耶利米書 4 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 4:1-31

1耶和華說:「以色列啊,

如果你回轉歸向我,

回轉歸向我,

從我眼前除掉可憎的神像,

不再離開我;

2如果你本著誠實、正直、公義,

憑永活的耶和華起誓,

你必成為萬國的祝福,

得到他們的尊敬4·2 你必成為萬國的祝福,得到他們的尊敬」或譯「萬國必得到耶和華的祝福,並以祂為榮」。。」

3耶和華對猶大人和耶路撒冷人說:

「要開墾你們的荒地,

不要在荊棘中撒種。

4你們要自行割禮,

除掉心中的污垢,歸向耶和華。

不然,我必因你們的惡行而發烈怒,如火燃燒,

無人能夠撲滅。

5「你們要在猶大耶路撒冷宣告,

『要在全國吹起號角』,高聲呼喊,

『要集合起來,

我們要逃進堅城。』

6你們要向錫安舉起旗幟,

趕快逃亡,不要遲延,

因為我要從北方降下災禍,

大肆毀滅。」

7毀滅列國者已發起攻擊,

如獅子衝出巢穴,

要使你們的土地荒涼,

城邑淪為廢墟,無人居住。

8為此,你們要腰束麻布,

嚎啕大哭,

因為耶和華向我們發的烈怒還沒有止息。

9耶和華說:「到那天,君王和官長必喪膽,祭司和先知必驚駭。」 10我說:「唉!主耶和華啊,你完全欺騙了這群百姓和耶路撒冷人,因為你說,『你們會安享太平。』其實劍鋒已指著他們的咽喉了。」

11那時,耶和華必對這群百姓和耶路撒冷人說:「一陣熱風從荒野光禿的山頭吹向我的子民,不是為揚場、吹淨糠秕。 12那是我發出的一陣強風。現在我要宣告我對他們的審判。」

13看啊,仇敵必如雲湧來,

他的戰車快如旋風,

他的戰馬比飛鷹還快。

我們有禍了!

我們滅亡了!

14耶路撒冷啊,

要洗去你內心的邪惡,

這樣你才能得救。

你心懷惡念要到何時呢?

15傳來消息,

以法蓮山區報出惡訊。

16耶和華說:「你們去通知列國,

耶路撒冷宣告,

『圍攻的人從遠方來,

猶大的城邑高聲喊殺,

17像看守田園一樣包圍耶路撒冷

因為耶路撒冷背叛了我。』

這是耶和華說的。

18你的所作所為給你招致這災禍,

是你自食惡果,你會痛徹心肺!」

19我的心啊,我的心啊!

我傷心欲絕,煩躁不安。

我無法保持緘默,

因為我聽見了號角聲和呐喊聲。

20惡訊頻傳,山河破碎,

我的帳篷忽然倒塌,

幔子頃刻破裂。

21我還要看這旌旗、

聽這號聲到何時呢?

22耶和華說:「我的子民愚頑,

不認識我,

是蒙昧無知的兒女,

只知行惡,不知行善。」

23我俯瞰大地,

一片空虛混沌;

我仰望天空,毫無亮光。

24我眺望群山,大山在顫抖,

小山在搖晃。

25我四下觀看,只見杳無人煙,

飛鳥絕跡。

26我四下觀看,只見良田變荒野,

城邑都在耶和華的烈怒下淪為廢墟。

27耶和華說:「遍地將要荒涼,

然而不會被我徹底毀滅。

28因此,地要悲哀,

天要昏暗,

因為我言出必行,

決不反悔。」

29各城的人聽到騎兵和弓箭手的呐喊,

都紛紛逃命。

有的跑入叢林,有的爬進岩洞。

各城荒棄,無人居住。

30你這荒涼的城啊!

你在做什麽?

縱然你穿上紅袍,

戴上金飾,

描眉畫眼,

又有什麼用呢?

你的情人藐視你,

要殺害你。

31我聽見好像婦人分娩時的喊叫聲,

好像婦人生頭胎時的痛苦呻吟。

那是錫安4·31 」希伯來文是「女子」,可能是對錫安的暱稱,下同6·223的喊叫聲,

她在喘息,伸出雙手說:

「噢!我有禍了,

我要死在殺戮者手上了。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 4:1-31

14:1 Yoe 2:12; Ezr 8:5; 2Fal 7:13; 21:4; Kum 4:30; Hos 12:6; Yer 16:18; 35:15“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli,

nirudie mimi,”

asema Bwana.

“Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu

na usiendelee kutangatanga,

24:2 Kum 10:20; Hes 14:21; Gal 3:8; Hos 4:15; Mwa 12:2; Isa 19:18; 65:16; Yer 12:16ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa,

‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’

ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye

na katika yeye watajitukuza.”

34:3 Hos 10:12; Mk 4:18Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu:

“Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu,

wala msipande katikati ya miiba.

44:4 Law 26:41; Rum 2:28-29; Sef 2:2; Amo 5:6; Ay 41:21; Kut 32:22; Yer 8:14; Yos 10:20; Yer 5:20; Hes 10:2-7; Ay 39:24Jitahirini katika Bwana,

tahirini mioyo yenu,

enyi wanaume wa Yuda

na watu wa Yerusalemu,

la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu

na kuwaka kama moto

kwa sababu ya uovu mliotenda,

ikiwaka pasipo wa kuizima.

Maafa Kutoka Kaskazini

5“Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema:

‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’

Piga kelele na kusema:

‘Kusanyikeni pamoja!

Tukimbilie katika miji yenye maboma!’

64:6 Yer 1:13-15; Isa 14:31; Za 74:4; Isa 31:9; Yer 50:2; 11:11; 18:11Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni!

Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa!

Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini,

maangamizi ya kutisha.”

74:7 Dan 7:4; Eze 12:20; Yer 2:15; Isa 6:11; Yer 25:38; Hos 5:14; Nah 2:12; Yer 6:26Simba ametoka nje ya pango lake,

mharabu wa mataifa amejipanga.

Ametoka mahali pake

ili aangamize nchi yenu.

Miji yenu itakuwa magofu

pasipo mtu wa kuishi humo.

84:8 1Fal 21:27; Yer 30:24; Isa 22:12; 3:24; Yer 6:26; Eze 7:18; Yer 7:29; 9:20Hivyo vaeni nguo za magunia,

ombolezeni na kulia kwa huzuni,

kwa kuwa hasira kali ya Bwana

haijaondolewa kwetu.

9“Katika siku ile,” asema Bwana

“mfalme na maafisa watakata tamaa,

makuhani watafadhaika,

na manabii watashangazwa mno.”

104:10 Eze 14:9; Kut 5:23; 2The 2:11; Isa 63:17; Yer 6:14; 8:11; Eze 13:10; Mik 3:5Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”

114:11 Mwa 41:6; Hos 13:15; Eze 17:10; Law 26:33; Ay 1:19Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa, 124:12 Isa 64:6; Yer 1:16upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”

134:13 Isa 5:28; 2Sam 22:10; Eze 26:10; Kum 28:49; Mao 4:19; Isa 66:15Tazama! Anakuja kama mawingu,

magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli,

farasi wake wana mbio kuliko tai.

Ole wetu! Tunaangamia!

144:14 Rut 3; 3; Yak 4:8; Za 51:2; Isa 45:22; Za 6:3Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe.

Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?

154:15 Yer 8:16; Mwa 30:6; Yer 31:6Sauti inatangaza kutoka Dani,

ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16“Waambie mataifa jambo hili,

piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu:

‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali,

likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.

174:17 2Fal 25:1-4; 1Sam 12:15; Yer 5:23Wamemzunguka kama watu walindao shamba,

kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’ ”

asema Bwana.

184:18 Za 107:17; Ay 20:6-11; Yer 2:17-19; Isa 1:28; Yer 5:25“Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe

yameleta haya juu yako.

Hii ndiyo adhabu yako.

Tazama jinsi ilivyo chungu!

Tazama jinsi inavyochoma moyo!”

194:19 Isa 16:11; Mao 1:20; Hes 10:9; Yer 20:9; Sef 1:16; Isa 22:4; Yer 6:24Ee mtima wangu, mtima wangu!

Ninagaagaa kwa maumivu.

Ee maumivu makuu ya moyo wangu!

Moyo wangu umefadhaika ndani yangu,

siwezi kunyamaza.

Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta,

nimesikia kelele ya vita.

204:20 Kum 31:17; Za 42:7; Hes 24:5; Mao 2:4; Yer 10:20Maafa baada ya maafa,

nchi yote imekuwa magofu.

Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa,

makazi yangu kwa muda mfupi.

214:21 Hes 2:2; Isa 18:3; Yos 6:20; Hos 5:8Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita

na kusikia sauti za tarumbeta?

224:22 1Kor 14:20; Yer 5:21; 13:23; Za 36:3; Rum 16:19; Yer 5:21; 10:8; Za 14:4“Watu wangu ni wapumbavu,

hawanijui mimi.

Ni watoto wasio na akili,

hawana ufahamu.

Ni hodari kutenda mabaya,

hawajui kutenda yaliyo mema.”

234:23 Ay 9:7; 30:26; Isa 5:30; 59:9; Mao 3:2Niliitazama dunia,

nayo haikuwa na umbo tena ni tupu;

niliziangalia mbingu,

mianga ilikuwa imetoweka.

244:24 Eze 38:20; Ay 9:6; Isa 5:25; Kut 19:18Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka,

vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.

254:25 Hos 4:3; Sef 1:3; Yer 7:20Nilitazama, wala watu hawakuwepo;

kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.

26Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa,

miji yake yote ilikuwa magofu

mbele za Bwana,

mbele ya hasira yake kali.

274:27 Amo 9:8; Yer 5:10; 12:12; Eze 20:17; Yer 46:28Hivi ndivyo Bwana asemavyo:

“Nchi yote itaharibiwa,

ingawa sitaiangamiza kabisa.

284:28 Yer 14:2; Hos 4:3; Hes 23:19; Isa 5:30; Yer 30:24; 23:20; 12:4-11Kwa hiyo dunia itaomboleza

na mbingu zilizo juu zitakuwa giza,

kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma,

nimeamua na wala sitageuka.”

294:29 Yer 8:16; Isa 6:12; 2Fal 25:4; Yer 6:23; 1Sam 26:20; Kut 33:22Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde

kila mji unakimbia.

Baadhi wanakimbilia vichakani,

baadhi wanapanda juu ya miamba.

Miji yote imeachwa,

hakuna aishiye ndani yake.

304:30 Isa 10:3-4; Eze 16:11; 23:40; 2Fal 9:30; Ay 19:14; Eze 23:9; Za 35:4Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa?

Kwa nini unajivika vazi jekundu

na kuvaa vito vya dhahabu?

Kwa nini unapaka macho yako rangi?

Unajipamba bure.

Wapenzi wako wanakudharau,

wanautafuta uhai wako.

314:31 Mwa 3:16; Mik 4:10; Isa 42:14; Mao 1:17; Yer 6:24; 13:21; 22:23; Za 9:14; Isa 42:14; Kum 32:25; Mao 2:21Nasikia kilio kama cha mwanamke

katika utungu wa kuzaa,

kilio cha uchungu kama cha anayemzaa

mtoto wake wa kwanza:

kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua,

akiinua mikono yake, akisema,

“Ole wangu! Ninazimia;

maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”