1. Chronik 24 – HOF & NEN

Hoffnung für Alle

1. Chronik 24:1-31

Die Dienstgruppen der Priester

1Auch die Nachkommen von Aaron wurden in verschiedene Gruppen aufgeteilt. Aarons Söhne hießen Nadab, Abihu, Eleasar und Itamar. 2Nadab und Abihu starben noch vor ihrem Vater und hinterließen keine männlichen Nachkommen. Eleasar und Itamar wurden Priester. 3David teilte die Priester in Dienstgruppen ein. Zadok, ein Nachkomme von Eleasar, und Ahimelech, ein Nachkomme von Itamar, halfen ihm dabei: 4Eleasar hatte mehr männliche Nachkommen als Itamar. Darum wurde die Sippe Eleasar in sechzehn Dienstgruppen eingeteilt, die Sippe Itamar in acht. Jede Gruppe wurde von einem Sippenoberhaupt geleitet. 5Die Diensteinteilung wurde durch das Los bestimmt, denn die Priester, die im Heiligtum vor Gott den höchsten Dienst versahen, sollten aus beiden Sippen stammen.

6Bei der Auslosung waren die Nachkommen von Eleasar und Itamar abwechselnd an der Reihe. Dabei waren anwesend: der König, die führenden Männer Israels, der Priester Zadok, Ahimelech, der Sohn von Abjatar, und die Sippenoberhäupter der Priester und Leviten. Der Schreiber Schemaja, ein Sohn von Netanel aus dem Stamm Levi, schrieb die Dienstgruppen in der Reihenfolge auf, in der sie ausgelost wurden:

7-181. Jojarib; 2. Jedaja; 3. Harim; 4. Seorim; 5. Malkija; 6. Mijamin; 7. Hakkoz; 8. Abija; 9. Jeschua; 10. Schechanja; 11. Eljaschib; 12. Jakim; 13. Huppa; 14. Jeschebab; 15. Bilga; 16. Immer; 17. Hesir; 18. Pizez; 19. Petachja; 20. Jeheskel; 21. Jachin; 22. Gamul; 23. Delaja; 24. Maasja.

19Dieser Einteilung entsprechend mussten die Priester in den Tempel des Herrn kommen und ihren Dienst versehen, so wie es der Herr, der Gott Israels, durch ihren Stammvater Aaron befohlen hatte.

Weitere Dienstgruppen der Leviten

20Weitere Sippenoberhäupter der Leviten waren:

Jechdeja, der über Schubaël von Amram abstammte;

21Jischija, ein Nachkomme von Rehabja;

22Jahat, der über Schelomit von Jizhar abstammte;

23Hebrons Söhne in der Reihenfolge ihres Alters: Jerija, Amarja, Jahasiël und Jekamam;

24Schamir, der über Micha von Usiël abstammte;

25Secharja, ein Nachkomme von Michas Bruder Jischija.

26Die Söhne von Merari hießen Machli, Muschi und Jaasija.24,26 Der hebräische Text ist nicht sicher zu deuten.

27Die Söhne von Jaasija, Meraris Sohn, waren Schoham, Sakkur und Ibri. 28-29Machlis Söhne hießen Eleasar und Kisch. Eleasar hatte keine Söhne, Kischs Sohn war Jerachmeel.

30Die Söhne von Muschi hießen Machli, Eder und Jeremot.

Dies waren weitere Sippen der Leviten.

31Wie für die Priester, so wurde auch für sie die Diensteinteilung durch das Los bestimmt. Dabei wurde die Familie eines Sippenoberhaupts genauso behandelt wie die seines jüngsten Bruders. Wieder waren König David, Zadok, Ahimelech und die Sippenoberhäupter der Priester und Leviten anwesend.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 24:1-31

Migawanyo Ya Makuhani

124:1 2Nya 5:11; Ezr 6:18; Kut 6:23; Hes 3:2-4; 26:60Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni:

Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari. 224:2 Law 10:1-2; Hes 3:4; 26:61Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani. 324:3 2Sam 8:17Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao. 4Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari. 524:5 1Nya 26:13; Mdo 1:26; Yos 18:10; Mit 16:33; 18:18Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.

624:6 1Nya 18:16; Neh 8:4; 1Fal 4:3Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.

724:7 Ezr 2:36; Neh 7:39; 12:6Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu,

ya pili Yedaya,

824:8 Ezr 10:21; Neh 12:4-6ya tatu Harimu,

ya nne Seorimu,

9ya tano Malkiya,

ya sita Miyamini,

1024:10 Neh 12:4, 17; Lk 1:5ya saba Hakosi,

ya nane Abiya,

11ya tisa Yeshua,

ya kumi Shekania,

12ya kumi na moja Eliashibu,

ya kumi na mbili Yakimu,

13ya kumi na tatu Hupa,

ya kumi na nne Yeshebeabu,

1424:14 Ezr 2:37; Yer 20:1ya kumi na tano Bilga,

ya kumi na sita Imeri,

1524:15 Neh 10:20ya kumi na saba Heziri,

ya kumi na nane Hapisesi,

16ya kumi na tisa Pethahia,

ya ishirini Yehezkeli,

17ya ishirini na moja Yakini,

ya ishirini na mbili Gamuli,

18ya ishirini na tatu Delaya,

ya ishirini na nne Maazia.

1924:19 1Nya 9:25; Hes 4:49; 2Fal 5:7; Lk 1:18-23Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.

Walawi Waliobaki

2024:20 1Nya 23:6-17Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki:

Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli;

kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.

21Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe:

Ishia alikuwa wa kwanza.

22Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi,

kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.

2324:23 1Nya 23:19; 15:9Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.

24Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika;

kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.

2524:25 1Nya 22:9Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia;

na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.

2624:26 1Nya 6:19; 23:21; Hes 3:20; Kut 6:19Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi.

Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.

27Wana wa Merari:

kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.

2824:28 1Nya 23:22Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.

29Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi:

alikuwa Yerameeli.

3024:30 1Nya 23:23Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi.

Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao. 31Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.