約書亞記 15 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約書亞記 15:1-63

猶大支派分到的土地

1猶大支派按宗族抽籤分到的土地,南到以東的邊界,到曠野的最南端。 2南面的邊界始於鹽海南端的海灣, 3沿亞克拉濱山坡南面,經,北上至加低斯·巴尼亞南面,經過希斯崙亞達珥,再繞過甲加4押們埃及小河,直到地中海岸。

5東面以鹽海南端到約旦河口為邊界。

北界從約旦河口的海灣開始, 6伯曷拉,經過伯·亞拉巴北面,直到呂便的兒子波罕所立的大石; 7亞割谷往北到底璧,到谷南亞都冥隘口對面的吉甲,經隱·示麥泉,直到隱·羅結8然後再沿著欣嫩子谷而上,直到耶布斯,即耶路撒冷的南面,再到欣嫩谷西面、利乏音谷北端的山頂; 9從山頂到尼弗多亞泉,到以弗崙山的各城,直到巴拉,即基列·耶琳10巴拉向西繞到西珥山,到耶琳山北坡,即基撒崙,到伯·示麥,經亭拿11再到以革倫山北坡,轉向施基崙,經巴拉山和雅比聶,直到地中海。

12西面的邊界是地中海沿岸。以上是猶大人根據宗族所得地業的四界。

13約書亞又照耶和華的吩咐,在猶大支派所分到的土地之中劃出基列·亞巴,即希伯崙,分給耶孚尼的兒子迦勒亞巴亞衲人的祖先。 14迦勒趕走了住在那裡的亞衲族的三個族長,即示篩亞希幔撻買15再從那裡起兵攻打底璧底璧以前的名字是基列·西弗16迦勒說:「誰攻取基列·西弗,我就把女兒押撒嫁給他。」 17迦勒的兄弟基納斯的兒子俄陀聶攻取了那城,迦勒便把女兒押撒嫁給他。 18押撒出嫁的時候,勸丈夫向她父親要一塊田。她剛下驢,迦勒便問她:「你想要什麼?」 19押撒答道:「請你賜福給我,你既然把南地給了我,就求你也把水泉賜給我。」迦勒就把上泉和下泉都給了她。

20以下是猶大支派按宗族所得的產業: 21在最南面靠近以東的城邑有甲薛以得雅姑珥22基拿底摩拿亞大達23基低斯夏瑣以提楠24西弗提鏈比亞綠25夏瑣·哈大他加略·希斯崙——即夏瑣26亞曼示瑪摩拉大27哈薩·迦大黑實門伯·帕列28哈薩·書亞別示巴比斯約他29巴拉以因以森30伊勒多臘基失何珥瑪31洗革拉麥瑪拿三撒拿32利巴勿實忻亞因臨門,共二十九座城及其附近的鄉村。

33在丘陵地帶有以實陶瑣拉亞實拿34撒挪亞隱·干寧他普亞以楠35耶末亞杜蘭梭哥亞西加36沙拉音亞底他音基底拉基底羅他音,共十四座城及其附近的鄉村。

37還有洗楠哈大沙麥大·迦得38底連米斯巴約帖39拉吉波斯加伊磯倫40迦本拉幔基提利41基低羅伯·大袞拿瑪瑪基大,共十六座城及其附近的鄉村。

42還有立拿以帖亞珊43益弗他亞實拿尼悉44基伊拉亞革悉瑪利沙,共九座城及其附近的鄉村。

45還有以革倫及其附近的城邑和鄉村。

46還有以革倫到地中海一帶所有靠近亞實突的城邑和鄉村, 47亞實突及其附近的城邑和鄉村,迦薩及其附近的城邑和鄉村,直到埃及小河和地中海沿岸。

48在山區有沙密雅提珥梭哥49達拿基列·薩拿——即底璧50亞拿伯以實提莫亞念51歌珊何倫基羅,共十一座城及其附近的鄉村。

52還有亞拉度瑪以珊53雅農伯·他普亞亞非加54宏他基列·亞巴——即希伯崙洗珥,共九座城及其附近的鄉村。

55還有瑪雲迦密西弗淤他56耶斯列約甸撒挪亞57該隱基比亞亭拿,共十座城及其附近的鄉村。

58還有哈忽伯·夙基突59瑪臘伯·亞諾伊勒提君,共六座城及其附近的鄉村。

60還有基列·巴力——即基列·耶琳拉巴兩座城及其附近的鄉村。

61在曠野有伯·亞拉巴密丁西迦迦62匿珊、鹽城、隱·基底,共六座城及其附近的鄉村。

63猶大人沒能把住在耶路撒冷耶布斯人趕出去,他們至今仍然跟猶大人一同居住。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 15:1-63

Mgawo Kwa Yuda

115:1 Hes 34:3; 13:21; Yos 18:5Mgawo kwa kabila la Yuda, ulienea ukoo kwa ukoo, ukishuka kufikia eneo la Edomu, hadi Jangwa la Sini mwisho kabisa upande wa kusini.

215:2 Mwa 14:3Mpaka wao wa kusini ulianzia kwenye ghuba iliyoko kwenye ncha ya kusini mwa Bahari ya Chumvi, 315:3 Hes 34:4; Kum 1:2ukakatiza kusini mwa Akrabimu, ukaendelea hadi Sini ukaenda hadi kusini mwa Kadesh-Barnea. Tena ukapitia Hesroni ukapanda hadi Adari na ukapinda hadi Karka. 415:4 Hes 34:5; Mwa 15:18; 1Fal 8:65Kisha ukaendelea mpaka Azmoni na kuunganika na Kijito cha Misri, na kuishia baharini. Huu ndio mpaka wao wa upande wa kusini.

515:5 Hes 34:10; Mwa 14:3Mpaka wa upande wa mashariki ni Bahari ya Chumvi ukienea mahali Mto Yordani unapoingilia.

Mpaka wa upande wa kaskazini ulianzia penye ghuba ya bahari mahali Mto Yordani unapoingilia, 615:6 Yos 18:17-21ukapanda hadi Beth-Hogla, na kuendelea kaskazini mwa Beth-Araba hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 715:7 Yos 10:3; 7:24, 26; Kum 11:30; Yos 18:16-17; 2Sam 17:17; 1Fal 1:9; Hos 2:15Kisha mpaka ulipanda hadi Debiri kutoka Bonde la Akori na kugeuka kaskazini hadi Gilgali inayotazamana na materemko ya Adumimu, kusini mwa bonde. Ukaendelea sambamba hadi maji ya En-Shemeshi na kutokeza huko En-Rogeli. 815:8 2Nya 28:3; Yer 19:6; Yos 18:16, 28; Amu 1:21; 19:10; 2Sam 5:6; 1Nya 11:4; Ezr 9:1; Yos 10:1; 2Fal 23:10; 2Sam 5:18, 22; 1Nya 14:9; Isa 17:5Kisha ukapanda kwa kufuata Bonde la Ben-Hinomu sambamba na mteremko wa kusini wa mji mkubwa wa Wayebusi (yaani Yerusalemu). Kutoka hapo ukapanda juu ya kilima magharibi ya Bonde la Hinomu mwisho wa ncha ya kaskazini mwa Bonde la Warefai. 915:9 Yos 18:15; 2Sam 6:2; 1Nya 13:9; Yos 9:17Kutoka juu ya kilima mpaka ule ukaendelea hadi kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa, ukatokea kwenye miji ya Mlima Efroni na kuteremka kuelekea Baala (yaani Kiriath-Yearimu). 1015:10 Hes 24:18; Yos 19:22; 21:16; Amu 1:33; 1Sam 6:9; 1Fal 4:9; 2Fal 14:11; Mwa 38:12Kisha ukapinda upande wa magharibi kutoka Baala hadi Mlima Seiri, ukafuatia sambamba mteremko wa kaskazini mwa Mlima Yearimu (yaani Kesaloni), ukaendelea chini hadi Beth-Shemeshi na kukatiza hadi Timna. 1115:11 Yos 13:3; 19:43Ukaelekea hadi kwenye mteremko wa kaskazini mwa Ekroni, ukageuka kuelekea Shikeroni, ukapita hadi Mlima Baala na kufika Yabineeli. Mpaka ule ukaishia baharini.

1215:12 Kum 11:2415:12 Hes 34:6Mpaka wa magharibi ni pwani ya Bahari Kuu.

Hii ndiyo mipaka ya watu wa Yuda kwa koo zao.

Nchi Aliyopewa Kalebu

(Waamuzi 1:11-15)

1315:13 1Sam 25:3; 30:14; Mwa 23:2; Yos 10:36; 21:12; 1Nya 6:56; Hes 13:22Kwa kufuata maagizo ya Bwana kwake, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune sehemu katika Yuda: Kiriath-Arba, yaani Hebroni (Arba alikuwa baba wa zamani wa Anaki). 1415:14 Hes 13:33; 13:12; Amu 1:10, 20Kutoka Hebroni Kalebu alifukuza hao wana watatu wa Anaki, nao ni Sheshai, Ahimani na Talmai, wazao wa Anaki. 1515:15 Yos 10:38Kutoka hapo akaondoka kupigana dhidi ya watu walioishi Debiri (jina la Debiri hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi). 1615:16 1Nya 2:49; Amu 1:12Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.” 1715:17 Amu 3:9; 1Nya 4:13; 27:15; Hes 32:12; Yos 14:6Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu yake Kalebu, akauteka; hivyo Kalebu akamtoa Aksa binti yake aolewe naye.

1815:18 Amu 1:14; Mwa 24:64; 1Sam 25:23Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”

1915:19 Yos 10:40; Mwa 36:24Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Basi Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.

Miji Ya Yuda

2015:20 Mwa 49:8-12; Kum 33:7Huu ndio urithi wa kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo:

2115:21 Yos 10:40; 2Sam 23:20; 1Nya 11:22; Mwa 35:21Miji ya kusini kabisa ya kabila la Yuda katika Negebu kuelekea mpaka wa Edomu ilikuwa:

Kabseeli, Ederi, Yaguri, 22Kina, Dimona, Adada, 2315:23 Yos 12:22; 11:1Kedeshi, Hazori, Ithnani, 2415:24 1Sam 23:14; 2Nya 11:8Zifu, Telemu, Bealothi, 25Hazor-Hadata, Kerioth-Hezroni (yaani Hazori), 2615:26 Yos 19:2; 1Nya 4:28; Neh 11:26Amamu, Shema, Molada, 27Hasar-Gada, Heshmoni, Beth-Peleti, 2815:28 Yos 19:3; 1Nya 4:28; Mwa 21:14Hasar-Shuali, Beer-Sheba, Biziothia, 2915:29 Yos 19:3; 1Nya 4:29Baala, Iyimu, Esemu, 3015:30 Yos 19:4; Hes 14:45Eltoladi, Kesili, Horma, 3115:31 Yos 19:5; 1Nya 4:30; 12:1; Neh 11:28; 1Nya 2:49Siklagi, Madmana, Sansana, 3215:32 Hes 34:11; Yos 19:7; Amu 20:45; 21:13; Zek 14:10Lebaothi, Shilhimu, Aini na Rimoni; hiyo yote ni miji ishirini na tisa, pamoja na vijiji vyake.

3315:33 Yos 19:41; Amu 13:25; 16:31; 18:2; 13:2; 18:11; 2Nya 11:10; Neh 11:29Kwenye shefela ya magharibi:

Eshtaoli, Sora, Ashna, 3415:34 Yos 15:34; 1Nya 4:18; Neh 3:13; 11:30; Yos 19:21; 21:29; 12:17Zanoa, En-Ganimu, Tapua, Enamu, 3515:35 Yos 10:3; Mwa 38:1; 1Fal 4:10; Yos 10:10Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka, 3615:36 1Sam 17:52; 1Nya 4:31; 12:4Shaaraimu, Adithaimu na Gedera (au Gederothaimu); yote ni miji kumi na minne, pamoja na vijiji vyake.

37Senani, Hadasha, Migdal-Gadi, 3815:38 Yos 11:3; 2Fal 14:7Dileani, Mispa, Yoktheeli, 3915:39 Yos 10:3; 2Fal 22:1; 14:19Lakishi, Boskathi, Egloni, 40Kaboni, Lamasi, Kitlishi, 4115:41 2Nya 28:18; Yos 19:27; 10:10Gederothi, Beth-Dagoni, Naama na Makeda; yote ni miji kumi na sita pamoja na vijiji vyake.

4215:42 Hes 33; 20; Yos 19:7; 1Sam 30:30; 1Nya 4:32; 6:59Libna, Etheri, Ashani, 43Yifta, Ashna, Nesibu, 4415:44 1Sam 23:1-2; 1Nya 4:19; Neh 3:17-18; Yos 19:29; Amu 1:31; Mik 1:14-15Keila, Akzibu na Maresha; yote ni miji tisa pamoja na vijiji vyake.

4515:45 Yos 13:3Ekroni, pamoja na viunga vyake na vijiji vyake; 4615:46 Yos 11:22magharibi ya Ekroni, maeneo yote yaliyokuwa karibu na Ashdodi, pamoja na vijiji vyake; 4715:47 Yos 11:22; Mwa 15:18; Hes 34:6Ashdodi, miji yake na vijiji vyake na Gaza viunga vyake na vijiji vyake, hadi kufikia Kijito cha Misri na Pwani ya Bahari Kuu.

4815:48 Amu 10:1; Yos 21:14; 1Sam 30:27; 1Nya 6:57Katika nchi ya vilima:

Shamiri, Yatiri, Soko, 4915:49 Yos 10:3Dana, Kiriath-Sana (yaani Debiri), 5015:50 Yos 11:21; 21:14; 1Sam 30:28Anabu, Eshtemoa, Animu, 5115:51 Yos 10:41; 21:15; Yer 48:21; 2Sam 15:12Gosheni, Holoni na Gilo; miji kumi na mmoja pamoja na vijiji vyake.

5215:52 Mwa 25:14Arabu, Duma, Ashani, 53Yanimu, Beth-Tapua, Afeka, 5415:54 Mwa 35:27; Yos 14:15; Amu 1:10Humta, Kiriath-Arba (yaani Hebroni), na Siori; miji tisa pamoja na vijiji vyake.

5515:55 Amu 10:12; 1Sam 23:24-25; 25:1-2; 1Nya 2:45; Yos 12:22; 21:16Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta, 5615:56 Yos 17:16; 19:18; Amu 6:33; 1Sam 25:43; 1Fal 18:45; 1Nya 3:1; Hos 1:5Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa, 5715:57 Yos 18:28; 24:33; Amu 19:12; 20:4; 2Sam 23:29; 1Nya 11:31; Mwa 38:12Kaini, Gibea na Timna; miji kumi pamoja na vijiji vyake.

5815:58 1Nya 2:45; 2Nya 11:7; Neh 3:16; 1Nya 4:36; 12:7Halhuli, Beth-Suri, Gedori, 59Maarathi, Beth-Anothi na Eltekoni; miji sita pamoja na vijiji vyake.

6015:60 Yos 9:17; Kum 3:11; Yos 18:14; 1Sam 7:1, 2; 1Nya 13:6Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu) na Raba; miji miwili pamoja na vijiji vyake.

6115:61 Yos 8:15Huko jangwani:

Beth-Araba, Midini, Sekaka, 6215:62 1Sam 23:29; 24:1; Eze 47:10Nibshani, Mji wa Chumvi, na En-Gedi; miji sita pamoja na vijiji vyake.

6315:63 Yos 16:10; 17:12; Amu 1:21; Yos 10:1; Eze 48:7; Amu 19:10-12; Hes 13:29; 2Sam 14:16, 18; 2Nya 3:1; Zek 9:7Yuda hakuweza kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wakiishi Yerusalemu; hadi leo Wayebusi huishi huko pamoja na watu wa Yuda.