路加福音 13 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

路加福音 13:1-35

不悔改的下場

1這時,有人把加利利人獻祭時被彼拉多屠殺的事告訴了耶穌。

2耶穌說:「你們以為這些人被殺,是因為他們的罪比其他加利利人的罪更重嗎? 3不!我告訴你們,你們若不悔改,同樣也必滅亡。 4西羅亞樓倒塌時曾壓死了十八個人。你們以為他們比耶路撒冷其他人更有罪嗎? 5不!我告訴你們,你們若不悔改,同樣也必滅亡。」

6於是,耶穌說了一個比喻:「有人在葡萄園裡種了一棵無花果樹,他去樹那裡找果子,卻找不到。 7他對園丁說,『三年來,我一直盼望它結果子,它卻一個也沒結。把它砍了,免得白佔土地。』

8「園丁請求說,『主人,再留它一年吧!讓我在它四周鬆土、施肥, 9明年如果結了果子就留它,否則再砍掉它。』」

治好駝背婦人

10有個安息日,耶穌在會堂裡講道。 11那裡有個婦人被邪靈纏身十八年,腰彎得很厲害,無法站直。 12耶穌看見她,便叫她過來,說:「婦人,你再不會被疾病纏身了!」 13耶穌雙手按在她身上,她的腰立刻直了,便頌讚上帝。

14會堂主管看到耶穌在安息日為人治病,十分惱怒,就對眾人說:「一週有六天可以工作,求醫應當在這六天之內,不可在安息日!」

15主說:「你們這些偽君子,莫非你們在安息日不解開棚裡的牛和驢,帶牠們去喝水嗎? 16這婦人身為亞伯拉罕的女兒,受撒旦的捆綁十八年,難道不該在安息日為她解開捆索嗎?」 17反對祂的人聽了這番話後,都非常羞愧,眾人卻為耶穌的奇妙作為高興歡喜。

上帝國的比喻

18耶穌繼續說:「上帝的國好像什麼呢?我該把上帝的國比作什麼呢? 19上帝的國就像一粒芥菜種,有人把它種在園裡,它長成了一棵樹,連飛鳥也來棲息在它的樹枝上。」

20耶穌又說:「我該把上帝的國比作什麼呢? 21上帝的國就像麵酵,婦人拿來摻在三斗麵裡,使整團麵都發起來。」

努力進窄門

22耶穌繼續前往耶路撒冷,沿途在各城鎮教導人。 23有人問祂:「主啊,得救的人是否很少呢?」耶穌對他們說:

24「你們要努力進窄門,因為我告訴你們,將來有許多人想要進卻進不去。 25當主人起來把門關閉之後,你們才站在外面叩門哀求,說,『主啊,給我們開門吧!』主人必說,『我不認識你們,你們是從哪裡來的?』

26「那時,你們必說,『我們不是在一起用過餐嗎?你不是在街上教導過我們嗎?』

27「主人必說,『我告訴你們,我不認識你們,也不知道你們是從哪裡來的。你們這些作惡的人,走開!』

28「當你們看見亞伯拉罕以撒雅各和眾先知在上帝的國,自己卻被丟在門外,必要在那裡哀哭切齒。 29那時人們會從東西南北來參加上帝國的宴席。 30看啊,有些殿後的將要為首,有些為首的將要殿後。」

為耶路撒冷哀傷

31那時,有幾個法利賽人來告訴耶穌,說:「快離開這裡吧,希律要殺你!」

32耶穌說:「你們去告訴那個狐狸,『今天和明天,我要繼續趕鬼治病,到第三天,我的任務就完成了。』 33無論如何,今天、明天和後天我必須繼續前行,因為先知不能死在耶路撒冷以外的地方。

34耶路撒冷啊,耶路撒冷啊!你常殺害先知,又用石頭打死派到你那裡的使者。我多次想要招聚你的兒女,像母雞將小雞招聚在翅膀底下,可是你們卻不肯。 35看啊!你們的家園將一片荒涼。我告訴你們,在你們說『奉主名來的當受稱頌』之前,你們再也見不到我了。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 13:1-35

Tubu, La Sivyo Utaangamia

113:1 Mt 27:2Wakati huo huo, kulikuwa na watu waliomwambia Yesu habari za Wagalilaya ambao Pilato aliwaua, na damu ya hao watu akaichanganya na dhabihu yao waliyokuwa wanatoa. 213:2 Yn 9:2-3Yesu akawauliza, “Mnadhani kwamba hawa Wagalilaya ambao walikufa kifo cha namna hiyo walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote? 313:3 Za 7:12La hasha! Ninyi nanyi msipotubu, mtaangamia vivyo hivyo. 413:4 Yn 9:7-11Au wale watu kumi na wanane waliokufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu: mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu? 513:5 Mt 3:2; Mdo 2:38Nawaambia, la hasha! Ninyi nanyi msipotubu, wote mtaangamia vivyo hivyo.”

Mfano Wa Mti Usiozaa Matunda

613:6 Isa 5:2; Mt 21:19Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja. 713:7 Mt 3:10Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’

813:8 2Pet 3:9, 15“Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea. 9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’ ”

Yesu Amponya Mwanamke Kilema Siku Ya Sabato

1013:10 Mt 4:23Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato. 1113:11 Lk 13:16Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima. 12Yesu alipomwona, akamwita, akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.” 1313:13 Mt 5:23Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.

1413:14 Mt 12:2; Lk 14:3; Kut 20:9; Mk 5:22Lakini kiongozi wa sinagogi akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Akaambia ule umati wa watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi. Katika siku hizo, njooni mponywe, lakini si katika siku ya Sabato.”

1513:15 Lk 14:5Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ngʼombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato? 1613:16 Lk 3:8; 19:9; Mt 4:10Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka kifungo hicho siku ya Sabato?”

1713:17 Isa 66:5Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.

Mfano Wa Punje Ya Haradali

(Mathayo 13:31-32; Marko 4:30-32)

1813:18 Mt 3:2; 13:24Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini? 1913:19 Lk 17:6; Mt 13:32Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”

Mfano Wa Chachu

(Mathayo 13:33)

20Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini? 2113:21 1Kor 5:6Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”

Mlango Mwembamba

(Mathayo 7:13-14, 21-23)

2213:22 Lk 9:51Yesu akapita katika miji na vijiji, akifundisha wakati alisafiri kwenda Yerusalemu. 23Mtu mmoja akamuuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?”

2413:24 Mt 7:13Yesu akawaambia, “Jitahidini sana kuingia kupitia mlango mwembamba, kwa maana nawaambia wengi watajaribu kuingia, lakini hawataweza. 2513:25 Mt 7:23; 25:10-12Wakati mwenye nyumba atakapoondoka na kufunga mlango, mtasimama nje mkibisha mlango na kusema, ‘Bwana! Tufungulie mlango!’

“Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako.’

2613:26 Mt 7:22, 23“Ndipo mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, tena ulifundisha katika mitaa yetu.’

2713:27 Mt 25:41“Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’

2813:28 Mt 8:11-12“Ndipo kutakuwako kilio na kusaga meno, mtakapowaona Abrahamu, Isaki, Yakobo na manabii wote wakiwa katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi mkiwa mmetupwa nje. 2913:29 Mal 1:11; Isa 49:12; 59:19; Za 107:3; Lk 14:15Watu watatoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, nao wataketi kwenye sehemu walizoandaliwa karamuni katika Ufalme wa Mungu. 3013:30 Mt 19:30Tazama, kunao walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, nao wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”

Yesu Aomboleza Kwa Ajili Ya Yerusalemu

(Mathayo 23:37-39)

3113:31 Mt 14:1Wakati huo huo baadhi ya Mafarisayo wakamwendea Yesu na kumwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine kwa maana Herode anataka kukuua.”

3213:32 Ebr 2:10Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, ‘Ninafukuza pepo wachafu na kuponya wagonjwa leo na kesho, nami siku ya tatu nitaikamilisha kazi yangu.’ 3313:33 Mt 21:11Sina budi kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa: kwa maana haiwezekani nabii kufa mahali pengine isipokuwa Yerusalemu.

3413:34 Mt 23:37“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka! 3513:35 Yer 12:17; 25:2; Za 118:26; Mt 21:9Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. Ninawaambia, hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.’ ”