詩篇 71 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

詩篇 71:1-24

第 71 篇

一個老年人的祈禱

1耶和華啊,我投靠了你,

求你使我永不蒙羞。

2求你憑公義搭救我,

側耳聽我的懇求,拯救我。

3求你成為保護我的磐石,

讓我可以隨時投靠你。

求你下令救我,

因為你是我的磐石和堡壘。

4我的上帝啊,

求你從惡人手中拯救我,

從邪惡、殘暴之徒掌下拯救我。

5主耶和華啊,你是我的盼望,

我從小就信靠你。

6你使我出了母胎,

我從出生就依靠你,

我要永遠讚美你。

7我的遭遇使許多人感到驚駭,

但你是我堅固的避難所。

8我口中充滿對你的讚美,

終日述說你的榮耀。

9我年老時,求你不要丟棄我;

我體力衰微時,求你不要離棄我。

10我的仇敵議論我,

那些想殺害我的一起策劃陰謀,說:

11「上帝已經丟棄了他。

去追趕、捉拿他吧,

因為無人會救他。」

12上帝啊,不要遠離我;

我的上帝啊,求你快來幫助我!

13願我的仇敵在羞辱中滅亡,

願那些害我的人抱愧蒙羞。

14我必常常心懷盼望,

向你獻上更多的讚美。

15雖然我無法測度你的公義和拯救之恩,

但我要終日傳揚你的作為。

16主耶和華啊,

我要傳揚你大能的作為,

單單述說你的公義。

17上帝啊,

我從小就受你的教導,

直到今日我仍傳揚你奇妙的作為。

18上帝啊,

就是我年老髮白的時候,

求你也不要丟棄我,

好讓我把你的大能告訴下一代,世代相傳。

19上帝啊,你的公義高達穹蒼,

你成就了奇妙大事。

上帝啊,有誰能像你?

20你使我經歷了許多患難,

最終必使我重獲新生,

救我脫離死亡的深淵。

21你必賜我更大的尊榮,

你必再次安慰我。

22我的上帝啊,

我要彈琴讚美你的信實;

以色列的聖者啊,

我要伴隨著琴聲讚美你。

23你救贖了我的靈魂,

我的口和靈魂都要歡呼歌頌你。

24我要終日向人述說你的公義,

因為那些想害我的人已經蒙羞受辱。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 71:1-24

Zaburi 71

Kuomba Ulinzi Na Msaada Siku Zote Za Maisha

171:1 Kum 23:15; Rut 2:12; Za 22:5Ee Bwana, nimekukimbilia wewe,

usiache nikaaibika kamwe.

271:2 2Fal 19:1671:2 Kut 34:6Kwa haki yako uniponye na kuniokoa,

unitegee sikio lako uniokoe.

371:3 Za 18:2Uwe kwangu mwamba wa kimbilio,

mahali nitakapokimbilia kila wakati;

toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe

ni mwamba wangu na ngome yangu.

471:4 2Fal 19:19; Za 140:4; Mwa 48:16Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu,

kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.

571:5 Za 9:18; 25:5; Ay 4:6; Yer 17:7Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi,

tegemeo langu tangu ujana wangu.

671:6 Ay 3:16; Za 9:1; 22:9; 34:1; 52:9; 119:164; 145:2Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,

ulinitoa tumboni mwa mama yangu.

Nitakusifu wewe daima.

771:7 Kum 28:46; 1Kor 4:9; Za 61:3; 2Sam 22:3Nimekuwa kama kioja kwa wengi,

lakini wewe ni kimbilio langu imara.

871:8 Za 71:15; 51:15; 63:5; 96:6; 104:1Kinywa changu kimejazwa sifa zako,

nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.

971:9 Za 51:11; 92:14; Kum 4:31; 31:6Usinitupe wakati wa uzee,

wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

1071:10 Za 3:7; 10:8; 59:3; 31:13; Mt 1:10; 12:14Kwa maana adui zangu wananisengenya,

wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.

1171:11 Isa 40:27; 54:7; Mt 27:46; Za 7:2; 9:10; Mao 5:20Wanasema, “Mungu amemwacha,

mkimbilieni mkamkamate,

kwani hakuna wa kumwokoa.”

1271:12 Za 38:21, 22; 22:19Ee Mungu, usiwe mbali nami,

njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.

1371:13 Ay 8:22; Za 15:3; 70:2; Yer 18:19Washtaki wangu na waangamie kwa aibu,

wale wanaotaka kunidhuru

na wafunikwe kwa dharau na fedheha.

1471:14 Za 25:3; 42:5; 130:7; 131:3Lakini mimi, nitatumaini siku zote,

nitakusifu zaidi na zaidi.

1571:15 Za 71:8; 66:6; 51:14Kinywa changu kitasimulia haki yako,

wokovu wako mchana kutwa,

ingawa sifahamu kipimo chake.

1671:16 Za 77:12; 106:2; 118:15; 9:1; 145:4Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja

na kutangaza matendo yako makuu,

nitatangaza haki yako, yako peke yako.

1771:17 Yer 7:13; Ay 5:9; Za 26:7; 86:10; 96:3; Kum 4:5Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,

hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.

1871:18 Isa 46:4; Kut 9:16; Ay 8:8; Yoe 1:3; Za 78:4; 145:4; 22:30, 31Ee Mungu, usiniache,

hata niwapo mzee wa mvi,

mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho,

nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.

1971:19 Lk 1:49; Za 36:5; 35:10; 77:13; 89:8; 126:2Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu,

wewe ambaye umefanya mambo makuu.

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?

2071:20 Za 80:3, 19; 25:17; 85:4; 63:9; Hos 6:2Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu,

utanihuisha tena,

kutoka vilindi vya dunia

utaniinua tena.

2171:21 Za 18:35; 86:17; Isa 12:1; 40:1, 2; 49:13; 54:10Utaongeza heshima yangu

na kunifariji tena.

2271:22 Za 33:2; 92:3; 144:9; Ay 21:12; 2Fal 19:22Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi

kwa ajili ya uaminifu wako;

Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli,

nitakuimbia sifa kwa zeze.

2371:23 Za 20:5; Kut 15:13Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha

ninapokuimbia sifa,

mimi, ambaye umenikomboa.

2471:24 Za 35:28; Es 9:2Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki

mchana kutwa,

kwa maana wale waliotaka kunidhuru,

wameaibishwa na kufadhaishwa.