耶利米書 12 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 12:1-17

耶利米的抱怨

1耶和華啊,每次我與你爭論,

都顯明你是對的。

然而,我還是對你的公正有所不解:

為什麼惡人總是得勢?

為什麼詭詐之人反而生活安逸?

2你栽培他們,讓他們生根長大,

結出果實。

他們嘴上尊崇你,

心卻遠離你。

3但耶和華啊,你認識我,瞭解我,

察驗我的內心。

求你拖走他們,

就像拖走待宰的羊,

留到宰殺之日。

4大地哀慟、

田野的植物枯槁要到何時呢?

由於這地方居民的罪惡,

野獸和飛鳥都滅絕了。

他們說:「上帝看不見我們的行為12·4 上帝看不見我們的行為」參照《七十士譯本》,希伯來文也可譯作「他(指耶利米)看不見我們的結局」。。」

5耶和華說:「如果你與步行的人競走,

尚且感到疲乏,

又怎能與馬賽跑呢?

如果你在寬闊之地尚且跌倒,

約旦河邊的叢林中又會怎樣呢?

6你的弟兄和家人都背叛了你,

與你作對。

任他們甜言蜜語,你不要相信。

7「我已離開我的殿,

撇棄我的產業,

把我愛的子民交給他們的敵人。

8我的子民像林中的獅子一樣向我吼叫,

因此我憎惡他們;

9我的子民就像一隻帶斑點的鷙鳥,

被其他鷙鳥圍攻。

招聚野獸來吞吃牠吧!

10列國的首領毀壞我的葡萄園,

踐踏我美好的土地,

使它荒涼;

11他們使這片土地荒涼,

以致它在我面前哀哭。

遍地如此荒涼,卻無人在意。

12殺戮者已來到曠野中光禿的山嶺,

耶和華使刀劍橫掃全境,

無人倖免。

13我的子民播種麥子,

卻收割荊棘;

辛勤耕耘,卻一無所獲。

他們必因耶和華的烈怒而收穫羞辱。」

14耶和華說:「邪惡的鄰國侵佔了我賜給我以色列子民的土地,我要把這些惡鄰逐出他們的本土,正如我要逐出猶大一樣。 15我逐出他們以後,還要再憐憫他們,把他們帶回各自的家園和故土。 16如果他們真心接受我子民的信仰,憑永活的耶和華之名起誓,正如他們教導我子民向巴力起誓一樣,他們便能成為我的子民。 17如果哪一國不聽我的話,我必把它連根拔起,徹底毀滅。這是耶和華說的。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 12:1-17

Lalamiko La Yeremia

112:1 Ay 8:3; 12:6; Dan 9:14; Ay 21:7, 13; Ezr 9:15; Ay 5:8; Eze 18:25; Yer 5:27-28Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana,

niletapo mashtaka mbele yako.

Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako:

Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa?

Kwa nini wasio waaminifu

wote wanaishi kwa raha?

212:2 Isa 29:13; Eze 22:27; Yer 11:17; Mk 7:6; Ay 5:3; Yer 3:10; Mt 15:8; Tit 1:16Umewapanda, nao wameota,

wanakua na kuzaa matunda.

Daima u midomoni mwao,

lakini mbali na mioyo yao.

312:3 Yer 17:18; Za 7:9; 11:5; Yer 20:11; 16:18Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana;

unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe.

Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa!

Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!

412:4 Yer 4:25-28; Yoe 1:10-12; Kum 28:15-18; Za 107:34; Yer 4:26; 9:10Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini,

na majani katika kila shamba kunyauka?

Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu,

wanyama na ndege wameangamia.

Zaidi ya hayo, watu wanasema,

Bwana hataona yatakayotupata sisi.”

Jibu La Mungu

512:5 Yer 49:19; 50:44“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda,

unawezaje kushindana na farasi?

Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama,

utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?

612:6 Mit 26:24-25; Yer 9:4; Za 12:2Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe:

hata wao wamekusaliti;

wameinua kilio kikubwa dhidi yako.

Usiwaamini, ingawa wanazungumza

mema juu yako.

7“Nitaiacha nyumba yangu,

nitupe urithi wangu;

nitamtia yeye nimpendaye

mikononi mwa adui zake.

812:8 Amo 6:8; 2Nya 36:16; Za 17:12; Hos 9:15Urithi wangu umekuwa kwangu

kama simba wa msituni.

Huningurumia mimi,

kwa hiyo ninamchukia.

912:9 Kum 28:26; Isa 56:9; Yer 15:3; Eze 23:25; 39:17-20Je, urithi wangu haukuwa

kama ndege wa mawindo wa madoadoa

ambaye ndege wengine wawindao

humzunguka na kumshambulia?

Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni;

walete ili wale.

1012:10 Yer 25:34; Eze 33:2; Isa 5:1-7; Yer 9:10; 25:11Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu

na kulikanyaga shamba langu;

watalifanya shamba langu zuri

kuwa jangwa la ukiwa.

1112:11 Isa 42:25; Yer 23:10; Isa 5:6; 24:4; Yer 9:12; 14:4Litafanywa kuwa jangwa,

lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu;

nchi yote itafanywa jangwa

kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.

1212:12 Kum 32:41; Eze 33:2; Yer 3:2; Eze 21:3-4; Isa 31:8; Yer 46:10; Eze 14:17Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani

mharabu atajaa,

kwa maana upanga wa Bwana utawala,

kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine;

hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.

1312:13 Mik 6:15; Kut 15:7; Yer 4:26; Law 26:16-20; Kum 28:38Watapanda ngano lakini watavuna miiba;

watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote.

Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako

kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”

1412:14 Zek 2:7-9; Sef 2:8-10; Yer 32:37; 2Nya 7:20; Za 9:6; Kum 29:28Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao. 1512:15 Kum 30:3; Amo 9:14-15; Eze 28:25; Za 6:2Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe. 1612:16 Yer 4:2; Yos 23:7; Efe 2:20; Isa 26:18; 49:6; Yer 18:8; 3:17Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu. 1712:17 Mwa 27:29; Isa 60:12; Za 2:8-9Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.