1 Nyakati 18 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 18:1-17

Ushindi Wa Daudi

(2 Samweli 8:1-18)

1Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.

218:2 Hes 24:17; 21:29Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.

318:3 1Nya 19:6; Mwa 2:14; 15:18; Kum 11:24; 2Sam 8:3Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati. 418:4 Mwa 49:6; 2Sam 8:4Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.

518:5 2Fal 16:9; 1Nya 19:6Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao. 618:6 1Nya 17:8; Mit 21:31; Za 91:14; 121:8Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.

7Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu. 818:8 1Fal 7:23; 2Nya 4:12-16Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.

9Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba, 1018:10 2Sam 8:10akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.

1118:11 Hes 24:18-20Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.

1218:12 1Fal 11:15; 2Sam 7:13; 2Fal 14:7; 2Nya 25:11Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi. 1318:13 Mwa 27:29; Hes 24:18; 1Sam 10:3; 13:3; 14:1Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.

Maafisa Wa Daudi

1418:14 1Nya 29:26; 11:1-6Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote. 1518:15 2Sam 5:6-8Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu; 1618:16 2Sam 8:17; 1Nya 6:8; 24; 6Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi; 1718:17 1Sam 30:14; 2Sam 8:18naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Krønikebog 18:1-17

Davids sejre over nabofolkene

2.Sam. 8,1-14

1David besejrede efterhånden filistrene fuldstændigt og undertvang dem ved at indtage deres hovedstad, Gat, og de omliggende landsbyer. 2Han besejrede også moabitterne og gjorde dem til sine skattepligtige undersåtter.

3Kong Hadadezer af Zoba forsøgte at generobre sit gamle territorium syd for Eufratfloden.18,3 Et område, som Saul havde taget fra ham. Men David besejrede hans hær og forfulgte den helt til Hamat.18,3 I det nordvestlige Syrien, vest for Zoba området og ca. 200 km nord for Damaskus. 4Ved den lejlighed erobrede David 1000 stridsvogne og tog 7000 ryttere og 20.000 fodfolk til fange. Han skar haserne over på samtlige heste bortset fra 100 af dem. 5Da aramæerne rykkede ud fra Damaskus for at hjælpe Hadadezer, huggede David 22.000 af dem ned. 6I Damaskusområdet udstationerede han flere garnisoner og indlemmede aramæerne blandt sine skattepligtige undersåtter. Herren gav David sejr over alle hans fjender. 7David beslaglagde alle de guldskjolde, som kong Hadadezers officerer havde brugt, og førte dem til Jerusalem 8sammen med en stor ladning bronze fra Hadadezers byer Tibat og Kun. Det var blandt andet det bronze, kong Salomon senere brugte til at få lavet „bronzehavet” ved templet samt søjlerne og de forskellige bronzeredskaber.

9Da kong Tou af Hamat hørte om Davids triumf over Hadadezers hær, 10sendte han sin søn Hadoram af sted for at lykønske ham. Hadadezer og Tou var nemlig ærkefjender. Hadoram forærede David mange gaver af guld, sølv og bronze, 11og David indviede dem til Herren sammen med det guld og sølv, han havde taget i krigsbytte fra edomitterne, moabitterne, ammonitterne, filistrene og amalekitterne.

12I Saltdalen slog Abishaj, Zerujas søn, en edomitisk hær på 18.000 mand, 13hvorefter han etablerede en række garnisoner i Edom, så edomitterne kom under Davids herredømme. Således gav Herren David sejr, hvor som helst han kom frem.

Davids embedsmænd

2.Sam. 8,15-18

14David var en retfærdig konge i Israel, og han gav alle en fair behandling. 15Joab var øverstbefalende for hæren; Joshafat, Ahiluds søn, var kongens øverste embedsmand med ansvar for arkiverne; 16Zadok, Ahitubs søn, og Ahimelek, Ebjatars søn, var de ledende præster; Shavsha var statssekretær; 17Benaja, Jojadas søn, var chef for livgarden; og Davids egne sønner var ledere ved kongens side.