1 Nyakati 26 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 26:1-32

Mabawabu

126:1 1Nya 9:17; Hes 26:9-11; 2Nya 23:19; Hes 16:1-2; 1Nya 15:18; Yud 11; 1Nya 6:39Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu:

Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.

226:2 1Nya 9:21Meshelemia alikuwa na wana wafuatao:

Zekaria mzaliwa wa kwanza,

Yediaeli wa pili,

Zebadia wa tatu,

Yathnieli wa nne,

3Elamu wa tano

Yehohanani wa sita

na Eliehoenai wa saba.

4Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao:

Shemaya mzaliwa wa kwanza,

Yehozabadi wa pili,

Yoa wa tatu,

Sakari wa nne,

Nethaneli wa tano,

526:5 Mwa 33; 5; 2Sam 5:10; 1Nya 13:13-14; Za 127:3Amieli wa sita,

Isakari wa saba,

na Peulethai wa nane.

(Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)

6Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa. 7Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo. 8Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.

9Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.

1026:10 Kum 21:16-17; 1Nya 16:38; 5:1; Mwa 4:7; 49:3Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza), 11Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.

12Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo. 1326:13 1Nya 24:5; 25:8; Mit 18:18; Yos 18:10; Yn 1:7; Mdo 1:26; 10:34; Gal 3:28; Kol 3:11Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.

1426:14 1Nya 9:18-21Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia.26:14 Shelemia jina lingine ni Meshelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia. 1526:15 1Nya 13:13; 2Nya 25:24Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe. 1626:16 1Fal 10:5; 1Nya 24:31; Neh 12:24; 2Nya 9:4; 1Nya 25:8Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa.

Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa: 17Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala. 18Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.

1926:19 Neh 7:1; Eze 44:11Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.

Watunza Hazina Na Maafisa Wengine

2026:20 2Nya 24:5; 1Nya 28:12; 22:14-16; Kum 12:6; 1Fal 7:51; 14:26; 1Nya 9:26-29; Mal 3:10; 2Nya 31:11-12Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.

2126:21 1Nya 6:17; 23:8; 29:8Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli, 22wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.

2326:23 Hes 3:27; Kut 6:18; 1Nya 23:12Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:

2426:24 1Nya 23:16-18; 24:20Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina. 2526:25 1Nya 23:18; 24:22Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi. 2626:26 2Sam 8:11Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi. 2726:27 Hes 31:50; Yos 6:19, 24; 1Nya 22:14-16; 2Nya 15:11, 18; 2Fal 12:14; 22:4-5; Neh 10:32Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana. 2826:28 1Sam 9:9Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.

2926:29 Kum 17:8-13; Neh 11:16; 2Nya 19:8-11; 1Nya 23:4Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.

3026:30 1Nya 27:17Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme. 3126:31 1Nya 23:19; 2Sam 5:4; Isa 16:9; Yer 48:32; 1Fal 2:11; 1Nya 29:27; Yos 21:39Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi. 3226:32 2Nya 19:11Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 26:1-32

聖殿的守衛

1以下是殿門守衛的班次:

可拉亞薩的後代有可利的兒子米施利米雅2米施利米雅的長子是撒迦利亞,次子是耶疊,三子是西巴第雅,四子是耶提聶3五子是以攔,六子是約哈難,七子是以利約乃4俄別·以東的長子是示瑪雅,次子是約薩拔,三子是約亞,四子是沙甲,五子是拿坦業5六子是亞米利,七子是以薩迦,八子是毗烏利太。上帝特別賜福俄別·以東6他兒子示瑪雅有幾個兒子都很能幹,在各自的家族中做首領。 7他們是俄得尼利法益俄備得以利薩巴。他們的親族以利戶西瑪迦也很能幹。 8這些都是俄別·以東的子孫,他們和他們的兒子及親族共有六十二人,都是能幹稱職的人。 9米施利米雅的兒子及親族共十八人,都很能幹。 10米拉利的後代何薩的長子是申利,他本來不是長子,是被他父親立為長子的。 11次子是希勒迦,三子是底巴利雅,四子是撒迦利亞何薩的兒子及親族共十三人。

12這些按族長分成小組的殿門守衛在耶和華的殿裡按班次供職,與他們的親族一樣。 13他們無論大小,都按照族系抽籤,以決定看守哪個門。 14示利米雅抽中東門,他兒子撒迦利亞是個精明的謀士,抽中北門。 15俄別·以東抽中南門,他兒子抽中庫房。 16書聘何薩抽中西門和上行之路的沙利基門,兩班相對而立。 17每天有六個利未人守東門,四人守北門,四人守南門,守庫房的二人一組。 18守衛西面街道的有四人,守衛走廊的有二人。 19以上是可拉的子孫和米拉利的子孫守門的班次。

聖殿裡的其他職務

20利未亞希雅負責掌管上帝殿裡的庫房和放奉獻之物的庫房。 21革順拉但的子孫中做族長的有耶希伊利22耶希伊利的兩個兒子西坦約珥負責管理耶和華殿裡的庫房。 23暗蘭族、以斯哈族、希伯崙族、烏歇族也各有其職。 24摩西的孫子——革舜的兒子細布業是庫房的主管。 25細布業的親族有以利以謝以利以謝的兒子是利哈比雅利哈比雅的兒子是耶篩亞耶篩亞的兒子是約蘭約蘭的兒子是細基利細基利的兒子是示羅密26示羅密及其親族負責管理庫房中的奉獻之物,這些物品是大衛王、眾族長、千夫長、百夫長和將領獻給上帝的聖物。 27他們把戰爭中擄掠的財物獻出來,以備建造耶和華的殿。 28撒母耳先見、基士的兒子掃羅尼珥的兒子押尼珥洗魯雅的兒子約押及其他人奉獻的聖物都由示羅密及其親族管理。

29以斯哈族的基拿尼雅及其眾子做官長和士師,為以色列管理聖殿以外的事務。 30希伯崙族的哈沙比雅及其親族一千七百人都很能幹,他們在以色列約旦河以西辦理耶和華和王的事務。 31按家譜記載,希伯崙宗族的族長是耶利雅大衛執政第四十年,經過調查,在基列雅謝希伯崙族中找到一些能幹的人。 32耶利雅的親族有兩千七百人,都是能幹的族長。大衛王派他們在呂便支派、迦得支派和瑪拿西半個支派中辦理一切有關上帝和王的事務。