1 Nyakati 29 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 29:1-30

Matoleo Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Hekalu

129:1 1Fal 3:7; 2Nya 13:7; Mit 4:3; 1Nya 22:5Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana. 229:2 Ezr 6:5; Ufu 21:18; Hag 2:8; Isa 54:11; 1Nya 22:2-5; Kut 28:9Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno. 329:3 2Nya 24:10; Za 28:9; 2Nya 35:8; Za 26:8; 27:4; Mit 3:9Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu: 429:4 Mwa 10:29; 1Nya 22:14; Ay 22:24; 1Fal 9:28; 2Nya 8:18talanta 3,00029:4 Talanta 3,000 za dhahabu sawa na tani 110. za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,00029:4 Talanta 7,000 za fedha ni sawa na tani 260. za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu, 5kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”

629:6 1Nya 28:1; Kut 36:2; Ezr 7:15Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.

7Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,00029:7 Talanta 5,000 za dhahabu ni sawa na tani 190. na darkoni 10,00029:7 Darkoni 10,000 za dhahabu ni sawa na kilo 84. za dhahabu, talanta 10,00029:7 Talanta 10,000 za fedha ni sawa na tani 375. za fedha, talanta 18,00029:7 Talanta 18,000 za shaba ni sawa na tani 675. za shaba na talanta 100,00029:7 Talanta 100,000 za chuma ni sawa na tani 3,750. za chuma. 829:8 Kut 35:27; 1Nya 26:21Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni. 929:9 1Fal 8:61; 2Kor 9:7Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.

Maombi Ya Daudi

1029:10 1Fal 8:15-16; 2Nya 6:4; Za 72:18; Eze 3:12Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema:

“Uhimidiwe wewe, Ee Bwana,

Mungu wa Israeli baba yetu,

tangu milele hata milele.

1129:11 Za 24:8; 89:11; Mt 6:13; Ufu 5:12-13; Dan 4:34-35; 1Tim 1:17Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana,

na utukufu na enzi na uzuri,

kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani

ni chako wewe.

Ee Bwana, ufalme ni wako;

umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.

1229:12 Ezr 7:27; Mhu 5:19; 2Nya 20:6; Rum 11:36; Kum 8:18; 1Sam 2:7-8; Za 75:6; Mit 10:22; Yak 1:17Utajiri na heshima vyatoka kwako;

wewe ndiwe utawalaye vitu vyote.

Mikononi mwako kuna nguvu na uweza

ili kuinua na kuwapa wote nguvu,

13Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru

na kulisifu Jina lako tukufu.

14“Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako. 1529:15 Mwa 47:9; 23:4; Ebr 11:13; Mhu 6:12; Za 102:11; Ay 14:2; Za 39:12; 1Pet 2:11; Za 90:9; 144:4Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini. 16Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako. 1729:17 Mit 17:3; Yer 11:20; Za 15:1-5; Mit 11:20; Ebr 4:13; Kum 8:2; 1Sam 16:7; 1Nya 28:9; Za 7:9; Yer 17:10; Mit 16:2Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe. 1829:18 Za 10:17; Yer 10:23Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako. 1929:19 1Fal 8:61; Isa 38:3; 1Nya 22:14; Za 72:1Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”

20Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.

Solomoni Akubalika Kuwa Mfalme

21Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli. 2229:22 1Nya 12:40; 1Sam 2:35; 1Fal 1:33-39Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile.

Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani. 2329:23 1Fal 2:12; 1Nya 17:14Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii. 2429:24 Mwa 24:2; 47:29; Eze 17:18; 2Nya 30:8Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.

2529:25 1Fal 10:7; 3:13; Mhu 2:9; 2Nya 1:12; Dan 5:18-19; Ebr 2:9Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.

Muhtasari Wa Utawala Wa Daudi

2629:26 1Nya 18:14Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote. 2729:27 2Sam 5:4-5; 1Fal 2:11Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.

2829:28 Mwa 15:15; Mdo 13:36; 1Nya 23:1; Mwa 25:8; Hes 23:10; Ay 5:26Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

2929:29 1Sam 9:9; 22:5; 2Sam 7:2; Ay 5:26Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi, 3029:30 Dan 2:21pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.

O Livro

1 Crónicas 29:1-30

As ofertas para a construção do templo

1David voltou-se depois para toda a assembleia: “O meu filho Salomão, que Deus escolheu para ser o próximo rei de Israel, ainda é novo e inexperiente e a tarefa que está à sua frente é enorme, porque o templo que terá de construir não é uma edificação qualquer; é algo a ser dedicado ao Senhor Deus! 2Usando todos os recursos que estavam à minha disposição, juntei tudo o que me foi possível para essa construção: ouro, prata, bronze, ferro, madeira, grandes quantidades de ónix e outras pedras preciosas, joias e mármore. 3Visto que amo a casa do meu Deus, do meu tesouro pessoal dediquei também muita coisa para essa obra, além dos materiais de construção que estão armazenados. 4Essas contribuições pessoais consistem em 100 000 quilos de ouro de Ofir e 235 toneladas de prata pura, para ser usada na cobertura das paredes do edifício. 5Este ouro e prata também serão utilizados no fabrico de utensílios e nas decorações. Quem quer agora seguir o meu exemplo? Quem quer consagrar-se a si próprio e tudo o que tem ao Senhor?”

6Então os chefes dos clãs, os cabeças das tribos, os oficiais do exército, os responsáveis da administração da casa real 7ofereceram voluntariamente um total de 170 toneladas, mais 84 quilos de ouro, 340 toneladas de prata, 610 toneladas de bronze e 3400 toneladas de ferro. 8Também ofereceram grande quantidade de joalharia, que foi depositada no tesouro do templo, à guarda de Jeiel, descendente de Gerson. 9Toda a gente estava feliz com esta oportunidade de serviço, pois deram de coração ao Senhor. O rei David ficou profundamente comovido de alegria.

David louva o Senhor

10Ainda na presença de toda a assembleia, David expressou os seus louvores ao Senhor desta maneira:

Senhor, Deus do nosso pai Israel,

que o teu nome seja louvado sempre e sempre!

11Teu é o poder e a glória e a majestade e a vitória.

Tudo o que há nos céus e na Terra te pertence,

ó Senhor, e este reino é teu.

Adoramos-te porque tudo está sob o teu controlo.

12Riquezas e honra vêm apenas por ti;

tu és o juiz de toda a humanidade.

Teu é o poder e a força.

É por tua vontade que os homens se tornam grandes

e recebem força.

13Ó nosso Deus, nós te louvamos

e celebramos o teu nome glorioso!

14Quem sou eu e quem é o meu povo para te oferecermos tais coisas? Tudo o que temos vem de ti; nós apenas te damos aquilo que vem de ti! 15Nós vivemos aqui na Terra apenas por um curto espaço de tempo, como estrangeiros numa terra que era dos nossos pais. Os nossos dias na Terra são como uma sombra que passa rapidamente, sem deixar vestígios. 16Ó Senhor, nosso Deus, todos estes materiais que juntámos para construir um templo para o teu santo nome te pertencem! 17Eu sei, Deus meu, que provas os homens para veres se são retos, porque te agradas de homens sinceros. Sabes que fiz tudo isto com as mais puras intenções e que velei para que o povo oferecesse os seus donativos voluntariamente e com alegria. 18Senhor, Deus dos nossos pais Abraão, Isaque e Israel, faz com que o teu povo queira sempre obedecer-te e que o seu amor por ti nunca se altere! 19Dá ao meu filho Salomão um coração reto para contigo, para que queira obedecer às tuas leis, mandamentos e preceitos, e procure empenhadamente finalizar a construção do teu templo para o qual fiz estes preparativos.”

20Depois David disse a todo o povo: “Deem louvores ao Senhor, vosso Deus!” E todos louvaram o Senhor, Deus dos seus antepassados, inclinando-se diante do Senhor e do rei.

Salomão reconhecido como rei

21No dia seguinte trouxeram 1000 novilhos, 1000 carneiros e 1000 cordeiros e ofereceram-nos em holocausto ao Senhor. Também apresentaram ofertas de vinho e muitos outros sacrifícios em favor de todo o Israel. 22Seguidamente, comeram e beberam perante o Senhor, com grande alegria.

Novamente consagraram Salomão, o filho do rei David, como seu rei. Ungiram-no perante o Senhor como seu chefe e Zadoque como seu sacerdote. 23Desta forma, Salomão sucedeu ao seu pai David no trono do Senhor; prosperou grandemente e todo o Israel lhe obedeceu. 24Os líderes nacionais, os comandantes do exército e todos os seus irmãos submeteram-se ao rei Salomão.

25O Senhor deu-lhe grande popularidade junto de todo o povo de Israel. Conseguiu angariar mais riquezas e honra do que qualquer outro rei que reinou anteriormente em Israel.

A morte de David

(1 Rs 2.10-12)

26David, filho de Jessé, reinou em Israel 27durante 40 anos; 7 anos em Hebrom e 33 anos em Jerusalém. 28Morreu numa idade avançada, rico e honrado. O seu filho Salomão reinou em seu lugar.

29A história do rei David foi escrita nas crónicas do profeta Samuel, na história escrita pelo profeta Natã e na história do vidente Gad. 30Estas narrativas dizem respeito ao seu reino, ao seu poder e a tudo o que lhe aconteceu, a si e a Israel, assim como aos reis dos povos vizinhos.