መዝሙር 119 – NASV & NEN

New Amharic Standard Version

መዝሙር 119:1-176

መዝሙር 119119 የዚህ መዝሙር የግጥም ስንኞች መነሻ ወይም መነሻና መድረሻ ሆህያት ቍልቍል ሲነበቡ ትርጕም ዐዘል ናቸው። እያንዳንዱ ስንኝ ተመሳሳይ በሆነ በዕብራይስጥ ፊደል ይጀምራል።

ውዳሴ ለሕገ እግዚአብሔር

א አሌፍ

1መንገዳቸው ነቀፋ የሌለበት፣

በእግዚአብሔርም ሕግ የሚሄዱ የተባረኩ ናቸው።

2ምስክርነቱን የሚጠብቁ፣

በፍጹምም ልብ የሚሹት የተባረኩ ናቸው፤

3ዐመፅን አያደርጉም፤

ነገር ግን በመንገዱ ይሄዳሉ።

4ጠንቅቀን እንጠብቃት ዘንድ፣

አንተ ሥርዐትን አዝዘሃል።

5ሥርዐትህን እጠብቅ ዘንድ፣

ምነው መንገዴ ጽኑ በሆነልኝ ኖሮ!

6ወደ ትእዛዞችህ ስመለከት፣

በዚያን ጊዜ አላፍርም።

7የጽድቅ ፍርድህን ስማር፣

በቅን ልብ ምስጋና አቀርብልሃለሁ።

8ሥርዐትህን እጠብቃለሁ፤

ፈጽመህ አትተወኝ።

ב ቤት

9ጕልማሳ መንገዱን እንዴት ያነጻል?

በቃልህ መሠረት በመኖር ነው።

10በሙሉ ልቤ ፈለግሁህ፤

ከትእዛዞችህ ፈቀቅ እንዳልል አድርገኝ።

11አንተን እንዳልበድል፣

ቃልህን በልቤ ሰወርሁ።

12እግዚአብሔር ሆይ፤ አንተ ቡሩክ ነህ፤

ሥርዐትህን አስተምረኝ።

13ከአንደበትህ የሚወጣውን ደንብ ሁሉ፣

በከንፈሬ እናገራለሁ።

14ሰው በሀብቱ ብዛት ደስ እንደሚለው፣

ምስክርነትህን በመከተል ደስ ይለኛል።

15ድንጋጌህን አሰላስላለሁ፤

ልቤን በመንገድህ ላይ ጥያለሁ።

16በሥርዐትህ ደስ ይለኛል፤

ቃልህንም አልዘነጋም።

ג ጊሜል

17ሕያው እንድሆን፣ ቃልህንም እንድጠብቅ፣

ለአገልጋይህ መልካም አድርግ።

18ከሕግህ ድንቅ ነገርን እንዳይ፣

ዐይኖቼን ክፈት።

19እኔ በምድር ላይ መጻተኛ ነኝ፤

ትእዛዞችህን ከእኔ አትሰውር።

20ዘወትር ደንብህን በመናፈቅ፣

ነፍሴ እጅግ ዛለች።

21ከትእዛዞችህ የሳቱትን፣

እብሪተኞችንና ርጉሞችን ትገሥጻለህ።

22ምስክርነትህን ጠብቄአለሁና፣

ስድብንና ንቀትን ከእኔ አርቅ።

23ገዦች ተቀምጠው ቢዶልቱብኝ እንኳ፣

አገልጋይህ ሥርዐትህን ያሰላስላል።

24ምስክርነትህ ለእኔ ደስታዬ ነው፤

መካሪዬም ነው።

ד ዳሌት

25ነፍሴ ከዐፈር ተጣበቀች፤

እንደ ቃልህ መልሰህ ሕያው አድርገኝ።

26ስለ መንገዴ ገልጬ ነገርሁህ፤ አንተም መለስህልኝ፤

ሥርዐትህን አስተምረኝ።

27የድንጋጌህን መንገድ እንዳስተውል አድርገኝ፤

እኔም ድንቅ ሥራህን አሰላስላለሁ።

28ነፍሴ በሐዘን ተዝለፈለፈች፤

እንደ ቃልህ አበርታኝ።

29የሽንገላን መንገድ ከእኔ አርቅ፤

ሕግህን በጸጋህ ስጠኝ።

30የእውነትን መንገድ መርጫለሁ፤

ሕግህንም ፊት ለፊቴ አድርጌአለሁ።

31እግዚአብሔር ሆይ፤ ከምስክርነትህ ጋር ተጣብቄአለሁ፤

አሳልፈህ ለውርደት አትስጠኝ።

32ልቤን አስፍተህልኛልና፣

በትእዛዞችህ መንገድ እሮጣለሁ።

ה ሄ

33እግዚአብሔር ሆይ፤ የሥርዐትህን መንገድ አስተምረኝ፤

እኔም እስከ መጨረሻው እጠብቀዋለሁ።

34ሕግህን እንድጠብቅ፣ በፍጹም ልቤም እንድታዘዘው፣ ማስተዋልን ስጠኝ።

35በእርሷ ደስ ይለኛልና፣

በትእዛዝህ መንገድ ምራኝ።

36ከራስ ጥቅም ይልቅ፣

ልቤን ወደ ምስክርነትህ አዘንብል።

37ከንቱ ነገር ከማየት ዐይኖቼን መልስ፤

በራስህ መንገድ119፥37 አንዳንድ ትርጕሞች እንደ ቃልህ ይላሉ። እንደ ገና ሕያው አድርገኝ።

38ትፈራ ዘንድ፣

ለአገልጋይህ የገባኸውን ቃል ፈጽም።

39የምፈራውን መዋረድ ከእኔ አርቅ፤

ደንብህ መልካም ነውና።

40እነሆ፤ ድንጋጌህን ናፈቅሁ፤

በጽድቅህ ሕያው አድርገኝ።

ו ዋው

41እግዚአብሔር ሆይ፤ ምሕረትህ ወደ እኔ ይምጣ፤

ማዳንህም እንደ ቃልህ ይላክልኝ።

42በቃልህ ታምኛለሁና፣

ለሚሰድቡኝ መልስ እሰጣለሁ።

43ሕግህን ተስፋ አድርጌአለሁና፣

የእውነትን ቃል ከአፌ ፈጽመህ አታርቅ።

44ከዘላለም እስከ ዘላለም፣

ሕግህን ዘወትር እጠብቃለሁ።

45ሥርዐትህን እሻለሁና፣

እንደ ልቤ ወዲያ ወዲህ እመላለሳለሁ።

46ምስክርነትህን በነገሥታት ፊት እናገራለሁ፤

ይህን በማድረግም ዕፍረት አይሰማኝም።

47እኔ እወድደዋለሁና፣

በትእዛዝህ ደስ ይለኛል።

48እጆቼን ወደምወዳቸው119፥48 ወይም ለምወድዳቸው ትእዛዞችህ አነሣለሁ፤

ሥርዐትህንም አሰላስላለሁ።

ז ዛይን

49ለአገልጋይህ የገባኸውን ቃል ዐስብ፤

በዚያ ተስፋ ሰጥተኸዋልና።

50ቃልህ ሕያው ያደርገኛልና፣

ይህች በመከራዬ መጽናኛዬ ናት።

51እብሪተኞች እጅግ ተሣለቁብኝ፤

እኔ ግን ከሕግህ ንቅንቅ አልልም።

52እግዚአብሔር ሆይ፤ ከጥንት የነበረውን ድንጋጌህን አሰብሁ፤ በዚህም ተጽናናሁ።

53ሕግህን ከተዉ ክፉዎች የተነሣ፣

ቍጣ ወረረኝ።

54በእንግድነቴ አገር፣

ሥርዐትህ መዝሙሬ ናት።

55እግዚአብሔር ሆይ፤ ስምህን በሌሊት ዐስባለሁ፤

ሕግህንም እጠብቃለሁ።

56ሥርዐትህን እከተላለሁ፤

ይህችም ተግባሬ ሆነች።

ח ኼት

57እግዚአብሔር ዕድል ፈንታዬ ነው፤

ቃልህን ለመታዘዝ ቈርጫለሁ።

58በፍጹም ልቤ ፊትህን ፈለግሁ፤

እንደ ቃልህ ቸርነትህን አሳየኝ።

59መንገዴን ቃኘሁ፤

አካሄዴንም ወደ ምስክርህ አቀናሁ።

60ትእዛዝህን ለመጠበቅ፣

ቸኰልሁ፤ አልዘገየሁምም።

61የክፉዎች ገመድ ተተበተበብኝ፤ እኔ ግን ሕግህን አልረሳሁም።

62ስለ ጻድቅ ሥርዐትህ፣

በእኩለ ሌሊት ላመሰግንህ እነሣለሁ።

63እኔ ለሚፈሩህ ሁሉ፣

ሥርዐትህንም ለሚጠብቁ ባልንጀራ ነኝ።

64እግዚአብሔር ሆይ፤ ምድር በምሕረትህ ተሞላች፤

ሥርዐትህን አስተምረኝ።

ט ቴት

65እግዚአብሔር ሆይ፤ እንደ ቃልህ፣

ለአገልጋይህ በጎ ውለሃል።

66በትእዛዞችህ አምናለሁና፣

በጎ ማስተዋልንና ዕውቀትን አስተምረኝ።

67እንዲያው ሳይቸግረኝ መንገድ ስቼ ሄድሁ፤

አሁን ግን ቃልህን እጠብቃለሁ።

68አንተ መልካም ነህ፤ የምታደርገው መልካም ነው፤

እንግዲህ ሥርዐትህን አስተምረኝ።

69እብሪተኞች ስሜን በሐሰት አጠፉ፤

እኔ ግን ትእዛዝህን በፍጹም ልብ እጠብቃለሁ።

70ልባቸው የሠባና የደነደነ ነው፤

እኔ ግን በሕግህ ደስ ይለኛል።

71ሥርዐትህን እማር ዘንድ፣

በመከራ ውስጥ ማለፌ መልካም ሆነልኝ።

72ከአእላፋት ብርና ወርቅ ይልቅ፣

ከአፍህ የሚወጣው ሕግ ይሻለኛል።

י ዮድ

73እጆችህ ሠሩኝ፤ አበጃጁኝም፤

ትእዛዞችህን እንድማር ማስተዋልን ስጠኝ።

74ቃልህን ተስፋ አድርጌአለሁና፣

የሚፈሩህ እኔን አይተው ደስ ይበላቸው።

75እግዚአብሔር ሆይ፤ ፍርድህ የጽድቅ ፍርድ፣

ያስጨነቅኸኝም በታማኝነት እንደ ሆነ ዐወቅሁ።

76ለአገልጋይህ በገባኸው ቃል መሠረት፣

ምሕረትህ ለመጽናናት ትሁነኝ።

77ሕግህ ደስታዬ ነውና፣

በሕይወት እኖር ዘንድ ቸርነትህ ትምጣልኝ።

78እብሪተኞች ያለ ምክንያት በደል አድርሰውብኛልና ይፈሩ፤

እኔ ግን ትእዛዞችህን አሰላስላለሁ።

79አንተን የሚፈሩህ፣

ምስክርነትህንም የሚያውቁ ወደ እኔ ይመለሱ።

80እኔ እንዳላፍር፣ ልቤ በሥርዐትህ ፍጹም ይሁን።

כ ካፍ

81ነፍሴ ማዳንህን እጅግ ናፈቀች፤

ቃልህንም ተስፋ አደርጋለሁ።

82“መቼ ታጽናናኛለህ?” እያልሁ፣

ዐይኖቼ ቃልህን በመጠባበቅ ደከሙ።

83ጢስ የጠጣ የወይን አቍማዳ ብመስልም፣

ሥርዐትህን አልረሳሁም።

84የባሪያህ ዕድሜ ስንት ቢሆን ነው?

ታዲያ፣ በሚያሳድዱኝ ላይ የምትፈርደው መቼ ይሆን?

85በሕግህ መሠረት የማይሄዱ እብሪተኞች

ማጥመጃ ጕድጓድ ቈፈሩልኝ።

86ትእዛዞችህ ሁሉ አስተማማኝ ናቸው፤

ሰዎች ያለ ምክንያት አሳድደውኛልና ርዳኝ።

87ከምድር ላይ ሊያስወግዱኝ ጥቂት ቀራቸው፤

እኔ ግን ትእዛዞችህን አልተውሁም።

88እንደ ምሕረትህ መልሰህ ሕያው አድርገኝ፤

እኔም የአፍህን ምስክርነት እጠብቃለሁ።

ל ላሜድ

89እግዚአብሔር ሆይ፤ ቃልህ በሰማይ፣

ለዘላለም ጸንቶ ይኖራል።

90ታማኝነትህ ከትውልድ እስከ ትውልድ ሁሉ ይኖራል፤

ምድርን መሠረትሃት፤ እርሷም ጸንታ ትኖራለች።

91ሁሉም አገልጋይህ ነውና፣

በሕግህ መሠረት እስከ ዛሬ ድረስ ጸንተው ይኖራሉ።

92ሕግህ ደስታዬ ባይሆን ኖሮ፣

በመከራዬ ወቅት በጠፋሁ ነበር።

93በእርሱ ሕያው አድርገኸኛልና፣

ትእዛዝህን ከቶ አልረሳም።

94እኔ የአንተ ነኝ፤ እባክህ አድነኝ፤

ሕግህንም ፈልጌአለሁና።

95ክፉዎች ሊያጠፉኝ አድብተዋል፤

እኔ ግን ምስክርነትህን አሰላስላለሁ።

96ለፍጹምነት ሁሉ ዳርቻ እንዳለው አየሁ፤

ትእዛዝህ ግን እጅግ ሰፊ ነው።

מ ሜም

97አቤቱ፤ ሕግህን ምንኛ ወደድሁ!

ቀኑን ሙሉ አሰላስለዋለሁ።

98ትእዛዞችህ ምንጊዜም ስለማይለዩኝ፣

ከጠላቶቼ ይልቅ አስተዋይ አደረጉኝ።

99ምስክርነትህን አሰላስላለሁና፣

ከአስተማሪዎቼ ሁሉ የላቀ አስተዋይ ልብ አገኘሁ።

100መመሪያህን ተከትዬ እሄዳለሁና፣

ከሽማግሌዎች ይልቅ አስተዋይ ሆንሁ።

101ቃልህን እጠብቅ ዘንድ፣

እግሬን ከክፉ መንገድ ሁሉ ከለከልሁ።

102አንተው ራስህ አስተምረኸኛልና፣

ከድንጋጌህ ዘወር አላልሁም።

103ቃልህ ለምላሴ ምንኛ ጣፋጭ ነው!

ለአፌም ከማር ወለላ ይልቅ ጣዕም አለው።

104ከመመሪያህ ማስተዋልን አገኘሁ፤

ስለዚህ የሐሰትን መንገድ ሁሉ ጠላሁ።

נ ኑን

105ሕግህ ለእግሬ መብራት፣

ለመንገዴም ብርሃን ነው።

106የጽድቅ ሕግህን ለመጠበቅ፤

ምያለሁ፤ ይህንኑ አጸናለሁ።

107እጅግ ተቸግሬአለሁ፤

እግዚአብሔር ሆይ፤ እንደ ቃልህ መልሰህ ሕያው አድርገኝ።

108እግዚአብሔር ሆይ፤ ፈቅጄ ያቀረብሁትን የአፌን የምስጋና መሥዋዕት ተቀበል፤

ሕግህንም አስተምረኝ።

109ነፍሴ ዘወትር አደጋ ላይ ናት፤

ሕግህን ግን አልረሳሁም።

110ክፉዎች ወጥመድ ዘረጉብኝ፤

እኔ ግን መመሪያህን አልተላለፍሁም።

111ምስክርነትህ የዘላለም ውርሴ ናት፤

ልቤ በዚህ ሐሤት ያደርጋልና።

112ትእዛዝህን ለዘላለም፣ እስከ ወዲያኛው ለመፈጸም፣

ልቤን ወደዚያው አዘነበልሁ።

ס ሳሜክ

113መንታ ልብ ያላቸውን ጠላሁ፤

ሕግህን ግን ወደድሁ።

114አንተ መጠጊያዬና ጋሻዬ ነህ፤

ቃልህን በተስፋ እጠብቃለሁ።

115የአምላኬን ትእዛዞች እጠብቅ ዘንድ፣

እናንት ክፉ አድራጊዎች ከእኔ ራቁ።

116እንደ ቃልህ ደግፈኝ፤ እኔም ሕያው እሆናለሁ፤

ተስፋዬም መና ቀርቶ አልፈር።

117ያለ ሥጋት እቀመጥ ዘንድ ደግፈህ ያዘኝ፤

ሥርዐትህንም ዘወትር እመለከታለሁ።

118መሠሪነታቸው በከንቱ ነውና፣

ከሥርዐትህ ውጭ የሚሄዱትን ሁሉ ወዲያ አስወገድሃቸው።

119የምድርን ክፉዎች ሁሉ እንደ ጥራጊ አስወገድሃቸው፤

ስለዚህ ምስክርህን ወደድሁ።

120ሥጋዬ አንተን በመፍራት ይንቀጠቀጣል፤

ፍርድህንም እፈራለሁ።

ע ዐዪን

121ፍትሕና ጽድቅ ያለበትን ሠርቻለሁ፤

ለሚጨቍኑኝ አሳልፈህ አትስጠኝ።

122ለባሪያህ በጎነት ዋስትና ሁን፤

እብሪተኞች እንዲጨቍኑኝ አትፍቀድላቸው።

123ዐይኖቼ ማዳንህን፣

የጽድቅ ቃልህን በመጠባበቅ ደከሙ።

124ለባሪያህ እንደ ምሕረትህ መጠን አድርግ፤

ሥርዐትህንም አስተምረኝ።

125እኔ ባሪያህ ነኝ፤

ምስክርነትህን ዐውቅ ዘንድ ማስተዋልን ስጠኝ።

126እግዚአብሔር ሆይ፤

ሕግህ እየተጣሰ ነውና፣

ጊዜው አንተ የምትሠራበት ነው።

127ስለዚህ ከወርቅ፣ ከንጹሕ ወርቅ ይልቅ፣

ትእዛዞችህን ወደድሁ።

128መመሪያህ ሙሉ በሙሉ ልክ ነው አልሁ፤

ስለዚህ የሐሰትን መንገድ ሁሉ ጠላሁ።

פ ፔ

129ምስክርነትህ ሁሉ ድንቅ ነው፤

ስለዚህ ነፍሴ ትጠብቀዋለች።

130የቃልህ ትርጓሜ ያበራል፤

አላዋቂዎችንም አስተዋዮች ያደርጋል።

131ትእዛዝህን ናፍቄአለሁና፣

አፌን ከፈትሁ፤ አለከለክሁም።

132ስምህን ለሚወድዱ ማድረግ ልማድህ እንደ ሆነ ሁሉ፣

ወደ እኔ ተመልሰህ ምሕረት አድርግልኝ።

133አካሄዴን እንደ ቃልህ ቀና አድርግልኝ፤

ኀጢአትም በላዬ እንዲሠለጥን አትፍቀድ።

134ትእዛዝህን መጠበቅ እንድችል፣

ከሰዎች ጥቃት ታደገኝ።

135በባሪያህ ላይ ፊትህን አብራ፤

ሥርዐትህንም አስተምረኝ።

136ሕግህ ባለመከበሩ፤

እንባዬ እንደ ውሃ ይፈስሳል።

צ ጻዴ

137እግዚአብሔር ሆይ፤ አንተ ጻድቅ ነህ፤

ፍርድህም ትክክል ነው።

138ምስክርነትህን በጽድቅ አዘዝህ፤

እጅግ አስተማማኝም ነው።

139ጠላቶቼ ቃልህን ዘንግተዋልና፣

ቅናት አሳረረኝ።

140ቃልህ እጅግ የነጠረ ነው፤

ባሪያህም ወደደው።

141እኔ ታናሽና የተናቅሁ ነኝ፤

ነገር ግን መመሪያህን አልዘነጋሁም።

142ጽድቅህ ዘላለማዊ ጽድቅ ነው፤

ሕግህም እውነት ነው።

143መከራና ሥቃይ ደርሶብኛል፤

ነገር ግን ትእዛዝህ ደስታዬ ነው።

144ምስክርነትህ ለዘላለም የጽድቅ ምስክርነት ነው፤

በሕይወት እኖር ዘንድ ማስተዋልን ስጠኝ።

ק ቆፍ

145እግዚአብሔር ሆይ፤ በፍጹም ልቤ እጮኻለሁና መልስልኝ፤

ሥርዐትህንም እጠብቃለሁ።

146ወደ አንተ እጣራለሁና አድነኝ፤

ምስክርነትህንም እጠብቃለሁ።

147ትረዳኝ ዘንድ ጎሕ ሳይቀድድ ተነሥቼ እጮኻለሁ፤

ቃልህንም ተስፋ አደርጋለሁ።

148ቃልህን አሰላስል ዘንድ፣

ዐይኔ ሌሊቱን ሙሉ ሳይከደን ያድራል።

149እንደ ቸርነትህ መጠን ድምፄን ስማ፤

እግዚአብሔር ሆይ፤ እንደ ሕግህ መልሰህ ሕያው አድርገኝ።

150ደባ የሚያውጠነጥኑ ወደ እኔ ቀርበዋል፤

ከሕግህ ግን የራቁ ናቸው።

151እግዚአብሔር ሆይ፤ አንተ ግን ቅርብ ነህ፤

ትእዛዞችህም ሁሉ እውነት ናቸው።

152ለዘላለም እንደ መሠረትሃቸው፣

ከጥንት ምስክርነትህ ተረድቻለሁ።

ר ሬሽ

153ሕግህን አልረሳሁምና፣ ሥቃዬን ተመልከት፤ ታደገኝም።

154ተሟገትልኝ፤ አድነኝም፤

እንደ ቃልህም ሕያው አድርገኝ።

155ሥርዐትህን ስለማይሹ፣

ድነት ከክፉዎች የራቀ ነው።

156እግዚአብሔር ሆይ፤ ርኅራኄህ ታላቅ ነው፤

እንደ ሕግህ ሕያው አድርገኝ።

157የሚያሳድዱኝ ጠላቶቼ ብዙዎች ናቸው፤

እኔ ግን ከምስክርህ ዘወር አላልሁም።

158ቃልህን አይጠብቁምና፣

ከዳተኞችን አይቼ አርቃቸዋለሁ።

159መመሪያህን እንዴት እንደምወድድ ተመልከት፤

እግዚአብሔር ሆይ፤ እንደ ምሕረትህ ሕያው አድርገኝ።

160ቃልህ በሙሉ እውነት ነው፤

ጻድቅ የሆነው ሕግህም ዘላለማዊ ነው።

ש ሲን እና ሺን

161ገዦች ያለ ምክንያት አሳደዱኝ፤

ልቤ ግን ከቃልህ የተነሣ እጅግ ፈራ።

162ትልቅ ምርኮ እንዳገኘ ሰው፣

በቃልህ ደስ አለኝ።

163ሐሰትን እጠላለሁ፤ እጸየፋለሁ፤

ሕግህን ግን ወደድሁ።

164ጻድቅ ስለ ሆነው ሕግህ፣

በቀን ሰባት ጊዜ አመሰግንሃለሁ።

165ሕግህን የሚወድዱ ብዙ ሰላም አላቸው፤

ዕንቅፋትም የለባቸውም።

166እግዚአብሔር ሆይ፤ ማዳንህን ተስፋ አደርጋለሁ፤

ትእዛዝህንም እፈጽማለሁ።

167ነፍሴ ምስክርነትህን ትጠብቃለች፤

እጅግ እወድደዋለሁና።

168መንገዴ ሁሉ በፊትህ ግልጽ ነውና፣

ሕግህንና ምስክርነትህን እጠብቃለሁ።

ת ታው

169እግዚአብሔር ሆይ፤ ጩኸቴ ከፊትህ ይድረስ፤

እንደ ቃልህም ማስተዋልን ስጠኝ።

170ልመናዬ ከፊትህ ይድረስ፤

እንደ ቃልህም ታደገኝ።

171ሥርዐትህን አስተምረኸኛልና፣

ከንፈሮቼ ምስጋናን አፈለቁ።

172ትእዛዞችህ ሁሉ የጽድቅ ትእዛዞች ናቸውና፣

አንደበቴ ስለ ቃልህ ይዘምር።

173ትእዛዝህን መርጫለሁና፣

እጅህ እኔን ለመርዳት ዝግጁ ይሁን።

174እግዚአብሔር ሆይ፤ ማዳንህን ናፈቅሁ፤

ሕግህም ደስታዬ ነው።

175አመሰግንህ ዘንድ በሕይወት ልኑር፤

ሕግህም ይርዳኝ።

176እንደ ጠፋ በግ ተቅበዘበዝሁ፤

ትእዛዞችህን አልረሳሁምና፣

ባሪያህን ፈልገው።

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 119:1-176

Zaburi 119119:0 Zaburi hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi 22 za alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T).

Sifa Za Sheria Ya Bwana

Kujifunza Sheria Ya Bwana

1119:1 Mwa 17:1; Za 1:2; 128:1; Kum 18:13; Mit 11:20Heri wale walio waadilifu katika njia zao,

wanaoenenda katika sheria ya Bwana.

2119:2 Za 40:16; 112:1; 119:146; Isa 56:2; Kum 10:12; Mit 9:7; 1Nya 16:11Heri wale wanaozishika shuhuda zake,

wamtafutao kwa moyo wao wote.

3119:3 Za 59:4; 128:1; Yn 3:9; 5:18; Yer 6:16; 7:23; Rum 7:16, 17Wasiofanya lolote lililo baya,

wanaoenenda katika njia zake.

4119:4 Za 103:18; 119:56; Kum 6:17Umetoa maagizo yako

ili tuyatii kwa ukamilifu.

5119:5 Law 19:37; Yer 31:33; 2Kor 3:5; Rum 7:22, 23Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara

katika kuyatii maagizo yako!

6119:6 Za 119:46, 80, 117; Ay 22:26; 1Yn 2:28Hivyo mimi sitaaibishwa

ninapozingatia amri zako zote.

7119:7 Kum 4:8119:7 Za 90:13; 103:13; 119:47Nitakusifu kwa moyo mnyofu

ninapojifunza sheria zako za haki.

8119:8 Za 38:21Nitayatii maagizo yako;

usiniache kabisa.

Kutii Sheria Ya Bwana

9119:9 Za 119:65, 169; 39:1; Mit 1:4, 10Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani?

Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.

10119:10 Za 119:21, 118; 9:1; 2Nya 15:15Ninakutafuta kwa moyo wangu wote,

usiniache niende mbali na amri zako.

11119:11 Isa 63:13; Mit 3:23; Za 119:133, 165; 18:22-23; Kum 6:6; Lk 2:19; Ay 22:22Nimelificha neno lako moyoni mwangu

ili nisikutende dhambi.

12119:12 Isa 63:13; Lk 2:19Sifa ni zako, Ee Bwana,

nifundishe maagizo yako.

13119:13 Za 119:72Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote

zinazotoka katika kinywa chako.

14119:14 Za 119:111Ninafurahia kufuata sheria zako

kama mtu afurahiaye mali nyingi.

15119:15 Za 119:97, 148; 1:2Ninatafakari maagizo yako

na kuziangalia njia zako.

16119:16 Za 112:1Ninafurahia maagizo yako,

wala sitalipuuza neno lako.

Furaha Katika Sheria Ya Bwana

17119:17 Za 13:6; 116:7; 119:67; 103:20Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi;

nitalitii neno lako.

18Yafungue macho yangu nipate kuona

mambo ya ajabu katika sheria yako.

19119:19 Mwa 23:4; Ebr 11:13Mimi ni mgeni duniani,

usinifiche amri zako.

20119:20 Za 84:2; 119:131; 42:2; 63:1; Isa 26:9Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa

juu ya sheria zako wakati wote.

21119:21 Za 119:10, 51; 5:5; Ay 30:1; Yer 20:7; 50:32; Kum 27:26; Dan 4:37; Mal 3:15Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa

waendao mbali na amri zako.

22119:22 Za 39:8; 119:2Niondolee dharau na dhihaka,

kwa kuwa ninazishika sheria zako.

23Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia,

mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.

24Sheria zako ni furaha yangu,

nazo ni washauri wangu.

Kuamua Kuitii Sheria Ya Bwana

25119:25 Za 44:25; 143:11; 119:9, 50, 107Nimelazwa chini mavumbini,

yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.

26119:26 Za 25:4; 27:11; 86:11; 1Fal 8:36Nilikueleza njia zangu ukanijibu,

nifundishe sheria zako.

27119:27 Za 105:2; 145:5Nijulishe mafundisho ya mausia yako,

nami nitatafakari maajabu yako.

28119:28 Za 119:9; 116:3; 18:1; 6:7; Yer 45:3; Isa 51:11; 40:29; 41:10Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni,

uniimarishe sawasawa na neno lako.

29119:29 Za 26:4; Hes 6:25; Mit 30:8; Ebr 8:10Niepushe na njia za udanganyifu,

kwa neema unifundishe sheria zako.

30119:30 Yos 24:22; Za 26:3; 108:1Nimechagua njia ya kweli,

nimekaza moyo wangu katika sheria zako.

31119:31 Kum 10:20Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana,

usiniache niaibishwe.

32119:32 1Fal 4:29; Isa 60:5; 2Kor 6:11Nakimbilia katika njia ya maagizo yako,

kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.

Maombi Ili Kupata Ufahamu Wa Sheria

33119:33 Za 119:12Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako,

nami nitayashika mpaka mwisho.

34119:34 Za 119:27, 69, 73, 144, 169; Mit 2:6; Ay 32:8; Yak 1:5; Kum 6:25; Dan 2:21Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako

na kuitii kwa moyo wangu wote.

35119:35 Za 119:32; 1:2; 25:4, 5Niongoze kwenye njia ya amri zako,

kwa kuwa huko napata furaha.

36119:36 Yos 24:23; Ebr 13:5; Mk 7:21; 12:15; Eze 33:31; 1Tim 6:10Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako,

na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.

37119:37 Za 119:9, 25; 71:20; Ay 31:1Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa,

uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.

38119:38 Hes 23:19; 2Sam 7:25Mtimizie mtumishi wako ahadi yako,

ili upate kuogopwa.

39119:39 Za 119:22; 69:9; 89:51; Isa 25:8; 51:7; 54:4Niondolee aibu ninayoiogopa,

kwa kuwa sheria zako ni njema.

40119:40 Za 119:20, 25, 149, 154Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako!

Hifadhi maisha yangu katika haki yako.

Kuitumainia Sheria Ya Bwana

41119:41 Za 6:4; 119:76, 116, 154, 170Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie,

wokovu wako sawasawa na ahadi yako,

42119:42 Mit 27:11; Za 42:10ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki,

kwa kuwa ninalitumainia neno lako.

43119:43 Za 119:74, 81, 114, 147; 1Fal 17:24Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.

44119:44 Za 119:33, 34, 55; Kum 6:25Nitaitii amri yako daima,

naam, milele na milele.

45119:45 Za 119:94, 155; Yn 8:32, 36; Rum 8:2Nitatembea nikiwa huru,

kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

46119:46 Mt 10:18; Mdo 26:1, 2; Za 119:6Nitasema sheria zako mbele za wafalme

wala sitaaibishwa,

47119:47 Za 119:77, 97, 127, 143, 159, 163, 165kwa kuwa ninazifurahia amri zako

kwa sababu ninazipenda.

48119:48 Mwa 24:63Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu,

nami ninatafakari juu ya maagizo yako.

Matumaini Katika Sheria Ya Bwana

49119:49 Za 119:9, 43Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako,

kwa sababu umenipa tumaini.

50119:50 Za 119:25; 27:13; Yer 15:16; Rum 5:3-5; Ebr 6:17-19Faraja yangu katika mateso yangu ni hii:

Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.

51119:51 Za 119:21; Ay 16:10; 17:2; 23:11; Yer 20:7Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka,

hata hivyo sitaiacha sheria yako.

52119:52 Za 103:18Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani,

nazo zinanifariji.

53119:53 Kut 32:19; 33:4; Za 89:30; Ezr 9:3Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu,

ambao wameacha sheria yako.

54119:54 Za 119:172; 101:1; 138:5Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu

popote ninapoishi.

55119:55 Za 119:44, 62, 72; 1:2; 42:8; 63:6; 77:2; Isa 26:9; Mdo 16:25Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako,

nami nitatii sheria yako.

56119:56 Za 119:4, 100, 134; Hes 15:40Hili limekuwa zoezi langu:

nami ninayatii mausia yako.

Kujitolea Katika Sheria Ya Bwana

57119:57 Kum 32:9; Yer 51:19; Za 119:17, 67, 101; Mao 3:24Ee Bwana, wewe ni fungu langu,

nimeahidi kuyatii maneno yako.

58119:58 Kum 4:29; Ezr 9:8; 1Nya 16:11; Za 34:4; 119:41; Mwa 43:29Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote,

nihurumie sawasawa na ahadi yako.

59119:59 Yoe 2:13; Lk 15:17; Yos 24:14, 15Nimezifikiri njia zangu

na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.

60119:60 Za 119:115Nitafanya haraka bila kuchelewa

kuzitii amri zako.

61119:61 Za 119:83, 109, 153, 176Hata waovu wanifunge kwa kamba,

sitasahau sheria yako.

62119:62 Za 119:55; 119:7; Mdo 16:25Usiku wa manane ninaamka kukushukuru

kwa sababu ya sheria zako za haki.

63119:63 Za 15:4; 101:6, 7; 103:11; 119:56; 111:10Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao,

kwa wote wanaofuata mausia yako.

64119:64 Za 33:5; 119:12, 108Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako,

nifundishe maagizo yako.

Thamani Ya Sheria Ya Bwana

65119:65 Isa 50:2; 59:1; Za 119:9, 17; 125:4; Mik 2:7Mtendee wema mtumishi wako

Ee Bwana, sawasawa na neno lako.

66119:66 Za 51:6Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri,

kwa kuwa ninaamini amri zako.

67119:67 Za 116:10; 95:10; 119:17; Ebr 12:11; Yer 8:4; 31:18; Kum 32:15; Ufu 3:19Kabla sijapata shida nilipotea njia,

lakini sasa ninalitii neno lako.

68119:68 Za 100:5; 106:1; 107:1; 135:3; Kut 18:20; 34:6; Mt 19:17Wewe ni mwema, unalotenda ni jema,

nifundishe maagizo yako.

69119:69 Ay 13:4; Za 109:2Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo,

nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.

70119:70 Mdo 28:27; Za 17:10; Isa 29:13Mioyo yao ni katili na migumu,

bali mimi napendezwa na sheria yako.

71119:71 Za 119:67, 75; Ebr 12:10Ilikuwa vyema mimi kupata shida

ili nipate kujifunza maagizo yako.

72119:72 Ay 28:17; Za 19:10; Mt 8:10Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu

kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.

Haki Ya Sheria Ya Bwana

73119:73 Mwa 1:27; Ay 4:17; 10:8; Za 139:13-16; 100:3; 138:8Mikono yako ilinifanya na kuniumba,

nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.

74119:74 Za 34:2; 119:9; 130:5Wakuchao wafurahie wanaponiona,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.

75119:75 Za 89:30, 31; 119:7, 138, 172; Ebr 12:5-11Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki,

katika uaminifu wako umeniadhibu.

76119:76 Za 6:4; 119:41Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu,

sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.

77Huruma yako na inijie ili nipate kuishi,

kwa kuwa naifurahia sheria yako.

78119:78 Za 119:51; 35:19; 119:86, 161; 25:3; Yer 50:32Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu,

lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.

79119:79 Za 119:27, 125Wale wakuchao na wanigeukie mimi,

hao ambao wanazielewa sheria zako.

80119:80 Za 119:1; 119:6; 1Fal 8:61; Mwa 26:5Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako,

ili nisiaibishwe.

Maombi Kwa Ajili Ya Kuokolewa

81119:81 Za 119:20, 43, 123; 84:2; 73:26Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako,

lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.

82119:82 Mao 2:11; Za 6:7; 69:3; 119:41, 123Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako;

ninasema, “Utanifajiri lini?”

83119:83 Za 119:61; 119:84; Ay 30:30; Ufu 6:10; Yer 12:3; 15:15; 20:11; Za 39:4; 6:3; 119:51; 7:6Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi,

bado sijasahau maagizo yako.

84Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini?

Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?

85119:85 Za 35:7; 119:51; 57:6; Yer 18:20, 22Wenye majivuno wananichimbia mashimo,

kinyume na sheria yako.

86119:86 Za 109:26; 7:1-5; 35:19; 119:78, 138Amri zako zote ni za kuaminika;

unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.

87119:87 Isa 1:4, 28; 59:13; 58:2; Za 119:150Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia,

lakini sijaacha mausia yako.

88119:88 Za 41:2; 119:2, 100, 124, 129, 134, 168; 51:1; 109:26Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako,

nami nitatii sheria za kinywa chako.

Imani Katika Sheria Ya Bwana

89119:89 Za 119:111, 144; 111:8; Isa 51:6; Mt 5:18; 1Pet 1:25Ee Bwana, neno lako ni la milele,

linasimama imara mbinguni.

90119:90 Za 36:5; 45:17; 148:6; Ay 8:19Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote,

umeiumba dunia, nayo inadumu.

91119:91 Yer 33:25; 31:35; Za 148:6; 104:2-4; Mwa 8:22Sheria zako zinadumu hadi leo,

kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.

92119:92 Za 37:4, 5; 112:1; 119:50, 67; Rum 15:4Kama nisingefurahia sheria yako,

ningeangamia katika taabu zangu.

93119:93 Za 119:83; 103:5Sitasahau mausia yako kamwe,

kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.

94119:94 Za 119:45, 146; 54:1; 116:4; Yer 17:14; 31:18; 42:11; Hos 2:7, 16Uniokoe, kwa maana mimi ni wako,

kwa kuwa nimetafuta mausia yako.

95119:95 Za 69:4; 119:99Waovu wanangojea kuniangamiza,

bali mimi ninatafakari sheria zako.

96119:96 Za 19:7; Isa 40:8; Mt 5:18Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo,

lakini amri zako hazina mpaka.

Kuipenda Sheria Ya Bwana

97119:97 Za 1:2; 119:15, 47Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu.

Ninaitafakari mchana kutwa.

98119:98 2Tim 3:17; Kum 4:6, 8; 19:7; Isa 48:17Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu,

kwa kuwa nimezishika daima.

99119:99 2Tim 3:15; Za 119:15Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote,

kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.

100119:100 Ay 12:12; 32:7; Za 119:56; Kum 6:17Nina ufahamu zaidi kuliko wazee,

kwa kuwa ninayatii mausia yako.

101119:101 Mit 1:15; 2Kor 7:1; Za 119:57Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya,

ili niweze kutii neno lako.

102119:102 Kum 17:20; 4:5Sijaziacha sheria zako,

kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.

103119:103 Mit 24:13, 14; 8:11; Za 19:10Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu,

matamu kuliko asali katika kinywa changu!

104119:104 Za 111:10; 119:7Ninapata ufahamu kutoka mausia yako,

kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.

Nuru Kutoka Kwenye Sheria Ya Bwana

105119:105 Mit 6:23; 20:27; 2Pet 1:19; Za 119:130Neno lako ni taa ya miguu yangu

na mwanga katika njia yangu.

106119:106 Neh 10:29; Za 119:7Nimeapa na nimethibitisha,

kwamba nitafuata sheria zako za haki.

107119:107 Za 119:25Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana,

sawasawa na neno lako.

108119:108 Za 51:15; 109:30; 63:5; 119:64; 71:8; Ebr 13:15; Hos 14:2Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu,

nifundishe sheria zako.

109119:109 Amu 12:3; Za 119:61; Ay 13:14Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote,

sitasahau sheria yako.

110119:110 Za 25:15; 64:5; 119:10; Isa 8:14; Amo 3:5Waovu wamenitegea mtego,

lakini sijayakiuka maagizo yako.

111119:111 Kum 33:4; Za 119:14, 162Sheria zako ni urithi wangu milele,

naam ni furaha ya moyo wangu.

112119:112 Za 108:1; 119:33Nimekusudia moyoni mwangu

kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.

Usalama Ndani Ya Sheria Ya Bwana

113119:113 1Fal 18:21; Yak 1:8; 4:8; Za 119:47Ninachukia watu wa nia mbili,

lakini ninapenda sheria yako.

114119:114 Za 18:2; 119:43; 32:7; Mwa 15:1Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu,

nimeweka tumaini langu katika neno lako.

115119:115 Za 6:8; Mt 7:23Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya,

ili niweze kushika amri za Mungu wangu!

116119:116 Za 18:35; 41:3; 55:22; 119:41; Isa 46:4; Rum 5:5; 9:33Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi;

usiache matumaini yangu yakavunjwa.

117119:117 Isa 41:10; 46:4; Za 34:4; 119:6; 71:6; Yn 10:28; Rum 14:4Nitegemeze, nami nitaokolewa,

nami daima nitayaheshimu maagizo yako.

118119:118 Za 119:10Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako,

kwa maana udanganyifu wao ni bure.

119119:119 Isa 1:22, 25; Eze 18:19; Za 119:47Waovu wa nchi unawatupa kama takataka,

kwa hivyo nazipenda sheria zako.

120119:120 Ay 4:14Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe,

ninaziogopa sheria zako.

Kuitii Sheria Ya Bwana

121119:121 2Sam 8:15; Ay 27:6Nimetenda yaliyo haki na sawa,

usiniache mikononi mwa watesi wangu.

122119:122 Ay 17:3Mhakikishie mtumishi wako usalama,

usiache wenye kiburi wanionee.

123119:123 Isa 38:14; Za 119:81, 82Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako,

na kuitazamia ahadi yako ya kweli.

124119:124 Za 119:12, 88; 25:7Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako

na unifundishe maagizo yako.

125119:125 Za 116:16; 119:79Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu

ili niweze kuelewa sheria zako.

126119:126 Hes 15:31Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia,

kwa kuwa sheria yako inavunjwa.

127119:127 Efe 3:8; Za 19:10; 119:47; Ay 3:21; Mit 3:13, 18; 8:11Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu,

naam, zaidi ya dhahabu safi,

128119:128 Za 19:8; 31:6; 119:104, 163; Mit 13:5na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili,

nachukia kila njia potovu.

Shauku Ya Kuitii Sheria Ya Bwana

129119:129 Za 119:18, 22, 88Sheria zako ni za ajabu,

hivyo ninazitii.

130119:130 Za 119:105; 19:7, 10; Mit 1:4; 2Pet 1:19Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru,

kunampa mjinga ufahamu.

131119:131 Za 42:1; 119:20Nimefungua kinywa changu na kuhema,

nikitamani amri zako.

132119:132 2Sam 24:14; Kut 4:31; Za 6:4; 9:13; 5:11; 106:4; 1Sam 1:11Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote

wale wanaolipenda jina lako.

133119:133 Kum 6:12; Za 119:9, 11, 122; Rum 6:16Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako,

usiache dhambi yoyote initawale.

134119:134 Lk 1:74; Za 119:56, 88, 122Niokoe na uonevu wa wanadamu,

ili niweze kutii mausia yako.

135119:135 Hes 6:25; Za 4:6; 80:3; 4:6; 119:12Mwangazie mtumishi wako uso wako

na unifundishe amri zako.

136119:136 Yer 9:1; 9:1, 18; 13:17; 14:17; Mao 1:16; 3:48; Isa 22:4; 42:24; Eze 9:4; Za 6:6; 119:158; 106:25Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu,

kwa kuwa sheria yako haifuatwi.

Haki Ya Sheria Ya Bwana

137119:137 Kut 9:27; Ezr 9:15; Neh 9:13, 33; Yer 12:1; Dan 9:7Ee Bwana, wewe ni mwenye haki,

sheria zako ni sahihi.

138119:138 Za 119:75, 86; 19:7Sheria ulizoziweka ni za haki,

ni za kuaminika kikamilifu.

139119:139 Za 69:9; Yn 2:17Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu

wanayapuuza maneno yako.

140119:140 Yos 23:14; Za 12:6; 119:47Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu,

mtumishi wako anazipenda.

141119:141 Za 22:6; 119:61, 134; Mit 15:16; Amo 7:2; Lk 6:20; 2Kor 8:9; Yak 2:5Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa,

sisahau mausia yako.

142119:142 Za 119:151, 160; 19:7, 9; Yn 17:17; Efe 1:3Haki yako ni ya milele,

na sheria yako ni kweli.

143119:143 Za 119:24, 47Shida na dhiki zimenipata,

lakini amri zako ni furaha yangu.

144119:144 Za 119:34Sheria zako ni sahihi milele,

hunipa ufahamu ili nipate kuishi.

Maombi Kwa Ajili Ya Kuokolewa

145119:145 Za 119:10, 22, 55Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote,

nami nitayatii maagizo yako.

146119:146 Za 119:94Ninakuita; niokoe

nami nitazishika sheria zako.

147119:147 Za 3:3; 57:8; 108:2Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada;

nimeweka tumaini langu katika neno lako.

148119:148 Za 63:6; 63:1, 6Sikufumba macho yangu usiku kucha,

ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.

149119:149 Za 27:7; 124; 119:40Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako,

Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.

150119:150 Za 37:7Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami,

lakini wako mbali na sheria yako.

151119:151 Flp 4:5; Za 34:18; 119:142; 145:18Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu,

na amri zako zote ni za kweli.

152119:152 Za 119:7, 73, 89; 111:8; Lk 21:33Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako

kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.

Maombi Kwa Ajili Ya Msaada

153119:153 Za 13:3; 3:7; 44:17; Mao 5:1Yaangalie mateso yangu, uniokoe,

kwa kuwa sijasahau sheria yako.

154119:154 Za 119:24, 41; 35:1; 1Sam 24:15; Yer 50:34; Mik 7:9Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe,

uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.

155119:155 Za 119:94, 118; Ay 5:4Wokovu uko mbali na waovu,

kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.

156119:156 Neh 9:27; Yak 5:11; Za 119:25, 149Ee Bwana, huruma zako ni kuu,

uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.

157119:157 Za 7:1; 44:18Adui wanaonitesa ni wengi,

lakini mimi sitaziacha sheria zako.

158119:158 Za 119:104, 136; Kut 32:19Ninawatazama wasioamini kwa chuki,

kwa kuwa hawalitii neno lako.

159119:159 Za 119:25; 41:2Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako;

Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.

160119:160 Za 119:89; 111:8Maneno yako yote ni kweli,

sheria zako zote za haki ni za milele.

Kujiweka Wakfu Kwa Sheria Ya Bwana

161119:161 Za 119:23, 122, 157; 119:120; 1Sam 24:14-15Watawala wamenitesa bila sababu,

lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.

162119:162 Za 119:25; 41:2Nafurahia ahadi zako

kama mtu aliyepata mateka mengi.

163Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo,

lakini napenda sheria yako.

164119:164 Za 119:111; 1Sam 30:16; Isa 9:3; 53:12Ninakusifu mara saba kwa siku,

kwa ajili ya sheria zako za haki.

165119:165 Za 119:11; 37:11; 37:24; Isa 26:3, 12; 27:5; 32:17; 57:19; 66:12; 1Yn 2:10; Mit 3:2Wanaopenda sheria yako wana amani tele,

wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.

166119:166 Za 119:81Ee Bwana, ninangojea wokovu wako,

nami ninafuata amri zako,

167119:167 Za 119:47Ninazitii sheria zako,

kwa sababu ninazipenda mno.

168119:168 Za 139:3; Ay 10:4; 23:10; Mit 5:21Nimetii mausia yako na sheria zako,

kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.

Kuomba Msaada

169119:169 Ay 16:18; Za 119:9, 34Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako,

nipe ufahamu sawasawa na neno lako.

170119:170 1Fal 8:30; 2Nya 6:24; Za 28:2; 140:6; 143:1; 3:7; 22:20; 59:1; 119:41Maombi yangu na yafike mbele zako,

niokoe sawasawa na ahadi yako.

171119:171 Za 51:15; 63:3; 94:12; Isa 2:3; Mik 4:2Midomo yangu na ibubujike sifa,

kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.

172119:172 Za 51:14; 119:7, 75Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,

kwa kuwa amri zako zote ni za haki.

173119:173 Za 37:24; 73:23; Isa 41:10; Lk 10:42; Yos 24:22; Mit 1:29Mkono wako uwe tayari kunisaidia,

kwa kuwa nimechagua mausia yako.

174119:174 Za 119:16, 24, 166Ee Bwana, ninatamani wokovu wako,

na sheria yako ni furaha yangu.

175119:175 Za 119:116, 159; Isa 55:3Nijalie kuishi ili nipate kukusifu,

na sheria zako zinitegemeze.

176119:176 Za 119:10; 95:10; Yer 50:17; Eze 34:11; Lk 15:4Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.

Mtafute mtumishi wako,

kwa kuwa sijasahau amri zako.