Salmo 56 – CST & NEN

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Salmo 56:1-13

Salmo 56

Al director musical. Sígase la tonada de «La tórtola en los robles lejanos». Mictam de David, cuando los filisteos lo apresaron en Gat.

1Ten compasión de mí, oh Dios,

pues hay gente que me persigue.

Todo el día me atacan mis opresores,

2todo el día me persiguen mis adversarios;

son muchos los arrogantes que me atacan.

3Cuando siento miedo,

pongo en ti mi confianza.

4Confío en Dios y alabo su palabra;

confío en Dios y no siento miedo.

¿Qué puede hacerme un simple mortal?

5Todo el día tuercen mis palabras;

siempre están pensando hacerme mal.

6Conspiran, se mantienen al acecho;

ansiosos por quitarme la vida,

vigilan todo lo que hago.

7¡En tu enojo, Dios mío, humilla a esos pueblos!

¡De ningún modo los dejes escapar!

8Toma en cuenta mis lamentos;

registra mi llanto en tu libro.56:8 registra mi llanto en tu libro. Lit. pon mis lágrimas en tu frasco.

¿Acaso no lo tienes anotado?

9Cuando yo te pida ayuda,

huirán mis enemigos.

Una cosa sé: ¡Dios está de mi parte!

10Confío en Dios y alabo su palabra;

confío en el Señor y alabo su palabra;

11confío en Dios y no siento miedo.

¿Qué puede hacerme un simple mortal?

12He hecho votos delante de ti, oh Dios,

y te presentaré mis ofrendas de gratitud.

13Tú, oh Dios, me has librado de tropiezos,

me has librado de la muerte,

para que siempre, en tu presencia,

camine en la luz de la vida.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 56:1-13

Zaburi 56

Kumtumaini Mungu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi.

156:1 Za 6:2; 57:1-3; 17:9; 31:9Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali;

mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.

256:2 Za 57:3; 35:1, 25; 124:3Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa,

wengi wananishambulia kwa kiburi chao.

356:3 1Sam 30:6; 2Nya 20:3; Za 55:4-5, 23Wakati ninapoogopa,

nitakutumaini wewe.

456:4 Ebr 13:5, 6; 13:6; Za 27:1; 118:6; Mt 10:28Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,

katika Mungu ninatumaini; sitaogopa.

Mwanadamu apatikanaye na kufa,

atanitenda nini?

556:5 Za 41:7; 2Pet 3:16Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu,

siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.

656:6 Mk 3:6; Za 59:3; 94:21; 71:16; 17:11; Mdo 4:27, 28Wananifanyia hila, wanajificha,

wanatazama hatua zangu,

wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.

756:7 Mt 19:5; Eze 17:15; Rum 2:3; Ebr 12:25; Za 36:12; 55:23Wasiepuke kwa vyovyote,

Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.

856:8 2Fal 20:5; Isa 4:3; Dan 7:10; 12:1; Mal 3:16Andika maombolezo yangu,

orodhesha machozi yangu katika gombo lako:

je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?

956:9 Rum 8:31; Za 9:3; 102:2; Hes 14:8; Kum 31:6Ndipo adui zangu watarudi nyuma

ninapoita msaada.

Kwa hili nitajua kwamba Mungu

yuko upande wangu.

10Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,

katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,

11katika Mungu ninatumaini, sitaogopa.

Mwanadamu anaweza kunitenda nini?

1256:12 Za 50:14; 116:14-16Ee Mungu, nina nadhiri kwako,

nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.

1356:13 Za 30:3; 33:19; 49:15; 86:13; 107:20; 116:8; Ay 33:30Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti

na miguu yangu kwenye kujikwaa,

ili niweze kuenenda mbele za Mungu

katika nuru ya uzima.