התגלות 5 – HHH & NEN

Habrit Hakhadasha/Haderekh

התגלות 5:1-14

1ראיתי לימין היושב על הכסא מגילה כתובה בפנים ובחוץ וחתומה בשבעה חותמות. 2מלאך גיבור הופיע וקרא בקול גדול: ”מי ראוי לשבור את החותמות ולפתוח את המגילה?“ 3ולא נמצא איש בשמים, בארץ או מבין המתים אשר היה מסוגל לפתוח את המגילה או להביט בכתוב.

4פרצתי בבכי מר, כי איש לא נמצא ראוי לפתוח את המגילה ולקרוא בה. 5אך אחד מעשרים־וארבעה הזקנים אמר אלי: ”אל תבכה. ראה, האריה משבט יהודה ושורש דויד ניצח, והוכיח את עצמו ראוי לשבור את החותמות ולפתוח את המגילה.“

6הבטתי במרכז כסא־המלכות, שמוקף בארבע החיות ובעשרים־וארבעה הזקנים, וראיתי שה שעליו פצעים וחבורות אשר גרמו פעם למותו. לשה היו שבע קרניים ושבע עיניים, שהן שבע רוחות האלוהים שנשלחות אל כל קצווי העולם. 7השה בא ולקח את המגילה מימינו של היושב על כיסא המלכות. 8בלקחו את המגילה השתחוו לפניו ארבע החיות ועשרים־וארבעה הזקנים. כל אחד מהזקנים אחז כינור וקערת זהב מלאה קטורת, אשר היא תפילת בני־האלוהים הקדושים. 9הם שרו שיר חדש, ואלו מילותיו:

”ראוי אתה לקחת את המגילה

ולפתוח את חותמיה,

כי אתה נשחטת,

ובדמך קנית לאלוהים את בניו

מכל עם, גזע ולשון.

10ממלכת כוהנים לאלוהינו עשית אותם,

והם ימלכו על הארץ.“

11לאחר מכן שמעתי בחיזיון קול מלאכים רבים סביב כסא המלכות, ארבע החיות והזקנים. 12הם שרו שירה אדירה:

”ראוי השה הטבוח

לקבל עוז,

עושר וחכמה,

גבורה והדר,

כבוד וברכה.“

13וכל בריה בשמים, בארץ, מתחת לארץ ובים, שמעתי קוראים:

”ליושב על הכסא ולשה

הברכה וההדר והעוז,

לעולם ועד!“

14ארבע החיות אמרו: ”אמן!“ ועשרים וארבעה הזקנים נפלו על פניהם והשתחוו לו.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 5:1-14

Kitabu Na Mwana-Kondoo

15:1 Ufu 4:2, 9; Eze 2:9-10; Isa 29:11; Dan 12:4Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nje, kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba. 25:2 Ufu 10:1Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, akisema, “Ni nani anayestahili kuzivunja hizo lakiri na kukifungua kitabu?” 35:3 Ufu 5:13Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu wala hata kutazama ndani yake. 4Nikalia sana sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake. 55:5 Mwa 49:9; Isa 11:1, 10; Rum 15:12Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba.”

65:6 Yn 1:29; Zek 4:10Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne na miongoni mwa wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba5:6 Roho saba za Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake. za Mungu zilizotumwa duniani pote. 75:7 Ufu 4:2Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka kwenye mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi. 85:8 Ufu 14:2; Za 141:2Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu. 95:9 Za 149:1; Ufu 14:3-4; 4:11; Ebr 9:12; 1Kor 6:20Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema:

“Wewe unastahili kukitwaa kitabu

na kuzivunja lakiri zake,

kwa sababu ulichinjwa

na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu

kutoka kila kabila, kila lugha,

kila jamaa na kila taifa.

105:10 1Pet 5:5Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani

wa kumtumikia Mungu wetu,

nao watatawala duniani.”

115:11 Dan 7:10; Yud 14Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu. 125:12 Ufu 4:11Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema:

“Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa,

kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu

na heshima na utukufu na sifa!”

135:13 Flp 2:10; Mal 1:6; Rum 11:36Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba:

“Sifa na heshima na utukufu na uweza

ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi

na kwa Mwana-Kondoo,

milele na milele!”

145:14 Ufu 4:9-10; 19:4Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee ishirini na wanne wakaanguka kifudifudi wakaabudu.