ኤርምያስ 51 – NASV & NEN

New Amharic Standard Version

ኤርምያስ 51:1-64

1እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤

“እነሆ፤ በባቢሎንና51፥1 ሌብ ካማይ የከላውዴዎን ማለትም የባቢሎን ስም ነው። በምድሯ ላይ፣

የሚያጠፋ ነፋስ አስነሣለሁ።

2እንዲያበጥሯትና እንዲያወድሟት፣

ባዕዳንን በባቢሎን ላይ እልካለሁ፤

በመከራዋም ቀን፣

ከብበው ያስጨንቋታል።

3ቀስተኛው ቀስቱን እስኪገትር፣

የጦር ልብሱንም እስኪለብስ ፋታ አትስጡት፤

ለወጣቶቿ አትዘኑ፤

ሰራዊቷንም ፈጽማችሁ አጥፉ።51፥3 አጥፉ ለሚለው የዕብራይስጡ ቃል የሚያመለክተው ነገሮችን ወይም ሰዎችን ዳግም ላይመለሱ ለእግዚአብሔር ሙሉ በሙሉ መስጠት ነው።

4በባቢሎን51፥4 ወይም ከላውዴዎን ምድር ታርደው፣

በአደባባዮቿም እስከ ሞት ቈስለው ይወድቃሉ።

5ምድራቸው51፥5 ወይም የባቢሎናውያን ምድር በእስራኤል ቅዱስ ፊት፣

በበደል የተሞላች ብትሆንም፣

እስራኤልንና ይሁዳን አምላካቸው

የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር አልጣላቸውም።

6“ከባቢሎን ሸሽታችሁ ውጡ!

ፈጥናችሁም ሕይወታችሁን አትርፉ!

በኀጢአቷ ምክንያት አትጥፉ።

የእግዚአብሔር የበቀል ጊዜ ነው፤

እርሱም የሥራዋን ይከፍላታል።

7ባቢሎን በእግዚአብሔር እጅ የወርቅ ጽዋ ነበረች፤

ምድርንም ሁሉ አሰከረች።

ሕዝቦች ከወይን ጠጇ ጠጡ፤

ስለዚህ አሁን አብደዋል።

8ባቢሎን በድንገት ወድቃ ትሰበራለች፤

ዋይ በሉላት!

ምናልባት ልትፈወስ ስለምትችል፣

ለቍስሏ የሚቀባ መድኀኒት ፈልጉላት።

9“ ‘ባቢሎንን ለመፈወስ ሞክረን ነበር፤

እርሷ ግን ልትፈወስ አትችልም፤

ፍርዷ እስከ ሰማይ ስለ ደረሰ፣

እስከ ደመናም ድረስ ከፍ ስላለ፣

ትተናት ወደየአገራችን እንሂድ።’

10“ ‘እግዚአብሔር ቅንነታችንን መሰከረ፤

ኑ፤ አምላካችን እግዚአብሔር ያደረገውን፣

በጽዮን እንናገር።’

11“ፍላጾችን ሳሉ፤

ጋሻዎችን አዘጋጁ፤

የእግዚአብሔር ሐሳብ ባቢሎንን ለማጥፋት ስለሆነ፣

የሜዶንን ነገሥታት አነሣሥቷል፤

እግዚአብሔር ይበቀላል፤

ስለ ቤተ መቅደሱ ይበቀላል።

12በባቢሎን ቅጥር ላይ ዐላማ አንሡ

ጥበቃውን አጠናክሩ፤

ዘብ ጠባቂዎችን አቁሙ፤

ደፈጣ ተዋጊዎችን አዘጋጁ

እግዚአብሔር በባቢሎን ሕዝብ ላይ የወሰነውን፣

ዐላማውን ያከናውናል።

13አንቺ በብዙ ውሃ አጠገብ የምትኖሪ፣

በሀብትም የበለጸግሽ ሆይ፤

የምትወገጂበት ጊዜ ወጥቷል፤

ፍጻሜሽ ደርሷል።

14የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር እንዲህ ሲል በራሱ ምሏል፤

ብዛቱ እንደ አንበጣ መንጋ የሆነ ሰራዊት ያጥለቀልቅሻል፤

እነርሱም በድል አድራጊነት በላይሽ ያቅራራሉ።

15“ምድርን በኀይሉ የሠራ፣

ዓለምን በጥበቡ የመሠረተ፣

ሰማያትንም በማስተዋሉ የዘረጋ እርሱ ነው።

16ድምፁን ባንጐደጐደ ጊዜ በሰማይ ውሆች ይናወጣሉ፤

ጉሙን ከምድር ዳርቻ ወደ ላይ እንዲወጣ ያደርገዋል፤

መብረቅን ከዝናብ ጋር ይልካል፤

ነፋስንም ከግምጃ ቤቱ ያወጣል።

17“እያንዳንዱ ሰው ጅልና ዕውቀት የለሽ ነው፤

የወርቅ አንጥረኛው ሁሉ በሠራው በጣዖቱ ዐፍሯል፤

የቀረጻቸው ምስሎቹ የሐሰት ናቸው፤

እስትንፋስ የላቸውም።

18እነርሱ ከንቱ የፌዝ ዕቃዎች ናቸው፣

ፍርድ ሲመጣባቸው ይጠፋሉ።

19የያዕቆብ ዕድል ፈንታ የሆነው ግን እንደ እነዚህ አይደለም፤

እርሱ የሁሉ ነገር ፈጣሪ ነውና፤

እስራኤልም የርስቱ ነገድ ነው።

ስሙ የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር ነው።

20“አንቺ የእኔ ቈመጥ፣

የጦር መሣሪያዬ ነሽ፤

በአንቺ ሕዝቦችን እሰባብራለሁ፤

በአንቺ መንግሥታትን አጠፋለሁ፤

21በአንቺ ፈረሱንና ፈረሰኛውን እሰባብራለሁ፤

በአንቺ ሠረገላውንና ሠረገላ ነጂውን እሰባብራለሁ፤

22በአንቺ ወንዱንና ሴቱን እሰባብራለሁ፤

በአንቺ ሽማግሌውንና ወጣቱን እሰባብራለሁ።

በአንቺ ጐረምሳውንና ኰረዳዪቱን እሰባብራለሁ።

23በአንቺ እረኛውንና መንጋውን እሰባብራለሁ፣

በአንቺ ገበሬውንና በሬውን እሰባብራለሁ፤

በአንቺ ገዦችንና ባለሥልጣኖችን እሰባብራለሁ።

24“በጽዮን ላይ ስላደረሱት ጥፋት ሁሉ ለባቢሎንና በባቢሎን51፥24 ወይም ከላውዴዎን፤ 35 ይመ። ለሚኖሩት ሁሉ ዐይናችሁ እያየ ዋጋቸውን እከፍላቸዋለሁ” ይላል እግዚአብሔር

25“አንቺ ምድርን ሁሉ ያጠፋሽ፣

አጥፊ ተራራ ሆይ፤ እኔ በአንቺ ላይ ነኝ፣”

ይላል እግዚአብሔር

“እጄን በአንቺ ላይ አነሣለሁ፤

ከገመገም ቍልቍል አንከባልልሻለሁ፤

የተቃጠለም ተራራ አደርግሻለሁ።

26ከአንቺ ለማእዘን የሚሆን ድንጋይ፣

ለመሠረትም የሚሆን ዐለት አይወሰድም፤

ለዘላለም ባድማ ትሆኛለሽ፤”

ይላል እግዚአብሔር

27“በምድር ሁሉ ላይ ሰንደቅ ዐላማ አንሡ!

በሕዝቦች መካከል መለከትን ንፉ!

ሕዝቦችን ለጦርነት በእርሷ ላይ አዘጋጁ፤

የአራራትን፣ የሚኒንና የአስከናዝን መንግሥታት፣

ጠርታችሁ በእርሷ ሰብስቧቸው፤

የጦር አዝማች ሹሙባት፤

ፈረሶችንም እንደ አንበጣ መንጋ ስደዱባት።

28የሜዶንን ነገሥታት፣

ገዦቿንና ባለሥልጣኖቿን ሁሉ፣

በግዛታቸው ሥር ያሉትን አገሮች ሁሉ፣

እነዚህን ሕዝቦች ለጦርነት አዘጋጁባት።

29ሰው በዚያ መኖር እስከማይችል ድረስ፣

የባቢሎንን ምድር ባድማ ለማድረግ፣

እግዚአብሔር በባቢሎን ላይ ያቀደው ስለሚጸና፣

ምድር ትናወጣለች፤ በሥቃይም ትወራጫለች።

30የባቢሎን ጦረኞች መዋጋት ትተዋል፤

በምሽጎቻቸው ውስጥ ተቀምጠዋል፤

ኀይላቸው ተሟጥጧል፤

እንደ ሴት ሆነዋል፤

በማደሪያዎቿም እሳት ተለኵሷል፤

የደጇም መወርወሪያ ተሰብሯል።

31ከተማዪቱ ሙሉ በሙሉ መያዟን፣

ለባቢሎን ንጉሥ ለመንገር፣

አንዱ ወሬኛ ሌላውን ወሬኛ፣

አንዱ መልእክተኛ ሌላውን መልእክተኛ ወዲያው ወዲያው ይከተላል፤

32መልካዎቿ እንደ ተያዙ፣

የወንዝ ዳር ምሽጎቿ እንደ ተቃጠሉ፣

ወታደሮቿም እንደ ተደናገጡ ሊነግሩት ይሯሯጣሉ።”

33የእስራኤል አምላክ የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤

“የባቢሎን ሴት ልጅ በመረገጥ ላይ እንዳለ፣

የእህል መውቂያ አውድማ ናት፤

የመከር ወራቷም ፈጥኖ ይደርስባታል።”

34“የባቢሎን ንጉሥ ናቡከደነፆር በላን፣

አድቅቆ ፈጨን፤

እንደ ባዶ ማድጋ አደረገን፤

እንደ ዘንዶ ዋጠን፣

እንደ ጣፋጭ በልቶን ሆዱን ሞላ፤

በኋላም አንቅሮ ተፋን፤

35የጽዮን ነዋሪዎች፣ እንዲህ ይላሉ፤

በሥጋችን51፥35 ወይም በእኛና በልጃችን ላይ የተፈጸመው ላይ የተፈጸመው ግፍ በባቢሎን ላይ ይሁን፤”

ኢየሩሳሌም እንዲህ ትላለች፤

“ደማችን በባቢሎን ምድር በሚኖሩት ላይ ይሁን።”

36ስለዚህ እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤

“እነሆ፤ እሟገትልሻለሁ፣

በቀልሽንም እኔ እበቀልልሻለሁ፤

ባሕሯን አደርቃለሁ፣

የምንጮቿንም ውሃ።

37ባቢሎን የፍርስራሽ ክምር፣

የቀበሮዎች መፈንጫ፣

የድንጋጤና የመሣለቂያ ምልክት ትሆናለች፤

የሚኖርባትም አይገኝም።

38ሕዝቦቿ ሁሉ እንደ ደቦል አንበሳ ያገሣሉ፤

እንደ አንበሳ ግልገልም ያጕረመርማሉ።

ጕረሯቸው በደረቀ ጊዜ

ድግስ አዘጋጅላቸዋለሁ፤

እንዲሰክሩም አደርጋቸውና

39በሣቅ እየፈነደቁ፣

ለዘላለም ላይነቁ ይተኛሉ።”

ይላል እግዚአብሔር

40“እንደ ጠቦት፣

እንደ አውራ በግና እንደ ፍየል፣

ወደ መታረድ አወርዳቸዋለሁ።

41“ሼሻክ51፥41 ሼሻክ የባቢሎን ስውር ስም ነው። እንዴት ተማረከች!

የምድር ሁሉ ትምክሕትስ እንዴት ተያዘች!

ባቢሎን በሕዝብ ሁሉ ዘንድ፣

ምንኛ አስደንጋጭ ሆነች።

42ባሕር በባቢሎን ላይ ይወጣል፤

ሞገዱም እየተመመ ይሸፍናታል።

43ከተሞቿ ሰው የማይኖርባቸው፣

ዝርም የማይልባቸው፣

ደረቅና በረሓማ ቦታ፣

ባድማ ምድርም ይሆናሉ።

44ቤልን በባቢሎን ውስጥ እቀጣለሁ፤

የዋጠውን አስተፋዋለሁ፤

ሕዝቦች ከእንግዲህ ወደ እርሱ አይጐርፉም፤

የባቢሎንም ቅጥር ይወድቃል።

45“ሕዝቤ ሆይ፤ ከመካከሏ ውጡ!

ሕይወታችሁን አትርፉ!

ከአስፈሪው የእግዚአብሔር ቍጣ አምልጡ።

46ወሬ በምድሪቱ ሲሰማ፣

ተስፋ አትቍረጡ፤ አትፍሩም፤

ገዥ በገዥ ላይ ስለ መነሣቱ፣

ዐመፅም በምድሪቱ ስለ መኖሩ፣

አንድ ወሬ ዘንድሮ፣ ሌላውም ለከርሞ ይመጣል፤

47የባቢሎንን ጣዖታት የምቀጣበት ጊዜ፣

በርግጥ ይመጣልና።

ምድሯ በሙሉ ትዋረዳለች፤

የታረዱትም በሙሉ በውስጧ ይወድቃሉ።

48ሰማይና ምድር በውስጣቸውም ያለው ሁሉ፣

በባቢሎን ላይ እልል ይላሉ፤

አጥፊዎች ከሰሜን ወጥተው፣

እርሷን ይወጓታልና፤”

ይላል እግዚአብሔር

49“በምድር ሁሉ የታረዱት፣

በባቢሎን ምክንያት እንደ ወደቁ፣

ባቢሎንም በእስራኤል በታረዱት ምክንያት መውደቅ ይገባታል።

50ከሰይፍ ያመለጣችሁ ሆይ፤

ሂዱ! ጊዜ አትፍጁ፤

በሩቅ ምድር ያላችሁ እግዚአብሔርን አስታውሱ፤

ኢየሩሳሌምንም አስቧት።”

51“ባዕዳን ሰዎች ወደ ተቀደሰው፣

ወደ እግዚአብሔር ቤት ስለ ገቡ፣

እኛ ተሰድበናል፤

ዕፍረትም ፊታችንን ሸፍኗል፤

ውርደትም ተከናንበናል።”

52“እንግዲህ ጣዖቶቿን የምቀጣበት ዘመን ይመጣል፤”

ይላል እግዚአብሔር

“በምድሯም ሁሉ፤

ቍስለኞች ያቃስታሉ።

53ባቢሎን ወደ ሰማይ ብትወጣም፣

ከፍ ያለ ምሽጓን ብታጠናክርም፣

አጥፊዎች እሰድድባታለሁ፤”

ይላል እግዚአብሔር

54“ከባቢሎን ጩኸት፣

ከባቢሎናውያንም51፥54 ወይም ከለዳውያን ምድር፣

የታላቅ ጥፋት ድምፅ ይሰማል።

55እግዚአብሔር ባቢሎንን ያጠፋታል፤

ታላቅ ጩኸቷንም ጸጥ ያደርጋል።

ሞገዳቸው እንደ ታላቅ ውሃ ይተምማል፤

ጩኸታቸውም ያስተጋባል።

56በባቢሎን ላይ አጥፊ ይመጣል፤

ጦረኞቿ ይማረካሉ፤

ቀስታቸውም ይሰበራል፤

እግዚአብሔር ግፍን የሚበቀል፣

ተገቢውንም ሁሉ የሚከፍል አምላክ ነውና።

57ባለሥልጣኖቿንና ጥበበኞቿን፣

ገዦቿንና መኳንንቷን፣ ጦረኞቿንም አሰክራለሁ፤

ለዘላለም ይተኛሉ፤ አይነቁምም፤”

ይላል ስሙ የሰራዊት ጌታ

እግዚአብሔር የሆነው ንጉሥ።

58የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤

“ወፍራሙ የባቢሎን ቅጥር ፈጽሞ ይፈርሳል፤

ከፍ ያሉት ደጆቿም በእሳት ይቃጠላሉ፤

ሰዎቹ በከንቱ ይደክማሉ፤

የሕዝቡም ልፋት ለእሳት ይሆናል።”

59የይሁዳ ንጉሥ ሴዴቅያስ በነገሠ በአራተኛው ዓመት፣ የንጉሡ የግቢ አስከልካይ የነበረው የመሕሤያ ልጅ የኔርያ ልጅ ሠራያ ከንጉሡ ጋር ወደ ባቢሎን በሄደ ጊዜ፣ ነቢዩ ኤርምያስ የሰጠው መልእክት ይህ ነው። 60ኤርምያስ ስለ ባቢሎን ጽፎ ያስቀመጠውን ሁሉ፣ በባቢሎን ላይ የሚመጣውን ጥፋት ሁሉ በብራና ጥቅልል ላይ ጻፈው። 61ለሠራያም እንዲህ አለው፤ “ባቢሎን በደረስህ ጊዜ፣ ይህን ቃል ሁሉ ድምፅህን ከፍ አድርገህ ማንበብ አትዘንጋ። 62እንዲህም በል፤ ‘እግዚአብሔር ሆይ፤ ይህችን ስፍራ ሰውም ሆነ እንስሳ እስከማይኖርባት ድረስ ለዘላለም ባድማ አደርጋታለሁ ብለሃል።’ 63ይህን ብራና አንብበህ ከጨረስህ በኋላ፣ ድንጋይ አስረህበት ኤፍራጥስ ወንዝ ውስጥ ጣለው፤ 64እንዲህም በል፤ ‘ባቢሎንም እኔ ከማመጣባት ጥፋት የተነሣ፣ እንደዚሁ ትሰጥማለች፤ ከእንግዲህም አትነሣም፤ ሕዝቧም ይወድቃል።’ ”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 51:1-64

151:1 Isa 41:16; Mt 3:12; Yer 50:14; Isa 13:5-951:1 Yer 46:4; Isa 41:25; Yer 50:28, 45; Isa 13:3; Yer 50:9; Isa 21:5; 41:2Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.51:1 Leb-Kamai ni Ukaldayo, yaani Babeli, kwa fumbo.

2Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

351:3 Yer 50:29; 46:4Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

451:4 Isa 13:15-18; Yer 50:30Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.

551:5 Law 26:44; Isa 54:6-8; Za 91:14; Hos 4:1Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

651:6 Ufu 18:4; Isa 48:20; Yer 50:8, 15; Ay 21:19; Isa 1:24; Mao 3:64; Hes 16:26“Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi cha Bwana,

atamlipa kile anachostahili.

751:7 Isa 51:22; Ufu 17:4; Yer 25:15-16; 49:12; Ufu 14:8-10Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

851:8 Isa 14:15; Ufu 14:8; Yer 8:22; Ufu 18:9; Yer 46:11; Isa 21:9Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

951:9 Isa 13:14; 31:9; Ufu 18:4-5; Yer 50:16“ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu hadi mawinguni.’

1051:10 Mik 7:8-9; Za 64:9; Yer 50:28“ ‘Bwana amethibitisha haki yetu;

njooni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’

11“Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwana atalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

1251:12 Za 20:5; 2Sam 18:24; Eze 33:2Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwana atatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

1351:13 Yer 50:38; Ufu 17:15; Eze 22:27; Hab 2:9; Isa 45:3Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

1451:14 Mwa 22:16; Amo 6:8; Nah 3:15; Yer 50:15Bwana Mwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

1551:15 Ay 9:8; Isa 40:26; Mdo 14:15; Za 104:24; 136:5“Aliiumba dunia kwa uweza wake;

akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

1651:16 Za 18:11-13; Kum 28:12; Yn 1:12; Ay 28:26; Za 135:7Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua,

naye huuleta upepo kutoka ghala zake.

1751:17 Isa 44:20; Hab 2:18-19; Yer 50:2“Kila mtu ni mjinga na hana maarifa;

kila sonara ameaibishwa na sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yavyo.

1851:18 Yer 18; 15; Yn 2:8Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.

1951:19 Za 119:57; Kut 34:9Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwani ndiye Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

2051:20 Isa 10:5; Zek 9:13; Mik 4:13; Ay 34:24; Isa 45:1“Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita:

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

2151:21 Kut 15:1; Isa 43:17; Yer 50:37kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

2251:22 2Nya 36:17; Isa 13:17-18kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

2451:24 Kum 32:41; Mao 3:64; Yer 50:15; Isa 45:1“Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.

2551:25 Yer 21:13; 50:23; Kut 3:20; Zek 4:7“Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asema Bwana.

“Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

2651:26 Isa 13:19-22; Yer 50:12Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asema Bwana.

2751:27 Isa 13:2; Za 20:5; Mwa 8:4; 10:3; Yer 25:14“Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

2951:29 Isa 13:20; Yer 50:13; Amu 5:4; Yer 49:21; Za 33:11; Yer 48:9Nchi inatetemeka na kugaagaa,

kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.

3051:30 Yer 50:24; 2Sam 19:16; Mao 2:9; Nah 3:13; Isa 47:14; 45:2Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

3151:31 Yer 50:24; 2Sam 18:19-31; Dan 5:30Tarishi mmoja humfuata mwingine,

na mjumbe humfuata mjumbe,

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

3251:32 Isa 47:14; Yer 50:36Vivuko vya mito vimekamatwa,

mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

3351:33 Isa 21:10; 17:5; Hos 6:11; Mt 13:30; Isa 13:22Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

3451:34 Yer 50:17; Nah 2:12; Hos 8:8“Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35Jeuri iliyofanyiwa miili yetu51:35 Au: Jeuri tuliyofanyiwa sisi na watoto wetu. na iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

3651:36 Za 140:12; Mao 3:58; Yer 20:12; Rum 12:19; Hos 13:15; Yer 50:34; Isa 11:15Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

3751:37 Isa 13:22; Ufu 12:8; Yer 50:39; 18:16; Ufu 18:2; Nah 3:6; Mal 2:9Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

3951:39 Isa 21:5; Yer 50:24; Za 13:3Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asema Bwana.

40“Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

4151:41 Yer 25:26; Isa 13:19; Dan 4:30; Yer 50:13“Tazama jinsi Sheshaki51:41 Sheshaki ni Babeli kwa fumbo. atakamatwa,

majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

4251:42 Za 18:4; Isa 8:7-8Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

4351:43 Isa 13:20; Yer 2:6; Isa 21:1Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

4451:44 Isa 21:9; 2Fal 25:4; Isa 25:12; 46:1; Yer 50:15Nitamwadhibu Beli katika Babeli,

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

4551:45 Ufu 18:4; Yer 50:8; Isa 48:20; Za 76:10; 79:6“Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali ya Bwana.

4651:46 Yer 46:27; 2Fal 19:7; Za 18:45Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi,

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

4751:47 Isa 46:1-2; Yer 50:12; 27:7; 50:12Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu,

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

4851:48 Isa 44:23; Ufu 18:20; Yer 25:26; Isa 41:25; Za 149:2; Ay 3:7Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asema Bwana.

4951:49 Za 137:8; Yer 50:29“Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

5151:51 Za 44:13-16; 79:4; Mao 1:10“Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”

5251:52 Ay 24:12“Lakini siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

5351:53 Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Ay 15:21; Yer 49:16Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asema Bwana.

54“Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

5551:55 Za 18:4; Isa 25:5Bwana ataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

5651:56 Ay 15:21; Mwa 4:24; Za 46:9; Hab 2:8; Za 94:1-2Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

5751:57 Za 76:5; Yer 25:27; Isa 6:5; Yer 46:18; Ay 5:13; Isa 21:7Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.

5851:58 2Fal 25:4; Isa 15:4; 47:14; Hab 2:13; Isa 13:2Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”

5951:59 Yer 36:4; 52:1; 28:1Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 6051:60 Kut 17:14; Yer 30:2; 36:2Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli. 61Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa. 6251:62 Isa 13:20; Yer 9:11; 50:13Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’ 6351:63 Mwa 2:14Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati. 6451:64 Ay 31:40; Za 18:21; Eze 26:21; 28:19Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.