耶利米哀歌 2 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米哀歌 2:1-22

耶和華懲罰耶路撒冷

1主的怒氣像烏雲一樣遮蓋錫安2·1 」希伯來文是「女子」,可能是對錫安的暱稱,下同2·4104·22

祂使以色列的榮美從天上墜下。

祂發怒的時候並不顧念自己的腳凳。

2主毫不留情地毀滅雅各一切的住處,

祂在烈怒中夷平猶大的堡壘,

以色列及其首領蒙羞。

3祂發烈怒毀滅以色列全軍。

敵人襲來時,祂收回大能的手。

祂像烈焰一樣吞噬雅各

4祂抬起右手張弓搭箭,

宛若仇敵,

殺戮一切悅人眼目的人,

將祂的怒火撒向錫安城的帳篷。

5主像敵人一樣毀滅以色列

吞噬她的宮殿,夷平她的堡壘,

使猶大人哀哭不止。

6祂摧毀自己的居所,

如同摧毀花園;

祂摧毀自己規定的聚會之處,

使錫安的人民忘記安息日和節期。

祂在烈怒中棄絕所有的君王和祭司。

7主撇棄自己的祭壇,

憎惡自己的聖所,

耶路撒冷的殿牆交給敵人。

他們像過節一樣,

在耶和華的殿中喧嚷吵鬧。

8耶和華決意拆毀錫安的城牆,

祂拉了準線,

定意毀滅,決不停止。

祂使城牆和壁壘一同悲哀哭泣。

9錫安的城門陷入地中,

主摧毀、砍斷她的門閂。

她的君王和首領流落異鄉,

律法不復存在,

她的先知得不到從耶和華而來的異象。

10錫安城的長老腰束麻布,

頭蒙灰塵,坐在地上,

默然不語;

耶路撒冷的少女垂頭至地。

11我哭得眼睛失明,

心如刀割,肝膽欲碎,

因為人民慘遭毀滅,

兒童和嬰孩昏倒在街頭。

12孩子們問母親:

「哪裡有餅和酒呢?」

他們像受傷的勇士,

昏倒在城中的街頭,

在母親懷中奄奄一息。

13耶路撒冷啊,我該說什麼呢?

誰能與你的苦難相比呢?

錫安啊,我用什麼話語才能安慰你呢?

你的傷口深如海洋,

誰能醫治你呢?

14你的先知所見的異象虛假無用。

他們沒有揭露你的罪惡,

以致你被擄。

他們給你的預言虛假謬誤。

15路人都拍掌嘲笑你。

他們向耶路撒冷城搖頭,

嗤笑道:

「這就是那被譽為完美無瑕、

普世喜悅的城嗎?」

16敵人都幸災樂禍地譏諷你,

他們咬牙切齒地說:

「我們吞滅了她!

這是我們期待已久的日子!

我們終於見到這一天了!」

17耶和華實現了祂的計劃,

成就了祂很久以前的應許。

祂毫不留情地毀滅了你,

使你的仇敵幸災樂禍,

耀武揚威。

18錫安的城牆啊,

你要從心裡向主呼求!

你的眼淚要像江河一樣晝夜湧流,

不歇不眠。

19你要在夜間起來,

在主面前整夜呼求,

向祂傾心吐意;

你要為餓昏街頭的孩童向主舉手禱告。

20「耶和華啊,求你看看,

你曾這樣對付過誰呢?

母親豈能吃自己的孩子?

祭司和先知豈能在主的聖所中被殺?

21「老人和小孩陳屍街頭,

少男少女都喪身刀下。

你在發怒的日子殺了他們,

毫不留情。

22「你從四面八方召人攻擊我,

如同召集人過節。

耶和華發怒的日子,

無人得以逃脫,無人得以倖免。

敵人殺光了我養育的孩子。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Maombolezo 2:1-22

2 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 12:1 Mao 3:44; Za 132:7; 1Nya 28:2; Yer 12:7; Za 99:5; Mt 11:23; 2Sam 1:19Tazama jinsi Bwana alivyomfunika Binti Sayuni

kwa wingu la hasira yake!

Ameitupa chini fahari ya Israeli

kutoka mbinguni mpaka duniani,

hakukumbuka kiti chake cha kuwekea miguu

katika siku ya hasira yake.

22:2 Mao 3:43; Mik 5:11; Isa 25:12; Za 89:39-40; 21:9Bila huruma Bwana ameyameza

makao yote ya Yakobo;

katika ghadhabu yake amebomoa

ngome za Binti Yuda.

Ameuangusha ufalme wake na wakuu wake

chini kwa aibu.

32:3 Za 75:5; 74:11; Isa 42:25; Ay 16:15; Yer 21:4-5Katika hasira kali amevunja

kila pembe2:3 Pembe inawakilisha nguvu; pia 2:17. ya Israeli.

Ameuondoa mkono wake wa kuume

alipokaribia adui.

Amemteketeza Yakobo kama moto uwakao

ule uteketezao kila kitu kinachouzunguka.

42:4 Isa 63:10; Ay 3:23; Mao 3:12-13; Yer 7:20; Eze 24:16; 2Nya 34:21; Eze 20:34Ameupinda upinde wake kama adui,

mkono wake wa kuume uko tayari.

Kama vile adui amewachinja

wote waliokuwa wanapendeza jicho,

amemwaga ghadhabu yake kama moto

juu ya hema la Binti Sayuni.

52:5 Yer 30:14; Ay 13:24; Yer 9:17-20; Isa 29:2; Yer 7:20Bwana ni kama adui;

amemmeza Israeli.

Amemeza majumba yake yote ya kifalme

na kuangamiza ngome zake.

Ameongeza huzuni na maombolezo

kwa ajili ya Binti Yuda.

62:6 Yer 52:13; Sef 3:18; Yer 7:14; Isa 43:28; Mao 4:16; 5:12; Za 80:12; Isa 5:5; 1:8Ameharibu maskani yake kama bustani,

ameharibu mahali pake pa mkutano.

Bwana amemfanya Sayuni kusahau

sikukuu zake zilizoamriwa na Sabato zake;

katika hasira yake kali amewadharau

mfalme na kuhani.

72:7 Eze 7:1-2; Isa 64:10-11; Yer 7:12-14; Law 26:31; Yer 33:4-5; 52:13; Za 78:59-61; Mik 3:12; Yer 7:12-14; Mt 24:2Bwana amekataa madhabahu yake

na kuacha mahali patakatifu pake.

Amemkabidhi adui kuta

za majumba yake ya kifalme;

wamepiga kelele katika nyumba ya Bwana

kama katika siku ya sikukuu iliyoamriwa.

82:8 2Fal 21:13; Isa 34:11; 3:26; Yer 39:8; Za 48:13; Amu 7:7Bwana alikusudia kuangusha

ukuta uliomzunguka Binti Sayuni.

Ameinyoosha kamba ya kupimia

na hakuuzuia mkono wake usiangamize.

Alifanya maboma na kuta ziomboleze,

vyote vikaharibika pamoja.

92:9 Yer 16:13; Amo 8:11-12; Hos 3:4; 2Nya 15:3; Yer 14:14; Isa 45:2; 2Fal 24:15; Kum 28:36; 2Fal 25:7; Za 74:9; Mik 3:6, 7Malango yake yamezama ardhini,

makomeo yake ameyavunja na kuyaharibu.

Mfalme wake na wakuu wake wamepelekwa uhamishoni

miongoni mwa mataifa,

sheria haipo tena,

na manabii wake hawapati tena

maono kutoka kwa Bwana.

102:10 Ay 2:12-13; Isa 3:24, 26; Eze 27:30-31; Isa 15:3; Mao 3:28; 4:5; Isa 47:1-5Wazee wa Binti Sayuni

wanaketi chini kimya,

wamenyunyiza mavumbi kwenye vichwa vyao

na kuvaa nguo za gunia.

Wanawali wa Yerusalemu

wamesujudu hadi ardhini.

112:11 Isa 15:3; Ay 30:27; Za 22:14; Ay 16:13; Mao 3:48-51; Za 119:82; 6:7Macho yangu yamedhoofika kwa kulia,

nina maumivu makali ndani,

moyo wangu umemiminwa ardhini

kwa sababu watu wangu wameangamizwa,

kwa sababu watoto na wanyonyao wanazimia

kwenye barabara za mji.

12Wanawaambia mama zao,

“Wapi mkate na divai?”

wazimiapo kama watu waliojeruhiwa

katika barabara za mji,

maisha yao yadhoofikavyo

mikononi mwa mama zao.

132:13 Isa 37:22; Yer 14:17; 30:12-15; Dan 9:12; 2Fal 19:2; Ay 5:1Ninaweza kusema nini kwa ajili yako?

Nikulinganishe na nini,

ee Binti Yerusalemu?

Nitakufananisha na nini,

ili nipate kukufariji,

ee Bikira Binti Sayuni?

Jeraha lako lina kina kama bahari.

Ni nani awezaye kukuponya?

142:14 Isa 58:1; Yer 8:11; 20:6; Eze 13:3; Yer 28:3; 28:15; Eze 22:28Maono ya manabii wako

yalikuwa ya uongo na yasiyofaa kitu,

hawakuifunua dhambi yako

ili kukuzuilia kwenda utumwani.

Maneno waliyokupa

yalikuwa ya uongo na ya kupotosha.

152:15 Hes 24:20; Eze 25:6; Nah 3:19; Za 45:11; Eze 16:14; Za 48:2; Yer 19:8; 1Fal 9:8Wote wapitiao njia yako

wanakupigia makofi,

wanakudhihaki na kutikisa vichwa vyao

kwa Binti Yerusalemu:

“Huu ndio ule mji ulioitwa

mkamilifu wa uzuri,

furaha ya dunia yote?”

162:16 Za 22:13; 56:2; Ay 16:19; Za 35:25; Eze 36:3; Mao 3:46Adui zako wote wanapanua

vinywa vyao dhidi yako,

wanadhihaki na kusaga meno yao

na kusema, “Tumemmeza.

Hii ndiyo siku tuliyoingojea,

tumeishi na kuiona.”

172:17 Kum 28:15-45; Eze 8:18; Isa 44:26; Mao 1:5; Law 26:16; Za 38:16Bwana amefanya lile alilolipanga;

ametimiza neno lake

aliloliamuru siku za kale.

Amekuangusha bila huruma,

amewaacha adui wakusimange,

ametukuza pembe ya adui yako.

182:18 Za 119:145; Mao 1:16; 3:19; Yer 9:1; 14:7Mioyo ya watu

inamlilia Bwana.

Ee ukuta wa Binti Sayuni,

machozi yako na yatiririke kama mto

usiku na mchana;

usijipe nafuu,

macho yako yasipumzike.

192:19 Mk 13:35; 1Sam 1:15; Za 62:8; Isa 51:20; Neh 3:10; Isa 26:9; Mao 4:1Inuka, lia usiku,

zamu za usiku zianzapo;

mimina moyo wako kama maji

mbele za Bwana.

Mwinulie yeye mikono yako

kwa ajili ya maisha ya watoto wako,

ambao wanazimia kwa njaa

kwenye kila mwanzo wa barabara.

202:20 Kum 28:53; Eze 5:10; Mao 4:10; Yer 23:11-12; 19:9; Za 78:64; Yer 14:15; Kut 32:11; Law 26:29“Tazama, Ee Bwana, ufikirie:

Ni nani ambaye umepata

kumtendea namna hii?

Je, wanawake wakule wazao wao,

watoto waliowalea?

Je, kuhani na nabii auawe

mahali patakatifu pa Bwana?

212:21 Kum 32:25; 2Nya 36:17; Yer 13:14; Zek 11:6“Vijana na wazee hujilaza pamoja

katika mavumbi ya barabarani,

wavulana wangu na wasichana

wameanguka kwa upanga.

Umewaua katika siku ya hasira yako,

umewachinja bila huruma.

222:22 Za 31:13; Yer 6:25; Ay 27:14; Hes 9:13; Yer 20:10“Kama ulivyoita siku ya karamu,

ndivyo ulivyoagiza hofu kuu

dhidi yangu kila upande.

Katika siku ya hasira ya Bwana

hakuna yeyote aliyekwepa au kupona;

wale niliowatunza na kuwalea,

adui yangu amewaangamiza.”