1 Nyakati 27 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 27:1-34

Vikosi Vya Jeshi

1Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.

227:2 2Sam 23:8; 1Nya 11:11Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake. 327:3 Mwa 38:29Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.

427:4 2Sam 23:9-20Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

527:5 1Fal 4:5Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000. 627:6 2Sam 23:20-23Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.

727:7 2Sam 2:18; 1Nya 11:26-28; 2Sam 23:24Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

8Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

927:9 2Sam 23:26; 1Nya 11:28Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

10Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1127:11 2Sam 21; 18; 1Nya 11:29Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1227:12 2Sam 23:27; 1Nya 11:30-31Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1327:13 2Sam 23:28; 1Nya 11:36Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1427:14 2Sam 23:30; 1Nya 11:31Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1527:15 2Sam 23:29; Yos 15:17; Amu 3:9Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

Maafisa Wa Makabila

16Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa:

Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri;

kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;

1727:17 1Nya 26:30; 2Sam 8:17; 1Nya 12:28kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli;

kwa Aroni: Sadoki;

1827:18 1Sam 16:6kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi;

kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;

19kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia;

kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;

20kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia;

kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;

21kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria;

kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;

22kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu.

Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.

2327:23 2Sam 24:1; 1Nya 21:2-5; Mwa 12:2; 15:5; Kut 32:13; Ebr 11:12Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani. 2427:24 2Sam 24:15; 1Nya 21:7Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.

Wasimamizi Wa Mali Za Mfalme

25Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme.

Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.

26Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.

2727:27 Wim 8:11Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu.

Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.

2827:28 1Fal 10:27; 2Nya 1:15Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi.

Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.

29Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni.

Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.

30Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia.

Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.

3127:31 1Nya 5:10Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi.

Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.

3227:32 2Sam 21:21Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.

3327:33 2Sam 15:12, 37Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme.

Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme. 3427:34 1Sam 22:20; 2Sam 2:13; 1Nya 11:6Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari.

Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

Swedish Contemporary Bible

1 Krönikeboken 27:1-34

Befälhavare i armén

1Förteckning över israeliterna, familjeöverhuvuden, högre och lägre befälhavare, deras officerare, som tjänade kungen i allt som hade med avdelningarna att göra, och som var i tjänst en månad var under årets alla månader. Varje avdelning bestod av 24 000 man:

2Befälhavare över första avdelningen, som tjänstgjorde under första månaden, var Jishbaal, Savdiels son. Hans avdelning bestod av 24 000 man. 3Jishbaal hörde till Peres släkt och hade högsta befälet över alla officerare i hären som tjänstgjorde under första månaden.

4Befälhavare över andra månadens avdelning var Dodaj av Achoachs släkt, fursten Miklot var befälhavare över sin avdelning som bestod av 24 000 man.

5Den tredje befälhavaren, för tredje månaden, var Benaja, översteprästen Jojadas son. Hans avdelning bestod av 24 000 man. 6Denne Benaja var en hjälte bland de trettio och hade befälet över de trettio. Hans son Ammisavad hade befälet över hans avdelning.

7Den fjärde, för fjärde månaden, var Asael, Joavs bror, och senare hans son Sevadja. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

8Den femte, för femte månaden, var befälhavaren Shamhut av Serachs ätt. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

9Den sjätte, för sjätte månaden, var Ira, Ickeshs son, från Tekoa. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

10Den sjunde, för sjunde månaden, var Heles från Pelet av Efraims stam. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

11Den åttonde, för åttonde månaden, var Sibbekaj av Hushas släkt, som hörde till Serachs ätt. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

12Den nionde, för nionde månaden, var Avieser från Anatot i Benjamins stam. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

13Den tionde, för tionde månaden, var Mahraj från Netofa av Serachs ätt. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

14Den elfte, för elfte månaden, var Benaja från Piraton av Efraims stam. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

15Den tolfte, för tolfte månaden, var Heldaj från Netofa, som hörde till Otniels släkt. Hans avdelning bestod av 24 000 man.

Stamledare

16Furstarna för Israels stammar var:

Elieser, Sikris son, för Rubens stam,

Shefatja, Maakas son, för Simons stam,

17Hashavja, Kemuels son, för Levis stam, och Sadok för Aron,

18Elihu, en av Davids bröder, för Judas stam,

Omri, Mikaels son, för Isaskars stam,

19Jishmaja, Obadjas son, för Sebulons stam,

Jerimot, Asriels son, för Naftalis stam,

20Hosea, Asasjas son, för efraimiterna,

Joel, Pedajas son, för ena hälften av Manasses stam,

21Jiddo, Sakarjas son, för andra hälften av Manasses stam, den som var i Gilead,

Jaasiel, Avners son, för Benjamins stam,

22Asarel, Jerochams son, för Dans stam.

Dessa var ledarna för Israels stammar.

23David tog inte med i folkräkningen dem som var tjugo år eller yngre, för Herren hade lovat att israeliterna skulle bli lika oräkneliga som himlens stjärnor. 24Joav, Serujas son, påbörjade folkräkningen men avslutade den aldrig, för Guds vrede kom över Israel, och slutsumman blev aldrig införd i kung Davids krönika.

Tjänstemän i riket

25Asmavet, Adiels son, hade ansvaret för de kungliga förråden.

Jonatan, Ussias son, ansvarade för förråden på landsbygden, i städer, byar och vakttorn.

26Esri, Keluvs son, hade ansvaret för alla som arbetade med jordbruk ute på fälten.

27Shimi från Rama hade ansvaret för vingårdarna och Savdi från Shefam för vinförråden i vingårdarna.

28Baal Hanan från Geder hade ansvaret för kungens olivplanteringar och för mullbärsfikonträden på låglandet i väster.

Joash var ansvarig för oljeförråden.

29Shitraj från Sharon var ansvarig för boskapen som betade i Sharon och Shafat, Adlajs son, för boskapen i dalarna.

30Ovil, ismaeliten, var ansvarig för kamelerna, Jechdeja från Meronot för åsnorna 31och hagarén Jasis för småboskapen.

Dessa män var uppsyningsmän över kung Davids egendom.

32Davids farbror, Jonatan, var rådgivare. Han var en vis och skriftlärd man27:32 Eller: vis man och kungens sekreterare. Jechiel, Hakmonis son, tjänstgjorde för kungens söner.

33Achitofel var också rådgivare till kungen. Hushaj från Erek var kungens vän. 34Achitofel efterträddes av Jojada, Benajas son, och av Evjatar.

Joav var överbefälhavare för kungens här.