1 Nyakati 27 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 27:1-34

Vikosi Vya Jeshi

1Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.

227:2 2Sam 23:8; 1Nya 11:11Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake. 327:3 Mwa 38:29Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.

427:4 2Sam 23:9-20Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

527:5 1Fal 4:5Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000. 627:6 2Sam 23:20-23Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.

727:7 2Sam 2:18; 1Nya 11:26-28; 2Sam 23:24Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

8Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

927:9 2Sam 23:26; 1Nya 11:28Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

10Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1127:11 2Sam 21; 18; 1Nya 11:29Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1227:12 2Sam 23:27; 1Nya 11:30-31Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1327:13 2Sam 23:28; 1Nya 11:36Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1427:14 2Sam 23:30; 1Nya 11:31Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

1527:15 2Sam 23:29; Yos 15:17; Amu 3:9Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.

Maafisa Wa Makabila

16Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa:

Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri;

kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;

1727:17 1Nya 26:30; 2Sam 8:17; 1Nya 12:28kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli;

kwa Aroni: Sadoki;

1827:18 1Sam 16:6kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi;

kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;

19kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia;

kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;

20kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia;

kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;

21kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria;

kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;

22kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu.

Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.

2327:23 2Sam 24:1; 1Nya 21:2-5; Mwa 12:2; 15:5; Kut 32:13; Ebr 11:12Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani. 2427:24 2Sam 24:15; 1Nya 21:7Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.

Wasimamizi Wa Mali Za Mfalme

25Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme.

Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.

26Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.

2727:27 Wim 8:11Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu.

Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.

2827:28 1Fal 10:27; 2Nya 1:15Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi.

Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.

29Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni.

Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.

30Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia.

Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.

3127:31 1Nya 5:10Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi.

Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.

3227:32 2Sam 21:21Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.

3327:33 2Sam 15:12, 37Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme.

Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme. 3427:34 1Sam 22:20; 2Sam 2:13; 1Nya 11:6Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari.

Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

La Bible du Semeur

1 Chroniques 27:1-34

L’organisation de l’armée

1Voici la liste des Israélites, chefs de groupe familial qui furent les commandants des « milliers » ou des « centaines » et les administrateurs qui assistaient le roi pour tout ce qui concernait les divisions militaires appelées tour à tour à prendre mensuellement leur service. Chaque division comptait 24 000 hommes27.1 Comme dans de nombreux autres textes, il pourrait s’agir de vingt-quatre « milliers » d’hommes. Un « millier » était peut-être un corps d’armée comprenant quelques centaines d’hommes..

2A la tête de la première division affectée au premier mois27.2 Mois de la Pâque (Ex 12.2 ; Esd 6.19). se trouvait Yashobeam, fils de Zabdiel. Sa division comptait 24 000 hommes. 3Il était de la lignée de Pérets et commandait tous les chefs d’armée du premier mois. 4A la tête de la division du second mois comprenant également 24 000 hommes se trouvait Dodaï l’Ahohite. Miqloth était le chef de sa division. 5Le commandant de la troisième armée pour le troisième mois était Benaya, fils du grand-prêtre Yehoyada. Il avait dans sa division 24 000 hommes. 6Ce Benaya était l’un des guerriers du groupe des trente, il était à sa tête. Son fils Ammizadab avait sa division sous ses ordres. 7Le quatrième commandant affecté au quatrième mois était Asaël, frère de Joab. Son fils Zebadia lui succéda. Sa division comprenait 24 000 hommes. 8Le cinquième, pour le cinquième mois, était le commandant Shamehouth de la famille d’Yizrah. Sa division comptait 24 000 hommes. 9Pour le sixième mois : Ira fils d’Iqqesh, le Teqoïte. Sa division comptait 24 000 hommes. 10Le septième, pour le septième mois : Hélets le Pelonite, des descendants d’Ephraïm. Sa division comptait 24 000 hommes. 11Le huitième, pour le huitième mois : Sibbekaï, le Houshatite, de la famille des Zérahites. Sa division comptait 24 000 hommes. 12Le neuvième, pour le neuvième mois : Abiézer, d’Anatoth, des Benjaminites. Sa division comptait 24 000 hommes. 13Le dixième, pour le dixième mois : Maharaï, de Netopha, de la famille des Zérahites. Sa division comptait 24 000 hommes. 14Le onzième, pour le onzième mois : Benaya, de Piratôn, des Ephraïmites. Sa division comptait 24 000 hommes. 15Le douzième, pour le douzième mois : Heldaï, de Netopha, descendant d’Otniel. Sa division comptait 24 000 hommes.

Les chefs des tribus

16Voici les chefs des tribus d’Israël : les Rubénites avaient comme chef Eliézer, fils de Zikri ; les Siméonites : Shephatia, fils de Maaka. 17Pour Lévi, c’était Hashabia, fils de Qemouel ; pour Aaron, Tsadoq ; 18pour Juda : Elihou, frère de David ; pour Issacar : Omri, fils de Michaël ; 19pour Zabulon : Yishmaya, fils d’Abdias ; pour Nephtali : Yerimoth, fils d’Azriel ; 20pour les descendants d’Ephraïm : Osée, fils d’Azazia ; pour la demi-tribu de Manassé : Joël, fils de Pedaya ; 21pour la demi-tribu de Manassé en Galaad : Yiddo, fils de Zacharie ; pour Benjamin : Yaasiel, fils d’Abner ; 22pour Dan : Azaréel, fils de Yeroham. Ce sont là les chefs des tribus d’Israël.

23David ne comptait pas dans le dénombrement les moins de vingt ans, car l’Eternel avait promis de rendre Israël aussi nombreux que les étoiles du ciel27.23 Voir Gn 15.5 ; 22.17 ; 26.4.. 24Joab, fils de Tserouya, avait commencé le recensement ; mais il ne l’acheva pas. D’ailleurs, à cause de ce recensement, l’Eternel se mit en colère contre Israël. C’est pourquoi les chiffres de ce recensement n’ont pas été reportés dans les Annales du roi David27.24 Voir 1 Ch 21..

Les administrateurs des biens du roi

25Le responsable des trésors du roi était Azmaveth, fils d’Adiel. Le responsable des trésors entreposés à la campagne, dans les villes, les villages, et les tours, était Jonathan, fils d’Ozias. 26Le responsable des ouvriers agricoles qui cultivaient la terre était Ezri, fils de Keloub. 27Le responsable des vignobles était Shimeï, de Rama ; celui des réserves de vin dans les vignes était Zabdi, de Shepham. 28Le responsable des plantations d’oliviers et de sycomores du Bas-Pays27.28 C’est-à-dire la plaine côtière du littoral méditerranéen, célèbre pour sa fertilité. Les sycomores ne doivent pas être confondus avec les arbres portant ce nom dans nos régions : ce sont des figuiers aux feuilles semblables à celle du mûrier qui croissent en abondance de l’Egypte à la Syrie (voir Lc 19.4). était Baal-Hanân, de Guéder ; celui des réserves d’huile était Joas. 29Le responsable des troupeaux de bétail qui avaient leur pâture dans la plaine du Saron27.29 Partie nord de la plaine côtière qui s’étend de Jaffa au pied du mont Carmel. était Shitraï, de Saron ; celui du bétail qui se trouvait dans les vallées était Shaphath, fils d’Adlaï. 30Le responsable des chameaux était Obil, l’Ismaélite27.30 Donc un descendant d’Ismaël (voir Gn 16.11-12 ; 25.12-18). ; celui des ânesses était Yéhdeya, de Méronoth. 31Le responsable des troupeaux de moutons et de chèvres était Yaziz, l’Agarénien. Tous ceux-là étaient les intendants des biens du roi David.

Les conseillers privés de David

32Jonathan, oncle de David, et son conseiller, un homme intelligent, qui était secrétaire, avait la charge, avec Yehiel, fils de Hakmoni, de l’éducation des fils du roi. 33Ahitophel était conseiller du roi. Houshaï, l’Arkien, était son confident. 34Après Ahitophel, il y eut Yehoyada, fils de Benaya, et Abiatar. Joab était chef des armées du roi.