撒母耳記上 25 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記上 25:1-44

大衛與亞比該

1撒母耳死了,以色列人都聚在一起哀悼他,把他安葬在拉瑪他自己的墳地裡。之後,大衛到了巴蘭的曠野。 2瑪雲有個富翁擁有三千隻綿羊和一千隻山羊,他的產業在迦密。當時他正在迦密剪羊毛。 3他名叫拿八,是迦勒族人,妻子名叫亞比該,既聰慧又漂亮。拿八粗暴兇惡。 4大衛在曠野得知拿八正在剪羊毛, 5就派十個部下到迦密去見拿八,吩咐他們以他的名義向拿八問安, 6拿八說:「願你和你全家平安,願你一切順利! 7我聽說你正在剪羊毛。你的牧人與我們在迦密的時候,我們沒有欺負過他們,他們沒有丟過任何東西。 8你問問你的僕人就知道了。請你恩待我的部下,因為今天是好日子,求你隨手賞一點東西給晚輩我和我的部下。」

9大衛的部下就去把大衛的話告訴拿八,等候他的答覆。 10拿八說:「大衛是誰?耶西的兒子是誰?這些日子有很多僕人逃離主人, 11我怎能把餅、水和為剪羊毛者預備的肉分給一群來歷不明的人呢?」 12大衛的部下回去把拿八的話稟告大衛13大衛聽了,就吩咐眾人備刀,他自己也帶了刀去拿八那裡。大衛帶了四百人去,留下二百人看守營地。

14拿八的一個僕人告訴拿八的妻子亞比該說:「大衛從曠野派人來向我們主人問安,主人卻辱罵他們。 15大衛的僕人對我們很好,從來不欺負我們。我們跟他們一起在田野的時候,從來沒有丟過任何東西。 16我們在他們附近牧羊的時候,他們晝夜不斷地保護我們。 17所以,請你趕快想個法子,不然主人和他全家恐怕都會大難臨頭。主人是個兇暴的人,沒有人敢跟他說話。」

18亞比該連忙用驢馱上二百塊餅、兩皮袋酒、五隻宰好了的羊、三十七升烤麥、一百塊葡萄餅和二百塊無花果餅, 19又吩咐僕人說:「你們先去吧!我隨後就來。」她沒有把這事告訴丈夫拿八20她騎著驢下山的時候,就看見大衛和他的部下迎面而來。 21大衛曾說:「我在曠野保護這人的羊群,使牠們不致丟失,真是枉費功夫。他竟以怨報德。 22如果我讓他家裡一個男子活到明早,願上帝重重地懲罰我!」

23亞比該看見大衛,連忙下驢俯伏下拜。 24她俯伏在大衛腳前說:「我主啊,我願意承擔一切的罪過,請聽婢女說。 25請不要理會拿八那個惡徒,他人如其名25·25 拿八」意思是「愚蠢」。,是個名符其實的蠢人。當時婢女沒有見到你派來的使者。 26我主啊,既然耶和華阻止你親手殺人報仇,我就憑永活的耶和華和你的性命起誓,願你的仇敵和傷害你的人都像拿八一樣沒有好下場。 27現在,請把婢女帶來的禮物分給你的部下吧。 28請饒恕婢女的罪過,耶和華必使你的子孫世代做王,因為你是在為耶和華而戰,願你一生沒有過錯。 29你就是被人追殺,也會在你的上帝耶和華的保護下安然無恙。你敵人的性命卻要像石頭一樣被耶和華用投石器拋出去。 30-31如果你現在沒有殺人報仇,傷害無辜,到了耶和華照應許賜福給你、立你做以色列王的時候,你就不會心裡不安了。我主啊,耶和華賜福給你的時候,求你不要忘了婢女。」

32大衛亞比該說:「以色列的上帝耶和華當受稱頌!祂今天派你來見我。 33你很有見識,你今天攔阻我親手殺人復仇,值得稱讚。 34我憑阻止我殺你的以色列的上帝——永活的耶和華起誓,若不是你趕來迎接我,拿八家中不會有一個男子活到明天早上。」 35大衛接受了亞比該的禮物,對她說:「安心回家吧,我答應你的請求。」

36她回到家時,拿八正在大擺宴席,排場如御宴。她見拿八心情愉快,喝得酩酊大醉,就什麼也沒告訴他,等第二天早上再說。 37次日清晨,拿八酒醒以後,他妻子把發生的一切告訴他,他嚇得昏死過去,身體僵硬如石。 38過了十天,耶和華擊打拿八,他就死了。

39大衛聽見拿八的死訊,就說:「讚美耶和華!拿八羞辱我,祂為我申了冤,又阻止僕人行惡。祂使拿八得到了報應。」後來,大衛差遣使者去向亞比該求婚。 40他的使者就啟程到迦密去向亞比該傳達大衛的心意。 41亞比該聽了,立刻俯伏在地上說:「婢女願意效勞,為我主的僕人洗腳。」 42她連忙騎上驢,帶了五個侍女,跟隨大衛的使者前去,做了大衛的妻子。 43大衛已經娶了耶斯列亞希暖,她們二人就同做大衛的妻子。 44掃羅已經把自己的女兒——大衛的妻子米甲嫁給了迦琳拉億的兒子帕提

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 25:1-44

Daudi, Nabali Na Abigaili

125:1 1Sam 28:3; Law 10:6; Hes 20:29; Kum 34:8; Mwa 21:2; 1Sam 7:17; 2Nya 33:20Basi Samweli akafa, nao Israeli wote wakakusanyika na kumwombolezea; wakamzika nyumbani kwake huko Rama.

Kisha Daudi akateremka kwenye Jangwa la Maoni. 225:2 Yos 15:55; 2Sam 19:32; Mwa 31:19; 1Sam 23:24; Mwa 38:13; 2Sam 13:23Mtu mmoja huko Maoni, aliyekuwa na makao huko Karmeli, alikuwa tajiri sana. Alikuwa na mbuzi elfu moja na kondoo elfu tatu, aliokuwa akiwakata manyoya huko Karmeli. 325:3 Mit 31:10; Yos 14:13; 15:13; Rut 4:11; Mit 14:1; 24:3, 4; Isa 32:5, 7Jina la mtu huyo lilikuwa Nabali, naye mkewe aliitwa Abigaili. Alikuwa mwanamke mwenye busara na mzuri wa sura, lakini mumewe, ambaye alikuwa wa ukoo wa Kalebu, alikuwa mwenye hasira na mchoyo katika utendaji wake.

425:4 Mwa 38:13; 2Sam 13:23Daudi alipokuwa huko jangwani, akasikia kuwa Nabali alikuwa anakata kondoo manyoya. 525:5 1Sam 18:28; Lk 10:5Basi akatuma vijana kumi na kuwaambia, “Pandeni kwa Nabali huko Karmeli, mkamsalimie kwa jina langu. 625:6 Za 122:7; Mt 10:12; 1Nya 12:18Mwambieni: ‘Amani iwe kwako! Amani iwe kwako pamoja na wa nyumbani mwako! Pia amani iwe pamoja na vyote ulivyo navyo!

7“ ‘Nasikia kuwa huu ni wakati wa kukata kondoo manyoya. Wachunga mifugo wako walipokuwa pamoja nasi, hatukuwatendea mabaya na wakati wote waliokuwa huko Karmeli hakuna chochote chao kilipotea. 825:8 Neh 8:10; Es 9:19Waulize watumishi wako nao watakuambia. Kwa hiyo uwatendee wema vijana wangu, kwani tumekuja wakati wa furaha. Tafadhali wape watumishi wako na mwanao Daudi chochote kitakachokuja mkononi mwako kwa ajili yao.’ ”

9Watu wa Daudi walipofika wakampa Nabali ujumbe huu kwa jina la Daudi. Kisha wakangojea.

1025:10 Amu 9:28; Za 73:7, 8; 123:3, 4Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Huyu Daudi ni nani? Huyu mwana wa Yese ni nani? Watumishi wengi wanakimbia kutoka kwa bwana zao siku hizi. 1125:11 Amu 8:6Kwa nini nichukue mkate wangu, maji yangu na nyama niliyochinja kwa ajili ya wakata manyoya wangu, na kuwapa watu ambao hakuna anayejua wanakotoka?”

12Watu wa Daudi wakageuka na kurudi. Walipofika, wakaarifu kila neno. 1325:13 1Sam 22:2; 21:10; 23:13; 30:24; Hes 31:27Daudi akawaambia watu wake, “Jifungeni panga zenu!” Basi wakajifunga panga zao, naye Daudi akajifunga upanga wake. Watu kama mia nne hivi wakapanda pamoja na Daudi, na watu mia mbili wakabaki na vifaa.

1425:14 1Sam 13:10Mmoja wa watumishi akamwambia Abigaili, mkewe Nabali: “Daudi alituma wajumbe kutoka jangwani kumpa bwana wetu salamu zake, lakini akawavurumishia matukano. 15Hata hivyo watu hawa walikuwa wema sana kwetu. Hawakututendea mabaya, na wakati wote tulipokuwa nje huko mashambani karibu nao, hatukupotewa na kitu chochote. 1625:16 Kut 14:22; Ay 1:10; Za 139:5; Zek 2:5Usiku na mchana walikuwa ukuta wakituzunguka wakati wote tulipokuwa tukichunga kondoo zetu karibu nao. 1725:17 Kum 13:13; 1Sam 20:7Sasa fikiri juu ya jambo hili na uone unaweza kufanya nini, kwa sababu maafa yanakaribia juu ya bwana wetu na nyumba yake yote. Yeye ni mtu mwovu kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuzungumza naye.”

1825:18 Law 23:14; 1Sam 17:17; 1Nya 12:40; Mwa 42:26; 2Sam 16:1; Isa 30:6Abigaili akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili, viriba viwili vya divai, kondoo watano waliochinjwa vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu kavu, mikate mia mbili ya tini, akavipakia juu ya punda. 1925:19 Mwa 32:20; 1Sam 25:36Kisha akawaambia watumishi wake, “Tangulieni; mimi nitakuja nyuma yenu.” Lakini hakumwambia Nabali mumewe.

20Ikawa alipokuwa amepanda punda wake kwenye bonde la mlima, tazama, Daudi na watu wake wakawa wanateremka kumwelekea, naye akakutana nao. 2125:21 Za 109:5; 1Sam 19:4; Mwa 44:4; Za 35:12; Mit 17:13; Yer 18:20; 1Pet 2:20; 3:17Daudi alikuwa amesema, “Ilikuwa ni kazi bure kuchunga kwangu kote mali za huyu mtu huko jangwani hivi kwamba hakuna chochote chake kilichopotea. Yeye amenilipa baya kwa ajili ya wema. 2225:22 Rut 1:17; 1Fal 14:10; 21:21; 2Fal 9:8; 1Sam 20:13Bwana na amshughulikie Daudi, tena kwa ukali, ikiwa kesho asubuhi nitambakizia mwanaume hata mmoja aliye hai miongoni mwa watu wake wote!”

2325:23 Mwa 19:1; 1Sam 20:41; Yos 15:18; Amu 1:14Abigaili alipomwona Daudi, akashuka haraka kwenye punda wake, akainama kifudifudi uso wake mpaka nchi mbele ya Daudi. 2425:24 2Sam 14:9Akamwangukia miguuni pake na kusema: “Bwana wangu, kosa hili na liwe juu yangu mwenyewe. Tafadhali mruhusu mtumishi wako aseme nawe. Sikia kile mtumishi wako atakachosema. 2525:25 Mit 17:12; 12:16; 14:16; 20:3; Isa 32:5Bwana wangu na asimjali huyo mtu mwovu Nabali. Yeye anafanana na jina lake; jina lake ni Mpumbavu, nao upumbavu huenda pamoja naye. Lakini kwangu mimi, mtumishi wako, sikuwaona hao watu waliotumwa na bwana wangu.

2625:26 Ebr 10:30; 2Sam 18:32; 2Fal 2:2; Mwa 20:6; Rum 12:19; 2Sam 18:32“Basi sasa, kwa kuwa Bwana amekuzuia, wewe bwana wangu, kutokumwaga damu na kutolipiza kisasi kwa mikono yako mwenyewe, hakika kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, maadui zako na wote wanaokusudia kumdhuru bwana wangu wawe kama Nabali. 2725:27 Mwa 33:11; 1Sam 30:26Nayo zawadi hii ambayo mtumishi wako amemletea bwana wangu, wapewe watu wanaofuatana nawe. 2825:28 2Sam 14:9; 7:11, 26; 1Sam 18:17; 24:11; 1Fal 9:5; 1Nya 17:16Tafadhali samehe kosa la mtumishi wako, kwa kuwa Bwana kwa hakika ataifanya imara nyumba ya ufalme kwa bwana wangu, kwa sababu anapigana vita vya Bwana. 2925:29 1Sam 20:1; Yer 10:18; 22:26; 1Sam 17:50; 2Sam 4:8; Za 66:9; Mit 10:29, 30; Mdo 17:28Hata ingawa yuko mtu anayekufuatia kuuondoa uhai wako, usiruhusu baya lolote kuonekana kwako siku zote za maisha yako, uhai wa bwana wangu utafungwa salama kwenye furushi la walio hai na Bwana Mungu wako. Lakini uhai wa adui zako atavurumishwa kama vile jiwe kutoka kwenye kombeo. 3025:30 1Sam 12:12; 13:14Bwana atakapokuwa ameshamtendea bwana wangu kila kitu chema alichoahidi kumhusu yeye na kumweka kuwa kiongozi wa Israeli, 3125:31 Mwa 40:14; 2Sam 3:10bwana wangu hatakuwa na dhamiri inayolemewa na mzigo kwa kumwaga damu kusiko na sababu, au kujilipizia kisasi yeye mwenyewe. Bwana atakapomletea bwana wangu mafanikio, umkumbuke mtumishi wako.”

3225:32 Mwa 24:27; Kut 18:10; Lk 1:68; Ezr 7:27; Za 41:12, 13; 72:18; 2Kor 8:16Daudi akamwambia Abigaili, “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli aliyekutuma kunilaki leo. 33Ubarikiwe kwa uamuzi wako mzuri na kwa kunizuia nisimwage damu leo na kulipiza kisasi kwa mikono yangu. 34La sivyo, hakika kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisiwadhuru, kama usingekuja haraka kunilaki, hakuna hata mwanaume mmoja wa Nabali angeachwa hai kufikia mapambazuko.”

3525:35 Mwa 19:21; 2Fal 5:19; 1Sam 20:42; 2Sam 15:9; Lk 7:50Ndipo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake kile alichokuwa amemletea, naye akasema, “Nenda nyumbani kwako kwa amani; nimesikia maneno yako na kukujalia ombi lako.”

3625:36 Rut 3:7; Mit 20:1; Mhu 10:17; Isa 5:11, 22; 22:13; 28:7; 56:12; Hos 4; 11; 2Sam 13:23Abigaili alipokwenda kwa Nabali, alikuwa ndani ya nyumba yake akifanya karamu kama ile ya mfalme. Naye alikuwa ana furaha nyingi, akiwa amelewa sana. Kwa hiyo Abigaili hakumwambia mumewe kitu chochote mpaka asubuhi yake. 3725:37 Kut 15:16; Kum 28:28; Ay 15:21Basi asubuhi, Nabali alipokuwa amelevuka, mkewe akamwambia mambo yote, nao moyo wake ukazimia, akawa kama jiwe. 3825:38 Kum 32:35; 1Sam 24:12; 26:10; 2Sam 6:7; 12:15; Kut 12:29; 2Sam 6:7; Ay 12:10; Za 104:29; Mdo 12:23Baada ya siku kumi, Bwana akampiga Nabali, naye akafa.

3925:39 Mit 22:23; 2Sam 3:28, 29; 1Fal 2:44; Es 7:10; Za 7:16Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “Ahimidiwe Bwana, ambaye amenitetea shauri langu dhidi ya Nabali kwa kuwa alinitendea kwa dharau. Amemzuia mtumishi wake asitende mabaya na Bwana ameuleta ubaya wa Nabali juu ya kichwa chake mwenyewe.”

Kisha Daudi akatuma ujumbe kwa Abigaili kumwomba awe mke wake. 40Watumishi wa Daudi wakaenda mpaka Karmeli na kumwambia Abigaili, wakisema, “Daudi ametutuma kwako kukuchukua uwe mkewe.”

4125:41 Rut 2:10, 13; Mit 15:33; 18:12Akainama chini uso wake mpaka ardhini, akasema, “Mjakazi wako yuko hapa, tayari kuwatumikia na kuwanawisha miguu watumishi wa bwana wangu.” 4225:42 2Sam 2:2; 3:3; 1Nya 3:1Abigaili akainuka kwa haraka, akapanda punda wake, akihudumiwa na wajakazi wake watano, akaenda pamoja na wajumbe wa Daudi, naye akawa mkewe. 4325:43 2Sam 3:2; 1Nya 3:1; 1Sam 30:5; 2Sam 2:2; Yos 15:56Pia Daudi alikuwa amemwoa Ahinoamu wa Yezreeli, wote wawili wakawa wake zake. 4425:44 2Sam 3:15; Isa 10:30Lakini Sauli alikuwa amemwoza Mikali binti yake, aliyekuwa mkewe Daudi, kwa Palti mwana wa Laishi, kutoka Galimu.