Zaburi 128
Thawabu Ya Kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1128:1 Za 103:11; 119:1-3Heri ni wale wote wamchao Bwana,
waendao katika njia zake.
2128:2 Za 58:11; 109:11; Isa 3:10; Mwa 39:3; Mit 10:22Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3128:3 Mwa 49:22; Ay 29:5; Mit 5:15; Eze 19:10; Za 52:8; 144:12Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4128:4 Za 1:1; 112:1Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.
5128:5 Za 122:9; 134:3Bwana na akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6128:6 Mwa 50:23; 48:11; Za 125:5nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.
Amani iwe juu ya Israeli.