Yak 4:7; Kol 2:5; Mdo 14:22Mpingeni, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kwamba mateso kama hayo yanawapata ndugu zenu pote duniani.

105:10 2Kor 4:17; 2The 2:17Nanyi mkiisha kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atawarejesha na kuwatia nguvu, akiwaimarisha na kuwathibitisha. 115:11 Rum 11:36; 1Pet 4:11; Ufu 1:6Uweza una yeye milele na milele. Amen.

Salamu Za Mwisho

125:12 2Kor 1:19; Ebr 13:22Kwa msaada wa Silvano,5:12 Yaani Sila. ambaye ninamhesabu kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia waraka huu mfupi ili kuwatia moyo, na kushuhudia kwamba hii ni neema halisi ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo.

135:13 Mdo 12:12Kanisa lililoko Babeli, lililochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu; vivyo hivyo mwanangu Marko anawasalimu. 145:14 Rum 16:16; Efe 6:23Salimianeni kwa busu la upendo.

Amani iwe nanyi nyote mlio katika Kristo.

New International Reader’s Version

1 Peter 5:1-14

To Older and Younger Believers

1I’m speaking to the elders among you. I was a witness of Christ’s sufferings. And I will also share in the glory that is going to come. I’m making my appeal to you as one who is an elder together with you. 2Be shepherds of God’s flock, the believers under your care. Watch over them, though not because you have to. Instead, do it because you want to. That’s what God wants you to do. Don’t do it because you want to get money in dishonest ways. Do it because you really want to serve. 3Don’t act as if you were a ruler over those under your care. Instead, be examples to the flock. 4The Chief Shepherd will come again. Then you will receive the crown of glory. It is a crown that will never fade away.

5In the same way, I’m speaking to you who are younger. Follow the lead of those who are older. All of you, put on a spirit free of pride toward one another. Put it on as if it were your clothes. Do this because Scripture says,

“God opposes those who are proud.

But he gives grace to those who are humble.” (Proverbs 3:34)

6So make yourselves humble. Put yourselves under God’s mighty hand. Then he will honor you at the right time. 7Turn all your worries over to him. He cares about you.

8Be watchful and control yourselves. Your enemy the devil is like a roaring lion. He prowls around looking for someone to swallow up. 9Stand up to him. Remain strong in what you believe. You know that you are not alone in your suffering. The family of believers throughout the world is going through the same thing.

10God always gives you all the grace you need. So you will only have to suffer for a little while. Then God himself will build you up again. He will make you strong and steady. And he has chosen you to share in his eternal glory because you belong to Christ. 11Give him the power for ever and ever. Amen.

Final Greetings

12I consider Silas to be a faithful brother. With his help I have written you this short letter. I have written it to encourage you. And I have written to speak the truth about the true grace of God. Remain strong in it.

13The members of the church in Babylon send you their greetings. They were chosen together with you. Mark, my son in the faith, also sends you his greetings.

14Greet each other with a kiss of friendship.

May God give peace to all of you who believe in Christ.