مزمور 79 – NAV & NEN

Ketab El Hayat

مزمور 79:1-13

الْمَزْمُورُ التَّاسِعُ وَالسَّبْعُونَ

مَزْمُورٌ لآسَافَ

1يَا اللهُ، إِنَّ الأُمَمَ قَدْ دَخَلَتْ مِيرَاثَكَ وَنَجَّسَتْ هَيْكَلَكَ الْمُقَدَّسَ وَجَعَلَتْ أُورُشَلِيمَ أَكْوَاماً. 2جَعَلُوا جُثَثَ عَبِيدِكَ مَأْكَلاً لِطُيُورِ السَّمَاءِ، وَلُحُومَ قِدِّيسِيكَ لِوُحُوشِ الأَرْضِ. 3سَفَكُوا دِمَاءَهُمْ كَالْمَاءِ حَوْلَ أُورُشَلِيمَ، وَلَيْسَ هُنَاكَ مَنْ يَدْفِنُهُمْ. 4قَدْ صِرْنَا عَاراً عِنْدَ جِيرَانِنَا، وَمَثَارَ هُزْءٍ وَأُضْحُوكَةً لِمَنْ حَوْلَنَا. 5إِلَى مَتَى يَدُومُ هَذَا يَا رَبُّ؟ أَتَبْقَى غَاضِباً تَتَّقِدُ غَيْرَتُكَ كَالنَّارِ إِلَى الأَبَدِ؟ 6صُبَّ غَضَبَكَ عَلَى الأُمَمِ الَّذِينَ لَمْ يَعْرِفُوكَ، وَعَلَى الْمَمَالِكِ الَّتِي لَمْ تَدْعُ بِاسْمِكَ، 7فَإِنَّهُمْ قَدِ افْتَرَسُوا يَعْقُوبَ وَقَوَّضُوا مَسْكَنَهُ.

8لَا تَذْكُرْ عَلَيْنَا آثَامَ أَجْدَادِنَا، بَلْ دَعْ مَرَاحِمَكَ تُوَافِينَا سَرِيعاً، لأَنَّنَا قَدْ تَذَلَّلْنَا جِدّاً. 9أَغِثْنَا أَيُّهَا الإِلَهُ مُخَلِّصُنَا مِنْ أَجْلِ مَجْدِكَ. أَنْقِذْنَا وَاغْفِرْ لَنَا خَطَايَانَا مِنْ أَجْلِ اسْمِكَ. 10لِمَاذَا تَسْأَلُنَا الأُمَمُ: أَيْنَ إِلَهُكُمْ؟ دَعْنَا نَرَى كَيْفَ يَذِيعُ بَيْنَ الأُمَمِ خَبَرُ انْتِقَامِكَ لِدِمَاءِ عَبِيدِكَ الْمَسْفُوكَةِ. 11لِيَتَصَاعَدْ أَمَامَكَ أَنِينُ الْمَأْسُورِ. حَافِظْ بِعَظَمَةِ قُوَّتِكَ عَلَى الْمَحْكُومِ عَلَيْهِمْ بِالْمَوْتِ. 12رُدَّ يَا رَبُّ عَلَى الأُمَمِ سَبْعَ مَرَّاتٍ مَا عَيَّرُوكَ وَأَهَانُوكَ بِهِ، 13فَنَحْمَدَكَ نَحْنُ شَعْبَكَ وَغَنَمَ مَرْعَاكَ إِلَى الأَبَدِ وَنُذِيعَ تَسْبِيحَكَ مِنْ جِيلٍ إِلَى جِيلٍ.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 79:1-13

Zaburi 79

Maombi Kwa Ajili Ya Wokovu Wa Taifa

Zaburi ya Asafu.

179:1 Kut 34:9; Law 20:3; 2Fal 25:9; Neh 4:2; Isa 6:11; Yer 26:18Ee Mungu, mataifa yameuvamia urithi wako,

wamelinajisi Hekalu lako takatifu,

wameifanya Yerusalemu kuwa magofu.

279:2 Ufu 19:17-18; Kum 28:26; Yer 7:33Wametoa maiti za watumishi

kuwa chakula cha ndege wa angani

na nyama ya watakatifu wako

kwa wanyama wa nchi.

379:3 Ufu 11:9; Yer 25:33; 16:4Wamemwaga damu kama maji

kuzunguka Yerusalemu yote,

wala hakuna yeyote wa kuwazika.

479:4 Eze 5:14; Za 39:8; 44:13Tumekuwa kitu cha aibu kwa jirani zetu,

cha dharau na mzaha kwa wale wanaotuzunguka.

579:5 Za 74:10; 74:1; 85:5; Kum 29:20; Za 89:46; Sef 3:8; Eze 36:5Hata lini, Ee Bwana? Je, wewe utakasirika milele?

Wivu wako utawaka kama moto hadi lini?

679:6 Ufu 16:1; Za 2:5; 110:5; 14:4; 53:4; 147:20; 69:24; Yer 10:25; Isa 45:4Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali,

juu ya falme za hao wasioliitia jina lako,

779:7 Isa 9:12; Yer 10:25kwa maana wamemrarua Yakobo

na kuharibu nchi ya makao yake.

879:8 Mwa 9:25; Yer 44:21; Za 116:6; 142:6Usituhesabie dhambi za baba zetu,

huruma yako na itujie hima,

kwa maana tu wahitaji mno.

979:9 2Nya 14:11; 25:11; 31:3; Yer 14:7; Yos 7:9Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie,

kwa ajili ya utukufu wa jina lako;

tuokoe na kutusamehe dhambi zetu

kwa ajili ya jina lako.

1079:10 Za 42:3; 94:1; Ufu 6:10; Za 79:3Kwa nini mataifa waseme,

“Yuko wapi Mungu wenu?”

Mbele ya macho yetu,

dhihirisha kati ya mataifa

kwamba unalipiza kisasi damu iliyomwagwa

ya watumishi wako.

1179:11 Hes 14:17Kilio cha huzuni cha wafungwa kifike mbele zako;

kwa nguvu za mkono wako

hifadhi wale waliohukumiwa kufa.

1279:12 Isa 65:6; Yer 32:18; Mwa 4:15Walipize jirani zetu mara saba vifuani mwao

aibu walizovurumisha juu yako, Ee Bwana.

1379:13 Za 44:8; 74:1; Isa 43:21Ndipo sisi watu wako, kondoo wa malisho yako,

tutakusifu milele;

toka kizazi hadi kizazi

tutasimulia sifa zako.