1 Nyakati 23 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 23:1-32

Jamaa Za Walawi Na Utendaji Wao

123:1 1Fal 1:30-33; 1Nya 28:5; 29:28; 29:22-25Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.

2Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi. 323:3 Hes 8:24; 4:3-49Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000. 423:4 Ezr 3:8; 2Nya 19:8; Kum 16:18; Eze 44:24; Kum 16:18; 1Nya 26:29Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi, 523:5 1Nya 15:16; Za 92:3; Neh 12:45; Amo 6:5; 2Nya 29:25-26na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”

623:6 2Nya 23:18; 29:25; 8:14; Kut 6:16; Hes 26:57; 2Nya 35:10; 31:2; Ezr 6:18Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.

Wagershoni

7Wana wa Wagershoni walikuwa wawili:

Ladani na Shimei.

8Wana wa Ladani walikuwa watatu:

Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.

9Wana wa Shimei walikuwa watatu:

Shelomothi,23:9 Yaani Shelomithi; maana yake ni Mpenda amani. Hazieli na Harani.

Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.

10Nao wana wa Shimei walikuwa wanne:

Yahathi, Zina,23:10 Tafsiri zingine zinamwita Ziza. Yeushi na Beria.

11Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.

Wakohathi

1223:12 Mwa 46:11; Kut 6:18-20; 1Nya 6:2Wana wa Kohathi walikuwa wanne:

Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

1323:13 Kut 30:7-10; 28:1; Kum 21:5; Hes 6:23; 16:40; Ebr 5:4; Hes 16:40; 1Sam 2:28Wana wa Amramu walikuwa:

Aroni na Mose.

Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele. 1423:14 Kum 33:1Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.

1523:15 Kut 18:4; 2:22Wana wa Mose walikuwa:

Gershomu na Eliezeri.

1623:16 1Nya 26:24-28Wazao wa Gershomu:

Shebueli alikuwa wa kwanza.

17Wazao wa Eliezeri:

Rehabia alikuwa wa kwanza.

Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.

18Wana wa Ishari:

Shelomithi alikuwa wa kwanza.

1923:19 1Nya 24:23; 26:31Wana wa Hebroni walikuwa:

Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.

20Wana wa Uzieli walikuwa:

Mika wa kwanza na Ishia wa pili.

Wamerari

2123:21 1Nya 6:19; 24:26Wana wa Merari walikuwa:

Mahli na Mushi.

Wana wa Mahli walikuwa:

Eleazari na Kishi.

2223:22 Hes 36:6Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.

2323:23 1Nya 24:30Wana wa Mushi:

Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.

2423:24 Hes 4:3; 10:17-21Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana. 25Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele, 26Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.” 27Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.

2823:28 Neh 13:9; Mal 3:3Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu. 2923:29 Kut 25:30; Law 2:4-7; 6:20-23; 19:35-36; 1Nya 9:29-32Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 3023:30 1Nya 9:33; Ufu 5:8-14; 2Nya 31:2; 1Nya 6:31-33; Za 135:1-3; Ufu 14:3Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni 3123:31 2Fal 4:23; Law 23:4; Kol 2:16; Hes 10:10; Za 81:3; Isa 1:13-14na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.

3223:32 Hes 1:53; 1Nya 6:48; Hes 3:6-8; 2Nya 31:2; Eze 44:14Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

New International Version – UK

1 Chronicles 23:1-32

The Levites

1When David was old and full of years, he made his son Solomon king over Israel.

2He also gathered together all the leaders of Israel, as well as the priests and Levites. 3The Levites thirty years old or more were counted, and the total number of men was thirty-eight thousand. 4David said, ‘Of these, twenty-four thousand are to be in charge of the work of the temple of the Lord and six thousand are to be officials and judges. 5Four thousand are to be gatekeepers and four thousand are to praise the Lord with the musical instruments I have provided for that purpose.’

6David separated the Levites into divisions corresponding to the sons of Levi: Gershon, Kohath and Merari.

Gershonites

7Belonging to the Gershonites:

Ladan and Shimei.

8The sons of Ladan:

Jehiel the first, Zetham and Joel – three in all.

9The sons of Shimei:

Shelomoth, Haziel and Haran – three in all.

(These were the heads of the families of Ladan.)

10And the sons of Shimei:

Jahath, Ziza,23:10 One Hebrew manuscript, Septuagint and Vulgate (see also verse 11); most Hebrew manuscripts Zina Jeush and Beriah.

These were the sons of Shimei – four in all.

11(Jahath was the first and Ziza the second, but Jeush and Beriah did not have many sons; so they were counted as one family with one assignment.)

Kohathites

12The sons of Kohath:

Amram, Izhar, Hebron and Uzziel – four in all.

13The sons of Amram:

Aaron and Moses.

Aaron was set apart, he and his descendants for ever, to consecrate the most holy things, to offer sacrifices before the Lord, to minister before him and to pronounce blessings in his name for ever. 14The sons of Moses the man of God were counted as part of the tribe of Levi.

15The sons of Moses:

Gershom and Eliezer.

16The descendants of Gershom:

Shubael was the first.

17The descendants of Eliezer:

Rehabiah was the first.

(Eliezer had no other sons, but the sons of Rehabiah were very numerous.)

18The sons of Izhar:

Shelomith was the first.

19The sons of Hebron:

Jeriah the first, Amariah the second,

Jahaziel the third and Jekameam the fourth.

20The sons of Uzziel:

Micah the first and Ishiah the second.

Merarites

21The sons of Merari:

Mahli and Mushi.

The sons of Mahli:

Eleazar and Kish.

22(Eleazar died without having sons: he had only daughters. Their cousins, the sons of Kish, married them.)

23The sons of Mushi:

Mahli, Eder and Jerimoth – three in all.

24These were the descendants of Levi by their families – the heads of families as they were registered under their names and counted individually, that is, the workers twenty years old or more who served in the temple of the Lord. 25For David had said, ‘Since the Lord, the God of Israel, has granted rest to his people and has come to dwell in Jerusalem for ever, 26the Levites no longer need to carry the tabernacle or any of the articles used in its service.’ 27According to the last instructions of David, the Levites were counted from those twenty years old or more.

28The duty of the Levites was to help Aaron’s descendants in the service of the temple of the Lord: to be in charge of the courtyards, the side rooms, the purification of all sacred things and the performance of other duties at the house of God. 29They were in charge of the bread set out on the table, the special flour for the grain offerings, the thin loaves made without yeast, the baking and the mixing, and all measurements of quantity and size. 30They were also to stand every morning to thank and praise the Lord. They were to do the same in the evening 31and whenever burnt offerings were presented to the Lord on the Sabbaths, at the New Moon feasts and at the appointed festivals. They were to serve before the Lord regularly in the proper number and in the way prescribed for them.

32And so the Levites carried out their responsibilities for the tent of meeting, for the Holy Place and, under their relatives the descendants of Aaron, for the service of the temple of the Lord.