1 Nyakati 11 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 11:1-47

Daudi Atiwa Mafuta Kuwa Mfalme Wa Israeli

(2 Samweli 5:1-10)

111:1 1Nya 9:1; Mwa 13:18; 23:19; 2Sam 5:1; 1Nya 12:23Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako. 211:2 1Sam 18:5, 16; Za 78:71; Mt 2:6; 1Nya 5:2Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’ ”

311:3 1Sam 16:1-13; 2Sam 5:3; Rum 8:31Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.

Daudi Ateka Yerusalemu

411:4 Yos 3:10; Amu 1:21; 2Sam 5:6; Mwa 10:16; 15:21; Kut 3:17; Amu 19:10Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo 5wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.

611:6 2Sam 2:13; 8:16Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.

711:7 2Sam 5:7Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi. 811:8 2Sam 5:9; 2Nya 32:5Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu. 911:9 2Sam 3:1; Es 9:4Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.

Mashujaa Wa Daudi

(2 Samweli 23:8-39)

1011:10 1Nya 11:1; 12:23; 2Sam 23:8; 1Sam 16:1, 12Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi. 1111:11 2Sam 17:10Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi:

Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.

12Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu. 1311:13 1Sam 17:1Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti. 1411:14 Kut 14:30; 1Sam 17:10; Mit 21:31Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.

1511:15 1Nya 14:9Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai. 1611:16 2Sam 5:17Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu. 17Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!” 1811:18 Kum 12:16Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana. 19Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa.

Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.

2011:20 1Sam 26:6Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu. 2111:21 2Sam 23:24; 1Nya 27:7Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.

2211:22 Yos 15:21; 1Sam 17:36; 2Sam 1:23; 23:20; 1Nya 12:8Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba. 2311:23 1Sam 26:6Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano.11:23 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao. 24Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu. 25Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.

2611:26 1Nya 2:18; 2Sam 23:24; 1Nya 27:7Wale watu mashujaa walikuwa:

Asaheli nduguye Yoabu,

Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,

2711:27 1Nya 27:8Shamothi Mharori,

Helesi Mpeloni,

2811:28 1Nya 27:12Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa,

Abiezeri kutoka Anathothi,

2911:29 2Sam 21:18Sibekai Mhushathi,

Ilai Mwahohi,

30Maharai Mnetofathi,

Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,

3111:31 1Nya 27:14; Amu 12:13Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini,

Benaya Mpirathoni,

32Hurai kutoka mabonde ya Gaashi,

Abieli Mwaribathi,

33Azmawethi Mbaharumi,

Eliaba Mshaalboni,

34wana wa Hashemu Mgiloni,

Yonathani mwana wa Shagee Mharari,

35Ahiamu mwana wa Sakari Mharari,

Elifale mwana wa Uru,

36Heferi Mmekerathi,

Ahiya Mpeloni,

37Hezro Mkarmeli,

Naarai mwana wa Ezbai,

38Yoeli nduguye Nathani,

Mibhari mwana wa Hagri,

39Seleki Mwamoni,

Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,

4011:40 Yos 15:48; 1Nya 2:50-53Ira Mwithiri,

Garebu Mwithiri,

4111:41 2Sam 11:6; 1Nya 2:36Uria Mhiti,

Zabadi mwana wa Alai,

42Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,

43Hanani mwana wa Maaka,

Yoshafati Mmithni,

4411:44 Kum 1:4Uzia Mwashterathi,

Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,

45Yediaeli mwana wa Shimri,

nduguye Yoha Mtizi,

46Elieli Mmahawi,

Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu,

Ithma Mmoabu,

47Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 11:1-47

大衛做以色列人的王

1以色列人都聚集到希伯崙來見大衛,對他說:「我們是你的骨肉同胞。 2從前,即使掃羅做王的時候,率領以色列人出征打仗的仍是你。你的上帝耶和華也曾應許讓你做祂以色列子民的牧者和首領。」 3以色列的長老都到希伯崙大衛王,大衛與他們在耶和華面前立約,他們膏立大衛以色列的王,這應驗了耶和華藉撒母耳所說的話。 4大衛以色列眾人來到耶路撒冷,即耶布斯。那時耶布斯人住在那裡。 5耶布斯人對大衛說:「你攻不進來。」可是,大衛攻取了錫安的堡壘,即後來的大衛城。 6大衛說:「誰先攻打耶布斯人,誰就做元帥。」洗魯雅的兒子約押首先進攻,於是就做了元帥。 7大衛佔據了堡壘,因此那堡壘就叫大衛城。 8大衛又從米羅開始,在四圍修建城牆,其餘的部分由約押修建。 9大衛日漸強盛,因為萬軍之耶和華與他同在。

大衛的勇士

10以下是大衛手下眾勇士的統領,他們和以色列百姓竭力擁護大衛做王,正如耶和華對以色列的應許。 11大衛的勇士有哈革摩尼雅朔班,他是三勇士之首,曾在一次交戰中揮矛刺死了三百人。 12其次是亞合朵多的兒子以利亞撒,他是三勇士之一。 13他曾在巴斯·達閔大衛一起抵抗非利士人。那裡有一塊大麥田,以色列人戰敗逃跑, 14他們卻堅守陣地,奮勇殺敵。耶和華使以色列人大獲全勝。 15一次,三十位勇士中有三位到亞杜蘭洞附近的磐石那裡見大衛,當時非利士的軍隊駐紮在利乏音谷。 16那時大衛留守在堡壘裡,非利士人的駐軍在伯利恆17大衛渴了,說:「真想有人打一些伯利恆城門旁的井水給我喝!」 18那三位勇士就衝過非利士人的營地,到伯利恆城門旁的井打水,帶回來給大衛大衛卻不肯喝,他把水澆奠在耶和華面前, 19說:「我的上帝啊!這三人冒死去打水,這些水就像是他們的血,我決不能喝。」因此,大衛不肯喝。這是三勇士的事蹟。

20約押的兄弟亞比篩是這三個勇士的統領,他曾揮矛刺死三百人,在三勇士中出了名, 21最有聲望,因此做了他們的統領,只是不及前三位勇士。

22甲薛耶何耶大的兒子比拿雅是位勇士,做過非凡的事。他曾殺死摩押的兩個勇猛戰士,也曾在下雪天跳進坑中殺死一頭獅子, 23還曾殺死一個兩米多高的埃及巨人。當時埃及人拿著織布機軸般粗的長矛,比拿雅只拿著棍子迎戰,他奪了對方的長矛,用那矛刺死了對方。 24這是耶何耶大的兒子比拿雅的事蹟,他在這三個勇士中出了名, 25比那三十個勇士更有聲望,只是不及前三位勇士。大衛派他做護衛長。

26其他勇士有約押的兄弟亞撒黑伯利恆朵多的兒子伊勒哈難27哈律沙瑪比倫希利斯28提哥亞益吉的兒子以拉亞拿突亞比以謝29戶沙西比該亞合以萊30尼陀法瑪哈萊尼陀法巴拿的兒子希立31便雅憫支派基比亞利拜的兒子以太比拉頓比拿雅32迦實溪戶萊亞拉巴亞比33巴路米押斯瑪弗沙本以利雅哈巴34基孫哈深的眾子、哈拉沙基的兒子約拿單35哈拉沙甲的兒子亞希暗吾珥的兒子以利法勒36米基拉希弗比倫亞希雅37迦密希斯羅伊斯拜的兒子拿萊38拿單的兄弟約珥哈基利的兒子彌伯哈39亞捫洗勒、為洗魯雅的兒子約押拿兵器的比錄拿哈萊40以帖以拉以帖迦立41烏利亞亞萊的兒子撒拔42示撒的兒子亞第拿——呂便支派中率領三十人的首領、 43瑪迦的兒子哈難彌特尼約沙法44亞施他拉烏西亞亞羅珥何坦的兒子沙瑪耶利45提洗申利的兒子耶疊和他的兄弟約哈46瑪哈未以利業伊利拿安的兒子耶利拜約沙未雅摩押伊特瑪47以利業俄備得米瑣巴雅西業