مزمور 63 – NAV & NEN

Ketab El Hayat

مزمور 63:1-11

الْمَزْمُورُ الثَّالِثُ وَالسِّتُّونَ

مَزْمُورٌ لِدَاوُدَ عِنْدَمَا كَانَ فِي بَرِّيَّةِ يَهُوذَا

1يَا اللهُ أَنْتَ إِلَهِي وَإِيَّاكَ أَطْلُبُ بَاكِراً. عَطِشَتْ إِلَيْكَ نَفْسِي وَيَشْتَاقُ إِلَيْكَ جِسْمِي فِي أَرْضٍ قَاحِلَةٍ يَابِسَةٍ لَا مَاءَ فِيهَا، 2حَتَّى أُعَايِنَ قُدْرَتَكَ وَمَجْدَكَ، مِثْلَمَا رَأَيْتُكَ فِي مَوْضِعِكَ الْمُقَدَّسِ. 3لأَنَّ رَحْمَتَكَ خَيْرٌ مِنَ الْحَيَاةِ، لِذَلِكَ تُسَبِّحُكَ شَفَتَايَ. 4أَحْمَدُكَ عَلَى بَرَكَاتِكَ مَدَى حَيَاتِي، وَبِاسْمِكَ أَرْفَعُ يَدَيَّ مُبْتَهِلاً. 5تَشْبَعُ نَفْسِي كَأَنَّهَا أَكَلَتْ مِنَ الشَّحْمِ وَالدَّسَمِ، وَيُسَبِّحُكَ فَمِي بِشَفَتَيْنِ مُبْتَهِجَتَيْنِ 6أَذْكُرُكَ عَلَى فِرَاشِي وَأَتَأَمَّلُ فِيكَ فِي أَثْنَاءِ اللَّيْلِ. 7لأَنَّكَ كُنْتَ عَوْناً لِي، فَإِنِّي فِي ظِلِّ جَنَاحَيْكَ أُرَنِّمُ مُبْتَهِجاً.

8تَتَعَلَّقُ نَفْسِي بِكَ. يَمِينُكَ تَدْعَمُنِي 9أَمَّا طَالِبُو نَفْسِي لِيُهْلِكُوهَا فَسَيَدْخُلُونَ أَسْفَلَ أَعْمَاقِ الأَرْضِ. 10يُسَلَّمُونَ إِلَى حَدِّ السَّيْفِ وَيَضْحَوْنَ مَأْكَلاً لِبَنَاتِ آوَى. 11أَمَّا الْمَلِكُ فَيَفْرَحُ بِاللهِ وَيَفْتَخِرُ بِهِ كُلُّ مَنْ يُقْسِمُ (صَادِقاً) لأَنَّ أَفْوَاهَ النَّاطِقِينَ بِالْكَذِبِ تُسَدُّ.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 63:1-11

Zaburi 63

Shauku Kwa Ajili Ya Uwepo Wa Mungu

Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda.

163:1 Za 42:2; 84:2; 143:6Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu,

nakutafuta kwa moyo wote;

nafsi yangu inakuonea kiu,

mwili wangu unakuonea wewe shauku,

katika nchi kame na iliyochoka

mahali ambapo hapana maji.

263:2 Za 15:1; 27:4; 68:24; Kut 16:7; 1Nya 16:11Nimekuona katika mahali patakatifu

na kuuona uwezo wako na utukufu wako.

363:3 Isa 30:13; Yn 3:16; Za 36:7; 69:16; 106:45; 109:21Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,

midomo yangu itakuadhimisha.

463:4 Za 28:3; 104:33; 146:2; Isa 38:20; 1Tim 2:8Nitakusifu siku zote za maisha yangu,

na kwa jina lako nitainua mikono yangu.

563:5 Za 17:15; 36:8; Mt 5:6; Isa 25:6Nafsi yangu itatoshelezwa

kama kwa wingi wa vyakula;

kwa midomo iimbayo

kinywa changu kitakusifu wewe.

663:6 Kum 6:4-9; Za 119:148; 16:7; 140:5; Mt 14:25Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe,

ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.

763:7 Za 27:9; 118:7; Rum 2:12; Isa 26:9Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu,

chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.

863:8 Hes 32:12; Hos 6:3; Isa 26:9; Za 41:12Nafsi yangu inaambatana nawe,

mkono wako wa kuume hunishika.

963:9 Za 40:14; 55:15; 71:20; 95:4; 139:15Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa,

watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.

1063:10 Yer 18:21; Eze 35:5; Amo 1:11; Mao 5:18Watatolewa wafe kwa upanga,

nao watakuwa chakula cha mbweha.

1163:11 Sef 1:5; Isa 19:18; 45:23; 65:16; Ay 5:16; Rum 3:19Bali mfalme atafurahi katika Mungu,

wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu,

bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.