詩篇 88 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

詩篇 88:1-18

第 88 篇

求上帝眷顧

可拉後裔的詩,就是以斯拉人希幔的訓誨詩,交給樂長,調用「麻哈拉利暗俄」88·0 麻哈拉利暗俄」意為「受苦」。

1耶和華,拯救我的上帝啊,

我晝夜不停地呼求你。

2求你垂聽我的禱告,

傾聽我的呼求。

3我飽經患難,

生命在死亡的邊緣。

4我被列在下墳墓的人中,

我的精力耗盡。

5我被扔在死人中,

如同被殺的人躺在墳墓裡,

被你遺忘,不再蒙你眷顧。

6你已經把我扔在漆黑的深淵。

7你的烈怒重重地壓著我,

如洶湧波濤把我淹沒。(細拉)

8你使我眾叛親離,遭人唾棄。

我陷入困境,無路可逃。

9我的眼睛因哭泣而視力模糊。

耶和華啊,我天天呼求你,

舉手向你呼求。

10你要行神蹟給死人看嗎?

死人會起來讚美你嗎?(細拉)

11墳墓裡的死人怎能宣揚你的慈愛呢?

滅亡的人怎能傳揚你的信實呢?

12黑暗之地有誰知道你的神蹟呢?

在被遺忘之地有誰知道你的公義作為呢?

13耶和華啊,我向你呼求,

我在清晨向你禱告。

14耶和華啊,你為何棄絕我?

為何掩面不理我?

15我從小受苦,幾乎喪命。

你使我驚恐不已,陷入絕望。

16你的烈怒吞噬了我,

你可怕的攻擊毀滅了我。

17這些災難如洪濤整天環繞我,

徹底圍住我。

18你使我的親朋好友離我而去,

只有黑暗與我相伴。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 88:1-18

Zaburi 88

Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada

Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.

188:1 Za 51:14; 3:4; 22:2; Lk 18:7Ee Bwana, Mungu uniokoaye,

nimelia mbele zako usiku na mchana.

2Maombi yangu yafike mbele zako,

utegee kilio changu sikio lako.

388:3 Ay 33:22; Isa 38:10; Za 6:3; 25:17; 107:18Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,

na maisha yangu yanakaribia kaburi.88:3 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

488:4 Za 31:12; 18:1Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,

niko kama mtu asiye na nguvu.

588:5 Za 31:22Nimetengwa pamoja na wafu,

kama waliochinjwa walalao kaburini,

ambao huwakumbuki tena,

ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.

688:6 Za 30:1; 69:15; Mao 3:55; Yon 2:3Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,

katika vina vya giza nene.

788:7 Za 7:11; 42:7Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,

umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.

888:8 Ay 3:23; 19:13; Za 31:11; Yer 32:2; 33:1Umenitenga na rafiki zangu wa karibu

na kunifanya chukizo kwao.

Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;

988:9 Za 38:10; 5:2; 143:6; Ay 11:13nuru ya macho yangu

imefifia kwa ajili ya huzuni.

Ee Bwana, ninakuita kila siku,

ninakunyooshea wewe mikono yangu.

1088:10 Za 6:5Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?

Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?

1188:11 Za 30:9Je, upendo wako hutangazwa kaburini,

uaminifu wako katika Uharibifu?88:11 Yaani Abadon.

1288:12 Ay 10:21; 31:12; Mhu 8:10Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,

au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

1388:13 Za 30:2; 5:3; 55:17; 119:147Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie;

asubuhi maombi yangu huja mbele zako.

1488:14 Za 43:2; 13:1Ee Bwana, kwa nini unanikataa

na kunificha uso wako?

1588:15 Dan 9:26; Za 9:12; 129:1; Yer 22:21; Eze 16:22; Hos 2:15; Isa 53:8; Ay 6:4; 18:11; 2Kor 4:8Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;

nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.

1688:16 Za 7:11; Ay 6:4Ghadhabu yako imepita juu yangu;

hofu zako zimeniangamiza.

1788:17 Za 124:4Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;

zimenimeza kabisa.

1888:18 Za 88:8; 38:11; Ay 19:13Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;

giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.