1 Nyakati 27 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 27:1-34

Vikosi Vya Jeshi

1Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.

227:2 2Sam 23:8; 1Nya 11:11Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake. 327:3 Mwa 38:29Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.

427:4 2Sam 23:9-20Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

527:5 1Fal 4:5Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000. 627:6 2Sam 23:20-23Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.

727:7 2Sam 2:18; 1Nya 11:26-28; 2Sam 23:24Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

8Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

927:9 2Sam 23:26; 1Nya 11:28Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

10Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1127:11 2Sam 21; 18; 1Nya 11:29Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1227:12 2Sam 23:27; 1Nya 11:30-31Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1327:13 2Sam 23:28; 1Nya 11:36Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1427:14 2Sam 23:30; 1Nya 11:31Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1527:15 2Sam 23:29; Yos 15:17; Amu 3:9Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

Maafisa Wa Makabila

16Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa:

Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri;

kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;

1727:17 1Nya 26:30; 2Sam 8:17; 1Nya 12:28kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli;

kwa Aroni: Sadoki;

1827:18 1Sam 16:6kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi;

kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;

19kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia;

kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;

20kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia;

kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;

21kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria;

kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;

22kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu.

Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.

2327:23 2Sam 24:1; 1Nya 21:2-5; Mwa 12:2; 15:5; Kut 32:13; Ebr 11:12Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani. 2427:24 2Sam 24:15; 1Nya 21:7Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.

Wasimamizi Wa Mali Za Mfalme

25Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme.

Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.

26Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.

2727:27 Wim 8:11Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu.

Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.

2827:28 1Fal 10:27; 2Nya 1:15Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi.

Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.

29Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni.

Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.

30Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia.

Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.

3127:31 1Nya 5:10Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi.

Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.

3227:32 2Sam 21:21Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.

3327:33 2Sam 15:12, 37Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme.

Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme. 3427:34 1Sam 22:20; 2Sam 2:13; 1Nya 11:6Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari.

Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 27:1-34

以色列的軍隊

1以色列人的族長、千夫長、百夫長及其他官長都分定班次,每班兩萬四千人,每年按月輪流服侍王。

2撒巴第業的兒子雅朔班負責第一班,在一月當值,他班內有兩萬四千人。 3他是法勒斯的子孫,統管一月當值的所有將領。 4亞哈希朵代負責二月的班次,他的副官是密基羅,他班內有兩萬四千人。 5祭司耶何耶大的兒子比拿雅負責第三班,在三月當值,他班內有兩萬四千人。 6比拿雅是當時的三十位勇士之一,也是三十位勇士之首。他兒子暗米薩拔在他班內做統領。 7約押的兄弟亞撒黑負責第四班,在四月當值,他班內有兩萬四千人,他兒子西巴第雅後來接替了他。 8伊斯拉珊合負責第五班,在五月當值,他班內有兩萬四千人。 9提哥亞益吉的兒子以拉負責第六班,在六月當值,他班內有兩萬四千人。 10以法蓮的子孫比倫希利斯負責第七班,在七月當值,他班內有兩萬四千人。 11謝拉族的戶沙西比該負責第八班,在八月當值,他班內有兩萬四千人。 12便雅憫的子孫亞拿突亞比以謝負責第九班,在九月當值,他班內有兩萬四千人。 13謝拉族的尼陀法瑪哈萊負責第十班,在十月當值,他班內有兩萬四千人。 14以法蓮的子孫比拉頓比拿雅負責第十一班,在十一月當值,他班內有兩萬四千人。 15俄陀聶族的尼陀法黑玳負責第十二班,在十二月當值,他班內有兩萬四千人。

以色列各支派的官長

16以下是以色列各支派的首領:呂便支派的首領是細基利的兒子以利以謝西緬支派的首領是瑪迦的兒子示法提雅17利未支派的首領是基姆利的兒子哈沙比雅亞倫子孫的首領是撒督18猶大支派的首領是大衛的哥哥以利戶以薩迦支派的首領是米迦勒的兒子暗利19西布倫支派的首領是俄巴第雅的兒子伊施瑪雅拿弗他利支派的首領是亞斯列的兒子耶利摩20以法蓮支派的首領是阿撒細雅的兒子何細亞瑪拿西半個支派的首領是毗大雅的兒子約珥21基列瑪拿西另半個支派的首領是撒迦利亞的兒子易多便雅憫支派的首領是押尼珥的兒子雅西業22支派的首領是耶羅罕的兒子亞薩列。以上這些人是以色列各支派的首領。 23大衛沒有統計二十歲以下的以色列人,因為耶和華曾經應許要使以色列的人數像天上的星那樣多。 24洗魯雅的兒子約押開始統計人數,但沒有完成,因為耶和華因此事而向以色列人發烈怒,因此統計的數目沒有收錄在大衛王記上。

王室產業的主管

25亞疊的兒子押斯馬威管理王室的庫房。烏西雅的兒子約拿單管理城邑、村莊和堡壘的庫房。 26基綠的兒子以斯利管理耕田種地的人。 27拉瑪示每管理葡萄園。實弗米撒巴底管理葡萄園的酒窖。 28基第利巴勒·哈南管理丘陵的橄欖樹和無花果樹。約阿施管理油倉。 29沙崙施提萊管理沙崙的牛群。亞第萊的兒子沙法管理山谷中的牛群。 30以實瑪利阿比勒管理駱駝群。米崙耶希底亞管理驢群。 31夏甲雅悉管理羊群。以上這些人都是替大衛王管理產業的。

32大衛的叔叔約拿單很精明,任謀士和書記。哈摩尼的兒子耶歇做眾王子的老師。 33亞希多弗也是王的謀士。亞基戶篩是王的朋友。 34後來,比拿雅的兒子耶何耶大亞比亞他接替亞希多弗做謀士。約押在王的軍隊中做元帥。