مزمور 71 – NAV & NEN

Ketab El Hayat

مزمور 71:1-24

الْمَزْمُورُ الْحَادِي وَالسَّبْعُونَ

1يَا رَبُّ بِكَ احْتَمَيْتُ فَلَا تَدَعْنِي أَخْزَى إِلَى الأَبَدِ. 2أَنْقِذْنِي وَفْقاً لِعَدْلِكَ وَنَجِّنِي. أَرْهِفْ إِلَيَّ أُذُنَكَ وَخَلِّصْنِي. 3كُنْ لِي صَخْرَةَ مَلْجَأٍ أَلُوذُ بِها دَائِماً. أَنْتَ أَمَرْتَ بِخَلاصِي لأَنَّكَ صَخْرَتِي وَحِصْنِي. 4يَا إِلَهِي أَنْقِذْنِي مِنْ يَدِ الشِّرِّيرِ، مِنْ قَبْضَةِ الأَثِيمِ وَالظَّالِمِ. 5فَإِنَّكَ أَنْتَ رَجَائِي أَيُّهَا السَّيِّدُ، وَمَوْضِعُ ثِقَتِي مُنْذُ صِبَايَ. 6عَلَيْكَ اعْتَمَدْتُ مُنْذُ وِلادَتِي، وَمِنْ بَطْنِ أُمِّي أَخْرَجْتَنِي، فَإِيَّاكَ أُسَبِّحُ فِي كُلِّ حِينٍ. 7صِرْتُ مَثَارَ اسْتِهْجَانٍ عِنْدَ كَثِيرِينَ، لَكِنَّكَ أَنْتَ مَلْجَإِي الْقَوِيُّ. 8لِيَمْتَلِئْ فَمِي مِنْ تَسْبِيحِكَ وَمِنْ تَمْجِيدِكَ طُولَ النَّهَارِ.

9لَا تَنْبِذْنِي فِي شَيْخُوخَتِي، وَلَا تَخْذِلْنِي عِنْدَ اضْمِحْلالِ قُوَّتِي. 10لأَنَّ أَعْدَائِي يَتَكَلَّمُونَ عَلَيَّ وَالْمُتَرَبِّصِينَ بِي يَتَآمَرُونَ مَعاً. 11قَائِلِينَ: «قَدْ تَرَكَهُ اللهُ، فَطَارِدُوهُ وَاقْبِضُوا عَلَيْهِ لأَنَّهُ لَا مُنْقِذَ لَهُ». 12لَا تَبْتَعِدْ عَنِّي يَا اللهُ. أَسْرِعْ إِلَى مَعُونَتِي يَا إِلَهِي. 13لِيَخْزَ وَيَبِدْ خُصُومُ نَفْسِي. لِيَكْتَسِ الْعَارَ وَالْهَوَانَ الْمُلْتَمِسُونَ أَذِيَّتِي. 14أَمَّا أَنَا فَإِيَّاكَ أَرْجُو دَائِماً، وَأُكْثِرُ مِنْ تَسْبِيحِكَ. 15أُخْبِرُ بِبِرِّكَ وَخَلاصِكَ طُولَ النَّهَارِ، وَإِنْ كَانَا يَفُوقَانِ إِدْرَاكِي. 16أَجِيءُ (مُؤَيَّداً) بِقُوَّةِ السَّيِّدِ الرَّبِّ، لأَذْكُرَ بِرَّكَ وَحْدَكَ.

17قَدْ عَلَّمْتَنِي يَا اللهُ مُنْذُ صِبَايَ، فَلَمْ أَكُفَّ لَحْظَةً عَنْ إِعْلانِ عَجَائِبِكَ. 18لَا تَتْرُكْنِي فِي الشَّيْخُوخَةِ وَالشَّيْبِ يَا اللهُ، حَتَّى أُخْبِرَ هَذَا الْجِيلَ بِأَعْمَالِ قُدْرَتِكَ، وَبِقُوَّتِكَ (الْجِيلَ) الآتِي. 19بِرُّكَ مُتَعَالٍ يَا اللهُ، وَأَعْمَالُكَ الَّتِي صَنَعْتَ عَظِيمَةٌ، فَمَنْ مِثْلُكَ يَا اللهُ! 20أَنْتَ الَّذِي اجْتَزْتَ بِنَا ضِيقَاتٍ كَثِيرَةً وَقَاسِيَةً، وَلَكِنَّكَ تَعُودُ فَتُحْيِينَا، وَتُصْعِدُنَا مِنْ جَدِيدٍ مِنْ أَعْمَاقِ الأَرْضِ. 21تَزِيدُنِي شَرَفاً وَتُطَوِّقُنِي بِتَعْزِيَتِكَ. 22سَأَحْمَدُكَ وَأُشِيدُ بِحَقِّكَ عَلَى الرَّبَابِ يَا إِلَهِي. أَشْدُو لَكَ عَلَى الْعُودِ يَا قُدُّوسَ إِسْرَائِيلَ. 23تَبْتَهِجُ شَفَتَايَ عِنْدَمَا أُرَنِّمُ لَكَ، وَكَذَلِكَ نَفْسِي الَّتِي فَدَيْتَهَا. 24وَيَلْهَجُ لِسَانِي بِبِرِّكَ الْيَوْمَ كُلَّهُ، لأَنَّ السَّاعِينَ إِلَى أَذِيَّتِي يَحِلُّ حَتْماً بِهِمِ الْخِزْيُ وَالْعَارُ.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 71:1-24

Zaburi 71

Kuomba Ulinzi Na Msaada Siku Zote Za Maisha

171:1 Kum 23:15; Rut 2:12; Za 22:5Ee Bwana, nimekukimbilia wewe,

usiache nikaaibika kamwe.

271:2 2Fal 19:1671:2 Kut 34:6Kwa haki yako uniponye na kuniokoa,

unitegee sikio lako uniokoe.

371:3 Za 18:2Uwe kwangu mwamba wa kimbilio,

mahali nitakapokimbilia kila wakati;

toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe

ni mwamba wangu na ngome yangu.

471:4 2Fal 19:19; Za 140:4; Mwa 48:16Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu,

kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.

571:5 Za 9:18; 25:5; Ay 4:6; Yer 17:7Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi,

tegemeo langu tangu ujana wangu.

671:6 Ay 3:16; Za 9:1; 22:9; 34:1; 52:9; 119:164; 145:2Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,

ulinitoa tumboni mwa mama yangu.

Nitakusifu wewe daima.

771:7 Kum 28:46; 1Kor 4:9; Za 61:3; 2Sam 22:3Nimekuwa kama kioja kwa wengi,

lakini wewe ni kimbilio langu imara.

871:8 Za 71:15; 51:15; 63:5; 96:6; 104:1Kinywa changu kimejazwa sifa zako,

nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.

971:9 Za 51:11; 92:14; Kum 4:31; 31:6Usinitupe wakati wa uzee,

wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

1071:10 Za 3:7; 10:8; 59:3; 31:13; Mt 1:10; 12:14Kwa maana adui zangu wananisengenya,

wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.

1171:11 Isa 40:27; 54:7; Mt 27:46; Za 7:2; 9:10; Mao 5:20Wanasema, “Mungu amemwacha,

mkimbilieni mkamkamate,

kwani hakuna wa kumwokoa.”

1271:12 Za 38:21, 22; 22:19Ee Mungu, usiwe mbali nami,

njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.

1371:13 Ay 8:22; Za 15:3; 70:2; Yer 18:19Washtaki wangu na waangamie kwa aibu,

wale wanaotaka kunidhuru

na wafunikwe kwa dharau na fedheha.

1471:14 Za 25:3; 42:5; 130:7; 131:3Lakini mimi, nitatumaini siku zote,

nitakusifu zaidi na zaidi.

1571:15 Za 71:8; 66:6; 51:14Kinywa changu kitasimulia haki yako,

wokovu wako mchana kutwa,

ingawa sifahamu kipimo chake.

1671:16 Za 77:12; 106:2; 118:15; 9:1; 145:4Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja

na kutangaza matendo yako makuu,

nitatangaza haki yako, yako peke yako.

1771:17 Yer 7:13; Ay 5:9; Za 26:7; 86:10; 96:3; Kum 4:5Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,

hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.

1871:18 Isa 46:4; Kut 9:16; Ay 8:8; Yoe 1:3; Za 78:4; 145:4; 22:30, 31Ee Mungu, usiniache,

hata niwapo mzee wa mvi,

mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho,

nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.

1971:19 Lk 1:49; Za 36:5; 35:10; 77:13; 89:8; 126:2Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu,

wewe ambaye umefanya mambo makuu.

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?

2071:20 Za 80:3, 19; 25:17; 85:4; 63:9; Hos 6:2Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu,

utanihuisha tena,

kutoka vilindi vya dunia

utaniinua tena.

2171:21 Za 18:35; 86:17; Isa 12:1; 40:1, 2; 49:13; 54:10Utaongeza heshima yangu

na kunifariji tena.

2271:22 Za 33:2; 92:3; 144:9; Ay 21:12; 2Fal 19:22Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi

kwa ajili ya uaminifu wako;

Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli,

nitakuimbia sifa kwa zeze.

2371:23 Za 20:5; Kut 15:13Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha

ninapokuimbia sifa,

mimi, ambaye umenikomboa.

2471:24 Za 35:28; Es 9:2Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki

mchana kutwa,

kwa maana wale waliotaka kunidhuru,

wameaibishwa na kufadhaishwa.