1 Nyakati 29 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 29:1-30

Matoleo Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Hekalu

129:1 1Fal 3:7; 2Nya 13:7; Mit 4:3; 1Nya 22:5Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana. 229:2 Ezr 6:5; Ufu 21:18; Hag 2:8; Isa 54:11; 1Nya 22:2-5; Kut 28:9Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno. 329:3 2Nya 24:10; Za 28:9; 2Nya 35:8; Za 26:8; 27:4; Mit 3:9Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu: 429:4 Mwa 10:29; 1Nya 22:14; Ay 22:24; 1Fal 9:28; 2Nya 8:18talanta 3,00029:4 Talanta 3,000 za dhahabu sawa na tani 110. za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,00029:4 Talanta 7,000 za fedha ni sawa na tani 260. za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu, 5kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”

629:6 1Nya 28:1; Kut 36:2; Ezr 7:15Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.

7Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,00029:7 Talanta 5,000 za dhahabu ni sawa na tani 190. na darkoni 10,00029:7 Darkoni 10,000 za dhahabu ni sawa na kilo 84. za dhahabu, talanta 10,00029:7 Talanta 10,000 za fedha ni sawa na tani 375. za fedha, talanta 18,00029:7 Talanta 18,000 za shaba ni sawa na tani 675. za shaba na talanta 100,00029:7 Talanta 100,000 za chuma ni sawa na tani 3,750. za chuma. 829:8 Kut 35:27; 1Nya 26:21Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni. 929:9 1Fal 8:61; 2Kor 9:7Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.

Maombi Ya Daudi

1029:10 1Fal 8:15-16; 2Nya 6:4; Za 72:18; Eze 3:12Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema:

“Uhimidiwe wewe, Ee Bwana,

Mungu wa Israeli baba yetu,

tangu milele hata milele.

1129:11 Za 24:8; 89:11; Mt 6:13; Ufu 5:12-13; Dan 4:34-35; 1Tim 1:17Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana,

na utukufu na enzi na uzuri,

kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani

ni chako wewe.

Ee Bwana, ufalme ni wako;

umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.

1229:12 Ezr 7:27; Mhu 5:19; 2Nya 20:6; Rum 11:36; Kum 8:18; 1Sam 2:7-8; Za 75:6; Mit 10:22; Yak 1:17Utajiri na heshima vyatoka kwako;

wewe ndiwe utawalaye vitu vyote.

Mikononi mwako kuna nguvu na uweza

ili kuinua na kuwapa wote nguvu,

13Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru

na kulisifu Jina lako tukufu.

14“Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako. 1529:15 Mwa 47:9; 23:4; Ebr 11:13; Mhu 6:12; Za 102:11; Ay 14:2; Za 39:12; 1Pet 2:11; Za 90:9; 144:4Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini. 16Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako. 1729:17 Mit 17:3; Yer 11:20; Za 15:1-5; Mit 11:20; Ebr 4:13; Kum 8:2; 1Sam 16:7; 1Nya 28:9; Za 7:9; Yer 17:10; Mit 16:2Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe. 1829:18 Za 10:17; Yer 10:23Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako. 1929:19 1Fal 8:61; Isa 38:3; 1Nya 22:14; Za 72:1Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”

20Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.

Solomoni Akubalika Kuwa Mfalme

21Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli. 2229:22 1Nya 12:40; 1Sam 2:35; 1Fal 1:33-39Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile.

Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani. 2329:23 1Fal 2:12; 1Nya 17:14Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii. 2429:24 Mwa 24:2; 47:29; Eze 17:18; 2Nya 30:8Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.

2529:25 1Fal 10:7; 3:13; Mhu 2:9; 2Nya 1:12; Dan 5:18-19; Ebr 2:9Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.

Muhtasari Wa Utawala Wa Daudi

2629:26 1Nya 18:14Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote. 2729:27 2Sam 5:4-5; 1Fal 2:11Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.

2829:28 Mwa 15:15; Mdo 13:36; 1Nya 23:1; Mwa 25:8; Hes 23:10; Ay 5:26Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

2929:29 1Sam 9:9; 22:5; 2Sam 7:2; Ay 5:26Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi, 3029:30 Dan 2:21pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.

Persian Contemporary Bible

اول تواريخ 29:1-30

هدايا برای ساختن خانهٔ خدا

1آنگاه داوود پادشاه رو به تمام آن گروه كرد و گفت: «پسرم سليمان كه خدا او را انتخاب كرده تا پادشاه آيندهٔ اسرائيل باشد، هنوز جوان و كم‌تجربه است و كاری كه در پيش دارد، كار بزرگی است. عبادتگاهی كه می‌خواهد بسازد، يک ساختمان معمولی نيست، بلكه خانهٔ خداوند است. 2برای بنای خانهٔ خدای خود تا آنجا كه توانسته‌ام طلا و نقره، مفرغ و آهن، چوب و سنگ جزع، سنگهای گران قيمت ديگر و جواهرات با ارزش و سنگ مرمر جمع كرده‌ام، 3و چون دلبستگی به خانهٔ خدا دارم، تمام طلا و نقرهٔ خزانهٔ شخصی خود را برای بنای آن بخشيده‌ام. اين علاوه بر آن مصالح ساختمانی است كه قبلاً تدارک ديده‌ام. 4اين هدايای شخصی شامل صد تن طلای خالص و دويست و چهل تن نقرهٔ خالص برای روكش ديوارهای خانهٔ خدا 5و تمام لوازمی است كه به دست صنعتگران ساخته می‌شود. حال چه كسی حاضر است خود را با هر چه دارد در اختيار خداوند بگذارد؟»

6‏-7آنگاه رؤسای قبايل و طوايف، فرماندهان سپاه و ناظران دارايی پادشاه، با اشتياق ۱۷۰ تن طلا، ۳۴۰ تن نقره، ۶۱۰ تن مفرغ و ۳,۴۰۰ تن آهن هديه كردند. 8كسانی هم كه سنگهای قيمتی داشتند آنها را به خزانهٔ خانهٔ خداوند آورده، به يحی‌ئيل (پسر جرشون) تحويل دادند. 9تمام بنی‌اسرائيل از اينكه چنين فرصتی برای ايشان پيش آمده بود تا با اشتياق هدايايی تقديم كنند، خوشحال بودند. داوود پادشاه نيز از اين بابت بسيار شاد شد.

دعای داوود

10داوود در حضور آن گروه خداوند را ستايش كرده، گفت: «ای خداوند، خدای جد ما يعقوب، نام تو از ازل تا به ابد مورد ستايش باشد! 11عظمت و قدرت، جلال و شكوه و بزرگی برازندهٔ توست. ای خداوند، هر چه در آسمان و زمين است مال توست. سلطنت از آن توست. تو بالاتر و برتر از همه هستی. 12ثروت و افتخار از تو می‌آيد؛ تو بر همه چيز حاكم هستی. قدرت و توانايی در دست تو است؛ اين تو هستی كه به انسان قدرت و بزرگی می‌بخشی. 13ای خدای ما، از تو سپاسگزاريم و نام باشكوه تو را ستايش می‌كنيم.

14«ولی من و قوم من چه هستيم كه چنين افتخاری نصيب ما ساخته‌ای كه به تو چيزی بدهيم؟ هر چه داريم از تو داريم، و از مال تو به تو داده‌ايم. 15ما در اين دنيا مانند اجداد خود غريب و مهمانيم. عمر ما روی زمين مثل سايه، زودگذر است و دوامی ندارد. 16ای خداوند، خدای ما، تمام اين چيزهايی كه به تو تقديم كرده‌ايم تا خانه‌ای برای نام قدوس تو ساخته شود، از تو به ما رسيده و همه مال توست. 17خدای من، می‌دانم كه تو از قلب انسانها آگاهی و كسی را كه به راستی عمل می‌كند، دوست داری. من تمام اين كارها را از صميم قلب انجام داده‌ام و شاهدم كه قوم تو با شادی و اشتياق هدايای خود را تقديم كرده‌اند. 18ای خداوند، ای خدای اجداد ما ابراهيم و اسحاق و يعقوب، اين اشتياق را هميشه در دل قوم خود نگه دار و نگذار علاقهٔ خود را نسبت به تو از دست بدهند. 19اشتياقی در دل پسرم سليمان بوجود آور تا از جان و دل تمام اوامر تو را نگاه دارد و بنای خانهٔ تو را كه برايش تدارک ديده‌ام به اتمام برساند.»

20سپس داوود به تمام بنی‌اسرائيل گفت: «خداوند، خدای خود را ستايش كنيد.» و تمام جماعت در حضور خداوند، خدای اجداد خود و پادشاه زانو زدند و خداوند را ستايش كردند.

تاجگذاری سليمان

21روز بعد بنی‌اسرائيل هزار گاو، هزار قوچ و هزار بره برای قربانی سوختنی و نيز هدايای نوشيدنی به خداوند تقديم كردند. علاوه بر اينها، قربانیهای ديگری نيز به خداوند تقديم نموده، گوشت آنها را بين تمام قوم تقسيم كردند. 22آنها جشن گرفتند و با شادی فراوان در حضور خداوند خوردند و نوشيدند.

بنی‌اسرائيل بار ديگر پادشاهی سليمان، پسر داوود را تأييد كردند و او را به عنوان پادشاه و صادوق را به عنوان كاهن تدهين نمودند. 23به اين ترتيب سليمان به جای پدرش داوود بر تخت نشست تا بر قوم خداوند سلطنت كند. 24مقامات و فرماندهان سپاه و نيز تمام پسران پادشاه پشتيبانی خود را از سليمان پادشاه اعلام داشتند. 25خداوند، سليمان را در نظر تمام قوم اسرائيل بسيار بزرگ ساخت و به او جلالی شاهانه بخشيد، به طوری كه به هيچ پادشاه اسرائيل قبل از او داده نشده بود.

مرگ داوود پادشاه

26‏-27داوود پسر يسی مدت چهل سال پادشاه اسرائيل بود. از اين چهل سال، هفت سال در حبرون سلطنت كرد و سی و سه سال در اورشليم. 28او در كمال پيری، زمانی كه در اوج ثروت و افتخار بود، از دنيا رفت و سليمان به جای او پادشاه شد. 29شرح تمام رويدادهای دوران سلطنت داوود در كتب سه نبی، يعنی سموئيل، ناتان و جاد نوشته شده است. 30اين نوشته‌ها شرح سلطنت و قدرت او و پيش‌آمدهايی است كه برای او و اسرائيل و ساير اقوام همسايه رخ داد.