1 Nyakati 22 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 22:1-19

122:1 Kum 12:5; Mwa 28:17; 1Nya 21:18-28; 2Nya 3:1; Kum 12:5; 2Sam 24:18Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”

Maandalizi Kwa Ajili Ya Hekalu

222:2 Kum 20:11; 1Fal 9:21; 5:17-18; Ezr 3:7Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu. 322:3 1Fal 7:47Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika. 422:4 1Fal 5:6Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.

522:5 1Fal 3:7; 1Nya 29:1Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.

622:6 Mdo 7:47Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli. 722:7 1Nya 17:2; 2Sam 7:2; 1Fal 8:17; Kum 12:5-11; Mdo 7:48Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu. 822:8 1Fal 5:3; 1Nya 28:3Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu. 922:9 Yos 14:15; 2Sam 12:24; 1Fal 4:20; 5:4; 1Nya 28:5Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake. 1022:10 1Nya 17:12; 2Sam 7:13-14; 2Nya 6:15; 1Fal 5:5; 1Nya 28:6; Za 89:26-27; Ebr 1:5Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’

1122:11 1Sam 18:12; Rum 8:31“Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya. 1222:12 1Fal 3:11; 2Nya 1:10; Kum 4:6Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako. 1322:13 1Nya 28:7; Kum 31:6-7; Yos 1:6-9; 1Fal 6:12-13; 9:4-5; Isa 3:10; 1Nya 28:20Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.

1422:14 1Nya 29:2-5, 19“Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,00022:14 Talanta 100,000 za dhahabu ni sawa na tani 3,750. za dhahabu, talanta 1,000,00022:14 Talanta 1,000,000 za fedha ni sawa na tani 37,500. za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza. 15Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi 16wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”

1722:17 1Nya 28:1-6Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe. 1822:18 1Fal 8:6; Kum 12:10; Yos 22:4Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake. 1922:19 2Nya 20:3; 1Fal 8:6; 2Nya 5:7; 6:11Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”

New International Version – UK

1 Chronicles 22:1-19

1Then David said, ‘The house of the Lord God is to be here, and also the altar of burnt offering for Israel.’

Preparations for the temple

2So David gave orders to assemble the foreigners residing in Israel, and from among them he appointed stonecutters to prepare dressed stone for building the house of God. 3He provided a large amount of iron to make nails for the doors of the gateways and for the fittings, and more bronze than could be weighed. 4He also provided more cedar logs than could be counted, for the Sidonians and Tyrians had brought large numbers of them to David.

5David said, ‘My son Solomon is young and inexperienced, and the house to be built for the Lord should be of great magnificence and fame and splendour in the sight of all the nations. Therefore I will make preparations for it.’ So David made extensive preparations before his death.

6Then he called for his son Solomon and charged him to build a house for the Lord, the God of Israel. 7David said to Solomon: ‘My son, I had it in my heart to build a house for the Name of the Lord my God. 8But this word of the Lord came to me: “You have shed much blood and have fought many wars. You are not to build a house for my Name, because you have shed much blood on the earth in my sight. 9But you will have a son who will be a man of peace and rest, and I will give him rest from all his enemies on every side. His name will be Solomon,22:9 Solomon sounds like and may be derived from the Hebrew for peace. and I will grant Israel peace and quiet during his reign. 10He is the one who will build a house for my Name. He will be my son, and I will be his father. And I will establish the throne of his kingdom over Israel for ever.”

11‘Now, my son, the Lord be with you, and may you have success and build the house of the Lord your God, as he said you would. 12May the Lord give you discretion and understanding when he puts you in command over Israel, so that you may keep the law of the Lord your God. 13Then you will have success if you are careful to observe the decrees and laws that the Lord gave to Moses for Israel. Be strong and courageous. Do not be afraid or discouraged.

14‘I have taken great pains to provide for the temple of the Lord a hundred thousand talents22:14 That is, about 3,400 metric tons of gold, a million talents22:14 That is, about 34,000 metric tons of silver, quantities of bronze and iron too great to be weighed, and wood and stone. And you may add to them. 15You have many workers: stonecutters, masons and carpenters, as well as those skilled in every kind of work 16in gold and silver, bronze and iron – craftsmen beyond number. Now begin the work, and the Lord be with you.’

17Then David ordered all the leaders of Israel to help his son Solomon. 18He said to them, ‘Is not the Lord your God with you? And has he not granted you rest on every side? For he has given the inhabitants of the land into my hands, and the land is subject to the Lord and to his people. 19Now devote your heart and soul to seeking the Lord your God. Begin to build the sanctuary of the Lord God, so that you may bring the ark of the covenant of the Lord and the sacred articles belonging to God into the temple that will be built for the Name of the Lord.’