約書亞記 18 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約書亞記 18:1-28

其餘土地的分配

1征服了這些地方以後,以色列全體會眾都聚集在示羅,把會幕設立在那裡。 2這時,以色列還有七個支派沒有分到產業。 3約書亞對他們說:「你們等到什麼時候才去佔領你們祖先的上帝耶和華賜給你們的土地呢? 4你們每支派要派出三個人,我要差他們去偵察,按各支派應得的土地繪製地圖,然後回來稟告我。 5他們要把土地劃分作七份。猶大要留在南部自己的領土上,約瑟家族要留在北部自己的領土上。 6你們把這七份土地繪成地圖交給我,我要在我們的上帝耶和華面前為你們抽籤。 7你們當中的利未人沒有份,因為做耶和華的祭司這職任就是他們的產業。至於迦得支派、呂便支派和瑪拿西半個支派,摩西已把約旦河東的土地分給他們了。」

8那些畫地圖的人啟程出發的時候,約書亞囑咐他們說:「你們要走遍那裡,繪製地圖,然後回來稟告我,我要在示羅,在耶和華面前為你們抽籤。」 9於是,他們走遍那裡,把所有城邑分作七份,繪在冊上,然後回到示羅約書亞10約書亞便在示羅按照以色列的支派,在耶和華面前為他們抽籤分地。

便雅憫支派分到的土地

11便雅憫支派按宗族抽籤分到的領土,座落在猶大約瑟支派的領土之間。 12他們北部的邊界從約旦河起,沿耶利哥北面的山坡直上,往西穿過山區,直到伯·亞文的曠野; 13從那裡經路斯,即伯特利南面山坡到下伯·和崙南面山區的亞他綠·亞達14西面的邊界自伯·和崙對面山的西側向南直到猶大人的基列·巴力,即基列·耶琳15南部邊界從基列·耶琳的邊界開始向西直到尼弗多亞的水泉, 16又往下到欣嫩子谷對面的山麓,也就是利乏音谷北邊,然後往南,經欣嫩谷到耶布斯山南部,直到隱·羅結17然後,向北先後到隱·示麥亞都冥山坡對面的基利綠呂便的兒子波罕所立的大石, 18以及亞拉巴的對面,再往北下到亞拉巴19又沿著伯·曷拉的北面直到鹽海的北岸,也就是約旦河的南部河口。這是南部的邊界。 20東面以約旦河為界。這是便雅憫人按宗族分到的土地和四周的邊界。

21以下是便雅憫支派按宗族分到的城邑:耶利哥伯·曷拉伊麥·基悉22伯·亞拉巴西瑪蓮伯特利23亞文巴拉俄弗拉24基法·阿摩尼俄弗尼迦巴,共十二座城及其附近的鄉村。 25還有基遍拉瑪比錄26米斯巴基非拉摩撒27利堅伊利毗勒他拉拉28洗拉以利弗耶布斯——即耶路撒冷基比亞基列,共十四座城及其附近的鄉村。

這就是便雅憫各宗族所分到的土地。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 18:1-28

Mgawanyo Wa Nchi Iliyobaki

118:1 Yos 19:51; 21:2; Amu 18:31; 21:12; 1Sam 1:3; 3:21; 4:3; 1Fal 14:2; Za 78:60; Yer 7:12; 26:6; 41:5; Kut 27:21; 40:2; Mdo 7:45Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao, 2lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.

318:3 Amu 18:9; Sef 3:16; Mt 20:6; Yn 6:27; Flp 3:13-14Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa? 418:4 Mik 2:5Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia. 518:5 Yos 15:1; 16:1-4Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini. 618:6 Law 16:8; Yos 14:2Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu. 718:7 Yos 13:33; 13:8Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”

8Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.” 9Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo. 1018:10 Hes 34:13; Yer 7:12; Hes 33:54; Yos 19:51; Mit 16:33Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.

Mgawo Kwa Benyamini

11Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.

1218:12 Yos 8:15; 7:2Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni. 1318:13 Mwa 28:19; Yos 12:9; Hes 32:3; Yos 16:5; Amu 1:23; Hes 18:20; Kum 10:9; Eze 44:28Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.

1418:14 Yos 10:10; 9:17; 1Nya 13:6Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.

1518:15 Yos 15:9Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa. 1618:16 Yos 17:15; 15:7-8; 2Fal 23:10; 2Nya 28:3; 33:6; Isa 30:33; Yer 19:2; Yos 15:8Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli. 1718:17 Yos 22:10; 15:6-7Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 1818:18 Yos 15:6; 11:2; 16:1Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba. 1918:19 Yos 15:6; Mwa 14:3Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.

2018:20 1Sam 9:1; Yos 21:4, 17Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki.

Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

2118:21 Yos 6:26; 1Fal 16:34; Lk 10:30Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo:

Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi, 2218:22 Yos 15:6; 2Nya 13:4; Yos 16:1Beth-Araba, Semaraimu, Betheli, 2318:23 Kum 2:23; Amu 6:11, 24; 8:27, 32; 9:6; 1Sam 13:17Avimu, Para na Ofra, 2418:24 Yos 21:17; 1Sam 13:3, 16; 14:5; 1Fal 15:22; 2Fal 23:8; Isa 10:29; Amu 19:12-16; Ezr 2:26Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

2518:25 Yos 10:40; Amu 4:5; 19:13; 1Sam 2:11; 7:17; 25:1; Neh 11:33; 1Fal 15:17, 21; Neh 7:29Gibeoni, Rama na Beerothi, 2618:26 Yer 11:3; Yos 9:17; Ezr 2:25; Neh 7:29Mispa, Kefira, Moza, 27Rekemu, Irpeeli, Tarala, 2818:28 2Sam 21:14; Yos 15:8; 10:1; 15:57; 9:17; Eze 48:23; Mwa 46:21; Mdo 17:26Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake.

Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.