サムエル記Ⅰ 31 – JCB & NEN

Japanese Contemporary Bible

サムエル記Ⅰ 31:1-13

31

サウルの死

1その間に、ペリシテ人はイスラエル人と戦いを始めました。イスラエル軍はあえなく敗走し、ギルボア山で大多数が戦死しました。 2ペリシテ軍はサウルを追い詰め、息子のヨナタン、アビナダブ、マルキ・シュアを殺しました。

3-4なお、射手たちはサウルをねらい打ちにし、ついに致命傷を負わせました。王は苦しい息の下から、よろい持ちの護衛兵に言いました。「あの、神を知らぬペリシテ人に捕らえられて恥辱を受けるより、いっそ、おまえの剣で殺してくれ。」しかし、よろい持ちが恐れてためらっていると、王は自分の剣を取り、その切っ先の上にうつ伏せに倒れ、壮烈な最期を遂げました。 5王の死を見届けると、よろい持ちも、自ら剣の上にうつ伏せに倒れて殉死しました。 6こうして、同じ日のうちに、王と三人の息子、よろい持ち、それに兵士たちが次々に死んだのです。 7谷の向かい側やヨルダン川の対岸にいたイスラエル人は、味方の兵士たちが逃げ出し、王とその息子たちが死んだことを聞くと、町々を捨てて逃げ去りました。それで、その町々にはペリシテ人が住むようになったのです。

8翌日、ペリシテ人は死者たちの遺品をはぎ取りに来て、サウルと三人の息子の遺体をギルボア山で発見しました。 9彼らは王の首を切り、武具をはぎ取りました。そして、国中の偶像の神殿と国民とに、サウル王を討ち取ったという朗報を伝えました。 10サウル王の武具はアシュタロテの神殿に奉納され、しかばねはベテ・シャンの城壁にさらされました。 11ヤベシュ・ギルアデの住民は、このペリシテ人の仕打ちを聞くと、 12さっそく勇士たちが夜通しベテ・シャン目指して歩いて行って、サウル王とその息子たちの死体を城壁から降ろし、ヤベシュに運んで火葬にしたのです。 13その骨はヤベシュにある柳の木の根もとに葬られ、人々は七日の間断食して、喪に服しました。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 31:1-13

Sauli Ajiua

(1 Nyakati 10:1-12)

131:1 1Sam 28:4; 1Nya 10:1-12; 1Sam 29:1; 1Nya 8:33Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa. 231:2 1Sam 28:19; 18:1; 14:49; 1Nya 8:33Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua. 331:3 1Sam 28:4; 2Sam 1:6Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.

431:4 Amu 9:54; Mwa 34:14; 1Sam 14:6; 2Sam 1:6, 10Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.”

Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia. 5Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye. 631:6 1Sam 26:10; 12:25; 1Nya 10:6; Rum 6:23Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.

7Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.

831:8 2Sam 1:20Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa. 931:9 1Sam 1:20; 4:4; Amu 16:24Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao. 1031:10 Amu 2:12-13; 1Sam 7:3; Yos 17:11; 2Sam 21:12; 1Sam 21:9; Amu 1:27Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.

1131:11 Amu 21:8; 1Sam 11:1Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli, 1231:12 Za 76:5; Mwa 38:24; Amo 6:10; 2Nya 16:14; 1Sam 11:1-11; 2Sam 2:4-7; Yer 34:5; Amo 6:10mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto. 1331:13 2Sam 21:12-14; Mwa 21:33; 2Sam 3:35; 12:19-23; 1:12; Mwa 50:10; 1Sam 22:6; Mwa 50:10; Ay 2:13Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.