1 Petro 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Petro 1:1-25

Salamu

11:1 2Pet 1:1; Mt 24:22; Mdo 16:7Petro, mtume wa Yesu Kristo:

Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia. 21:2 Rum 8:29; 2The 2:13; Ebr 10:22; 12:24Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake:

Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.

Tumaini Lenye Uzima

31:3 1Kor 1:3; Efe 1:3; Tit 3:5; Yak 1:18; 1Pet 3:21Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, 41:4 1Tim 4:8; Mdo 20:32; Rum 8:17; 1Pet 5:4; Kol 1:5ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu, 51:5 1Sam 2:9; Yn 10:28; Rum 11:14; 8:18ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho. 61:6 Rum 5:2; 1Pet 5:10; 4:12Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi. 71:7 Mit 17:3; Isa 48:10; 1The 2:19Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa. 81:8 Yn 20:29; 1Yn 4:10; 2Kor 5:7; Ebr 11:1, 27Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka. 91:9 Rum 6:22Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.

101:10 Mt 22:24; 3:17Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa, 111:11 Mdo 16:7; Za 22:1; Isa 52:13; 53:12; Lk 24:26wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata. 121:12 Efe 3:10; Lk 2:13Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.

Mwito Wa Kuishi Maisha Matakatifu

131:13 Mdo 24:25; 1Pet 1:3, 21; Ebr 3:6; 1Pet 1:7, 10; 1Kor 1:7; Efe 5:19; Kol 3:16Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa. 141:14 Rum 12:2; Efe 4:18Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga. 151:15 Isa 35:8; 1The 4:7; 1Yn 3:3Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote. 161:16 Law 19:2; 20:7Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”

171:17 Mdo 10:34; Ebr 12:28Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni. 181:18 Mt 20:28; 1Kor 6:20Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu, 191:19 Yn 1:29; Kut 12:5bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa. 201:20 Mt 25:34; Ebr 9:26Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu. 211:21 Rum 10:9Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.

221:22 Yak 4:8; Rum 12:10; Ebr 13:1Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni. 231:23 Yn 1:13; Ebr 4:12Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. 241:24 Za 103:15; Isa 40:6Maana,

“Wanadamu wote ni kama majani,

nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni;

majani hunyauka na maua huanguka,

251:25 Isa 40:6-8; Yak 1:10-11lakini neno la Bwana ladumu milele.”

Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

彼得前書 1:1-25

1我是耶穌基督的使徒彼得,寫信給蒙上帝揀選,寄居在本都加拉太加帕多迦亞細亞庇推尼各地的人。 2你們蒙揀選是按照父上帝預先定好的旨意,藉著聖靈得以聖潔,好順服耶穌基督,並靠祂的血得到潔淨。

願上帝賜給你們豐豐富富的恩典和平安!

活潑的盼望

3願頌讚歸於我們主耶穌基督的父上帝!祂有無窮的憐憫,藉著耶穌基督從死裡復活使我們獲得重生,有活潑的盼望, 4可以承受那不會朽壞、沒有污點、不會衰殘、為你們存留在天上的產業。 5你們這些因信而蒙上帝用大能保守的人,必能得到那已經預備好、在末世要顯明的救恩。

6為此,即使現今你們必須暫時在百般試煉中忍受痛苦,也要滿懷喜樂。 7這樣,你們的信心經過試驗便顯明是真實的,比那經過火煉仍會壞掉的金子更加寶貴,使你們可以在耶穌基督顯現時得到稱讚、榮耀和尊貴。 8你們雖然沒有見過基督,卻愛祂;雖然現在看不見祂,卻信祂,並且有無法形容、充滿榮耀的喜樂。 9因為你們得到了信心帶來的果效,就是你們的靈魂得救。

10有關這救恩,那些預言恩典要臨到你們的眾先知早已詳細尋求查考了。 11基督的靈曾在他們心中指示他們,預言基督要受苦,然後得榮耀。他們便詳細查考這些事會在什麼時候、什麼情況下發生。 12他們得到啟示,知道他們傳講這些事不是為了自己,而是為了你們。現在,那些靠著從天上差來的聖靈向你們傳福音的人,已經將這些事傳給你們了。連天使也想把這些事看個明白。

要聖潔像主

13所以,要預備好你們的心,謹慎自律,專心盼望耶穌基督顯現時要帶給你們的恩典。 14你們既是順服的兒女,就不要再像從前無知的時候那樣放縱私慾。 15那呼召你們的是聖潔的,你們在一切事上也要聖潔。 16因為聖經上說:「你們要聖潔,因為我是聖潔的。」

17既然你們稱呼那位按各人的行為公正無私地審判人的上帝為父,就應該存著敬畏的心過你們在世上寄居的日子。 18要知道,你們從傳統的、沒有意義的生活中被救贖出來,不是靠金銀等會朽壞的東西, 19而是靠無瑕無疵的代罪羔羊——基督的寶血。 20基督是上帝在創世以前預先揀選的,卻在這末世為你們顯現。 21你們藉著基督信了使祂從死裡復活、賜祂榮耀的上帝,所以,你們的信心和盼望都在於上帝。

22你們既因順服真理,潔淨了自己的心,能夠真誠地愛弟兄姊妹,就當以清潔的心彼此切實相愛。 23你們獲得重生,不是藉著會腐爛的種子,而是藉著不會腐爛的種子——上帝活潑永存的道。 24因為

「芸芸眾生盡如草,

榮華不過草上花;

草必枯乾花必殘,

25唯有主道永長存。」

這道就是傳給你們的福音。