إشعياء 13 – NAV & NEN

Ketab El Hayat

إشعياء 13:1-22

نبوءة ضد بابل

1رُؤْيَا إِشَعْيَاءَ بْنِ آمُوصَ بِشَأْنِ بَابِلَ:

2انْصُبُوا رَايَةً فَوْقَ جَبَلٍ أَجْرَدَ. اصْرُخُوا فِيهِمْ. لَوِّحُوا بِأَيْدِيكُمْ حَتَّى يَدْخُلُوا أَبْوَابَ الْعُظَمَاءِ. 3إِنِّي أَمَرْتُ مُقَدَّسِيَّ وَاسْتَدْعَيْتُ جَبَابِرَتِي الْمُفْتَخِرِينَ بِعَظَمَتِي لِيُنَفِّذُوا عِقَابَ غَضَبِي. 4هَا جَلَبَةٌ عَلَى الْجِبَالِ مِثْلُ صَوْتِ أَقْوَامٍ غَفِيرَةٍ. صَوْتُ صَخَبِ مَمَالِكِ أُمَمٍ مُجْتَمِعَةٍ، لأَنَّ الرَّبَّ الْقَدِيرَ يَسْتَعْرِضُ جُنُودَ الْقِتَالِ. 5يُقْبِلُونَ مِنْ أَرْضٍ نَائِيَةٍ، مِنْ أَقْصَى السَّمَاوَاتِ. هُمْ جُنُودُ الرَّبِّ وَأَسْلِحَةُ سَخَطِهِ لِتَدْمِيرِ الأَرْضِ كُلِّهَا.

6وَلْوِلُوا، فَإِنَّ يَوْمَ الرَّبِّ بَاتَ وَشِيكاً قَادِماً مِنْ عِنْدِ الرَّبِّ مُحَمَّلاً بِالدَّمَارِ. 7لِذَلِكَ تَرْتَخِي كُلُّ يَدٍ، وَيَذُوبُ قَلْبُ كُلِّ إِنْسَانٍ. 8يَنْتَابُهُمُ الْفَزَعُ، وَتَأْخُذُهُمْ أَوْجَاعٌ وَمَخَاضٌ، يَتَلَوَّوْنَ كَوَالِدَةٍ تُقَاسِي مِنْ آلامِ الْمَخَاضِ. وَيُحَمْلِقُ بَعْضُهُمْ بِبَعْضٍ مَبْهُوتِينَ بِوُجُوهٍ مُلْتَهِبَةٍ.

9هَا هُوَ يَوْمُ الرَّبِّ آتٍ مُفْعَماً بِالْقَسْوَةِ وَالسَّخَطِ وَالْغَضَبِ الْعَنِيفِ، لِيَجْعَلَ الأَرْضَ خَرَاباً وَيُبِيدَ مِنْهَا الْخُطَاةَ. 10فَإِنَّ نُجُومَ السَّمَاءِ وَكَوَاكِبَهَا لَا تُشْرِقُ بِنُورِهَا، وَالشَّمْسَ تُظْلِمُ عِنْدَ بُزُوغِهَا، وَالْقَمَرَ لَا يُشِعُّ بِضَوْئِهِ. 11وَأُعَاقِبُ الْعَالَمَ عَلَى شَرِّهِ وَالْمُنَافِقِينَ عَلَى آثَامِهِمْ، وَأَضَعُ حَدّاً لِصَلَفِ الْمُتَغَطْرِسِينَ وَأُذِلُّ كِبْرِيَاءَ الْعُتَاةِ، 12فَيُصْبِحُ الرِّجَالُ لِقِلَّةِ عَدَدِهِمْ أَنْدَرَ مِنَ الذَّهَبِ النَّقِيِّ وَأَعَزَّ مِنْ ذَهَبِ أُوفِيرَ. 13وَأُزَلْزِلُ السَّمَاوَاتِ فَتَتَزَعْزَعُ الأَرْضُ فِي مَوْضِعِهَا مِنْ غَضَبِ الرَّبِّ الْقَدِيرِ فِي يَوْمِ احْتِدَامِ سَخَطِهِ. 14وَتُوَلِّي جُيُوشُ بَابِلَ الأَدْبَارَ حَتَّى يَنْهَكَهَا التَّعَبُ، عَائِدِينَ إِلَى أَرْضِهِمْ كَأَنَّهُمْ غَزَالٌ مُطَارَدٌ أَوْ غَنَمٌ لَا رَاعِيَ لَهَا. 15كُلُّ مَنْ يُؤْسَرْ يُطْعَنْ، وَمَنْ يُقْبَضْ عَلَيْهِ يُصْرَعْ بِالسَّيْفِ، 16وَيُمَزَّقْ أَطْفَالُهُمْ عَلَى مَرْأىً مِنْهُمْ، وَتُنْهَبْ بُيُوتُهُمْ، وَتُغْتَصَبْ نِسَاؤُهُمْ.

17هَا أَنَا أُثِيرُ عَلَيْهِمِ الْمَادِيِّينَ الَّذِينَ لَا يَكْتَرِثُونَ لِلْفِضَّةِ وَلا يُسَرُّونَ بِالذَّهَبِ، 18تُمَزِّقُ قِسِيُّهُمُ الْفِتْيَانَ وَلا يَرْحَمُونَ الأَوْلادَ أَوِ الرُّضَّعَ. 19أَمَّا بَابِلُ، مَجْدُ الْمَمَالِكِ وَبَهَاءُ وَفَخْرُ الْكَلْدَانِيِّينَ، فَتُصْبِحُ كَسَدُومَ وَعَمُورَةَ اللَّتَيْنِ قَلَبَهُمَا اللهُ. 20لَا يُسْكَنُ فِيهَا، وَلا تُعْمَرُ مِنْ جِيلٍ إِلَى جِيلٍ، لَا يَنْصِبُ فِيهَا بَدَوِيٌّ خَيْمَتَهُ، وَلا يُرْبِضُ فِيهَا رَاعٍ قُطْعَانَهُ. 21إِنَّمَا تَأْوِي إِلَيْهَا وُحُوشُ الْقَفْرِ وَتَعِجُّ بُيُوتُ خَرَائِبِهَا بِالْبُومِ، وَتَلْجَأُ إِلَيْهَا بَنَاتُ النَّعَامِ، وَتَتَوَاثَبُ فِيهَا الْمَاعِزُ الْبَرِّيَّةُ، 22وَتَتَعَاوَى الضِّبَاعُ بَيْنَ أَبْرَاجِهَا، وَبَنَاتُ آوَى بَيْنَ قُصُورِهَا الْفَخْمَةِ. إِنَّ وَقْتَ عِقَابِهَا بَاتَ وَشِيكاً، وَأَيَّامَهَا لَنْ تَطُولَ!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 13:1-22

Unabii Dhidi Ya Babeli

113:1 Isa 14:28; 21:9; 48:14; Ufu 14:8; Mwa 10:10; Mal 1:1; Isa 14:4; 46:1-2Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:

213:2 Za 20:5; 50:2; Yer 51:27; 51:58; 50:2; Isa 24:12; 45:2; 24:2Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu,

wapazieni sauti,

wapungieni mkono waingie

katika malango ya wenye heshima.

313:3 Yer 51:11; Yoe 3:11; Za 149:2; Isa 21:2; Kum 5:28; Ay 40:11Nimewaamuru watakatifu wangu;

nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu:

wale wanaoshangilia ushindi wangu.

413:4 Yoe 3:14; Za 46:6; Isa 42:13; 47:4; Yer 50:41Sikilizeni kelele juu ya milima,

kama ile ya umati mkubwa wa watu!

Sikilizeni, makelele katikati ya falme,

kama mataifa yanayokusanyika pamoja!

Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya

jeshi kwa ajili ya vita.

513:5 Yos 6:17; Isa 5:26; 34:2; 54:16; 10:25; 34:2; Yer 50:25Wanakuja kutoka nchi za mbali sana,

kutoka miisho ya mbingu,

Bwana na silaha za ghadhabu yake,

kuangamiza nchi yote.

613:6 Amo 5:18; Eze 30:2; Yak 5:1; Isa 2:12; 14:31; 10:3; 15:2Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu,

itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.13:6 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania.

713:7 Eze 21:7; Yos 2:11; 2Fal 19:26; Ay 4:3; Yer 47:3Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea,

moyo wa kila mtu utayeyuka.

813:8 Nah 2:10; Yoe 2:6; Za 31:13; Isa 21:4; Za 48:5; Kut 15:14; Mwa 3:16; Yn 16:21Hofu itawakamata,

uchungu na maumivu makali yatawashika,

watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa.

Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake,

nyuso zao zikiwaka kama moto.

913:9 Isa 2:12; Yer 6:23; 51:2; Isa 9:19; 66:16; Yer 25:31; Yoe 3:2Tazameni, siku ya Bwana inakuja,

siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali,

kuifanya nchi kuwa ukiwa

na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.

1013:10 Kut 10:22; Ufu 8:12; Amo 5:20; Zek 14:7; Ay 9:7; Mt 24:29; Isa 5:30; 24:23Nyota za mbinguni na makundi ya nyota

havitatoa mwanga wake.

Jua linalochomoza litatiwa giza

na mwezi hautatoa nuru yake.

1113:11 Isa 3:11; 26:21; 65:6-7; 49:25-26; Za 125:3; Mit 16:18; Dan 5:23; 4:37; Eze 28:2Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake,

waovu kwa ajili ya dhambi zao.

Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi,

na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.

1213:12 Isa 4:1; Mwa 10:29Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi,

watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.

1313:13 Hag 2:6; Za 102:26; Isa 9:19; 14:16; 34:4; Mt 24:7; Ay 9:5; 9:6; Mk 13:8Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke,

nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake

katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote,

katika siku ya hasira yake iwakayo.

1413:14 Nah 3:7; Yn 10:11; Yer 51:9; 46:16; 4:9; Mit 6:5; Isa 17:13; 21:15; 33:3; Mt 9:36Kama swala awindwaye,

kama kondoo wasio na mchungaji,

kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.

1513:15 Yer 50:25; 51:4; Isa 14:19Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo,

wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.

1613:16 Nah 3:10; Hes 16:27; 13:16; Mwa 34:29; 2Fal 8:12Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande

mbele ya macho yao;

nyumba zao zitatekwa

na wake zao watatendwa jeuri.

1713:17 2Fal 18:14-16; Mit 19:24-25; Yer 51:11; 50:9, 41Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao,

ambao hawajali fedha

wala hawafurahii dhahabu.

1813:18 Za 7:12; Isa 41:2; Yer 49:26Mishale yao itawaangusha vijana,

hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga

wala hawataangalia watoto kwa huruma.

1913:19 Dan 4:30; Za 137:8; Ufu 14:8; Mwa 19:24-25; Rum 9:29; Isa 47:5; Dan 2:37-38Babeli, johari ya falme,

utukufu wa kiburi cha Wababeli,13:19 Wababeli hapa maana yake ni Wakaldayo.

itaangushwa na Mungu

kama Sodoma na Gomora.

2013:20 Isa 14:23; 34:10-15; 2Nya 17:11; Yer 51:29, 37-43, 62Hautakaliwa na watu kamwe

wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote.

Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko,

hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.

2113:21 Za 74:14; Ufu 18:2; Yer 14:6; Law 11:16-18; Kum 14:15-17; 2Nya 11:15Lakini viumbe wa jangwani watalala huko,

mbweha watajaza nyumba zake,

bundi wataishi humo

nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.

2213:22 Isa 34:14; Kum 32:25; Yer 48:16; 9:11; Isa 25:2; 32:14; Yer 50:39; Mal 1:3Fisi watalia ndani ya ngome zake,

mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari.

Wakati wake umewadia,

na siku zake hazitaongezwa.