1 Nyakati 18 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 18:1-17

Ushindi Wa Daudi

(2 Samweli 8:1-18)

1Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.

218:2 Hes 24:17; 21:29Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.

318:3 1Nya 19:6; Mwa 2:14; 15:18; Kum 11:24; 2Sam 8:3Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati. 418:4 Mwa 49:6; 2Sam 8:4Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.

518:5 2Fal 16:9; 1Nya 19:6Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao. 618:6 1Nya 17:8; Mit 21:31; Za 91:14; 121:8Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.

7Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu. 818:8 1Fal 7:23; 2Nya 4:12-16Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.

9Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba, 1018:10 2Sam 8:10akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.

1118:11 Hes 24:18-20Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.

1218:12 1Fal 11:15; 2Sam 7:13; 2Fal 14:7; 2Nya 25:11Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi. 1318:13 Mwa 27:29; Hes 24:18; 1Sam 10:3; 13:3; 14:1Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.

Maafisa Wa Daudi

1418:14 1Nya 29:26; 11:1-6Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote. 1518:15 2Sam 5:6-8Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu; 1618:16 2Sam 8:17; 1Nya 6:8; 24; 6Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi; 1718:17 1Sam 30:14; 2Sam 8:18naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 18:1-17

大衛的勝利

1後來,大衛打敗並征服了非利士人,奪取了迦特及其周圍的村莊。 2他又打敗了摩押人,使他們稱臣、進貢。 3瑣巴哈大底謝出來要鞏固他在幼發拉底河一帶的權勢,大衛打敗了他,一直攻到哈馬4俘獲一千輛戰車、七千騎兵、兩萬步兵,砍斷拉戰車的馬匹的蹄筋,只留下夠拉一百輛戰車的馬匹。 5大馬士革亞蘭人前來支援瑣巴哈大底謝大衛殺了他們兩萬二千人, 6還派軍駐守亞蘭國的大馬士革亞蘭人臣服大衛,向他進貢。耶和華使大衛無往而不勝。 7大衛奪走哈大底謝侍從的金盾牌,帶回耶路撒冷8又從哈大底謝統治的提巴兩座城中奪走大量的銅。後來所羅門用這些銅製造銅海、銅柱及各種銅器。

9哈馬陀烏聽說大衛打敗瑣巴哈大底謝全軍, 10就派兒子哈多蘭帶著許多金銀銅器去朝見大衛王,向他請安,祝賀他打敗了哈大底謝。因為陀烏常常和哈大底謝交戰。 11於是,大衛把這些器皿和他從以東摩押亞捫非利士亞瑪力各國奪來的金銀都分別出來,奉獻給耶和華。

12洗魯雅的兒子亞比篩在鹽谷擊殺了一萬八千名以東人。 13大衛以東駐兵,以東人都臣服他。耶和華使他無往而不勝。

14大衛在全以色列秉公行義,治理百姓。 15那時,洗魯雅的兒子約押做元帥,亞希律的兒子約沙法做史官, 16亞希突的兒子撒督亞比亞他的兒子亞希米勒做祭司長,沙威沙做書記, 17耶何耶大的兒子比拿雅統管基利提人和比利提人。大衛王的眾子都在他左右做首領。